TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 24, 2016

African Diaspora Leaders Policy Briefing. TAXES, ACCOUNTING AND LIFE INSURANCE SERVICES WAKALA WA VIPIMO (WMA) KUFANYA MSAKO WA MIZANI FEKI YA MADUKANI MKOANI ARUSHA PROF. MBARAWA ATOA MWEZI MMOJA KWA MAKANDARASI WOTE NCHINI KUTOA MIKATABA YA AJIRA KWA WAFANYAKAZI TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) WANAHABARI, WATAFITI KUTOKA COSTECH WAZURU KABURI LA BABA WA TAIFA BUTIAMA MKOANI MARA WATU WANAOSADIKIKA KUWA MAJAMBAZI WAPORA MILIONI 12 JIJINI DAR PANGAPANGUA YATINGA IDARA YA UHAMIAJI, WAZIRI KITWAGA AAGIZA KUFANYIKA MABADILIKO MAKUBWA WAKULIMA WILAYANI RORYA MKOANI MARA WAPATIWA MAFUNZO YA KUPATA HUDUMA ZA UGANI KWA NJIA YA SIMU Kichupa cha leo Kamikaze Shori Official Music Video BASI LA NATA RAHA LAPATA AJALI BUNDA LEO ASUBUHI LIPUMBA AMTAKA RAIS MAGUFULI ATANGAZE MSHAHARA WAKE DK KALEMANI: CHUNGUZENI MAOVU YA WAWEKEZAJI WAGENI FISI WALA WATU WAUA, KUJERUHI MKOANI TABORA MKUU WA RIADHA KENYA ASIMAMISHWA KWA MIEZI 6 BALOZI PIERRE MUTAMBA AWATAKA WAKONGO KUFANYAKAZI KWA BIDII, AKUNWA NA UTENDAJI KAZI WA RAIS MAGUFULI MAGAZETI YA LEO FEB 23, 2016 VODACOM TANZANIA KUPITIA PROGRAMU YA PAMOJA NA VODACOM WATOA MSAADA WA MASHINE YA KUDURUSU KARATASI SHULE YA SEKONDARI SHIMBWE. Zaidi ya trilioni 1 zilivyokusanywa na kugawanywa ndani ya mwezi mmoja Jerry Muro kawajibu wanaosema Yanga alipendelewa dhidi ya Simba Feb 20 2016 Mwanamuziki Linah Sanga Akiri 'Kubanjuka' na Wizkid Hotelini... MTANDAO WA MODEWJIBLOG WAPATA KWIKWI YA KIUFUNDI KURUDI HEWANI HIVI PUNDE IDRIS Sultan Amjibu Mange Kimambi Baada ya Mange Kumshauri Wema Atafute Manager wa Bank Mwenye Pesa Kuliko Vijana wa Laki Laki



Wakala wa Vipimo (WMA), Mkoa wa Arusha unatarajia kuanza kufanya msako wa mizani zisizokuwa na ubora katika maduka ya mkoani Arusha zinazodaiwa kutumika kuwapunja wananchi.
Meneja wa WMA wa mkoa huo, Dunford Manzi amesema leo kuwa mizani hizo zinadaiwa kutengenezwa nchini India na China.
Amesema kabla ya kuanza msako huo, watatoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa kutumia mizani zenye ubora.
Pia, amewataka wafanyabiashara wabadilishe mizani hizo na kuweka halisi kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Sheria ya Vipimo Sura 340 (19) inatutaka tufanye ukaguzi wa mara moja kwa mwaka, katika kipindi cha mwezi mmoja tulikagua mizani na mashine kwenye vituo vya mafuta tumebaini mizani zilizopo sokoni hazina ubora zinapaswa kuondolewa.
“Kwa kawaida mizani ikifanyiwa kazi kwa muda wa mwaka mmoja zinahitaji kukaguliwa,” amesema.
Amewataka wafanyabiashara kuitumia ofisi ya WMA kupata ushauri wa vipimo sahihi ili kuepuka kuwapa hasara wateja wao.Pia, amewataka wateja kukagua mizani kabla ya kununua bidhaa ili kujiridhisha na kuepuka kuibiwa.
Mkazi wa Kwamrombo, Zaidi Jonathani amesema wafanyabiashara wengi wanatumia mizani iliyorekebishwa kwa lengo la kujipatia faida kubwa isivyo halali kwani unaweza kupima bidhaa moja kwenye mizani mbili na ikakupa vipimo tofauti. “Wafanyabiashara wanakuwa na mizani halisi na iliyofanyiwa ujanja, lengo lao wakija watu wa vipimo wanaonyesha iliyokaguliwa,” amesema.
Muuza nyama katika Soko la Kilombero, Loishiye Mollel amesema mizani yake hukaguliwa mara mara huku akiwaondoa hofu watu wanaodhani wanapunjwa.

MWANANCHI
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ametoa mwezi mmoja kwa makandarasi wote nchini kuhakikisha wanasaini mikataba ya ajira na wafanyakazi katika miradi ya ujenzi wa barabara inayoendelea nchini kote.

Akizungumza jijini Arusha mara baada ya kufanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa barabara ya Sakina-Tengeru yenye urefu wa Km 14.1 na barabara ya mchepuo ya kusini (Arusha bypass) yenye urefu wa Km 42.4, Prof. Mbarawa amesema mkandarasi atakayeshindwa kutoa mikataba kwa mujibu wa sheria za Tanzania, atanyang’anywa kazi ya ujenzi kwa kuvunja sheria.

“Barabara zinajengwa kwa kodi za wananchi hivyo wajenzi wa barabara nao ni lazima wafuate sheria za nchi ili kuhakikisha Serikali inapata kodi stahili na wafanyakazi wazawa nao wanapata haki stahili kwa mujibu wa ajira zao", amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Amezitaka taasisi za TRA, NSSF na nyingine zinazosimamia ajira za wafanyakazi kufuatilia miradi ya ujenzi ili kuona fursa za mapato ambazo serikali inaweza kupata na kusajili wafanyakazi katika hifadhi ya mifuko ya jamii.

Waziri Prof. Mbarawa amewataka mameneja wa tanroads na maafisa kazi kukagua mikataba ya ajira za ujenzi katika maeneo yao ili kuona haki inatendeka kwa makandarasi na kwa wafanyakazi ili ujenzi wa barabara ukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Katika hatua nyingine Prof. Mbarawa amefungua mkutano wa Sita wa Baraza la Wafanyakazi la Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na kuwataka kuweka mikakati itakayowezesha kulinda hifadhi ya barabara, kudhibiti magari yanayozidisha uzito na kusimamia kasi katika miradi ya ujenzi wa barabara.

“Mmekua mkifanya kazi nzuri, endeleeni kufanya kazi kwa uadilifu, uwazi, weledi na kujiwekea malengo ya kujipima mwaka hadi mwaka ili muendelee kuwa tassisi ambayo watu watakuja kujifunza kwenu”, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Naye Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale amemhakikishia Waziri Mbarawa kuwa TANROADS imejipanga kuhakikisha miradi ipatayo 90 ya ujenzi wa barabara inayoendelea nchini kote inakamilika katika ubora unaotakiwa na unao uwiana na thamani ya fedha.

Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amemuagiza Meneja wa Wakala wa Majengo nchini (TBA), mkoa wa Arusha, Bw. Victor Baltazar kukusanya madeni yote kwa haraka ili kukamilisha miradi ya ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na za biashara inayosimamiwa na Wakala huo mjini Arusha kukamilika kwa wakati.

Prof. Mbarawa ambaye yuko katika ziara ya mikoa ya kanda ya kaskazini amezitaka taasisi zilizo chini wa wizara hiyo kuhakikisha zinafanya kazi kibiashara ili kuboresha mapato ya Serikali na hivyo kuiwezesha Serikali kutoa huduma bora kwa wananchi.

Wiki iliopita, mnamo tarehe 16 Februari, 2016, aliyekuwa mjumbe wa Timu ya Kampeni ya Chama Cha Wananchi (CUF), Ndugu Mohamed Ahmed Sultan Al-Mugheiry (maarufu kwa jina la Eddy Riyami), alipokea barua ya wito kutoka kwa Jeshi la Polisi Zanzibar ikimtaka kufika Makao Makuu ya Polisi, Ziwani, Zanzibar siku inayofuata, yaani tarehe 17 Februari, 2016, saa 2 asubuhi kwa kile kilichoelezwa kwamba “kuna mambo muhimu yanayomhusu” ambayo walitaka kuzungumza naye.

Bila ya kukosa, Eddy Riyami aliitikia wito huo na kufika Makao Makuu ya Polisi, Zanzibar na kuonana na SSP Simon S. Pasua wa Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (CID). Hata hivyo, hakuhojiwa na badala yake alipewa simu na kutakiwa azungumze na Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Bw. Salum Msangi ambaye alimwambia arudi tena Jumatatu, tarehe 22 Februari, 2016.

Eddy Riyami, akiwa raia mwema, alirudi tena jana kama alivyoagizwa. Alipofika hapo alihojiwa na Polisi na baadaye mwanasheria aliyefuatana naye akatakiwa kutafuta wadhamini wawili watakaomdhamini hadi atakapoitwa tena. Wakati mwanasheria wake aliporudi na wadhamini, akaelezwa kwamba Polisi imebadili uamuzi wake na imeamua kumuweka ndani hadi leo, tarehe 23 Februari, 2016. Mwanasheria na familia yake wakatakiwa kwenda tena Makao Makuu ya Polisi hiyo leo, saa 3 asubuhi. Walipofika leo asubuhi, wakaambiwa kwamba DCI kaacha maagizo kuwa suala la Eddy Riyami liachwe kwanza na wao warudi tena saa 6 mchana.

Hadi tunapotoa taarifa hii, hakujapatikana maelezo yoyote ya msingi juu ya kinachoendelea na wala Eddy Riyami hajafikishwa Mahkamani kusomewa mashtaka yoyote.
La ajabu zaidi, ni kwamba hata mke wake alipofika kituo cha polisi cha Madema anakoshikiliwa kwa ajili ya kwenda kumuona, hakuruhusiwa kumuona.

Kutokana na mwenendo huu, Chama Cha Wananchi (CUF) kinalichukulia suala hili kwamba ni mwendelezo wa vitendo vya unyanyasaji wa kisiasa dhidi ya wapinzani wa CCM, vitendo ambavyo tunaamini vinafanywa kwa shinikizo la wanasiasa.

Itakumbukwa kwamba kwa muda mrefu tokea wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, 2015 tumekuwa tukitoa tahadhari za kuwepo mipango ya kuwakamata viongozi wa CUF na wanaharakati wengine ili kufanikisha malengo ya kisiasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Tuna kila sababu ya kuamini kwamba hatua ya kumkamata Eddy Riyami na kumuweka ndani bila ya kumfikisha Mahkamani ni utekelezaji wa mipango hiyo. La si hivyo, ikiwa Eddy Riyami ametenda kosa basi angelishafikishwa Mahkamani ndani ya muda wa saa 24 tokea kukamatwa kama sheria inavyotaka.

Chama Cha Wananchi (CUF) kinalitaka Jeshi la Polisi kuacha kutumiwa na kutumika kisiasa kufanikisha malengo ya kisiasa ya CCM. Tunashangazwa kwamba siku zote wanaoitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani ni wanasiasa wa vyama vya upinzani na wanaharakati wengine lakini hatujawahi kushuhudia viongozi wa CCM kuitwa kuhojiwa, kukamatwa na kuwekwa ndani. CUF imetoa taarifa kadhaa kwa Jeshi la Polisi zinazohusu matamshi na vitendo vya viongozi wa CCM vyenye mwelekeo wa uhalifu lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa. Hizo ni dalili za waziwazi za Polisi kutumiwa na kukubali kutumika kisiasa.

Tunalitaka Jeshi la Polisi iwapo kweli lina kesi dhidi ya Eddy Riyami basi limfikishe Mahkamani haraka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake. Na iwapo hawana kesi, basi wamwachie huru mara moja.

Umefika wakati wa Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kitaalamu kama sheria na kanuni zao zinavyoagiza badala ya kuwatumikia wanasiasa wa CCM.

HAKI SAWA KWA WOTE 
HAMAD MASOUD HAMAD 
KAIMU MKURUGENZI WA HABARI NA MAWASILIANO NA UMMA - CUF
Wanahabari na Watafiti kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), waliokuwa katika ziara ya kuzungumza na wakulima wa mkoa wa Mwanza kuhusu changamoto za kulimo zinazo wakabili pamoja na matumizi ya bioteknolojia katika kilimo wakiwa mbele ya kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere walipozuru kaburi hilo hivi karibuni Kijiji cha Mwitongo Butiama mkoani Mara.
Watafiti na wanahabari hao wakiwa mbele ya makaburi ya wazazi wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknnolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (kushoto), na Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney wakiwa wamesimama ilipo sanamu ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Hapa ni picha ya pamoja katika sanamu ya Baba wa Taifa.
Mwendeshaji wa mtandao wa www. habari za jamii.com Dotto Mwaibale akivinjari katika moja ya jengo katika makazi ya Baba wa Taifa.
Matembezi yakiendelea katika makazi ya Baba wa Taifa.
Mratibu Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Afrika, Daniel Otunge (kushoto) Mtafiti Kiongozi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknnolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (katikati), na Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney wakiwa wamekaa katika kibanda alichokuwa akipenda kupumzika Hayati Nyerere wakati wa 
uhai wake.
Jamii inayofanya shughuli mbalimbali nyumbani kwa Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere wakionesha upendo kwa kunywa chai pamoja katika makazi ya Mwalimu Nyerere yaliyopo Kijiji cha Mwitongo, wilayani  Butiama mkoani Mara kama walivyonaswa na kamera yetu katika ziara hiyo.
Picha ya pamoja katika nyumba maalumu lilipo kaburi na Mwalimu Nyerere.
Dereva wa Msafara huo, Mr Stanley akiwa mbele ya gari na mtafiti Kutoka Kituo cha Utafiti cha Ukiriguru cha jijini Mwanza, Isabela Msuya.
Mwendeshaji wa mtandao wa www. habari za jamii.com Dotto Mwaibale akiweka maua kwenye kaburi la Baba wa Taifa.
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro.(Picha na Maktaba)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
MKAZI wa Mafinga,  David Isack ( 32) alivamiwa na majambazi na kuporwa sh.milioni 12 ambazo alikuwa akipeleka katika Benki ya  DTB, ambapo alivamiwa na  watu  watano wanatuhumiwa kuwa ni majambazi wakiwa na usafiri wa pikipiki  mbili aina ya boxer.

Akizungumza na waandishi wa habari ijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro amesema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 12 mwaka huu katika eneo la Uwanja Ndege , katika kurupushani za kutaka kuchukua fedha hizo walitokea askari na kuwazingira na kisha kuanza kukimbia na kuweza kudondosha bunduki aina ya SMG pamoja na risasi 24 ambazo zilitakiwa kutumika katika tukio hilo.

Amesema askari walipowakamata wananchi walikusanyika katika tukio hilo na kuanza kuwapiga watu wanaodaiwa kuwa majambazi mpaka kupoteza maisha kutokana kushambuliwa huko na wengine watatu waliweza kukimbia na kiasi hicho cha fedha.

Kamishna Sirro amesema Isac alikuwa akitokea benki ya NMB na kwenda kupeleka fedha hizo katika benki ya DTB iliyopo Quality Plaza.

Katika operesheni nyingine imefanikiwa kukamata bastola moja ambayo ilipatikana  Februari 19 mwaka huu maeneo ya Kiwalani Kwa Gude kutokana na polisi kupata taarifa juu ya watu kujificha katika kichaka kwa ajili ya kufanya uhalifu  na baada ya kugundua polisi wapo eneo hilo walikimbia na kuacha silaha hiyo na jeshi la polisi linafanyia kazi mmiliki wa silaha.

Hata hivyo Jedhi la Polisi Kanda Maalumu linawashikilia watu wane wanaodaiwa kuwa ni majambazi sugu waliowakamata eneo la  Buguruni kwa Mnyamani ambao ni Mohamed Hassan maarufu kwa jina Kidali (21)Mkazi wa Vingunguti Speco,Hamis Alli (20) Mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani, Adam Salum (23) Mkazi wa Buguruni  kwa Madenge, Bakari Hamis (19) Mkazi wa Buguruni.

Aidha amesema katika taarifa usalama Barabarani wameweza kukusanya zaidi ya Sh. Bilioni moja ya ni fedha iliyotokana na makosa ya magari kuanzia Januari 02 hadi Februari 22 mwaka huu.

CHANZO: MICHUZI BLOG
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto meza kuu), Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Injinia Hamad Masauni (kulia meza kuu) wakifurahi jambo pamoja na Watendaji Wakuu wa Idara ya Uhamiaji (kushoto) na Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (kulia), wakati wa kikao cha kujadili masuala mbalimbali ya utendaji kazi ndani ya Idara hiyo na Wizara kiujumla. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Wakwanza upande wa kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Simba Yahya, na wakwanza upande wa kushoto ni Kaimu Kamishna wa Uhamiaji, Victoria Lembeli. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga ameagiza yafanywe mabadiliko makubwa katika Vitengo mbalimbali vya Idara ya Uhamiaji ili kuboresha huduma na kuimarisha uadilifu katika Vitengo hivyo.
Mheshimiwa Kitwanga ametoa maagizo hayo leo wakati alipofanya kikao na Viongozi wa Idara ya Uhamiaji ambapo pia kilihudhuriwa na Viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakiwemo Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara.  Kikao hicho kilifanyika katika Makao Makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katika kikao hicho, Mheshimiwa Kitwanga ameagiza watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji walioko Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, wahamishwe na kupelekwa maeneo mengine nchini, wakiwemo wale wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
Wengine watakaohamishwa ni kutoka Kitengo cha Pasipoti, Uhasibu, Hati za Ukaazi na Kitengo cha Upelelezi, vyote vya Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Aidha ameagiza pia kuwa Wakuu wote wa Vitengo vya Upelelezi vya wilaya zilizopo jijini Dar es Salaam, na pia wale wa Vituo vya Tunduma, Mtukula, Holili na Kasumulo, wahamishiwe maeneo mengine, na pia watumishi wote waliokaa kwa zaidi ya miaka mitatu katika Vituo hivyo.
Amesema hatua hii inayochukuliwa sasa  ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa yatakayofanywa katika Idara ya Uhamiaji ili kuboresha huduma zinazotolewa na Idara hii ambayo ni moja ya Idara muhimu za Serikali.
Amesema katika kuisafisha Idara hii, uangalifu mkubwa utachukuliwa ili kuhakikisha kuwa hakuna mtumishi anayeonewa wala kupendelewa, lakini lengo kubwa ni kuvunja mtandao wa wapokea rushwa na wale wasiowajibika.
Amesema kufuatana na utafiti uliofanywa hivi karibuni umeonyesha kuwa matatizo ya rushwa katika Idara ya Uhamiaji yanashika nafasi ya kwanza kwa kuwa na asilimia 30, asilimia 20 ni uongozi mbovu na asilimia 20 ni matumizi mabaya ya madaraka. Asilimia 15 inahusisha vitendea kazi wa mifumo hafifu ya kufanya kazi, asilimia 10 huduma mbovu na asilimia 5 ukabila na upendeleo.
Amewataka Viongozi na watumishi wote wa Idara ya Uhamiaji kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya kazi na waepuke vitendo vya kupokea rushwa na kusaidia wahamiaji haramu na wauza madawa ya kulevya.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali 
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
23 Februari, 2016

Mtafiti Kiongozi Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk.Nicholaus Nyange (katikati), akizungumza na wakulima wa Wilaya ya Rorya Mkoani Mara katika mafunzo ya siku moja kwa wakulima hao ya kutumia simu kupashana habari za kilimo na kujua changamoto zinazo wakabili. Kulia ni Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia za Kilimo Afrika (OFAB), Daniel Otunge na kushoto ni Mtafiti Mkuu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney.
Maofisa Ugani wa Wilaya ya Rorya wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Ofisa Kilimo wa Wilaya ya Rorya, Dominick Ndentabura akizungumza na wakulima hao kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
Wakulima wa Rorya wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Mkulima Saye Okelo akizungumzia changamoto ya ukosefu wa mbegu katika mafunzo hayo.
Mkulima Sinde Mjinja akielezea changamoto ya bei kubwa ya pembejeo za kilimo.
Mkulima akizungumizia magonjwa ya mbegu za mhogo na pembejeo kuchelewa kuwafikia wakulima.
Mkulima Emmanuel Lugombo akizungumzia kuoza kwa mbegu ya mkombozi.
Mkulima Sophia Charles kutoka Kijiji cha Roche akizungumzia changamoto ya ukosefu wa soko la zao la mhogo ambapo wanategemea zaidi soko nchini Kenya.
Mkulima Charles Ruola akizungumzia changamoto ya kilimo cha mahindi.
Mkulima wa Kijiji cha Kowaki kilichopo Wilaya ya Rorya mkoani Mara, Elias Kaseno akizungumzia changamoto ya kilimo cha muhogo na mahindi mbele ya watafiti kutoka Jukwaa la Bioteknolojia (OFAB) na Watafiti kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), waliopo wilayani humo jana kujua changamoto mbalimbali za wakulima na kutoa mafunzo ya matumizi ya Bioteknolojia katika kilimo.
Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyinondi akielekeza jinsi ya kupiga simu wakati akiendesha mafunzo hayo kwa wakulima.
Wakulima wakiwa kwenye mafunzo.
Wakulima wakiwa mafunzo hayo.
Wakulima wakiwa kwenye mafunzo hayo.
Wakulima hao wakibadilishana mawazo baada ya kupiga picha.
Jengo la Halmshauri ya Wilaya ya Rorya.
Shamba la muhogo lililoshambuliwa na ugonjwa wa batobato  lililopo jirani na jengo la Halmshauri ya Rorya ambapo wapo wataalamu wa kilimo.

Na Dotto Mwaibale
KATIKA hali isiyotegemewa shamba lenye ukubwa wa ekari moja la zao la muhogo lililopo nyuma ya Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Rorya mkoani Mara ambapo ofisi ya wilaya ya kilimo ipo halipo katika matunzo ya kilaalamu ambapo mwandishi wa habari hii ambaye yupo katika ziara ya kilimo na watafiti kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) alitembelea. 

Mwandishi wa habari hii alidhani kuwa shamba hilo la muhogo ni maalumu kwa ajili ya kufundishia wakulima kuhusu ugonjwa unaoshambulia zao hilo ujulikanao kama batobato na athari zake kumbe ni shamba la mkulima ambalo limekosa huduma za ugani licha ya maofisa ugani kuwepo mita chache ya  eneo hilo.


Kutokana na hali hiyo inapaswa wakulima wa namna hiyo kupata huduma za kilimo kutoka maeneo mengine kutokana na maofisa ugani hao kushindwa kutoa elimu ambapo shamba hilo limekuwa ni chanzo cha kueneza ugonjwa huo katika maeneo mengine.


Akizungumza katika mafunzo ya matumizi ya simu katika kilimo kwa wakulima wa wilaya ya Rorya Mratibu wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Philbert Nyinondi alisema mafunzo hayo ya siku moja yatawasaidia wakulima kupashana habari za kilimo na changamoto zao.


"OFAB imeleta mafunzo haya kwa wakulima ambao ni wadau wetu ili waweze kupashana habari za kilimo, changamoto zinazo wakabili na kutafuta masoko ya mazao yao kwa njia ya simu badala ya kutumia simu hizo kupigiana kwa mambo ya kawaida" alisema Nyinondi.


Alisema kupitia mafunzo hayo wakulima hao wataweza kushirikiana na mitandao mingine ya kijamii ili kutatua changamoto zao za kilimo zikiwemo za wadudu waharibifu wa mazao, ukame na nyinginezo.


Alisema washiriki wa mafunzo hayo walikuwa ni 20 kutoka katika wilaya hiyo na kuwa shirikisha wataalamu wa kilimo.
 Watu wanne wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa wajeruhiwa leo asubuhi baada ya basi la Nata Raha toka Serengeti kuacha njia na kugonga nguzo eneo la Kwa Sabato, Bunda. Mganga Mkuu Nicholas Machochota athibitisha kutokea kwa vifo hivyo, pia majeruhi wamepelekwa katika hospitali ya Bungando kwa matibabu zaidi.
ENDELEA KUTUFUATILIA KWA TAARIFA ZAIDI

CHANZO: ITV TANZANIA


Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Rais John Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake, kwa kuwa amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge.
Katika makala yake itakayochapishwa kwa ukamilifu katika gazeti hili kesho, Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli amejipambanua kuwa kiongozi anayeguswa na matatizo ya wanyonge, hapendi makuu, anahimiza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na matumizi mazuri ya fedha za umma.
“...Hata hivyo, Watanzania hawajui mshahara wake ni kiasi gani?” alihoji Profesa Lipumba.
Profesa huyo aliyejikita katika masuala ya uchumi, alirejea mijadala mbalimbali iliyowahi kuibuliwa kuhusu mshahara wa Rais, ikiwamo ule uliyowahi kuibuliwa mwaka 2013 na Zitto Kabwe, wakati huo akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema kuwa Rais analipwa Sh32 milioni kwa mwezi.
Pia alirejea taarifa iliyochapishwa na Mwananchi, Julai 27, 2015, iliyoandikwa kutoka katika mtandao wa African Review kuwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete ni wa nne miongoni mwa marais wa Afrika kwa kupata mshahara mkubwa wa dola za Marekani 192,000 kwa mwaka sawa na dola 16,000 kwa mwezi, ambayo ni sawa na Sh32 milioni kwa mwezi. Hadi jana jioni, dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na Sh2,187.
“Taarifa ya Ikulu ilikanusha vikali habari zilizochapishwa na Mwananchi. Ikulu ilieleza kuwa habari hizo siyo za kweli. Hata hivyo, haikueleza mshahara wa Rais na marupurupu yake ni kiasi gani?
Pia, katika mjadala wa mshahara wa Rais, Naibu Spika wa Bunge lililopita ambaye ndiye Spika wa sasa, Job Ndugai alinukuliwa akieleza kuwa mshahara wa mtu ni siri yake. Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma wa wakati huo, Celina Kombani (kwa sasa ni marehemu) alisema kuwa ni kosa kutangaza mshahara wa Rais.
“…Kwa hivi sasa Rais Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake na kama mapato yake ni Sh32 milioni kwa mwezi, basi ajitolee alau nusu ya mapato hayo kuchangia elimu na afya ya wanyonge. Hatua hii itaimarisha taswira inayojengeka barani Afrika kuwa yeye ni Rais wa wanyonge,” ameandika Lipumba.
Wakati akizungumza na wazee wa Dar es Salaam wiki iliyopita, Rais Magufuli aliwataka mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wachangie Sh1 milioni katika mishahara yao kuchangia elimu.
Pia Rais alieleza kuwa yeye mwenyewe, makamu wake na waziri mkuu watachangia Sh6 milioni kila mmoja, ili zifike Sh100 milioni kusaidia changamoto za elimu bure Mkoa wa Dar es Salaam.
Kutokana na tangazo hilo, Profesa Lipumba alisema, “Ikiwa Sh6 milioni zitakatwa katika mshahara wake wa mwezi mmoja ni wazi mshahara wake na ule wa makamu wake na waziri mkuu ni zaidi ya Sh6 milioni kwa mwezi.
“Mishahara na marupurupu ya viongozi wa Tanzania hayako wazi. Watanzania hawajui kila mwezi Rais, Makamu wa Rais na viongozi wakuu wa Serikali wanalipwa kiasi gani? Malipo ya wabunge pia hayako wazi?” alihoji.
Profesa Lipumba ambaye amewahi kuwa msaidizi wa Rais katika masuala ya uchumi kati ya mwaka 1991 na 1993, alisema kwa kuwa Rais Magufuli amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge, anawajibika kuwaeleza Watanzania mshahara na marupurupu yake.
“Ikiwa mshahara ni mkubwa sana achukue hatua za kuupunguza kama alivyofanya Mwalimu Nyerere mwaka 1965.”
Hata hivyo, alisema kifungu cha Katiba cha 43 (2) kinaeleza kuwa mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais havitapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba.
Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli akitaka kupunguza mshahara wake itabidi kwanza abadilishe kifungu hicho cha Katiba.
“Anaweza kujitolea mchango wa kudumu utakaokatwa kutoka kwenye mshahara wake kusaidia sekta ya afya au elimu,”alisema.
Profesa Lipumba ambaye ni mshauri wa Benki ya Dunia (WB) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika masuala ya uchumi, alisema ili kuimarisha utawala bora ni muhimu uongozi ulio madarakani utumie mamlaka waliopewa kwa manufaa ya Taifa.
“Mishahara na marupurupu ya viongozi yawe wazi na yaamuliwe na kupangwa na taasisi iliyo huru. Kuweka utaratibu ulio wazi wa kuamua mishahara na marupurupu ya viongozi wa umma wakiwamo Rais na makamu wake, mawaziri, wabunge, majaji, makatibu wakuu na viongozi wengine,”alisema.
Alisema ni muhimu katika ujenzi wa utawala bora, uwajibikaji na uwazi wa viongozi wa umma kwa wananchi wanao waongoza.
“ Inasemekana mshahara wa mbunge katika Bunge lililopita ulikuwa Sh3.4 milioni kila mwezi. Pia mbunge alilipwa Sh8.2 milioni, nyingine kama posho ya jimbo, gharama za ofisi, mafuta, malipo ya wasaidizi wake na dereva.
“Vile Vile, mbunge anapohudhuria kikao cha Bunge alilipwa posho ya Sh80,000 za kujikimu, Sh50,000 za mafuta ya gari na Sh200,00 za kuhudhuria kikao cha Bunge, jumla ni Sh330,000 kwa siku.
“Posho ya siku moja ya mbunge ni zaidi ya mara mbili ya kima cha chini cha mshahara wa Serikali kwa mwezi mzima ambacho ni Sh150,000. Mishahara inakatwa kodi, marupurupu hayakatwi kodi,”alisema.

MWANANCHI

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani amekitaka Chama cha Wafanyakazi wa Migodi na Nishati Tanzania (Numet) kufuatilia unyanyasaji unaofanywa na wawekezaji katika sekta hiyo, dhidi ya watumishi wake.
Dk Kalemani alitoa rai hiyo juzi katika mkutano mkuu wa kwanza wa Numet, akisema njia pekee ya kumaliza matatizo ya wafanyakazi ni kufichua unyanyasaji unaofanywa na waajiri wageni.
“Shirikianeni na vyombo vingine vya uchunguzi kufuatilia maovu yanayofanywa migodini na wawekezaji, wajibu wenu ni kuishauri Serikali na kutupatia takwimu sahihi. Tutahakikisha tunazifanyia kazi taarifa mtakazotupatia.
“Undeni bodi itakayokisimamia chama, tasnia hii ina uwezo wa kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na |Taifa. Mkipata matatizo tushirikisheni tutakuwa bega kwa bega kuyapatia ufumbuzi,” alisema Dk Kalemani katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa chama hicho, Albert Machumu alisema walisajili wanachama 3,413 kwa miaka mitatu, lakini kwa sasa wapo 1,857 baada ya wengine kuachishwa kazi kutokana na sababu mbalimbali.
Katika mkutano huo, chama hicho kilitoa tamko la kujiunga na kushirikiana na vyama vingine kuunda muungano wa vyama vya wafanyakazi mbali na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) .


Kikosi cha Kuzuia Ujangili Kanda ya Magharibi kinamsaka fisi mmoja kati ya wawili waliowashambulia Samwel Gamalaya na kusababisha kifo chake na kumjeruhi Kusekwa Ngeleja wakati wakikata kuni katika pori lililopo Kitongoji cha Isukamahela Manispaa ya Tabora.
Fisi hao wawili walimshambulia kwa kumng’ata Gamalaya maeneo mbalimbali ya mwili na kusababisha kifo chake, huku wakimjeruhi Ngeleja mikono na miguu.
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Ujangili Kanda ya Magharibi, Charles Msilanga alisema jana (juzi) kuwa baada ya polisi kumpiga risasi fisi mmoja na kumuua, mwingine alikimbia.
Alisema wanaendelea kumsaka fisi huyo ili kuzuia madhara zaidi kwa wakazi wa kitongoji hicho.
“Fisi aliyekimbia anaweza kuleta madhara kwa watu na ndiyo maana tunamsaka kwa udi na uvumba,” alisema Msilanga.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Iddi Cheyo alisema Gamalaya alifariki dunia baada ya kukaa muda mrefu bila matibabu tangu aliposhambuliwa na fisi hao.
Baadhi ya wakazi wa kitongoji hicho, Sophia William na Juma Kapambala walisema tukio hilo limewastaajabisha kwani kwa miaka mingi wanafanya shughuli zao ndani ya msitu huo bila kushambuliwa na wanyama.
“Tunafanya shughuli zetu katika msitu huu kwa miaka mingi bila kuvamiwa, lakini hatujaona mnyama kuingia eneo hilo,” alisema Sophia.

MWANANCHI
Mkurugenzi mkuu wa shirikisho la riadha la Kenya bwana Isaac Mwangi amepigwa marufuku na shirikisho la riadha duniani IAAF, kwa siku 180.

Bwana Mwangi anatuhumiwa kwa kuwaitisha hongo wanariadha wawili waliopatikana na hatia ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu mwilini ilikupunguza kipindi cha marufuku yao.
Mwangi amekanusha madai dhidi yake.
Mkurugenzi huyo mkuu tayari amejiondoa kwa siku 21 ilikufanikisha uchunguzi dhidi yake.
Kufuatia marufuku hii yakamati ya maadili basi bwana Mwangi hatakuwa na mchango wowote katika mashindano ya olimpiki yatakayofanyika mjini Rio Brazil mwaka huu.
Kupitia kwa taarifa maalum mkuu wa kamati ya maadili bwana Michael Beloff QC amepigwa marufuku kwa kujaribu kuhujumu kampeini dhidi ya madawa ya kuongeza nguvu mwilini.

Marufuku yake inaanza mara moja yaani kuanzia tarehe 22 mwezi Februari 2016.
Mkurugenzi huyo alijipata matatani baada ya wanariadha wawili Joy Sakari na Francisca Koki Manunga kudai kuwa Mwangi alikuwa amewaitisha hongo ya takriban dola elfu hamsini ilikupunguza kipindi cha marufuku.
Joy Sakari na Francisca Koki Manunga walipatikana na hatia ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu mwilini katika mashindano ya riadha duniani yaliyofanyika huko Beijing Uchina.
Source: BBC

 Balozi Pierre Mutemba (katikati) akiimba wimbo wa Taifa.Na Maria Inviolata

Balozi mpya wa Jamhuri ya Kidemokrasi  ya Kongo nchini Tanzania (DRC)  Pierre Mutamba amewataka Wakongomani waishio nchini Tanzania kuwa na umoja na kufanyakazi kwa bidii  ili waweze kujenga nchi yao, amesema hayo wakati  Balozi huyo akianza kazi rasmi, leo katika ofisi za Ubalozi huo zilizopo Upanga jijini Dar es salaam.
Balozi Mutamba amewaambia wanajumuia hao kuwa falsafa yake ni “Ni hapa kazi tu” inayofuata nyayo za Kauli  Mbiu ya Rais John Pombe Magufuri wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Balozi Mutamba alitoa Bendera za Taifa lake kwa kila Kiongozi wa jumuia ya Wakongomani  waishio hapa nchini ikiwa ni ishara ya Uzalendo wa Taifa lao, Balozi huyo alisema kuwa Bendera ni Nembo  ya Nchi, kwa hiyo ni jukumu la kila Mkongomani kuijenga nchi yake.

No comments:

Post a Comment