TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 25, 2014

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA POLISI USALAMA BARABARANI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA



 

Hali ya usalama barabarani kiujumla kwa mwaka huu 2014 ni ya kuridhisha ukilinganisha na mwaka jana. Kwa mfano ukiangalia takwimu za ajali kwa miezi 11 ya mwaka 2013  Januari- Novemba kulinganisha na takwimu ya ajali kwa miezi 11 ya mwaka 2014 Januari-Novemba utagundua kuwa kuwa kuna upungufu wa ajali kwa asilimia 38.20 za ajali, asilimia 5.63 za vifo na asilimia 28.27 za majeruhi.


Jan-Nov 2013
Jan-Nov 2014
Tofauti
Asilimia (%)
Ajali
21,791
13,466
-8325
38.20
Vifo
3,642
3,437
-205
5.63
Majeruhi
18,813
13,495
-5318
28.27
 
Hata hivyo, pamoja na juhudi hizi bado matukio ya ajali yanaendelea na tunashuhudia yakichukua maisha ya ndugu na jamaa zetu huku yakiacha majeruhi, vilema na uharibifu wa mali.
 
Ndugu wanahabari,
Wito wangu wa leo napenda kuwakumbusha Madereva  na watumiaji wote wa barabara kuziheshimu sheria na kanuni za usalama barabarani husasani katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka kinachoambatana na sikukuu za Krismas na mwaka mpya.

Mtaungana na mimi kwamba kumekuwa na ongezeko kubwa la ajali za barabarani miaka iliyopita katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka ambapo sababu kubwa za ongezeko hilo ni za kibinadamu zikiwemo mwendo kasi, ulevi, matumizi ya simu za mkononi wakati wa kuendesha, uendeshaji wa hatari (overtaking), kutofuata alama,michoro na ishara za barabarani ,matumizi ya taa zenye mwanga mkali barabarani na uegeshaji mbaya wa magari barabarani.

Ndugu wanahabari,
Bado kuna ukiukwaji wa sheria inayowataka wapanda pikipiki (madereva na abiria) kuvaa kofia ngumu (helmet) muda wote wanapotumia vyombo hivyo. Tunawakumbusha watumiaji wa vyombo hivyo kuzingatia matumizi ya kofia ngumu muda wote wanapotumia vyombo hivyo hasa katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka.

Ndugu wanahabari,
Napenda pia kuchukua nafasi kuwakumbusha askari wote kusimamia sheria na kanuni za usalama barabarani kama wanavyoelekezwa, Kinyume na hapo hatua kali za kisheria na kinidhamu zitachuliwa dhidi ya yeyote atakayekiuka. Niwaombe tu wananchi mtoe ushirikiano kwa kutupatia taarifa za askari wanaokiuka taratibu zao za kazi katika maeneo mbalimbali.

Ndugu wanahabari,
Jeshi la polisi Kikosi cha usalama barabarani limejipanga kikamilifu hususani kimikakati  kupambana na ajali za  barabarani na kadhia zote za sikukuu za mwisho wa mwaka kama nauli na ubabaishaji katika usafiri wa abiria. Tumekuwa na kampeni  zinazoendelea katika maeneo mbalimbali nchini zinazolenga kutoa elimu ya usalama barabarani. Dhumuni kubwa ni kupambana na makosa hatarishi yanayochangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la ajali (mwendo kasi, ulevi, matumizi ya simu wakati wa kuendesha, kupita magari mengine na uendeshaji wa hatari)

Katika suala la nauli, tarehe 21/12/2014 kwa kutumia askari kanzu wa Jeshi la Polisi tuliwakamata watu 7 waliokuwa wakiuza tiketi kwa bei kubwa katika kituo kikuu cha Ubungo. Watuhumiwa hao tarehe 22/12/2014 walipelekwa mahakamani ambapo kesi zao zitatajwa tena tarehe 5/1/2015 na 6/1/2015 na wako gereza la Segerea wakisubiri tarehe hizo

1.Victor Kombe –Wakala wa KVC

2.Mussa Msangi- Karani wa tiketi HAPPY NATION

3.Walter Nkya - Karani wa tiketi IBRA LINE

4.Fredrick Lema- Karani wa tiketi MBAZI TRAVEL COACH

5.Ramadhani Mbaga –Usafiri wa TOYOTA NOAH

6.Stephen Amos – Usafiri wa TOYOTA NOAH

7.Jane Gabriel - Usafiri wa TOYOTA NOAH

Aidha jana tarehe 23/12/2014 asubuhi watu wengine 3 walikamatwa wakiuza tiketi kwa bei ya juu ambao leo taratibu zikikamilika watapelekwa mahakamani,
1.Kassim Azaria           - Usafiri wa NOAH
2.Kelvin Charles           - Wakala wa Islam
3. Mbaraka Tariba Kombo  - Wakala wa Islam

Nipende tu kuwajulisha watumiaji wote wa barabara kuwa  askari wataendelea kuwa wakali sana katika kipindi hiki  ambapo hatua kali za kisheria zitachuliwa kwa yeyote atakayekamatwa  akivunja sheria za usalama barabarani. Niwaombe tu watumiaji wote  wa barabara watii sheria bila shuruti .
Ndugu wanahabari,
Mwisho lakini sio kwa umuhimu napenda kuwaasa  wananchi na wadau wa usalama barabarani kwa ujumla, watupe ushirikiano zaidi kwa kutoa taarifa za uhalifu wa usalama barabarani, kufuata sheria, kanuni na maelekezo kwa ajili ya usalama wao watumiapo barabara. Kila mmoja atambue haki na wajibu wake akiwa barabarani ikiwa ni kuwa na subira na kujali watumiaji wengine wa barabara kwani wana haki sawa ya kutumia barabara. Watoto wasiachwe kutembea barabarani bila ya uangalizi wa watu wazima.
                     Ninawatakia heri ya Xmas na Mwaka Mpya.
˝Maamuzi yako barabarani ni hatima yetu-Fikiria kwanza”.
Imetolewa na:  
MOHAMMED R.MPINGA – DCP
KAMANDA WA POLISI,
KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI (T)

No comments:

Post a Comment