Makamu wa Pili wa Rais wa 
Zanzibar, Balozi Seif Ally Idd akiwahutubia wageni mbalimbali 
waliohudhuria sherehe sherehe za miaka 50 ya CBE leo jijini Dar es 
salaam.Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
…………………………………………………………………………………………………………
Mahmoud Ahmad Dar es Salaam
Chuo cha Biashara CBE kimetakiwa kufungua Tawi la chuo hicho 
Zanzibar na serikali itatoa ushirikiano kufanikisha ilikuweza kusogeza 
huduma ya chuo hicho na kuongeza wigo wa Udahili kwa wanafunzi wa Upande
 wa Zanzibar kwani kitawanufaisha wananchi hao bila ya kusahau utoaji wa
 elimu bora.
Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa 
Pili wa Raisi wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ali Idd 
wakati wa maadhimisho ya miaka hamsini ya chuo hicho yaliofanyika jijini
 hapa huku akisema kuwa Mtu wa miaka hamsini si nongwa kuwa na watoto 
watano akiwa na maana ya wao ya chuo hicho kufungua tawi 5 Zanzibar.
Balozi Idd alisema kuwa Serikali 
ya SMZ itasaidia katika kuanzishwa kwa Tawi la chuo hicho Zanzibar ili 
kuongeza udahili wa wanafunzi wengi wenye weledi kwa upande wa Zanzibar 
kwenye sekta ya Biashara utakaosaidia ukuaji wa maendeleo endelevu na 
nyadhifa ndani ya serikali huku akiwataka kutoa elimu bora yenye viwango
 vya kitamaifa.
Alisema kuwa serikali imesikia 
kilio cha uongozi wa chuo hicho kwenye changamoto mbali mbali zikiwemo 
za ukarabati wa majengo,kunakotokana na kutopata udhamini wa serikali na
 kuahidi kulishughulikia suala hilo na mengine ikiwemo pia suala za Oc 
za wafanyakazi kuwa endelevu na kupatikana.
Alisema kuwa taifa linategemea 
wataalamu wanaozalishwa katika chuo hicho katika kuhakikisha linajiletea
 maendeleo huku akitanabaisha kuwa utoaji wa elimu ya ujasiriamali 
chuoni hapo Serikali itasaidia ikitambua ni eneo muhimu kwa ukuaji wa 
kiuchumi kwa wananchi .
“Serikali itakaa pamoja na Bodi ya
 chuo kuhakikisha changamoto mbali mbali zinapatiwa Ufumbuzi na kuwa 
inatambua ongezeko la udahili linaenda na changamoto mbali mbali 
hususani kukarabati majengo ya chuo hicho”alisema Balozi Idd.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi
 ya chuo hicho prof.Methwer Luhanga alisema kuwa Ongezeko la udahili 
haliendani na uongezaji wa miundombinu ya chuo hivyo akaiomba serikali 
kuipatia udhamini chuo hicho ilikuweza kukarabati miundo mbinu yake 
kwani chuo kinauwezo wakulipa mikopo hiyo tena kwa wakati.
Luhanga alisema kuwa chuo kimepata
 mafaniko kwa kuongeza stashada tangia kilipoanzisha kutoka moja hadi 
kufikia tano na kuwa wapo mbioni kuanzisha stashahada ya TEHAMA mwakani 
ikiwa ni pamoja na kuongeza wakufunzi zaidi wenye shahada za uzamili na 
uzamivu kwani hapo awali hakukuwa na wakufunzi wenye kiwango hicho.
“Kupata dhamana ya Serikali ndio 
tatizo la kuweza kukabiliana na changamoto mbali mbali za chuo chetu 
hivyo tunakuomba utuwasilishie kadhia hiyo”aslisema Prof Luhanga
Nae Mkuu wa Chuo hicho Emanuel 
Mjema alisema kuwa chuo hicho kilichanzishwa mwaka 1965 na wanafunzi 25 
na kimepiga hatua na kimeweza kudahili wanafunzi elfu 14 hivi sasa 
kikiweza kutoa kuanzia Astashahada hadi digrii ya uzamivu haya ni 
mafanikio makubwa kwa kipindi cha mika hamsini tofauti na hapo 
kilipoanzishwa kikitoa wanafunzi cheti tu
Alisema kuwa chuo hicho kimeweka 
mikakati ya kutoa elimu bora itakayowasaidia wanafunzi wa chuo hicho 
kuendana Miataala ya soko la kimataifa itakayosaidia wahitimu kuzitumia 
fursa zilizopo hapa nchini tena kwa weledi.
Alisema kuwa chuo hicho kwa sasa 
kinatoa kozi ya shahada ya Mizani na vipimo ambapo ni chuo pekee kwa 
nchini za kusini jangwa kutoa somo hilo na kuwa wapo mbioni kutoa somo 
la Tehama chuoni hapo baadae mwaka huu,

No comments:
Post a Comment