TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, May 5, 2012

WATANZANIA WAFANYA MATEMBEZI YA AMANI KATIKA JIJI LA YOKOHAMA NCHINI JAPAN

  Maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini Japani, Jilly Maleko na Francis Mossongo wakijiandaa tayari kwa matembezi ya hisani yenye lengo la kuhamasisha juhudi za kufufua uchumi na utalii wa jiji la Yokohama.
      Maandalizi yakiendelea
Watanzania wanaoishi nchini Japani wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wengine kutoka mataifa ya Afrika katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa matembelezi hayo.
Watanzani wakipeperusha bendera ya Tanzania katika Matembezi ya hisani yaliyoandaliwa na jiji la Yokohama
Matembezi yamekolea, Mwenyekiti wa watanzania wanaoishi nchini Japani Radhid Njenga (mwenye kanzu) naye alikuwemo.
Noboru Ninomiya (mwenye picha ya tingatinga) mwenyeji wetu katika matembezi haya akiwa sambamba na Francis Mossongo, Afisa Ubalozi.
Maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini Japani, wamewaongoza watanzania wanaoishi hapa kushiriki katika matembezi ya hisani ya mji wa Yokohama, ikiwa ni moja ya hatua za kukuza urafiki kati ya jijini hilo na Tanzania.
 
Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania na hata mataifa ya Afrika kushiriki rasmi kwenye matembezi hayo ambayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka. Mwaka huu, Tanzania kutokana na historia yake ya kupenda, kusimamia na kutetea amani, umoja na mshikamano duniani.
Aidha katika siku za usoni, mji wa Yokohama una mpango wa kuanzisha uhusiano (Sistercity Friendship) na moja ya miji ya Tanzania, uhusiano ambao utajumuisha kupanda miti aina ya Cherry blossom katika mji utakaochaguliwa Tanzania.
Matembezi hayo yalianzishwa mwaka 1953 kwa lengo la kuhamasisha jitihada za kufufua uchumi na utalii wa mji wa Yokohama kufuatia uharibifu uliotokana na Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

No comments:

Post a Comment