TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, April 15, 2012

DIAMOND ASHINDA TUZO TATU KWA MPIGO KILIMANJARO MUSIC AWARD 2012

 Mwanamuziki Diamond (kulia)akipokea tuzo yake kutoka kwa George Kavishe meneja wa bia ya Kilimanjaro mara baada ya kutangazwa mshindi wa utunzi bora wa nyimbo katika hafla ya kukabidhi tuzo kwa wanamuziki bora  Kilimanjaro Music Award 2012 zinazofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam na kuhudhuria na waalikwa mbalimbali pamoja na wadau wa muziki kutoka ndani ya Tanzania  na nje ya nchi.

Msanii  Nassib Abdul ‘Diamond’ usiku huu ameng’ara kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Award, baada ya kujinyakulia tuzo tatu.
“Namshukuru Mungu, wakati mwingine uvumilivu na subira ni mzuri. Mwaka jana sikupata tuzo, nikamshukuru Mungu, nikaongeza bidii, nikafanya kazi nzuri, leo ninachukua tuzo ya tatu sasa hivi, alisema Diamond baada ya kushinda tuzo ya Video Bora ya Mwaka, kupitia wimbo Moyo Wangu, ambayo ilikuwa ya tatu usiku huu.
Diamond alizishinda nyimbo za Hakunaga ya Suma Lee, Wangu ya Jay Dee, Ndoa Ndoana ya Kassim na Bongo Fleva ya Dully Sykes.
 Mwanamuziki Diamond akipiga picha na mama yake wa pili kutoka kushoto na Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka kutoka kulia pamona na wanenguaji wake mara baada ya kupokea tuzo yake ya utuzni bora wa nyimbo.
 Mwimbaji wa muziki wa Taarab ambaye ameshinda tuzo ya mburudishaji bora kwa wanawake Malkia Khadija Omar Kopa akitumbuiza katika hafla hiyo usiku huu.
 Malkia Khadija Omar Kopa akishukuru wapenzi wake mara baada ya kushinda tuzo ya mburudishaji bora, wa pili kutoka kushoto ni mume wake na wengine ni watoto wake.
 Watoto wa Malkia wa Mipasho Khadija Omar Kopa wakishuka jukwaani mara baada ya kumtunza mama yao wakati alipokuwa akitumbuiza katika hafla hiyo.
 Kulia ni Msanii Profesa Jay na kushoto ni Mkubwa Fella meneja wa kundi la TMK Family wakimkabidhi tuzo Roma Msanii wa muziki wa Hiphop aliyejishindia tuzo ya msanii bora wa Hiphop.
 Burudani kutoka THT zikiendelea
 Burudani zikiendelea kwa nguzu zote.

MAMBO YANAZIDI KUPAMBA MOTO TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARD 2012 MLIMANI CITY USIKU HUU


 Mwanamuziki Diamond katikati akiwa jukwaani na wenzake kabla ya kuimba wimbo wa msondo katika hafla ya kukabidhi tuzo za wanamuzikii bora za Kilimanjaro Music Award zainazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam kulia ni Khalid Chokoraa wa bendi ya mapacha watatu.
 Msanii HBaba akiwa amezungukwa na vimwana katika hafla hiyo
 Mtayarishaji wa muziki P. Funk kulia akiwa na msanii wa muziki wa Hiphop Jay Moo.
 Wakurugenzi wa ASET kutoka kulia ni Asha Baraka akiwa na kaka yake Baraka pamoja na mdau mwingine katika hafla hiyo.
 Kulia ni Dina Marios wa Clouds akiwa na Asma Makau kutoka Clouds pia.
 Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange Kaburu kulia akibadilishana mawazo na Mulamu Ghambi katika hafla hiyo.
Mohamed Nasor kushoto akiwa na Evance Aveva wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla hiyo usiku huu.

UTOAJI WA TUZO ZA KILIMANJARO MUSIC AWARD 2012 moto MOTO USIKU HUU MLIMANI CITY

Mwanamuziki Ali Kiba akitoa shukuranbi zake kwa mashabiki wa muziki  mara baada ya kutangazwa mshindi katika tuzo za muziki za Kilimanjaro Music Award zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam ambapo ameshinda kwa wimbo wake unaoitwa Dushelele
Mwmnamuzki Ali Kiba akipokea tuzo yake kutoka kwa Mtangazaji wa Clouds Dina Marios mara baada ya kutangazwa mmoja wa washindi katika tuzo hizo, kushoto ni mtangazaji wa ITV na Radio One Rainfredy Masako
Kundi la THT likitumbuiza katika tuzo hozo usiku huu.
Wadau wakiwa katika hafla hoiyo ya kutoa tuzo za muziki kutoka kulia ni Steven Nyerere mchekeshaji, Meneja huduma kwa wateja wa Multchoice Ronald Shelukindo, Frank Mgoyo na wadau wengine.
Mchekeshaji Steve Nyerere akiwa katika picha ya pamoja na Sinta mwigizaji wa zamani.
Kulia ni Taji Liundi na mbunifu wa mavazi Asia Idarous wa Khamsini.
Mdau Kelvin Twisa ndani ya nyumba pia.
Meneja wa kinywaji cha Redds Vicktoria  Kimaro akiwa na wadau wengine katika hafla hiyo.
Kutoka kushoto ni wadau Benny Kisaka, Mabakila, Evance na Juma Pinto.
Kulia ni Oscar Shelukindo na kushoto ni Kabula Nshimo kutoka TBL na wadau wengine wakiwa katika hafla hiyo.
Meneja wa kinywaji cha Kilimanjaro George Kavishe kulia na Mumongae kutoka TBL.
Kutoka kulia ni mdau Henry Mdimu, na kushoto ni Juddy Moshi.
Mdau Nick Butty yupo ndani ya nyumba pia.

No comments:

Post a Comment