WAKAZI
 wa Kata Kibeberu na Magole, Kata ya Kitunda, Manispaa ya Ilala, Mkoa wa
 Dar es Salaam wamemlalamikia mkandarasi wa ujenzi wa daraja la Magole 
kwa kushindwa kukamisha ujenzi wa daraja hilo hadi sasa.Aidha
 wakazi hao wamesema pamoja na daraja hilo kuchelewa kukamilika pia kwa 
mtazamo wao wanaamini kuwa lipo chini ya viwango ambavyo vinatakiwa.Mjumbe
 wa Kamati ya Ujenzi wa daraja hilo Samir Ibrahim alisema daraja hilo 
lnatakiwa kukamilika ifikapo Februari mwaka huu lakini hadi sasa hakuna 
dalili za kukamilika kwake.
Ibrahim alisema pamoja na kuchelewa kukamilika kwa daraja 
hilo pia wamejaribu kutoa ushauri kuwa urefu wa daraja hilo hautaweza 
kuhimili maji mengi ambayo yanapita hasa wakati wa mvua.
Mjumbe huyo alisema jambo lingine ambalo linawatia shaka kwa 
kutodumu kwa daraja la Magole ni pamoja na aina ya nondo zinazotumika ni
 ishara tosha kuwa haliwezi kudumu kwa muda mrefu.
“Mimi ni mjumbe wa kamati ya ujenzi lakini
kusema ukweli hali ya ujenzi wa daraja hili naitilia shaka sana 
sidhani kuwa litadumu na ukiangalia mto huo ni mkubwa sana unahitaji 
daraja la viwango,” alisema.
Ibrahim alisema pamoja na jitihada zao za kutoa taarifa za 
hali ya daraja hilo kukosa ubora hakuna juhudi zozote ambazo 
zimechukuliwa na Serikali kufuatilia.
Kwa upande wake Aisha Athuman alisema iwapo daraja hilo la 
Magole halitakamilika kwa wakati ni wazi kuwa watoto na mama wajawazito 
wataathirika kwa kiwango kikubwa.
Athman alisema daraja hilo likipitisha maji watoto hawaendi shule jambo ambalo linawaathiri kitaaluma.
“Unajua hapa njia ya kuendea shule ya Msingi Magole ni moja 
tu hivyo iwapo hali ya daraja kutokamilika ka wakati itaendelea ni 
dhahiri kuwa madhara yataongezeka,” alisema Athuman.
Akizungumzia adha hiyo Mwendesha Boda Boda Mbonamengi Charles
 alisema kinachoonekana ni Serikali kuwasahau wakazi wa pembezoni hali 
ambayo inafifisha maendeleo.
Charles alisema kutokana na kutokamilika kwa daraja hilo mambo mengi ya maendeleo yamekuwa yakikwama kutokana kero ya eneo hilo.
Aidha Mkazi huyo alihoji kuwepo kwa vifusi kwa muda mrefu 
ambavyo vimewekwa barabarani bila kusambazwa huku wakiwa wameahidi kwa 
muda mrefu kuwa vitasambazwa.
Diwani wa Kata ya Kitunda Daniel Julias alipotakiwa kuelezea 
tatizo hilo la daraja kuchelewa alisema sababu kubwa ni ukosefu wa 
fedha.
Alisema mkataba kati ya Manispaa na Mkandarasi wa ujenzi wa 
daraja hilo unatarajiwa kuisha mwezi Februari hivyo anachoamini ni kuwa 
wakati huo ukifika hatua zingine zitachuliwa.
Diwani huyo alisema suala la vifusi kutosambazwa linatokana na maagizo yake kuwa visubiri daraja litakapo kamilika.
Julias aliwataka wakazi wa Magole kuwa wavumilivu kwani 
Serikali yao inafanya kila jitihada kuhakikisha kuwa changamoto 
mbalibali zinatatuliwa kwa wakati.
Mwisho.

No comments:
Post a Comment