TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 25, 2014

Marekani:IS haikuangusha ndege yetu

Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.
Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Rubani wa ndege iliodaiwa kudunguliwa na wapiganaji wa IS akamatwa
Picha za IS zinamuonyesha rubani wa ndege hiyo akikamatwa.
Wamemtaja rubani huyo kuwa Moaz Youssef al-Kasasbeh.
Wakati huohuo Jordan imesema kuwa hasara iliyopata ya kupoteza ndege yake moja ya kivita, katika anga linalodhibitiwa na waasi wa Islamic State, haitayumbisha majeshi yake kuendelea kukabiliana na matendo ya kigaidi.

No comments:

Post a Comment