TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 25, 2014

CHAMA CHA TENNIS TANZANIA (TTA) KUANDAA TENA MASHINDANO YA AFRIKA MASHARIKI

CHAMA CHA TENNIS TANZANIA (TTA) KUANDAA TENA MASHINDANO YA
AFRIKA MASHARIKI (EAST AFRICAN JUNIOR ZONAL CHAMPIONSHIPS) KWA VIJANA CHINI YA UMRI WA MIAKA 16, JANUARI 11-19 2015.

Chama cha Tennis Tanzania (TTA) kimepewa nafasi nyingine tena ya kuandaa mashindano ya vijana wa ukanda wa Afrika Mashariki  (East Africa zonal championships) na yatafanyika kuanzia tarehe 11 hadi 19 Januari 2015. Nchi shiriki kwa mwaka 2015 ni Burundi, Comoros, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Seychelles, Sudan na Tanzania. 

Tunategemea jumla ya washiriki wapatao 72 (pamoja na Tanzania). Tanzania itawakilishwa na vijana 22 ikiwa na team A na B.

TTA inajivunia kuanzishwa kwa mfumo wa renki unaotoa fursa kwa wachezaji kujikusanyia pointi kwenye orodha ya wachezaji wa tennis Tanzania. Hili limesaidia urahisi wa uchaguzi wa timu na kuepuka lawama za kupendelewa watu flani. Kila mchezaji wa chini ya umri 18 ana nafasi sawa ya kukusanya pointi kwa kushiriki mashindano yanayoandaliwa na TTA au watu binafsi yaliyoidhinishwa na chama. Timu ya Tanzania mwaka huu itawakilishwa na:
 
Boys




Categories
Jina
TTA Rank
Points
Club
Under 12
Deogratus Felex Ernest
1
115
AICC
Yusuph Laurence Godwin
2
100
AICC
Kanuti Omary Alagwa
4
30
AGC
Under 14
Hassan Hamisi Yambi
1
125
AICC
Emmanuel Frank Temba
3
30
AGC
Ali Hamza
4
30
DGC
Adam Mwambungu
3(12&U)
80
KJ
Under 16
Frank Menard Mshana
1
105
AGC
Emmanuel Mallya
5
10
AGC
Omary Hamisi Sulle
4
10
AGC
Hassan Mkajira

2
KJ





Girls




Categories
First Name


Club
Under 12
Ester Paulo Nankulange
1
140
AGC
Emiliana Katabalo
5
15
KJ
Maria Elisha Milanzi
4
25
AGC
Under 14
Emiliana Stanslaus
2
30
KJ
Shadya Maulid Kitenge
12
5
KJ
Jackline Kayuga
2(12&U)
75
KJ
Under 16
Adela Abraham Mollel
1
32
AGC
Georgina Kemmy Kaindoah
N/A
N/A
N/A
Round Robin




Kutokana na uhaba wa wachezaji wa kike kwenye kundi la umri wa chini ya miaka 16, nafasi moja itapiganiwa na wachezaji waliopo lakini hawajapata nafasi ya kushiriki mashindano ya ndani ili kupata pointi kwa mtindo wa mtoano (round robin).

TTA inafanya juhudi kuwataarifu wazazi wa watoto walioingia kwenye timu kwa ajili ya maandalizi. Timu ya Tanzania itasimamiwa na kocha Nico Jonas ambaye ni msimamizi wa High Performance Tennis (HPC) akishirikiana na Majuto Omari wote wakiwa ni makocha wa
level 2 kwa mujibu wa ITF.

Timu inatazamiwa kuingia kambini tarehe 27-12-2015 ambapo watapewa mafunzo mbali mbali pamoja na kufanya shindano la kujipima kabla ya mashindano yenyewe mwezi wa
kwanza.

TTA itafanya mkutano rasmi na waandishi wa habari kabla ya kuanza kwa mashindano
mwezi wa kwanza.

Kwa niaba ya uongozi mzima, tunawatakia sikuu njema ya krismasi.

Katibu Mkuu wa TTA.

MWISHO.

Kwa maelezo ya ziada wasiliana na:
1.    Nico Jonas – Kocha Mkuu - +255 754 250 097.
2.    Majuto Majaliwa – Kocha Mkuu msaidizi – 0718 849 889.
3.    William Kallaghe – Maswala yote ya mashindano - +255 754 210 437.

No comments:

Post a Comment