TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, December 27, 2014

Bi Gbagbo ashtakiwa Ivory Coast

Mke wa aliyekuwa rais wa Ivory Coast laurent Gbagbo,bi Simone Gbagbo amefunguliwa mashtaka ya ghasia za baada ya uchaguzi nchini Ivory Coast
Mke wa rais wa zamani wa Ivory Coast Laurent Gbagbo, Simone Gbagbo amefikishwa mahakamani kutokana na mashtaka ya kuhusika kwenye ghasia za baada ya uchaguzi ambapo zaidi ya watu 300 waliuwa.
Bi Gbagbo na watu wengine 82 akiwemo waziri mkuu wa zamani wameshtakiwa kwa kuhujumu usalama wa nchi, ukabila na kwa kubuni makundi ya uhalifu.
Rais wa zamani Laurent Gbagbo ambaye alikataa kukubali kushindwa kwenye uchaguzi mkuu miaka minne iliyopita anasubiri kesi yake kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC kutokana na mashtaka ya uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Zaidi ya watu 3000 waliuawa katika ghasia hizo baada ya rais huyo wa zamani kukataa kushindwa katika kura ya awamu ya pili.
Bi Gbagbo ambaye alikuwa anazuiliwa katika kifungo cha nyumbani kwa miaka mitatu ameshtakiwa kwa jaribio la kuhujumu usalama wa taifa hilo.
Aliyekuwa waziri mkuu Gilbert Ake N'Gbo na kiongozi wa chama cha FPI Affi N'Guessan pia wamefunguliwa mashtaka na bi Gbagbo.

No comments:

Post a Comment