TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, June 22, 2012

QML yaingia ubia na BEML Ltd ya India

Posted: 19 Jun 2012 11:16 PM PDT

Na Godfrey Ismaely

KAMPUNI ya Quality Motors Limited (QML) ambayo ni miongoni mwa kampuni zinazomilikiwa na Kampuni ya Quality Group nchini imeingia makubaliano ya usambazaji wa bidhaa mbalimbali na Kampuni ya BEML Limited kutoka nchini India.
Makubaliano hayo ambayo yalienda sambamba na kutiliana sahihi za mikataba jana nchini, yanahusisha usambazaji wa bidhaa za kampuni hiyo Afrika Mashariki, Sudani Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Malawi na Msumbiji.
Akisaini mkataba huo Meneja Mkuu wa Biashara za Kimataifa wa BEML Bw. Narayana Bhat alisema anayofuraha kubwa kushirikiana na kampuni kubwa kama Quality Group na kuahidi ushirikiano mzuri katika maendeleo ya nchi za Afrika kwa kusambaza bidhaa zenye viwango bora katika ujenzi na uchimbaji wa madini.
Alisema, Afrika Mashariki ina rasilimali kubwa ya madini hivyo ushirikiano huo wa kampuni hizo mbili utafaidisha kwa kiwango kikubwa Afrika.
"BEML imefungua hivi karibuni tawi lingine mjini Johannesburg, nchini Afrika  Kusini ili kuhudumia kwa ukaribu zaidi soko la Afrika Mashariki kwa ukaribu zaidi na kwa wakati mwafaka," alisema Bw. Bhat. 
                                 Kwa upande wake Mkurugenzi wa Quality Group Bw. Sridhar Thiruvengadam alisema kampuni yake imechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Tanzania katika maeneo mbalimbali kwa kuungana na kampuni kubwa duniani inayoshughulika na usambazaji wa bidhaa za uchimbaji madini, ujenzi, reli na ulinzi.
Hata hivyo Kampuni ya BEML ni miongoni mwa kampuni kubwa zaidi duniani inayomilikiwa na Serikali ya India ambayo ina uzoefu wa muda mrefu hususan utengenezaji na usambazaji wa vifaa vya ujenzi zikiwemo reli, uchimbaji wa migodi pamoja na ulinzi.
Pia kwa mujibu wa BEML kwa sasa baada ya kufungua tawi lake nchini AfrikaKusini, tayari shehena ya kwanza ya bidhaa mbalimbali ipo njiani na inategemewa kuwasili Dar es Salaam hivi karibuni
Posted: 19 Jun 2012 11:15 PM PDT

Na Mwandishi wetu

KAMPUNI  ya Mawasilino ya  Vodacom Tanzania, imezindua vifurushi vipya vya intaneti ambavyo vitawawezesha wateja wake kupata huduma ya intaneti kwa shilingi 250 kwa siku.
Huduma hiyo ya 'Wajanja Intanet' imeboreshwa zaidi ili kuwawezesha wateja kuelewa huduma za intaneti na kuchagua kikamilifu huduma zitakazowafaa hivyo kuweza kuperuzi na kupata taarifa kwa kasi na kwa bei nafuu kupitia mtandao wa Vodacom.
Hata hivyo, Vodacom ilisisitiza kuwa huduma ya kuperuzi facebook na twitter zitaendelea kuwa bure kwa wateja wote.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Bw. Rene Meza alisema kuwa  kampuni hiyo imerahisisha huduma hiyo kwa wateja wake ili kuwawezesha kuelewa kiasi ambacho wanatumia katika huduma za intaneti, suala ambalo limekuwa kikwazo kikubwa kwa watumiaji wa intaneti kote nchini.
Alibainisha kuwa Kampuni hiyo imeona umuhimu wa watoa huduma za mawasiliano kama Vodacom kuondoa utata ambao unawazuia wateja kutumia mfumo mpya  wa teknolojia ya intaneti katika mawasiliano.
“Tumeiweka huduma yetu katika njia ambayo ni rahisi kwa wateja wetu kuelewa kwani tunaamini kuwa hii ni njia rahisi ya kuongeza matumizi ya intaneti katika kueboresha maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Wateja wote wa malipo ya baada au ya kabla watapata huduma ya interneti kwa kasi kupitia simu zao za mkononi na modem.
Aliendelea kusema kuwa kutokana na huduma hiyo mpya, sasa Wateja wa Vodacom watapata huduma isiyo na kikomo na yenye kasi kwa siku saba mfululizo kwa Sh. 10,000 au Sh. 30,000 kwa siku thelathini
Posted: 19 Jun 2012 11:14 PM PDT

Posted: 19 Jun 2012 11:11 PM PDT

Heri Shaaban na Radhia Adam

SHIRIKISHO la Michezo la Mashirika ya Umma na Kampuni Binafsi Tanzanuia (SHIMMUTA), limeandaa Mkutano wa Halmashauri kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya maendeleo ya Shirikisho hilo kwa kipindi cha mwaka 2012 na 2013.
Kwa mujibu wa taarifa iliyomwa kwa vyombo vya habari juzi na Katibu Mkuu wa SHIMMUTA, Award Safari ilieleza kuwa mkutano huo utahusisha wajumbe kutoka kila taasisi mwanachama.
Safari alisema mkutano huo unatarajia kutafanyika Julai 12 mwaka huu.
"Agenda ya mkutano huo zitakuwa kupokea na kujadili taarifa za maendeleo za shirikisho kwa kipindi cha mwaka 2011/2012 ikihusisha taarifa za michezo iliyopita ya mwaka jana iliyofanyika jijini Tanga, pamoja na kujadili taarifa ya fedha ya mapato na matumizi.
Alisema katika mkutano huo wajumbe watapitia na kujadili bajeti ya mapato na matumizi ya mwaka 2012/2013, ikiwa pamoja na kupitisha mkoa ambao Kamati ya Utendaji ya SHIMMUTA imeuchagua kwa ajili ya kufanyia michezo ya mwaka huu.
Pia alisema shirikisho hilo linakaribisha wajumbe wawili kutoka katika taasisi, mashirika na kampuni ambayo hayakupelekewa barua za mwaliko, lakini yanataka kujiunga na kuhudhuria mkutano huo.
Aliwaomba wajumbe watakaoudhuria mkutano huo ambao utafanyika kwenye jengo la Benjamini Mkapa kuwa kila mjumbe atakayeshiriki gharama zote zitakuwa juu yake.
Posted: 19 Jun 2012 11:11 PM PDT


Na Mwandishi Wetu

MWNJILISTI Kabula George, anatarajia kugawa DVD za albamu ya Nitang’ara Tu kwa kila mtu atakayeingia kwenye Ukumbi wa kanisa la TAG Magomeni Mikumi Julai 8, mwaka huu wakati wa uzinduzi wake.
Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Mwinjilisti Kabula alisema ameamu kuweka utaratibu huo, ili kila mtu atakayeingia ukumbini humo aondoke na DVD kwa kuchangia kiasi cha sh. 5,000.
Mwinjilisti Kabula alisema tayari DVD hizo tayari zinapatikana katika maduka mbalimbali yaliyoteuliwa jijini Dar es Salaam.
DVD hizo pia zinapatikana katika mikoa mbalimbali ukiwemo Mwanza, Arusha, Dodoma na Kahama mji
Amewataka mashabiki wake kununua DVD halisi ili wanufaike na ubora wa nyimbo hizo, ambazo zinamafundisho kwa kila anayeziangalia.
Posted: 19 Jun 2012 11:09 PM PDT

Meneja wa bia ya Castle Lager, Kabula Nshimbo (kulia) akicheza mfano wa mpira wa miguu kwenye uzinduzi wa kampeni ya kumtafuta Shabiki Bora wa Castle kwenye kampeni ya Castle Super Fan, ambapo mshindi atapata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika timu ya Afrika ya Ushangiliaji (Africa United Super Fan) Afrika ya Kusini. Na Mpigapicha Wetu
Posted: 19 Jun 2012 11:07 PM PDT


Na Heri Shaaban

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imesema kuwa suala la dawa bandia ni tatizo la Dunia nzima hivyo amewataka wananchi kushirikiana na serikali kiziba mianya ya uingizaji dawa bandia ili kulinda maisha ya Watanzania kwa ujumla.
Hayo yalisemwa Dar es Salaam hivi karibuni na Mkurugenzi wa TFDA Bw.Hiti Silo
Bw.Silo alisema kuwa kutokana na tatizo hilo kuwa la kidunia hivyo akuna budi kwa wadau,taasisi wananchi kushirikiana na mamlaka hiyo pamoja na serikali kudhibiti njia za uingizaji wa bidhaa bandia.
"Kutokana na changamoto hizi TFDA imeweza kuunda vikosi kazi kwa ajili ya kusimamia udhibiti wa dawa bandia kila pembe ya nchi kwa kushirikiana na jeshi la polisi kulinda mifumo ya njia hizo," alisema Bw.Silo.
Aliwaomba wananchi wanapopata taarifa za uingizaji wa dawa bandia, kutoa taarifa ngazi zinazohusika ili wahusika waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Alisema kuwa mamlaka hiyo pia imeweza kuimarisha mipaka yote katika vituo vya forodha zinapoingia bidhaa kwa ajili ya ukaguzi kabla mzigo kurusiwa kuingia nchini.
Kwa upande wake Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt.Hussein Mwinyi alikabidhi cheti kwa  Mamlaka ya chakula na Dawa  Tanzania TFDA na taasisi zingine zilizoshiriki madhimisho hayo ya siku ya famasia na kuwataka kutoa elimu ya kutosha  kwa wananchi ili wajuwe matumizi ya dawa bandia.
Posted: 19 Jun 2012 11:05 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

WAKATI mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Klabu ya Yanga ukiendelea, wanachama walioweka pingamizi kwa baadhi ya wagombea wanaowania uongozi wa klabu hiyo akiwemo aliyekuwa Mfadhili wa klabu hiyo, Yusuph Manji wametakiwa kuwasilisha vielelezo vya pingamizi walizoweka kwa Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo.
Shughuli hiyo ya kupokea vielelezo itaanza saa nne asubuhi makao makuu ya klabu hiyo mitaa ya Twiga na Jangwani na watatakiwa kutetea hoja zao.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa kamati hiyo Jaji Mstaafu, John Mkwawa alisema juzi saa 10 jioni ilikuwa ni siku ya mwisho ya kupokea pingamizi mbalimbali za wagombea uongozi wa klabu hiyo.
"Tunashukuru zoezi limekwenda vizuri na wapo wagombea waliowekewa pingamizi mgombea Yusuph Manji, ambaye anawania nafasi ya uenyekiti amewekewa pingamizi na wanachama watatu wenye kadi namba 007933, 008272 na 006225," alisema Mkwawa na kuongeza;
"Sara Ramadhani ambaye pia anawania uenyekiti naye amewekewa pingamizi na mwanachama mwenye kadi namba 003353 na 001702, lakini kwa pingamizi lililoletwa dhidi yake inaonesha walioweka wanataka ufafanuzi kama kiongozi aliyejiuzulu anaweza kugombea, hivyo hilo linahitaji ufafanuzi tu''.
Alisema mgombea Yono Kavela, ambaye anawania Makamu Mwenyekiti naye amewekewa pingamizi na mwanachama mwenye kadi namba 003974 na Ali Mayai ambaye anawania Ujumbe wa Kamati ya Utendaji.
Alisema baada ya kupokea pingamizi hizo, kamati imepanga siku ya leo kupokea ushahidi ambao unaweza kuwa wa binafsi au kwa maandishi (document) na si lazima aliyeweka pingamizi kuwepo siku hiyo.
Mkwawa alisema usaili utafanyika Juni 22, mwaka huu tofauti na ilivyopangwa awali kutokana na kutoa nafasi kwa kupitia vielelezo vya ushahidi vitakavyotolewa.
Alitoa hadhari kwa watu wanaoanza kufanya kampeni kabla ya siku hazijafika pamoja na wale wanaoingilia kamati hiyo katika shughuli zake.
Mbali na hilo, Mkwawa alizungumzia pingamizi la mwanachama Abeid Abeid 'Falcon', kwamba wamelitupia mbali kutokana na kujichanganya katika maelezo aliyoyawasilisha kwa kamati hiyo.
Posted: 19 Jun 2012 11:04 PM PDT
Msanii wa kundi la Wanaume Halisi, Juma nature akifanya vitu vyake wakati wa tamasha maalumu la kuitambulisha airtel supa5 mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Arusha.
Posted: 19 Jun 2012 11:00 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

WAKATI mshambuliaji kutoka Zambia, Davies Mwape akioneshwa mlango wa kutokea timu ya Yanga, imempa nafasi ya mwisho Mghana Kenneth Asamoah kuonesha makali yake katika michuano ya Kombe la Kagame la sivyo naye watamuacha.
Mbali na hilo, kiungo mpya wa timu hiyo, Nizar Khalfan jana alianza rasmi kibarua cha kuitumikia timu hiyo kwa kufanya mazoezi ya pamoja na wachezaji wenzake zaidi ya 17 waliokuwepo katika mazoezi hayo.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mazoezi hayo kwenye Uwanja wa Kaunda, Dar es Salaam jana Kocha Msaidizi wa timu hiyo Fredy Felix 'Minziro', alisema Asamoah imeamuliwa abaki kwa ajili ya michuano ya Kombe la Kagame lakini Mwape tayari ameshamalizana kila kitu na uongozi.
"Ni kweli Mwape licha ya kwamba unamuona mazoezi lakini hatutakuwa naye kwa msimu ujao, tayari uongozi umeshamalizana naye na hata Asamoah, naye anaangaliwa katika Kombe la Kagame na kama akiendelea kuonesha kiwango kile kile naye tutafikiria cha kufanya," alisema Minziro.
Alisema wachezaji hao wanalipwa fedha nyingi, hivyo walipaswa kuonesha kiwango tofauti na wachezaji wazawa ambapo kwa Mwape alishindwa kufanya hivyo, ndiyo maana wakaamua kusitisha mkataba wake ila Asamoah watamuangalia katika michuano hiyo.
"Unajua ukiwa mshambuliaji ni lazima ufunge tu huna jinsi na usipofunga mashabiki hawatakuelewa, Mwape katika mechi na Zamaleki ndiyo iliyomuweka pabaya kwa kupoteza nafasi nyingi za wazi," alisema Minziro.
Akizungumzia maandalizi kwa ujumla, Minziro alisema kwa sasa anawajenga wachezaji wake kuwa na stemina, ambapo baada ya wiki moja ataendelea na programu nyingine.
Wakati huohuo, Nizar ameanza rasmi mazoezi na timu hiyo ambapo mashabiki waliojitokeza katika mazoezi hayo walionesha kufurahishwa na uamuzi wake wa kujiunga na timu yao, ambapo kila alipogusa mpira walimshangilia.
Wachezaji ambao jana walikuwepo mazoezini ni kipa Yaw Berko, Godfrey Taita, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Canavaro', Ibrahim Job, Athuman Idd 'Chuji', Hamis Kiiza, Stephano Mwasika, Jeryson Tegete, Idrisa Rajab, Juma Seif 'Kijiko', Pius Kisambale, Asamoah, Omega Seme, Salum Telela na wengine watatu wa timu yao ya vijana.
Posted: 19 Jun 2012 10:59 PM PDT


Na Mwandishi Wetu

MATAMASHA ya kuitambulisha huduma Airtel Supa5 utaendelea tena mwishoni mwa wiki ambapo safari hii itakuwa ni zamu ya jiji la Mwanza ambalo wakazi wake watapata burudani katika viwanja vya wazi vya Furahisha.
Akizungumzia tamasha hilo jana  la kuitambulisha Supa5 jijini Mwanza Ofisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde alisema lengo la kuunganisha utambulisho huu kwa burudani ni kuwavutia vijana na wateja wengi kuhudhuria na kujifunza faida za Supa5 ili waitumie zaidi.
Alisema tamasha hilo litafanyika kwa siku mbili mfululizo ambapo Jumamosi watatoa fursa kwa wasanii chipukizi kujitokeza kwa wingi kuonesha vipaji vyao sambamba na kupata huduma ya Airtel Supa5.
Ofisa huyo alisema Jumapili itakuwa uzinduzi kamili ambapo wasanii wakongwe watatoa burudani, akiwemo Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, Mwasiti 'Soja' na Roma Mkatoliki watatoa burudani kwa wateja watakaohuduria tamasha hilo ambalo ni la bure.
Matinde alisema lengo la huduma hiyo ni kuhakikisha Airtel inatimiza dhamira yake iliyojiwekea ya kufikisha na kupunguza gharama za mawasiliano nchini kote bila kuwasahau vijana na wanafunzi kunufaika kwa kupata internet bure wakati wa usiku, kutuma sms bure na faida nyingine nyingi.
Huduma ya Airtel Supa5 ilizinduliwa hivi karibuni jijini Dar es salaam na baadaye kuendelea na matamasha katika mikoa ya Dodoma, Morogoro, Iringa na Arusha.

No comments:

Post a Comment