TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, August 12, 2013

MASHINDANO YA MIJADALA YA SHULE ZA SEKONDARI MWANZA KUANZA SEPT. 2.

Mkurugenzi wa Stopper Entertainment,  Mukhsin Mambo, akifafanua  jambo  kuhusiana na Mashindano ya Shule za Sekondari(Interschools Debate Compatations)
 Mwalimu wa Shule ya Bwiru Boys, George George, akichangia jambo wakati wa Semina ya Walimu wa Shule za Sekondari..
 Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kitangiri ya jijini Mwanza, Luciana Ududa, akichangia jambo wakati wa Mafunzo hayo
 Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Nyabulogoya ya jijini Mwanza, Witness Mbogora, akichangia jambo wakati wa Mafunzo hayo
Baadhi ya Walimu wa Shule za Sekondari waliofanikiwa kuhudhuria Seminja hiyo katika Ukumbi wa Kimataifa wa JB. Bellemonte Hoteli jijini Mwanza leo.
(Picha Zote kwa Hissani ya Miss Demokrasia Tanzania).
===================================================
Mashindano ya Mijadala kwa shule za sekondari mkoani Mwanza (Interschools Debate Competition), yanatarajiwa kuanza septemba 02 mwaka huu.
Akizungumza katika semina elekezi, iliyowakutanisha baadhi ya walimu wa mijadala kutoka katika  shule mbalimbali za sekondari mkoani Mwanza, mkurugenzi wa Stoppers Entertainment ambao ndio waandaji wa shindano hilo, Bwana Mukhsin Mambo, amesema jumla ya shule 32 kutoka mkoani Mwanza, zitashiriki katika shindano hilo ambalo ni la kwanza kufanyika mkoani humo na Tanzania kwa ujumla.
Mambo, amesema shindano hilo pia litaonyeshwa kwenye moja ya runinga hapa nchini kuwapa fursa watazamaji kushuhudia vipaji vya wanafunzi katika kujieleza mbele ya jamii.
Amesema nia na madhumuni ya shjindano hilo, mbali na kuondoka na kitita cha zawadi kwa washindi lakini pia ni njia mojawapo ya kuinua kiwango cha elimu hapa nchini kwa wanafunzi kupata nafasi ya kujieleza mbele za watu, kufanya utafiti kutokana na mada itakayowekwa mezani, kuweka mahusiano mema dhidi ya wanafunzi na kujenga kizazi kipya katika nyanja ya elimu kupitia mfumo wa mijadala.
Miongoni mwa shule zitakazoshiriki shindano hilo ni pamojana Nsumba sekondari, Nganza Sekondari, Butimba sekondari, St. Joseph Girls Sekondari, Buswelu Sekondari, New Hellen Sekondari, Hill crest Sekondari, Bismark Sekondari.

No comments:

Post a Comment