TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, January 22, 2015

CBE WATAKIWA KUFUNGUA MTAWI ZANZIBAR

unnamed (59)
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akiwahutubia wageni mbalimbali waliohudhuria sherehe sherehe za miaka 50 ya CBE leo jijini Dar es salaam.Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
…………………………………………………………………………………………………………
Mahmoud Ahmad Dar es Salaam Chuo cha Biashara CBE kimetakiwa kufungua Tawi la chuo hicho Zanzibar na serikali itatoa ushirikiano kufanikisha ilikuweza kusogeza huduma ya chuo hicho na kuongeza wigo wa Udahili kwa wanafunzi wa Upande wa Zanzibar kwani kitawanufaisha wananchi hao bila ya kusahau utoaji wa elimu bora.
Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Raisi wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini ya chuo hicho yaliofanyika jijini hapa huku akisema kuwa Mtu wa miaka hamsini si nongwa kuwa na watoto watano akiwa na maana ya wao ya chuo hicho kufungua tawi 5 Zanzibar.
Balozi Idd alisema kuwa Serikali ya SMZ itasaidia katika kuanzishwa kwa Tawi la chuo hicho Zanzibar ili kuongeza udahili wa wanafunzi wengi wenye weledi kwa upande wa Zanzibar kwenye sekta ya Biashara utakaosaidia ukuaji wa maendeleo endelevu na nyadhifa ndani ya serikali huku akiwataka kutoa elimu bora yenye viwango vya kitamaifa.
Alisema kuwa serikali imesikia kilio cha uongozi wa chuo hicho kwenye changamoto mbali mbali zikiwemo za ukarabati wa majengo,kunakotokana na kutopata udhamini wa serikali na kuahidi kulishughulikia suala hilo na mengine ikiwemo pia suala za Oc za wafanyakazi kuwa endelevu na kupatikana.
Alisema kuwa taifa linategemea wataalamu wanaozalishwa katika chuo hicho katika kuhakikisha linajiletea maendeleo huku akitanabaisha kuwa utoaji wa elimu ya ujasiriamali chuoni hapo Serikali itasaidia ikitambua ni eneo muhimu kwa ukuaji wa kiuchumi kwa wananchi .
“Serikali itakaa pamoja na Bodi ya chuo kuhakikisha changamoto mbali mbali zinapatiwa Ufumbuzi na kuwa inatambua ongezeko la udahili linaenda na changamoto mbali mbali hususani kukarabati majengo ya chuo hicho”alisema Balozi Idd.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho prof.Methwer Luhanga alisema kuwa Ongezeko la udahili haliendani na uongezaji wa miundombinu ya chuo hivyo akaiomba serikali kuipatia udhamini chuo hicho ilikuweza kukarabati miundo mbinu yake kwani chuo kinauwezo wakulipa mikopo hiyo tena kwa wakati.
Luhanga alisema kuwa chuo kimepata mafaniko kwa kuongeza stashada tangia kilipoanzisha kutoka moja hadi kufikia tano na kuwa wapo mbioni kuanzisha stashahada ya TEHAMA mwakani ikiwa ni pamoja na kuongeza wakufunzi zaidi wenye shahada za uzamili na uzamivu kwani hapo awali hakukuwa na wakufunzi wenye kiwango hicho.
“Kupata dhamana ya Serikali ndio tatizo la kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali za chuo chetu hivyo tunakuomba utuwasilishie kadhia hiyo”aslisema Prof Luhanga
Nae Mkuu wa Chuo hicho Emanuel Mjema alisema kuwa chuo hicho kilichanzishwa mwaka 1965 na wanafunzi 25 na kimepiga hatua na kimeweza kudahili wanafunzi elfu 14 hivi sasa kikiweza kutoa kuanzia Astashahada hadi digrii ya uzamivu haya ni mafanikio makubwa kwa kipindi cha mika hamsini tofauti na hapo kilipoanzishwa kikitoa wanafunzi cheti tu
Alisema kuwa chuo hicho kimeweka mikakati ya kutoa elimu bora itakayowasaidia wanafunzi wa chuo hicho kuendana Miataala ya soko la kimataifa itakayosaidia wahitimu kuzitumia fursa zilizopo hapa nchini tena kwa weledi.
Alisema kuwa chuo hicho kwa sasa kinatoa kozi ya shahada ya Mizani na vipimo ambapo ni chuo pekee kwa nchini za kusini jangwa kutoa somo hilo na kuwa wapo mbioni kutoa somo la Tehama chuoni hapo baadae mwaka huu,

No comments:

Post a Comment