TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 17, 2015

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA WAZEE NA WATOTO, MHE. UMMY MWALIMU AZINDUA BODI MPYA YA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD.


Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Bwana Diwan Msemo (kushoto) akimuonyesha Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) jengo linalojengwa katika Hospitali hiyo ambalo litatumika kuweka mashine zitumikazo kufanyia mionzi kwa jili ya wagonjwa wa saratani hospitalini hapo. 

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyopo jijini Dar es Salaam, Bwana Diwan Msemo (kulia) akimueleza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) baadhi ya majukumu wayafanyayo katika Hospitali hiyo alipowasili kufanya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini hapo, ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika hiyo mapema 17 Desemba, 2015. 
Mama wa mgonjwa (kulia) akimueleza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) juu ya changamoto za gharama za kupata matibabu wazipatazo wakati Waziri huyo alipofanya ziara katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyolenga kufanya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini hapo, ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika hiyo mapema 17 Desemba, 2015. 
Muuguzi wa wagonjwa (kushoto) akimueleza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) juu ya changamoto za dripu wazipatazo wakati Waziri huyo alipofanya ziara katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyolenga kufanya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini hapo, ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika hiyo mapema 17 Desemba, 2015. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akimjulia hali mama mgonjwa wakati alipowasili katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyopo Dar es Salaam kufanya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini hapo, ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika hiyo mapema 17 Desemba, 2015. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akitoa hotuba fupi wakati aliwaposili katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road iliyopo Dar es Salaam kufanya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini hapo, ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika hiyo mapema 17 Desemba, 2015. 


Baadhi ya Wajumbe waliohudhuria katika Mkutano wa Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Hospitalini Saratani ya Ocean Road iliyopo jijini Dar es Salaam uliofanyika 17 Desemba, 2015 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (hayupo pichani). 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road jijini Dar es Salaam 17 Desemba, 2015. (Picha zote na Benedict Liwenga)


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) akipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Bwana Diwan Msemo (kushoto) mara alipowasili katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road ya Jijini Dar es Salaam kwenye Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road uliofanyika leo 17 Desemba, 2015.
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Bwana Diwan Msemo (aliyevaa suti) akimpeleka Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) katika chumba ambacho ukarabati wa mashine za matibabu zilizopata hitilafu ukiendelea katika Hospitali hiyo mara alipowasili hospitalini hapo mapema 17 Desemba, 2015. 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili kulia) akipatiwa maelezo toka kwa Mganga wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road juu ya matatizo ya kiufundi ilizozikumba mashine za matibabu hospitalini hapo wakati wa ziara yake ya Uzinduzi wa Bodi ya Taasisi ya Saratani ya ya hospitalini hapo uliofanyika leo 17 Desemba, 2015. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Bwana Diwan Msemo 
Baadhi ya Mafundi wakionekana kutengeneza mashine iliyopata matatizo wakati wa ziara ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu hospitalini hapo iliyolenga kufanya Uzinduzi ikiwemo kuangalia vitendea kazi na kero wazipatazo wagonjwa wenye matatizo ya saratani katika Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. 
Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Saratani ya Ocean Road, Bwana Diwan Msemo (kulia) akimpeleka Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (katikati) kuangalia jengo ambalo litatumika kwa ajili ya mashine maalum za kufanyia huduma za mionzi kwa wagonjwa wa saratani katika Hospitali hiyo. 


Na Shamimu Nyaki.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee Na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo amezindua Bodi Mpya ya Wadhamini ya Taasisi ya Saratani katika Hospitali ya Ocean Road Ambayo itasimamia programu za elimu ya afya kuhusu Saratani.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe. Ummy Mwalimu mbali na kutoa pongezi za uundwaji wa Bodi hiyo amewataka watendaji kuhakikisha wagonjwa wa Saratani wanapata huduma bora, ushauri wa namna ya kuzuia magonjwa ya Saratani, kufanya utafiti wa magonjwa ya Saratani kwa kushirikiana na wadau wengine wa ndani na Nje kwa kuwa Taasisi hiyo imeanzishwa ili kuwasaidia wagonjwa hao.

“Tumieni uzoefu wenu,vipaji vyenu, na taaluma zenu katika kutoa huduma kwa kuwa Taasisi hii inategemewa na watu wote”Alisema Mhe.Waziri.

Aidha Waziri huyo amewahakikishia watandaji wa Bodi hiyo kwamba atashirikiana nao kwa karibu zaidi katika kufanikisha ugojwa wa Saratani unatokomea au kupungua kwa vile Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) inaonyesha kuwa Tanzania ina jumla ya wagonjwa 33,884 lakini wanaopata huduma ni Wagojwa 3000 ambao ni sawa na asilimia 16 tu.

Mhe Ummy amesema atahakikisha Taasisi hiyo inatengewa fedha za kutosha ili iweze kutoa huduma na kupunguza tatizo la ugonjwa wa Saratani hapa nchini kwa kufanya tafiti muhimu Ktika maeneo tofauti na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ugojwa huo kwa vile wananchi wengi wanagundua ugonjwa huo ukiwa tayari umeshakuwa na athari kubwa.

No comments:

Post a Comment