TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, June 18, 2012

Semina ya Viongozi wa Kidini katika kukuza Utalii

Rais wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akitoa hutuba yake katika
ufunguzi wa semina ya siku moja kwa  Viongozi wa kidini katika kukuza
dhana ya Utalii kwa wote,iliyofanyika katika ukumbi wa Salama Bwawani
Hotel Mjini Unguja leo,(kulia) Msahauri wa Rais masuala ya Utalii,
Issa Ahmed Othman,na Waziri wa Habari,Utalii,Utamaduni na Michezo,
Said Ali Mbarouk,(kushoto) Katibu mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Ali
Halil Mirza.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu
Rais wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa
kidini katika kukuza dhana ya Utalii kwa wote,mara baada ya kuifungua
semina ya siku moja iliyofanyika leo  katika ukumbi wa Salama Bwawani

Baadhi ya Viongozi wa madhehebu mbali
mbali ya kidini wa Mkoa wa Mjini  Magharibi wakisikiliza  kwa makini
hotuba ua ufunguzi wa  semina ya siku moja ya Viongozi wa kidini
katika kukuza dhana ya Utalii kwa wote,iliyofunguliwa na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,
katika ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja leo.[Picha na

Ramadhan Othman,Ikulu.

WEMA SEPETU KUMSHUSHA NYOTA WA FILAMU OMOTOLA JALADE KUTOKA NIGERIA

Nyota wa filamu wa Nigeria, Omotola Jalade katika pozi matata
Nyota wa filamu wa Nigeria, Omotola Jaladekatika kivazi cha ofisini
Nyota wa filamu wa Nigeria, Omotola Jalade katika kivazi cha kutokea
MSHINDI wa Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu, anatarajia kumdondosha nyota wa filamu wa Nigeria, Omotola Jalade hapa nchini.
Wema Sepetu, ambaye kwa sasa anatamba kwenye tasnia ya filamu anatarajia kumleta Omotola kwa ajili ya kusindikiza uzinduzi wa filamu yake mpya iitwayo Super Star.
Filamu hiyo ya Super Star, inazungumzia maisha ya Wema kuanzia utotoni kushiriki kwake Miss Dar Indian Ocean, Miss Kinondoni, Miss Tanzania hadi kuingia kwenye filamu.
Kwenye filamu hiyo Wema ameshirikiana na wasanii mbalimbali akiwemo mwimbaji wa Machozi Band, aitwaye Mwinyi.
Omotola, ambaye atatua Tanzania wiki hii, alianza kutamba kwenye tasnia hiyo baada ya kutoka na filamu iitwayo Iva mwaka 1993.
Hadi sasa nyota huyo amecheza jumla ya filamu 52, zikiwemo, Ties That Bind (2011), A Private Storm
Ije (2010), My Last Ambition (2009), Beyonce & Rihanna (2008), Temple of Justice (2008), Tomorrow Must Wait (2008) na nyingine nyingi.

Wakazi wa arusha waipokea kwa shangwe huduma mpya ya Airtel Jiunge na Supa5

.Mmoja wa wasanii anaeitikisa anga ya muziki wa hip hop nchini,anatamba na tuzo mbili za muziki huo huo huo wa hip hop,Roma akiamsha amsha hadhira kubwa ya watu iliojitokeza jioni ya leo kushuhudia uzinduzi wa huduma mpya ya kampuni ya simu za mkononi ya Airtel,Airtel Jiunge na Supa5,uliofanyika jana kwenye viwanja vya NMC mjini  Arusha na kuhudhuriwa na umati mkubwa watu.
Sehemu ya Wakazi wa Arusha wakishangilia ujio wa huduma mpya ya Airtel Supa5
.Anajiita Mwamba wa Kaskazini,Msanii mwingine mahiri katika miondoko ya muziki wa hip hop nchini,Joe Makini  akitumbuiza kwenye jukwaa jana kwenye viwanja vya NMC jijini Arusha,wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel ilipokuwa ikizindua huduma yake mpya ya Airtel Jiunge na Supa5 kwa wakazi wa Arusha.
Wakazi wa jiji la Arusha wakiendelea kuhamia na kujiunga kwa wingi  na Airtel.
.Sehemu ya Wakazi wa Arusha wakishangilia ujio wa huduma mpya ya Airtel Supa5
Msanii  mahiri wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la Wanaume Halisi lenye maskani yake Temeke,jijini Dar es Salaam,Juma Nature akiwarusha baadhi ya wakazi wa jiji la Arusha waliojitokeza kwa wingi kwenye viwanja vya NMC, wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel ilipokuwa ikizindua huduma yake mpya ya Airtel Jiunge na Supa5 kwa wakazi wa Arusha.
 
Pichani kati ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya simu za Mikononi ya Airtel-Arusha,Bwa Stephen Akyoo akiwa katika picha ya pamoja na washindi walioielezea vyema huduma mpya ya  Airtel Jiunge na Supa5 na kujishindia  zawadi ya simu aina Samsung.Kulia ni Lucas George na shoto ni Swalehe Mohamed.
Meneja Mauzo wa Kampuni ya simu za Mikononi ya Airtel-Arusha,Bwa  Bw Stephen Akyoo akimkabidhi simu aina ya Samsung mmoja wa wakazi wa Arusha aitwaye Lucas George mara baada ya kushinda shindano la kughani ,wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel ilipokuwa ikizindua huduma yake mpya ya Airtel  Jiunge na Supa5,uliofanyika kwenye viwanja vya NMC mjini  Arusha. Huduma ya Airtel Jiunge na Supa5 ilizinduliwa rasmi hivi karibuni jijini Dar na baadaye kuendelea kuzinduliwa katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kuwapa kilicho bora wateja wake popote pale walipo.

WAKALI DANCERS WASHEREHEKEA MIAKA 4 DAR LIVE MBAGALA

SHEREHE za miaka minne ya kundi la Wakali Dancers jana zilifana ndani ya ukumbi wa kisasa wa burudani, Dar Live uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar. Vikundi vya taarab vya Kings, Coast Modern na Kidumbaki kutoka Zanzibar pamoja na Talent Band vilifanya ‘bonge la kufuru’ kwa mashabiki waliofika katika ukumbi huo kwa ajili ya kuburudika wikiendi.
Wakali Dancer wakiwa na bendera yenye nembo yao wakati wakisherehekea miaka 4 ya kuanzishwa kundi lao.
...wakizidi kunogesha sherehe hizo.
...wakicheza wimbo wa Thriller ulioimbwa na Michael Jackson.
...wakizidi kupagawisha.

MMOJA MBARONI KWA MAUAJI, HUKU AJALI KUSABABISHA KIFO


Kamanda wa Polisi Mkoa wa DODOMA, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Bw. Zelothe Stephen akisani taarifa kwa ajili ya vyombo vya habari(Press Release)

Na. Luppy Kung’alo,wa Jeshi la Polisi Dodoma
  Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la RAMADHANI S/O AMIR Mwenye umri wa miaka 24, Mkulima  na Mkazi wa Pahi wilayani Kondoa kwa tuhuma za mauaji.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Bw. Zelothe Stephen alisema tukio hilo la mauaji  lilitokea tarehe 17/06/2012 majira ya saa 17:15 jioni katika kitongoji cha Lusangi Kijiji na Tarafa ya Pahi Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodom.
Akizungumzia tukio hilo alisema kwamba mtuhumiwa huyo alimshambulia na kumpiga bwana  MOHAMED S/O IBRAHIM Mwenye umri wa miaka 60, Mkulima na Mkazi wa Lusangi  kwa kumpiga na kipande cha kuni kichwani  na kisha  kumchoma na kitu chenye ncha kali kifuani.
“Marehemu alikuwa nyumbani kwake na mara ghafla akatokea mtuhumiwa huyo na kuanza kumpiga na kumshambulia.” Alisema Kamanda Zelothe Stephen
Bw. Zelothe alisema  kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na  majirani wa eneo hilo walidai kwamba  mtuhumiwa ni mgonjwa wa akili, hata hivyo mtuhumiwa amekamatwa na atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Mkuu huyo wa Polisi Mkoa wa Dodoma alisema Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kondoa.

BODI YA UTALII TANZANIA YAPONGEZWA KWA KAZI NZURI


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bibi Maimuna Tarish (Kushoto) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania –TTB alipokuwa akifungua kikao cha baraza hilo kilichofanyika katika ukumbi wa chuo cha Utalii jijini Dar es salaam hivi karibuni. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye pia ni Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Dk. Aloyce Nzuki, na kulia ni Katibu wa Baraza hilo Bw Elirehema Maturo.
Na: Geofrey Tengeneza
Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imepongezwa kwa kazi nzuri inayofanya katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwa ni pamoja na jukumu kubwa la kuitangaza Tanzania kama eneo bora lenye vivutio vingi vya kitalii duniani pamoja na ushindani mkubwa kutoka nchi nyingine na hivyo kufanya idadi ya watalii wanotembelea nchi yetu kuendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka sambamba na kuongezeka kwa pato la Taifa litokanalo na sekta ya utalii.
Akifungua kikao cha  Baraza la Wafanyakazi wa Bodi ya Utalii hivi karibuni katika ukumbi wa Mikutano wa chuo cha Utalii jijini Dar es salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Bibi Maimuna Tarish amesema Bodi ya Utalii imeendelea kutekeleza vema majukumu yake na kwamba wafanyakazi wa taasisi wana kila sababu ya kujivunia mafanikio haya kwa kuwa kila mmoja kwa nafasi yake amechangia katika mafanikio hayo.   Amewataka wafanyakazi kuendelea kuwa wabunifu zaidi kwa kuibua mawazo mapya yatakayosaidia kuboresha utendaji wa Bodi siku hadi siku na kujipima kwa matokeo ya kazi na mipango wanayojiwekea. “Nawaomba sambamba na kuwa na mipango ya kazi mfanye kazi kwa matokeo na kuwa wabunifu kadri iwezekanavyo kwa kila mfanyakazi kujitahidi kuwa na mawazo mapya ambayo yatasaidia shirika kuboresha utekelezji wa majukumu majukumu yake” alisema Bibi Maimuna.
Akizungumzia mikutano ya Baraza la Wafanyakazi sehemu za kazi Katibu Mkuu huyo amesema jambo muhimu sana katika kutatua baadhi ya matatizo yanayoikabili taasisi husika kwa kuwa mikutano hiyo ndicho chombo cha juu kabisa ambacho wafanyakazi kupitia wawakilishi na viongozi wao wa vyama vya wafanyakazi na Menejimenti wanapata fursa ya kukaa pamoja na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu taasisi na wafanyakazi kwa ujumla. Amesema kwa kufanya hivyo ni kutekeleza kwa vitendo agizo la serikali linalolenga katika kuendeleza na kudumisha utawala bora jambo ambalo linadumisha umoja na mshikamano baina ya wafanyakazi.
Baraza hili jipya la wafanyakazi wa Bodi ya Utalii Tanzania pamoja na mambo mengine kadhaa katika kikao chake hicho cha siku mbili lilipokea na kujadili makadirio ya mapato na matumizi ya Bodi katika kipindi cha mwaka 2012/2013, na  taarifa ya utekelezaji wa mipango na kazi mbali mbali za Bodi katika kipindi cha Julai 2011 hadi Machi 2012.
Utalii nii Sekta ya pili nchini kwa kuchangia katika pato la Taifa ambapo inachangia kiasi cha asilimia 17.2 baada sekta ya Madini ambayo ndiyo inaongoza. Aidha kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2011 idadi ya watalii waliotembelea Tanzania kutoka nchi mbalimbali duniani iliongezeka kutoka watalii 782,699 mwaka 2010 hadi watalii 867,994. Nayo mapato yatokanayo na utalii yaliongezeka kutoka dola za Kimarekani 1,254.50 mwaka 2010 hadi ufikia dola za kimarekani 1,348,30

PHILIP GUCHA AKABIDHIWA PIKIPIKI YAKE ALIYOSHINDA KATIKA PROMOSHENI YA "VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO"


Mkazi wa Iringa Bw. Philip Gucha akiwa amepanda pikipiki mpya ambayo amejishindia katika promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO NA SBL, makabidhianoya pikipiki hiyo yalifanyika jana  mkoani Iringa mjini.
Kampuni ya Bia ya Serengeti jana imekabidhi zawadi ya bajaji mpya na pikipiki mpya kabisa kwa washindi wa zawadi hizo mkoani Iringa ambapo Bajaji ilikabidhiwa kwa Bw Fadhili Manzi katika mji mdogo wa Mafinga mkoa humo na pikipiki ilikabidhiwa kwa bw………… mjini Iringa ni katika promosheni ya VUMBUA HAZINA CHINI YA KIZIBO na SBL inayoendeshwa na kampuni ya bia ya Serengeti.
Ni wiki ya 6 sasa kati ya wiki 16 za promosheni hiyo ambapo katika droo ya sita iliyochezeshwa hivi karibuni washindi wawili walipatikana ambao ni bw. Deusdedit Tobias Njau 22 kutoka kiboroloni mkoani Kilimanjaro ambaye alijishindia jenereta mpya na Bw. Vicent Lymo 36 kutoka kibosho mkoani Kilimanjaro ambaye amejinyakulia pikipiki mpya kabisa ambayo naye atakabidhiwa zawadi yake siku chache zijazo pindi taratibu za usajili zitakapokamilika.
Makabidhiano hayo yalifanyika jana na kupata kuhudhuriwa na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini huku tukio zima likishuhudiwa na umati mkubwa wa watu ambao walitoa maoni mabalimbali juu ya zoezi zima la promosheni hiyo na kusema SBL inabadilisha maisha ya watanzania wengi hasa vijana jambo ambalo linapaswa kuigwa na makampuni na mashirika mengine hapa nchini.Washindi hao wameishukuru SBL nakuitaka iendelee na moto huohuo.
Akiongea na waandishin wa habari wakati wa kukabidhi zawadi hizo meneja wa masoko SBL mkoa wa Iringa  Bw. Philip Gucha amesema washindi hao walipatikana kihalali na kwamba kila mtanzania mweneye sifa zilizoainishwa katika vigezo na masharti ya promosheni hiyo ana haki na uwezo wa kushiriki na kushinda zawadi mojawapo au zaidi kati ya zawadi zilitajwa katika promosheni hiyo “leo tunawakabidhi hawa zawadi zao lakini zawadi hizi ni robot u ya zawadi zite ambazo tunawasubiri ninyi watanzania na wateja wetu wote kujishindia” alisemaGucha na kuwataka watanzania wote wenye mapenzi mema na kampuni ya bia ya Serengeti waendelee kushiriki kwani batahi ya mtu haiwezi kwenda kwa mwingine.
Hii ni droo ya sita wiki ya sita mfululizo ambapo bado takriban wiki 11 sasa ili kuisha kwa promosheni hiyo ya pekee na ya kwanza kutokea hapa nchini ambapo zaidi ya milioni 780 za kitanzania zinashindaniwa kote nchini
Kwa upande wake mshindi wa bajaj bw. Fadhili Manzi amesema kwasasa safari ya maisha yake na familia yake itabadilika kutokana na zawadi hiyo kwani ni sawa na mkulima hodari kuzawadiwa trekta “Sasa wale vijana wenye uwezo wa kuendesha bajaj walete vyeti na leseni zao za udereva wa bajaj ili niwape kazi kwani hii bajaj inaanza biashara haraka iwezekanavyo” alisema Manzi ambaye alionekana kujawa na furaha ya pekee na kutumia fursa hiyo kuishukuru kampuni ya bia ya Serengeti kwa kumwezesha kupiga hatua kubwa kimaisha.

WAKUFUNZI WA SENSA WAPIGWA MSASA

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi  ya Taifa ya Takwimu Dkt  Albina Chuwa akitoa ufafanuzi kwa wakufunzi wa Sensa  kwa ngazi ya kitaifa jana mjini Dodoma. Wakufunzi  hao wanaandaliwa kwa ajili ya kwenda katika mikoa mbalimbali nchini kwa ajili ya kuwaelimisha wengi watakaosaidia kufanikisha zoezi la sensa tarehe 26 mwezi Agosti mwaka huu.PICHA NA VICENT TIGANYA WA MAELEZO
Baadhi ya viongozi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu na wakufunzi wa Sensa kwa ngazi ya Kitaifa wakiwa watulia kimya kwa dakika mbili kwa ajili ya kuombeleza kifo cha Mhariri wa Jamboleo Willy Edward kilichotokea mjini Morogoro alipokuwa akihudhuria mafunzo ya sense kwa wahariri . Viongozi na wakufunzi hao walikuwa katika mafunzo  ya siku 10 tayari kwa ajili ya kwenda kufundisha hatua za mikoa . Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)yalianza jana mjini Dodoma.
Kamishna wa Sensa Hajjat Amina Mrisho akitoa neno la utangulizi kwa  wakufunzi wa Sensa kwa ngazi ya Kitaifa wakati wa  mafunzo  ya siku 10 tayari kwa ajili ya kwenda kufundisha hatua za mikoa . Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) yalianza jana mjini Dodoma.
Baadhi ya wakufunzi wa Sensa kwa ngazi ya Kitaifa wakiwa katika mafunzo  ya siku 10 tayari kwa ajili ya kwenda kufundisha hatua za mikoa wakifuatilia mafunzo kutoka kwa wataalam mbalimbali walikuwa wakitoa mada mbalimbali. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) yalianza  jana mjini Dodoma.

Shairi kutoka kwa mdau Mroki Mroki:Kapumzike kwa amani Wille wa Ogunde


Kapumzike kwa amani Wille wa Ogunde
Salaamu wasomaji, Moyo naupiga konde,
Sihitaji hata maji, kama viazi mviponde,
 
Nimejawa na simanzi, Kifo cha kaka Ogunde,
Kapumzike kwa amani, Wille mwana wa Ogunde.

Tusimlaumu Mungu, sote tulio waungwana,
Najua tuna uchungu, yowe ni kwamaulana,
Mola angetupa fungu, kifo siwe cha kijana,
Kapumzike kwa amani, Wille mwana wa Ogunde.

Twasema kasitukizwa, Wille kaenda kijana,
Alipo kuja hatukuulizwa, tulimwona tu mvulana,
Mungu we ndo muweza, kifo leo twakimbizana,
Kapumzike kwa amani, Wille mwana wa Ogunde.

Mwaka ule 74 machi saba, Wille ukaiona dunia,
Leo amegonga siku ya saba, ukamtwaa hii dunia,
Tena tarehe kumi na saba, Wille kaiga dunia,
Kapumzike kwa amani, Wille mwana wa Ogunde.

Wille ulilia kaka, siku  uliyo iona dunia,
Mpalule, Pinto,na  Mroki, sasa zamuyetu kulia,
Wengi wanatafuta kichaka, lini nao watatwaliwa,
Kapumzike kwa amani, Wille mwana wa Ogunde.

Pigo la wana habari, Tanzania na Afrika pia
Hakika kifo ni bahari, hakuna ajuae ilikoanzia,
Kifo ni jemedari, Wille amesha twalia,
Kapumzike kwa amani, Wile mwana wa Ogunde.


Salamu kawape jalia, wote walo kutangulia,
Mwakiteleko alotulia, na wote wana familia,
Wanahabari tunalia, Wille Ogunde kutangulia,
Kapumzike kwa amani, Wile mwana wa Ogunde.

Father Kidevu tamatia, nangoja nami kufuatia,
Siku itapo fikia, hakuna atakae bakia,
Kifo kitendawili, Mola ndie atakae kitegua,
Kapumzike kwa amani, Wile mwana wa Ogunde.

Mroki Mroki a.k.a Father Kidevu
0717002303/0755 373999

MATUKIO KUTOKA BARAZA LA WAWAKILISHI ZAZNIBAR

Mwakilishi wa Jimbo la Chakechake Omar Ali Sheheakiwa pamoja na Mwakilishi wa kuteuliwa Panya Othman CCM wakiingia katika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi huko Mbweni nje ya Mji wa Zanzibar.

Badhi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakisikiliza kwa makini hoja mbalimbali zinazotolewa ndani ya Baraza hilo huko Bweni Nje ya Mji wa Zanzibar.

PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.

WAFANYAKAZI BENKI YA UBA WAKIJIANDAA KWENDA KATIKA MAZOEZI KIGAMBONI AMBAKO PIA WALITOA MSAADA KITUO CHA HOPE FAMILY

Kushoto ni Bw. Rock Meneja mkazi wa benki ya UBA nchini na kushoto ni Victor Meneja wa tawi la benki ya UBA Kariakoo wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakijiandaa pamoja na wafanyakazi wengine wa benki hiyo katika tawi la City Centre Branch Posta,  kwenda Kigamboni ambako walikuwa na mazoezi ya viungo  na baadae walitoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ikiwa ni vyakula mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni mbili, katika kituo cha watoto yatima cha cha Hope Family kilichopo Kigamboni jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki iliyopita

ATCL yajipanga kuendeleza sekta ya usafiri wa anga

Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Kapteni Lusajo Lazaro akihutubia wahitimu wa Chuo cha Mafunzo cha ATCL baada ya kumaliza kozi ya utoaji huduma kwenye ndege katika hafla yakuwakabidhi vyeti iliyofankika Jijini Dar es Salaam jana. Picha na mpiga picha wetu.
Tumeiva sasa. Wahitimu wa Chuo cha Mafunzo cha ATCL wakionyesha vyeti  walivyokabidhiwa baada ya kumaliza kozi ya utoaji huduma kwenye ndege .Hafla hiyo ilifanyika Jijini Dar es Salaam jana. Picha na mpiga picha wetu.

Wahitimu wa Chuo cha Mafunzo cha ATCL wakipozi kwa picha ya pamoja katika hafla ya kukabidhiwa vyeti baada ya kumaliza kozi ya utoaji huduma kwenye ndege .Hafla hiyo ilifanyika Jijini Dar es Salaam jana. Picha na mpiga picha wetu.

Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Ndege la Air Tanzania (ATCL) limetangaza mpango wakuungana na Chuo cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) ilikutoa mafunzo mbalimbali yatakayowezesha upatikanaji wa wataalam mbalimbali wa sekta ya anga.
Akizungumza katika sherehe yakuwaga wanafunzi 39 wa Chuo cha Mafunzo cha Shirika la Ndege la Air Tanzania jijini Dar es Salaam wikiendi hii, Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa ATCL, Kapteni Lusajo Lazaro alisema mpango huo ambao utakuwa endelevu umewekwa kwa makusudi ilikuhakikisha wataalam katika sekta ya usafiri wa anga wanakuwa na ubora unaostahili hususani wakati huu ambapo sekta ya usafiri wa anga inakuwa kwa kasi zaidi na kuvutia wawekezaji zaidi.
“Tumeshasaini nyaraka za makubaliano (MOU)na NIT ilikuwezesha ufanisi wa swala hili. Nimatumaini yetu kuwa mpango huu utasaidia kupunguza tatizo la upungufu wa wataalam katika sekta ya anga nchini.
”Bila pingamizi lolote kuwa sasa tutahitaji wataalam zaidi ili kuboresha utoaji wa huduma zetu  hususani  katika kipindi hiki ambacho tumejikita katika utekelezaji wa  mpango wetu wa maendeleo wa miaka mitano ambao unalengo la kuongeza safari na ndege nyingine katika miaka michache ijayo,” alisema.
Lazaro akitoa maoni yake juu ya soko la pamoja la Afrika Mashariki ambalo limefungua milango kwa biashara huria za bidhaa na huduma ndani ya nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) alisema kuwa kampuni yake imejipanga kutumia fursa hiyo ipasavyo.
 “Soko hili huria la pamoja litatengeneza fursa nyingi sana na tayari sisi kama shirika tumejipanga kuchangamkia na kuzitumiua fursa hizo ipasavyo. Tupo katika mipango ya kuongeza safari zetu zaidi na pale inapowezekana kutafanyakazi pamoja na mashirika makubwa barani. Tunahitaji wafanyakazi wenye ujuzi na walio bora ambao watatusaidia kuleta ushindani kama shirika,” aliongeza.
Kwa upande wake, mhitimu wa Chuo cha Mafunzo cha Mafunzo ya Anga cha ATCL Yasmin Khanj akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzake waliohitimu alisema kuwa watatumia vizuri ujuzi wote walioupata katika chuo hicho ilikuchangia maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga nchini.
 “Hii ni hatua kubwa sana katika maisha yetu. Tunaiomba kampuni ya ATCL kutupa fursa ya kupata ujuzi zaidi kwa kutupatia nafasi kwenye kampuni ili tuweze kupata uzoefu unaohitajika ili tulete ushindani na kutoa huduma ipasavyo,” alisema.
Aidha, mkuu wa chuo cha mafunzo cha ATCL, Lawrence Mhomwa alisema kuwa wahitimu hao baada ya kumaliza mafunzo yao yaliyojumuisha mada saba katika chuo hicho zikiwa pamoja na huduma kwa wateja, usalama katika viwanja vya ndege, uhudumu ndani ya ndege, usalama ndani ya ndege na mada nyingine,wahitimu hao sasa wanauwezo wa kufanyakazi katika shirika lolote la ndege .

Epiq Bongo Star Search yamaliza kazi mkoani Dodoma

Na Mwandishi Wetu Dodoma
PAZIA la shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS) kwa mkoa wa Dodoma limefungwa rasmi huku vipaji kibao vikiwa vimejitokeza na kuwavutia majaji.
Kilichovutia zaidi ni washiriki wa miaka 16 ambao walionekana kuimba vema na kuwa kivutio hata kwa washiriki wenzao waliofurika katika ukumbi wa Royal Village.
Akizungumzia shindano hilo Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Benchmark Production inayoandaa shindano hilo Ritha Paulsen alisema kuwa amevutiwa na wingi wa washiriki mkoani hapa hasa idadi ya washiriki wasichana pia.
Alisema kuwa ikiwa ni mara ya kwanza kuruhusu washiriki wa miaka 16 kuingia katika usaili wa EBSS 2012 ameshuhudia hazina kubwa ya vipaji  vya washiriki wa umri huo.
Katika usaili huo kulikuwa na washiriki wa aina mbalimbali wakiwamo wanafunzi, wafanyabiashara ndogondogo, vijana wa mitaani na wadau wengineo wa muziki.
Kwa kuthamini umuhimu wa akina mama na watoto mshiriki aliefika kuonesha kipaji chake katika ukumbi huo alipewa nafasi ya kuimba ili aweze kuwahi kuondoka.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Zantel ambao ni wadhamini wakuu wa EBSS 2012  Awaichi Mawalla mbali na kuvutiwa na ushiriki wa vijana waliojitokeza pia alihamasisha upimaji wa damu kwa kuchangia damu kwa kituo cha damu mkoani Dodoma.
“ Kwa kupitia EBSS 2012 tunataka kuwafikia vijana sio tu katika muziki bali pia hata katika kuhamasisha masuala mbalimbali yahusuyo jamii kama vile hili la kuchangia damu na mengineo” alisema Awaichi.
Washindi watakaopatikana watatangazwa baadae katika vyombo vya habari. Baada ya Dodoma kwa sasa inafuata Zanzibar ijumaa ijayo katika eneo la Ngome Kongwe.

WANAFUNZI WASHIRIKI KATIKA MASHINDANO YA KUJADILI MUUNDO WA FAMILIA


Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Sekondary Khadija Ali Mohd akitoa hotuba ya kuwapongeza Wanafumzi walioshiriki katika Mashindano ya kujadili Muundo wa Familia za Kiislamu na Familia nyengine,huko katika Ukumbi wa Afisi  ya Jumuiya ya Utamaduni ya Irani iliokuweko Mlandege Zanzibar.
 
Mkurugenzi wa Jumuiya ya Utamaduni ya Irani sheikh Abulfadhili akitoa maelezo mafupi kuhusiana na madhumuni ya mashindano yalioshirikisha Wanafunzi kutoka Skuli ya Lumumba,Benmbela,Hailesalasie,
Kiponda na Bilal Islamic waliojadili  Muundo wa Familia za Kiislamu na Familia nyengine,huko katika Ukumbi wa Afisi  ya Jumuiya ya Utamaduni ya Irani iliokuweko Mlandege Zanzibar.



No comments:

Post a Comment