![]()  | 
| maandamano Drc Congo | 
Polisi nchini Jamhuri ya 
Kidemokrasi ya Congo wamewafyatulia risasi waandamanaji kwenye mji mkuu 
Kinshasa walio na hasira katika kile kinachoonekana kama jitihada za 
kutaka kuongoza uongozi wa rais Joseph Kabila.
Watu kadha 
walitolewa eneo la kati kati mwa mji wakiwa na majeraha ya risasi ambapo
 pia kulitoka makabiliano kwenye chuo kikuu cha mji huo.
Milio ya risasi iliripotiwa katika maandamano mengine katika mji ulio mashariki wa Goma.
Watu
 kadhaa walipatikana na majeruhi ya risasi katikati mwa mji huo huku 
ghasia zengine zikiripotiwa katika katika chuo kimoja kikuu.
![]()  | 
| rais wa Drc Congo Joseph Kabila | 
 Viongozi wa upinzani waliitisha maandamano hayo baada ya bunge dogo 
kuidhinisha sheria siku ya jumamosi inayoagiza kufanyika kwa hesabu ya 
idadi ya watu kabla ya uchaguzi wa urais utakaofanyika mwaka ujao.
Wabunge hao wa upinzani wamesema kuwa mpango huo utachelewesha uchaguzi huo ambao umekuwa ukingojwa kwa hamu kwa miaka kadhaa.
Rais
 Joseph Kabila ambaye amekuwa mamlakani kwa miaka 15 amehudumu miula 
miwili na hawezi kuwania tena urais kulingana na katiba.
Bunge kuu linatarajiwa kuungazia mswada huo wa uchaguzi hii leo.


No comments:
Post a Comment