TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, June 22, 2012

Katiba mpya iwe na dira ya maendeleo

Posted: 20 Jun 2012 11:02 PM PDT
Na Halfan Diyu

KATIBA muongozo ambao taifa lolote limejiwekea jinsi ya kuendesha shughuli za kila siku za taifa lao.
Taifa linakuwa imara linapokuwa na katiba imara na viongozi bora, wenye maono ya kuwaletea maendeleo wananchi wao.
Taifa lazima lisimamie misingi ya haki na ianishwe katika katiba kwani ni haki pekee huleta watu pamoja na kiondoa misingi yote ya unyonyaji.
Pia, ndio sheria mama nchini na katiba zote zinazotengenezwa na taasisi au vyama vya siasa zinapaswa kuakisi yale yote
yaliyopo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na si kupingana, kinyume na hapo itakuwa batili.
Maendeleo ya nchi nyingi zilizoendelea yamechangiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuwa na katiba imara na inayokidhi mahitaji ya sekta mbalimbali kama za elimu, afya, utamaduni, uchumi, siasa, uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa wananchi kuzungumza au kutoa maoni yake.
Hakuna ubishi kuwa nchi ya Marekani ni moja ya mataifa ambayo yamekuwa na katiba imara inayogusa sekta zote nilizotaja hapo juu na ambayo imedumu kwa muda mrefu bila
kufanyiwa marekebisho ya mara kwa mara.
Matokeo yake tunashuhudia Taifa hilo likisimama kwa muda mrefu kwa kuwa na uchumi imara duniani.
Nchini baada ya kuundwa kwa katiba mwaka 1977, tayari yameshafanyika marekebisho kumi na nne hadi mwaka 2005, ambapo ya kwanza yalifanyika mwaka 1979.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba nchini, Bw.Deus Kibamba anasema marekebisho ya kwanza ya mwaka 1979 yaliingiza moja ya mambo muhimu katika taifa letu, ambapo ni
kuanzishwa kwa Mahakama ya Rufaa.
Mwaka 1980 yalifanyika tena marekebisho katika Katiba na moja ya marekebisho hayo ni kuingizwa kwa katiba ya Zanzibar katika Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Mwaka 1982 yalifanyika marekebisho ya mfumo mpya wa kuchagua wakuu wa mikoa, mwaka 1984 marekebisho bora ambayo yalizingatia maoni ya wananchi ambapo suala la haki za binadamu liliingizwa katika katiba.
Hayo ni baadhi ya marekebisho machache tu ambayo yalifanyika katika hiyo miaka niliyoitaja hapo juu na kufikia hadi mwaka 2005 jumla ya mabadiliko kumi na nne yalifanyika na mengi yaligusa masuala ya siasa na muungano, achilia machache kama ya haki za binadamu ambayo yanagusa jamii yote bila kubagua.
Vilevile ubora na uimara wa katiba mpya ijayo uende sambamba na kudumu kwa miongo mingi na si kufanya marekebisho ya mara kwa mara ambayo yanagharimu fedha nyingi za walipa kodi.
Katika kipindi hiki Taifa lipo katika vuguvugu la kuanza mchakato wa kukusanya maoni ya katiba mpya, ambapo ifikapo tarehe 26 mwezi Aprili mwaka 2014 Katiba hiyo inatakiwa
iwe imekamilika.
Wananchi waelimishwe umuhimu wa kuchangia maoni ya masuala mbalimbali yanayogusa maisha yao ya kila siku na si kuwa na mawazo mgando ya kuchangia katika masuala ya
muungano na siasa tu, ingawa pia yana umuhimu katika mustakabali wa Taifa.
Nionavyo jamii inatakiwa kupata uelewa na nafasi ya kuchangia maoni yao ili kupatikana kwa katiba bora, imara itakayogusa sekta zote kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.
Posted: 20 Jun 2012 11:00 PM PDT

Posted: 20 Jun 2012 10:59 PM PDT

Na Mwandishi Wetu

BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa 'Wana Kibega', inatarajia kufanya ziara maalumu kwa mashabiki wake wa Kanda Ziwa mwishoni mwa wiki.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja wa bendi hiyo, Martin Sospeter alisema onesho la kwanza litafanyika Ijumaa mjini Kahama, mkoani Shinyanga.
Alisema Jumamosi watatoa burudani mjini Geita na Jumapili watakuwa jijini Mwanza.
Meneja huyo alisema wameandaa shoo ya nguvu kwa wapenzi wa mikoa hiyo ikiongozwa na Lilian Internert, akiwa na wengine ambao wataonesha shoo zao mpya zilizoundwa hivi karibuni.
Sospeter alisema katika maonesho hayo nyimbo zao zote zitapigwa, ikiwa pamoja na zilizokuwa hazijawahi kusikika kwenye vyombo vya habari.
"Kuna nyimbo mpya ambazo zitaanza kusikika huko huko, tunafanya kama kuwatambulisha wapenzi wa Kanda ya Ziwa waone mambo mapya ya Mashujaa," alisema Sospeter.
Alisema bendi hiyo itarejea Dar es Salaam Jumatatu na kuendelea na ratiba yake ya kila wiki, huku ikiandaa ziara yake ya mikoa ya Kusini ambayo itafanyika mwezi ujao.
Posted: 20 Jun 2012 10:56 PM PDT

Na Heri Shaaban, Pwani

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenela Mukangara amesema Mashindano ya Shule za Sekondari (UMISSETA) ya mwaka huu yatatumika kuunda timu ya pili ya Taifa ya wanawake (Twiga Stars).
Akizungumza katika ufunguzi wa mashindano hayo yaliyofanyika juzi mjini Kibaha, Waziri Fenela alisema haina budi kuunda timu B ya wanawake kwa kutumia wachezaji watakaopatikana katika michuano hiyo.
"Ombi langu la mapendekezo haya, najua litatekelezwa mara moja ili tuwe na timu mbili za wanawake za soka ili zije kuwa tishio siku za baadaye.
"Nimeshudia mechi ya mpira miguu ya wanawake kwa timu za Kanda Nyanda za Juu Kusini, iliyofungwa mabao 10-1 dhidi ya Kanda Mashariki ambazo zimeonesha mpira mzuri," alisema.
Alisema mashindano hayo ni chachu ya kuibua vipaji vya wanamichezo mbalimbali, ndiyo maana mwaka huu michezo hiyo imewashirikisha wadau mbalimbali katika sekta hiyo, ili waweze kuangalia vijana wenye vipaji.
Waziri huyo alisema michezo ni ajira inatakiwa kutambua mchango wake, hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISSEMI kwa ushirikiano na Wizara ya Mafunzo ya Ufundi zinatakiwa kufanikisha mashindano hayo ambayo ndiyo chachu ya kupata wachezaji wa timu ya Taifa wa baadaye.
Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Jumanne Sagin amezuia walimu wakuu kuuza maeneo ya viwanja vya shule badala yake vibaki kwa ajili ya michezo.
Posted: 20 Jun 2012 10:37 PM PDT

Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ufaransa (AF), Sullivan Benetier (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam juzi, kuhusu kituo hicho kuandaa Maadhimisho ya Siku ya Muziki Duniani inayofanyika leo, kwa kushirikisha bendi na vikundi mbalimbali vya muziki. Kulia ni Kiongozi wa Bendi ya FM Academia Nyoshi Saadat. (Picha na Charles Lucas) 
Posted: 20 Jun 2012 10:36 PM PDT

Na Mhaiki Andrew, Songea

WACHEZAJI 20 na viongozi watatu wa timu ya soka ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya mkoa wa Ruvuma, imeondoka jana mjini hapa kwenda jijini Dar es Salaam kushiriki mashindano ya Taifa ya Copa Coca-Cola 2012.
Akizungumza mjini hapa juzi usiku katika halfa ya kuwaaga vijana hao, Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa (FARU) Joseph Mapunda,  alisema kazi iliyokuwa mbele yao ni kuhakikisha wanatwaa ubingwa wa kombe hilo mwaka huu.
Wachezaji waliondoka pamoja na viongozi wao kuwa ni Joseph Hilly, Adeligoti Kipipa, Amosi Bandawe, Ramadhan Ramadhan, Peter Malekoni, Maneno Zuberi na Severin Mkandawile (Mbinga), Panjo Mshindo, Anthon Heneko, Omari Ally na Shaban Chitete (Tunduru).
Wengine ni Edward Songo, Mapunda Sandali, Ebroni Haule, Sunday Kalonga, William John, Juma Said, Ally Abdallah.
Aliwataja wachezaji wengine kuwa ni Shanely Michael na Hamis Yasin kutoka Manispaa ya Songea na Kocha Mkuu wa timu hiyo Francis Samatta, msaidizi wake Francis Kasembe na mkuu wa msafara, Emmanuel Kamba.
Mapunda alisema wilaya zingine tatu za Namtumbo, Nyasa na Songea Vijijini katika  wachezaji wake hawakuweza kuteuliwa baada ya  kushindwa kushiriki mashindano hayo.
Posted: 20 Jun 2012 10:35 PM PDT

Na Mwandishi Wetu

SIGARA ya Embassy kupitia chapa yake ya Club E, inakuja na pati ya Hollywood Glam Night. Pati hiyo itafanyika kesho jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Blue Pearl ulioko Ubungo Plaza kuanzia saa 2 usiku.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Dar es Salaam juzi na Tumaini Toroka ambaye ni Meneja wa Embassy ilieleza kwamba pati hiyo ambayo itakuwa na maudhui ya Hollywood, ambapo wanachama na wapenzi wa burudani watapata watashuhudia burudani mbalimbali na vivutio vya Hollywood.
Alisema wanachama wa Club E, wataingia bure kwenye pati hiyo kwa kupitia mwaliko maalumu na kwa watu wengine ambao si wanachama na wangependa kuhudhuria, watalipa sh. 30,000. Kiingilio hicho kitajumuisha vinywaji pamoja na chakula.
Alisema kwa miaka mitano iliyopita, Club E imejijengea jina kwa kufanya pati zenye ubora na hadhi ya hali ya juu kwa wanachama wake.
"Ukiacha suala la kuburudisha wanachama wake, kwa kipindi cha miaka mitano, Club E pia imeweza kutoa mchango wake kwa kuinua wanamuziki wetu wa ndani ambao wamepata muda wa kuimba kwenye jukwaa moja na wasanii mbalimbali wa bara la Afrika na Marekani.
Alisema Club E ilianzishwa mwaka 2007 kwa lengo la kuwaleta pamoja na kuwaburudisha wanachama wake, ambao ni wavutaji wa sigara ya Embassy.
"Tangu kuanzishwa kwake Club E imefanya pati nyingi na kuwaleta wasanii wengi wa ndani na nje ya nchi kutumbuiza. Wasanii walioletwa na Club E ni pamoja na Werrason, Miriam Makeba, Amani, Blue 3, Lady Jay Dee, Mbilia Bell, Tshalla Muana, JB Mpiana, FM Academia, Chaka Khan na Falii Ipupa," alisema.
Posted: 20 Jun 2012 10:34 PM PDT
Baadhi ya mashabiki wa soka wa klabu za Ligi Kuu ya England, waliojitokeza kwenye kushiriki mashindano ya kumsaka 'Shabiki Bomba' kwenye Castle Lager Superfans yaliyofanyika Kimara jijini Dar es Salaa jana (kulia) ni Msumi Maneno akifanyiwa usaili kwa ajili ya kinyang'anyiro hicho. Mshindi wa mashindano hayo atakwenda Afrika ya kusini kushuhudia Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani. (Na Mpigapicha Wetu)
Posted: 20 Jun 2012 10:31 PM PDT

Na Mhaiki Andrew, Songea

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu anatarajia kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa filamu ya Adelahida, ambayo imechezwa na waigizaji wazawa wa mkoa huo. Uzinduzi huo utafanyika katika Ukumbi wa Songea Klabu, Julai Mosi mwaka huu.

Akizungumza mjini hapa jana Mratibu wa filamu hiyo, Shukrani Faraja alisema filamu hiyo ni muhimu kwa vizazi vya sasa katika kuelewa historia ya zamani ya mababu.

Alisema filamu hiyo itakapoingiwa sokoni itasaidia kuelewa mila, desturi na tamaduni za mababu wa mkoa huo ambazo walikuwa wakiziendekeza ikiwemo kuuwa watoto watakaobainika wamezaliwa mapacha zaidi ya wawili kwa imani za kutokea mikosi katika ukoo wao.

Faraja alisema pamoja na filamu hiyo waigizaji wake wameelezea mambo mengi, huku wakiowanisha na kipindi chote ambacho Tanzania inajitawala.

Mratibu huyo alisema uzinduzi huo utakwenda sambamba na maigizo mbalimbali ikiwemo na wasanii wa kizazi kipya, ngoma za asili za makabila ya Mkoa wa Ruvuma na wazee wa kimila ikiwa ni tambiko lao kabla ya filamu hiyo kuingia sokoni.
Posted: 20 Jun 2012 10:29 PM PDT
Na Zahoro Mlanzi

WACHEZAJI wapya wa Yanga, Said Banahuzi na Juma Abdul 'Baba Ubaya', wameanza mazoezi na timu hiyo yanayoendelea katika Uwanja wa Kaunda, Dar es Salaam na kufanya timu hiyo kuzidi kuimarika.
Wachezaji hao wamesajiliwa msimu huu wakitokea Mtibwa Sugar ambapo wameungana na nyota mwingine, Nizar Khalfan katika kuhakikisha wanaimarisha timu hiyo inayojiandaa na michuano ya Kombe la Kagame na Ligi Kuu Bara.
Gazeti hili lilishuhudia wachezaji hao wakifanya mazoezi ya pamoja na wenzao ambao walianza tangu Jumatatu wakiwa chini ya Kocha Msaidizi, Fredy Felix 'Minziro' huku mashabiki wakionekana kuvutiwa nao.
Pamoja na kufanya mazoezi hayo, lakini kivutio kikubwa kilikuwa kwa Baba Ubaya ambaye hucheza beki wa kushoto, alikuwa akionesha umahiri wake katika kuuchezea mpira na kupiga pasi zenye uhakika.
Beki huyo ambaye ni tunda na Kituo cha Michezo cha Tanzania (TSA), baada ya kuonesha uwezo mkubwa akiwa kituoni hapo ndipo aliposajiliwa na Mtibwa akiichezea timu ya vijana (U-20) lakini msimu uliopita alipandishwa na kuchezea timu ya wakubwa.
Baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo, Minziro alisema anapata matumaini mapya baada ya kuona kila kukicha wachezaji waliosajiliwa na timu yake wanakuja, hivyo ataanza programu ya mazoezi siku si nyingi.
Alisema wachezaji waliokuwa katika timu ya Taifa (Taifa Stars) bado hawajaanza mazoezi, lakini ana imani baada ya siku chache za kupumzika watajiunga na wenzao kufanya mazoezi.
Timu hiyo ndiyo mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, ambalo walilitwaa mwaka jana chini ya aliyekuwa Kocha Mkuu, Sam Timbe lakini baadaye alifukuzwa na mikoba yake kuchukuliwa na Kostadin Papic.

No comments:

Post a Comment