TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, March 10, 2012

NYUMBA YA YA SPIKA WA BUNGE YAKABIDHIWA RASMI OFISI YA BUNGE

Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Bw. John Joel (kushoto) akijadili jambo na Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Teknologia ya Mawasiliano Bw. Didas Wambura mara tu kabla ya makabidhiano rasmi ya jengo la nymba atakayokuwa anatumia Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoko eneo la Uzunguni nje kidogo ya mji wa Dodoma leo.
Muonekano wa nyumba hiyo kwa mbele. Jengo hili ambalo litakuwa makazi ya Spika yeyote atakayeliongoza Bunge la Tanzania lilianza kujengwa Disemba 2009 na limegharimu takriban sh. 1.5 bilioni. Hapakuwahi kuwa na nyumba rasmi ya Spika wa Bunge Dodoma
Mshauri Mwelekezi (consultant) wa Pacha Building Construction Company ( ambayo ndiyo imejenga jengo hilo) Bw. Shaban Mwatawala (kulia) akitoa maelezo ya ujumla kabla ya kuwapitisha viongozi wa Ofisi ya Bunge katika jengo hili. Kulia kwake ni Mhandisi wa Miradi wa Pacha Bw. Johanes Maganga, Mkurugenzi wa Mipango na Teknolojia ya Mawasiliano wa Bunge Bw. Siegfied Kuwite, na Mkurugenzi wa Sgighuli za Bunge Bw. John Joel.
Bw. Siegfried Kuwite akitia saini makabidhiano hayo kwa niaba ya Katibu wa Bunge ambaye ndiye Mshitiri (client) wa jengo.
Bwana Mwatawala akimkabidhi Msanifu Majengo M. F. M Msangi (kulia) anyewakilisha Wakala wa Majengo ya Serikali. Wakala wa Majengo Tanzania ndiye Meneja wa Mradi huu.
Timu nzima iliyoshiriki katika makabidhiano hayo.
Picha zote na Prosper Minja-Bunge

No comments:

Post a Comment