TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, February 17, 2015

Oscar Pistorius apandishwa hadhi jela

Oscar Pistorius
Kuhusiana na mwanariadha Oscar Pistorius aliyeko kifungoni, imeelezwa kwamba sasa anaweza ama kuruhusiwa kukumbatiana na wageni wake na hata kuwabusu wanaomtembelea ,anaruhusiwa kusikiliza redio na hata kuvaa vitu vya thamani ikiwemo vito vya thamani akiwa ndani ya gereza.
Mtuhumiwa huyo wa mauaji,amepewa ruhusa ingine ya kuwa huru kupiga simu atakavyo,vile vile bajeti yake inayodaiwa kuwa kubwa, imekubaliwa aweze kununua vyoo atakavyo na hata akitaka chipsi ataletewa,na huu ni uamuzi wa bwana jela anaye angalia wafungwa na hadhi zao naye Pistorius yuko kundi B.
Ikumbukwe kwamba Oscar alimuua mpenzi wake mnamo mwezi kama huu na siku inayotajwa kuwa muhimu ulimwenguni tarehe ya kumi na nne Valentine's Day,mwaka wa jana akiwa nyumbani kwake.
Akiwa jela Pistorius anajaribu kuyazoea mazingira ya jela na inamuwia vigumu kukubali kuwa ameupoteza uhuru wake, na pia kuonekana kama tishio la usalama na hivyo yumo ndani
Msemaji wa familia ya Pistorius mwanamama,Annalise Burgess, amemzungumzia mwanariadha huyo aliyekuwa maarufu duniani kiasi cha kupachikwa jina la Blade Runner,sasa amepandishwa hadhi na kuwa daraja la A .

Familia ya Oscar ina Whatsapp la familia yao ambalo linafuatilia taarifa zote za mwanariadha huyo na pia hutumia akaunti hiyo kujadiliana masuala ya biashara za familia.
Inaelezwa kuwa watu wanaoongoza kumtembelea Oscar Pistorius Jela ni kaka na dadake Aimee Carl na wakiisha kuonana naye hutuma taarifa na picha katika kundi hilo na kinachoendelea kumhusu yeye gerezani.
Kupandishwa kwa Oscar kuna maanisha kuwa anaruhusiwa kutembelewa na wageni zaidi ikiwemo familia yake.Hapo mwanzo kila anayemtembelea huzungumza naye kwa njia ya simu akiwa ametengwa na mgeni wake na vioo, na hakuruhusiwi kuguswa,lakini mambo sasa yamebadilika.
Sasa Oscar mwenye umri wa miaka ishirini na nane, anaweza kuwakumbatia jamaa zake wamtembeleapo,na muda wa kumuona umeongezwa kutoka saa mbili hadi tatu kwa mwezi,na wageni wamtembeleao bado wanakabiliwa na sheria ya kupekuliwa kabla ya kuonana ma mfungwa huyo ambaye bado anatakiwa kuvaa sare za jela zenye rangi ya samawati ama ita orange

No comments:

Post a Comment