TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, October 18, 2014

Mkoa wa Katavi kuzindua kampeni ya kutokomeza magonjwa ya surua rubella

unnamed
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake  hawapo pichani wakati akielezea mkoa kufanyakuzindua kampeni ya chanjo ya magonjwa ya surua na Rubella  kuzinduliwa leo nchini ambapo mikoa 16 inshiriki na katavi ikiwemo,katika mkoa wa Katavi zinafanyika Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo.
………………………………………………………………
Na Kibada Kibada-Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Dkt Rajabu Rutengwe amesema Mkoa wa Katavi  kupitia  mpango  wa Taifa  wa chanjo  na  wadau  mbalimbali  utaendesha  kampeni  shirikishi ya  chanjo  dhidi  ya Surua Rubella, matone ya vitamin A, utoaji wa  dawa za minyoo na kinga dhidi  ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele.
Akizungumza katika mkutano wa Waandishi wa Habari   Dkt Rajabu Rutengwe  ameeleza kuwa katika kampeni  hiyo chanjo ya  surua-rubella itatolewa kwa watoto wote wenye umri kati ya miezi tisa hadi miaka mitano.
Matone ya Vitamini A’yatatolewa kwa watoto wenye umri kati ya miezi sita na miaka mitano, dawa dhidi  ya minyoo itatolewa kwa watoto wenye umri kati ya mwaka mmoja na miaka mitano, kinga tiba dhidi ya matende, mabusha au ngiri maji na usubi kwa wenye umri wa miaka mitano na kuendelea.
Mkuu wa Mkoa alisema Kampeni ya Chanjo ya surua inaendeshwa ikiwa ni muendelezo wa utaratibu wa kufanya kampeni kila baada ya miaka mitatu, utaratibu huu unaotokana na ukweli kwamba baadhi ya watoto hukosa chanjo ya surua  katika utaratibu wa kawaida  ,pia watoto 15 kati ya 100 wanaopewa chanjo ya surua hawajijengei kinga ya mwili ya dhidi ya surua, hali hii husababisha kutokea milipuko ya surua.
Amesema Wizara ya Afya  na ustawi wa Jamii kupitia Mpango wa Chanjo imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa ugonjwa wa surua,kila mtu anayejitokeza na dalili za surua sampuli huchukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara,sampuli huchukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara, Sampuli nyingi zilizochukuliwa zilithibitika kuwa ni ugonjwa wa Rubelle .
Akaongeza kuwa ugonjwa wa Rubella una dalili zinazofanana na surua ingawa husababishwa na vimelea  tofauti, njia za kuthibiti magonjwa haya mawili zinafanana ,kwa kuzingatia haya shirika la Afya ulimwenguni (WHO) liliamua kuunganisha chanjo ya surua na Rubella ili kuongeza ufanisi wa rasilimali na pia ni mkakati wa kidini kutokomeza surua na Rubella kwa pamoja ifikapo mwaka 2020.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Yahaya Husein anaeleza kuwa lengo kuu la kufanya kampeni hii ni kudumisha upungufu wa magonjwa ulemavu na vifo vinavyotokana na surua na Rubella,pamoja na kutoa matone yaVitamini A’na dawa ya kukinga ugonjwa minyoo tumbo,usubi,mabusha na matende,ngirimaji ili kutibu maradhi na kuimarisha afya.
Naye Katibu Tawala mkoa wa Katavi Mhandisi Emmanuel Kalobelo ameleza kuwa katika kampeni hiyo Mkoa wa Katavi umelenga kutoa chanjo ya surua –Rubella kwa watoto wapato 392,174,walengwa wa matone ya vitamin A’watoto 107,609,walengwa,wa kinga tiba dhidi ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni watu 451,683,na walengwa wa dawa dhidi minyoo ni 95,652.
Huduma hizi zitatolewa katika vituo maalum ambavyo vitahusisha vituo vya kutolea huduma za Afya ,Shule za Msingi,Sekondari na maeneo mengine yaliyopangwa.

No comments:

Post a Comment