TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 21, 2015

SHUGULI ZA BIASHARA ARUSHA ZASIMAMA KWA SABABU YA MGOMO

DALA
Shuguli mbalimbali ndani ya jiji la Arusha zikiwemo za kibiashara jana(leo)zimelazimika kusimama mara baada ya mabasi ya abiria (Daladala) kugoma kubeba abiria kwa madai kuwa utaratibu wa Ruti ndefu zilizopangwa na Sumatra ni uonevu mkubwa
hataivyo kugoma kwa daladala hizo pia kuliweza kuwaaathiri wanafunzi ambao wanatumia usafiri huo kwa ajili ya kwenda mashuleni hali ambayo iliwafanya wakose masomo lakini pia baadhi yao wafike mashuleni wakiwa wamechelewa.
Akiongea kwa niaba ya madereva daladala ambao wamegoma dereva,Jumaa isa alisema kuwa wanashangazwa sana na Sumatra kuweza kuwapangia Ruti ndefu wakati bado hata abiria wa Jiji la Arusha hawana uwezo wa kutumia hizo ruti ndefu.
Jumaa alisema kuwa kwa historia ya mji wa Arusha abiria wanakuwepo majira ya asubui na jioni kwa pekee ila kwa majira ya mchana abiria ni wachache sana sasa hali hiyo inafanya mparangano mkubwa sana barabarani.
“ivi kwa ruti hii hii hapa abiria tunawatafuta hivyo alafu ruti ndiyo hiyo ianzishwe refu bado tajiri anataka fungu lake la fedha jioni, kama haitoshi bado hatujashikwa na Matrafiki bado hatujala sisi na makonda wetu bado familia zetu hazijatudai kila siku je kwa hali hiyo tutafika kweli au ndio wanatufanya sasa tuwe majambazi tena wa kutumia Silaha”alihoji
aliendelea kwa kusema kuwa hapo awali kulikuwa na vikao ambavyo vilifanyika lakini hakuweza kukubalina muafaka wa ruti ndefu ambazo Sumatra walikuwa wanazitaka kitu cha kushangaza ni kwamba tayari wameshaambiwa kuanza ruti ndefu jambo ambalo wamelipinga.
“kama wanataka hizi ruti ndefu basi wanatakiwa wapandishe nauli lasivyo sisi kama madereva tutateseka sana kiasi cha kushidnwa kuwafkisha abiria mahali ambapo tunatakiwa kuwafikisha”aliongeza Jumaa
katika hatua nyingine akiongea kwa niaba ya abiria Bi Neema Palangyo kutoka katika eneo la kwa Muorombo alisema kuwa mgomo huo umesababisha madhara makubwa sana kwa wananchi wa Arusha kwani uzalishaji wa siku hiyo ya mgomo ni mkubwa sana.
“hapa arusha mjini kila mtu anategemea zaidi usafiri wa daladala ili kuweza kufika mjini sasa kama kuna mgomo tutafikaje mimi naishauri Serikali wakati mwingine kuweza kufanya mawasiliano ya kutosha kwani tunaoteseka ni sisi kina mama na watoto ambao tunategemea usafiri wa jumla”aliongeza Neema
Hataivyo zaidi ya daladala mia tano ambazo zote zinafanya shuguli zake za usafiri jijini Arusha ziliweza kugoma na kisha kupinga azimio hilo la ruti ndefu ambalo lilitolewa kwa kushirikiana na wadau wote wa Sumatra na usafirishaji Jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment