TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 1, 2013

Wasanii Richard wa Big Brother na Mwanamuziki Dully, usiku wa Mkesha wamekuwa ni miongoni mwa watu waliofanya shangwe katika kusherehekea kuingia mwaka 2013.

Shangwe hizo zimefanyika mara tu baada ya kugonga sekunde ya 60 ya kuthibitisha kuingia mwaka mpya ambapo walisikika wakipiga kelele na shangwe huku wakiwaomba mashabiki wao kuingia jukwaa kusakata Ngoma huku wakizongwa na maelfu ya wanawake na Vijana wa mji wa Moshi kutaka kucheza na kufurahi nao.
aidha alikuwa ni Richard ambaye muda wote alionekana akigandwa na wanawake wengi wa kizungu huku yeye akionekana kuwakwepa na kuendelea kucheza hadi furaha yake ilipokwisha na kwenda kujipumzisha
"kiukweli nimefurahi sana mpalule, kwani kumbuka kumaliza mwaka wakati mwingine inabidi ufurahi na kumshukuru Mungu, mimi hapa leo pia nimefurahi baada ya kukutana na rafiki yangu Dully na ndiyo kama unavyotuona hatuna budi kusherehekea kufika mwaka 2013, wapo wengi walitamani sana kufika lakini aikuwa hivyo" alisema Richi
na nilipomuuliza kuhusu kufuatwa na kundi la kina dada wa kizungu richi alisema" nina msimamo na mke wangu swahiba wangu mpalule, ni kweli kama unavyoona wengi wanapenda kucheza na mimi, na hata mimi siwezi kukataa kucheza na wao, ila kiukweli ni kwamba siwezi kufanya chochote kwa sababu nampenda sana mke wangu" alisema  Richard
na kwa Upande wake Dully yeye alionekana kuwa na furaha nyingi paspi mawaa, kwani apia alionekana kuwa na kundi kubwa la ulinzi, lakini hata hivyo pamoja na ulinzi huo aikutosha kuwafanya Walimbwende wa Mji wa Moshi ambao kwa sasa unafumuka kwa idadi  kubwa ya Soko la Wanawake wanaojiuza usiku(CHANGUDOA) kutotimiza wajibu wao , kutokana na kwamba baada ya Shangwe hizo Dully aliangukia mikononi mwa kichunchede ambaco alionekana kugandana nacho kisha kutokomea zao usiku wa Manane.
" nafurahi sana kufika hapa nilipo, pia namshukuru Mungu kwa kunifikisha 2013, nipo hapa Moshi mji mdogo lakini wa Starehe, ila napenda kuwaomba mashabiki wangu kuwa nipo na hata hivyo nitahakikisha mwaka huu nawapa vitu vipya kama ulivyo mwaka mpya, nahisi huu ni mwaka wangu tena Mpalule, subiri hata wewe utaona" alisema Dully
na kuhusu kugandwa na kuwa na kundi kumbwa la ulinzi Dully " hawa ni jamaa zangu yaani Mashabiki wangu, ambao siku zote wananipa sapoti kubwa, hivyo mara baada ya kuingia katika mji wa Moshi wamenipokea vizuri na ndiyo maana unawaona, na kuhusu kina dada hawa hilo siwezi kusema kwani wewe mwenyewe unajua mimi mashabiki wangu ni kina nani, na hata siku moja siwezi kuacha kuwasifia na kutaka kuja kwangu vile wapendavyo"alisema Dully huku akitoweka na Mmoja wa Wasichana waliokuwa wakimganda Tangu alipoingia ndani ya CLUB LA-LIGGA.


























































PICHA ZOTE NI TUKIO AMBALO LIMEFANYIKA WAKATI WA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA KWENYE UKUMBI WA KISASA WA -CLUB LA- LIGGA

No comments:

Post a Comment