![]()  | 
| Watu wazima hawana muda wa tendo la ndoa hali inayosababisha kupungua kwa idadi ya watu Japan | 
Asilimia 50 ya watu wazima nchini 
Japan hawashiriki katika tendo la ngono kulingana na utafiti, swala 
linalosababisha kupungua kwa idadi ya watu nchini humo.
Ripoti 
hiyo iliofanywa na shirika la upangaji uzazi nchini humo imebaini kwamba
 asilimia 49.3 ya watu 3000 waliohojiwa hawakushiriki ngono mwezi 
uliopita.
Kati ya asilimia 48.3 waliohojiwa walisema kuwa 
hawakushiriki katika ngono kwa mwezi moja huku asilimia 50.1 ya wanawake
 wakijizuia kushiriki ngono.Takwimu zote zilipanda kwa asilimia 5 kutoka
 kwa ufatiti uliofanywa awali mwaka 2012.
Walipoulizwa ni kwa nini
 hawashiriki katika tendo la ngono, asilimia 21.3 ya wanaume walio 
katika ndoa walidai kuchoka baada ya kutoka kazini huku asilimia 15.7 
wakisema kuwa hawana haja ya kushiriki katika tendo la ngono baad ya 
wake zao kujifungua.
Kati ya wanawake asilimia 23.8 walisema kuwa tendo la ngono linasumbua na asilimia 17.8 wakidai walikuwa wamechoka.
Swala
 jengine la kushangaza ni kuongezeka kwa idadi ya vijana ambao hawana 
hamu na tendo la ngono.Zaidi ya asilimia 20 ya wanaume walio kati ya 
umri wa miaka 25 na 29 hakuwa na hamu ya kufanya ngono.

No comments:
Post a Comment