TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, November 15, 2013

KIFO CHA MVUNGI CHAMTIKISA JK, KONTENA LA MENO YA TEMBO LANASWA, MJAMZITO AUAWA KWA KUCHINJWA

Posted: 13 Nov 2013 10:41 PM PST

Rais Dkt.Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakifariji familia ya Marehemu Dkt. Sengodo Mvungi nyumbani kwao Kibamba Dar es Salaam jana.
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZAZIDI KUMIMINIKA
  • MWILI WAKE KUWASILI KESHO,KUAGWA JUMAMOSI

 Na Waandishi Wetu
  Rais Jakaya Kikwete, amesema ameshtushwa na kufadhaishwa na taarifa za kifo cha Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Sengondo Mvungi, kilichotokea juzi kwenye Hospitali ya Milpark, Johannesburg, Afrika Kusini.

Katika salamu za rambirambi ambazo amemtumia Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba, Rais Kikwete alisema amepokea kwa mshtuko mkubwa na taarifa za kifo cha Dkt. Mvungi.
"Kwa hakika ni taarifa iliyonisumbua na kunipa huzuni kubwa," alisema Dkt. Kikwete. Rais Kikwete alisema hakuna shaka kuwa katika maisha yake Dkt. Mvungi alitoa mchango mkubwa katika maendeleo ya Tanzania kwa namna mbalimbali na kuwa kifo kimemfika wakati Taifa la Tanzania lilikuwa bado linahitaji busara, hekima na mchango wake katika mchakato mzima wa kusaka Katiba mpya.
"Kuanzia alipokuwa mwandishi wa habari katika Magazeti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Uhuru na Mzalendo, hadi uhadhiri wake katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, hadi uwakili katika Kampuni ya South Law Chambers, hadi uongozi wake katika Chama cha NCCR-Mageuzi, hadi uamuzi wake wa kugombea Urais wa Tanzania mwaka 2005 na sasa akiwa Mjumbe wa Tume ya Katiba, Dkt. Mvungi ametoa mchango wake mkubwa sana katika maendeleo ya nchi yetu. Na hili sitalisahau," alisema Rais Kikwete na kuongeza;
"Kwa masikitiko makubwa, nakutumia wewe Jaji Joseph Warioba, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba salamu za rambirambi za dhati ya moyo wangu nikiomboleza kifo cha Dkt. Mvungi.
“Nakupa pole nyingi wewe Mwenyekiti, wajumbe wa Tume na wafanyakazi wote wa Tume kwa kuondokewa na mwenzenu. Naungana nanyi kuombleza msiba huo mkubwa.
“Kupitia kwako, natuma pole nyingi kwa wana-familia, ndugu, marafiki na majirani wa Dkt. Mvungi kwa kuondokewa na mhimili, msimamizi wa familia na ndugu.
“Wajulishe kuwa niko nao katika msiba huu mkubwa. Wajulishe kuwa msiba wao ni msiba wangu pia. Muhimu waelewe kuwa binafsi naelewa machungu yao katika kipindi hiki kigumu na namwomba Mwenyezi Mungu awape subira waweze kuvuka kipindi hiki kigumu kwa sababu yote ni mapenzi yake.
Mbatia anena
Wakati huo huo, mwili wa Dkt. Mvungi unatarajia kuwasili nchini kesho na utapokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere na kisha kupelekwa nyumbani kwake Kibamba Msakuzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema baada ya mwili huo kuwasili itafanyika misa takatifu katika Kanisa la Mt. Joseph saa nne asubuhi Jumamosi.
Alisema baada ya misa hiyo saa sita mchana mwili wake utapelekwa viwanja vya Karimjee kwa ajili ya kuagwa na kisha kusafirisha kwenda Mwanga, mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko.
Alisema katika kipindi hiki cha msiba bendera za chama hicho zitapepea nusu mlingoti kwa muda wa wiki moja.
Waziri Chikawe
Naye Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, alisema msiba huo ni pigo kwa taifa kwani marehemu alikuwa ni kiungo muhimu na alitumia ujuzi, elimu na nafasi aliyonayo kwa jamii hasa katika kipindi hiki muhimu cha mchakato wa katiba mpya.
Alisema ni wananchi waelewe kuwa ikitokea kuyumba au kuwepo kwa pengo lolote katika mchakato huo basi litakuwa limechangiwa na kutokuwepo kwake Dkt. Mvungi.
Jaji Warioba amlilia
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba, alisema Dkt. Mvungi ni mtu muhimu ambaye alikuwa na mchango mkubwa kwenye Tume yake.
Alisema alitumia utaalam wake wa sheria na uzoefu katika kuhakikisha hoja zake alizokuwa akizitoa anazisimamia ipasavyo.
CUF yatuma rambirambi
Kwa upande wake Chama cha Wananchi (CUF), kimesema kimepokea kwa mshituko na majonzi makubwa taarifa ya kifo
 cha Dkt. Mvungi.
"Kifo cha Dkt.Mvungi kimeishtua Tanzania nzima hasa kwa vile tulitazamia kuwa angeishi kwa muda mrefu zaidi.
Kifo hicho kinazidi kusikitisha kwa vile kimetokana na kushambuliwa kikatili na watu wasiojulikana wanaodaiwa kuwa ni majambazi," ilieleza taarifa ya CUF.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi CUF, mimi mwenyewe na viongozi waandamizi wa CUF walimjua vizuri sana Marehemu Dkt. Mvungi kwani tulifanya kazi naye kwa karibu," alieleza taarifa ya CUF iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Maalim Seif, alisema Dkt. Mvungi alikuwa mpambanaji jasiri asiyeyumba katika mapambano ya kuiletea Tanzania mfumo wa kidemokrasia halisi unaolenga kulinda haki za kila Mtanzania bila ya ubaguzi wa aina yoyote ile.
Alisema Dkt. Mvungi alichukia uonevu, manyanyaso, ukandamizaji na dhuluma dhidi ya binadamu yoyote.
"Tulishirikiana naye kwa karibu katika mchakato wa kudai Katiba mpya ya Tanzania na pale vyama vya siasa vilipounda kamati ya kufanya rasimu ya Katiba mpya Marehemu Dkt. Mvungi ndiye aliyekuwa Mwanasheria wa Kamati hiyo.
Alitoa mchango mkubwa katika kuandaa na kukamilisha rasimu hiyo," alisema Maalim Seif na kuongeza;
"Wengi tulifarijika pale alipoteuliwa kuwa miongoni mwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Tanzania.
Tulijua uwezo wake, umahiri wake, utendaji kazi makini wake na dhamira yake ya kuona Tanzania inapata Katiba nzuri kwa masilahi ya wananchi wote bila kujali itikadi za vyama."
Alisema Dkt. Mvungi alikuwa ni wakili mahiri, msomi makini na kiongozi shupavu.
Alisema alikuwa jasiri hasa katika kuwatetea wanyonge na katika kutoa mawazo yake. Alikuwa ni mchambuzi hodari wa mambo ya kisheria, hasa sheria inayoambatana na masuala ya Katiba.
Hali kadhalika alikuwa mchambuzi aliyebobea katika masuala ya kijamii na ya kisiasa na aliguswa sana na umuhimu wa kuendeleza elimu bora nchini Tanzania.
Maalim Seif alisema kifo chake ni pigo zito kwa familia yake, Chama cha NCCR-Mageuzi, Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kwa jamii nzima ya Watanzania.
"Kwa niaba ya Profesa Ibrahim Haruna Lipumba, Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF na Wanachama wote wa CUF na kwa niaba yangu mwenyewe, tunatoa mkono wa tanzia kwa familia ya Marehemu, Mwenyekiti wa Taifa wa NCCR-Mageuzi, Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na wafiwa wote," alisema.
CCM yatoa pole
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesikitishwa na kifo cha Dkt. Mvungi na umeonya kuwa umaskini usifanye Watanzania kuwa chanzo cha kuua watu wengine.
Akizungumza Dar es Salaam jana Mkuu wa Idara ya Hamasa na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Paul Makonda, alisema wamepokea kwa masikitiko taarifa ya msiba huo.
"Umaskini wetu wa kipato, akili na mawazo, usiwe sababu ya kuumizana na kugharimu maisha ya mtu kwani hata wale waliomvamia na kumjeruhi huenda wamesukumwa na tamaa zao za kimaisha," alisema.
Polisi yanasa mwingine
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia mtu mmoja anayetuhuniwa kuhusika katika tukio la mauaji ya marehemu Dkt.Sengondo Mvungi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Kamishna wa Polisi Kanda, Maalum Suleiman Kova alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi katika maeneo ya Twiga Jangwani.
Kamishina Kova alisema kuwa; "mtuhumiwa alitambuliwa na kukamatwa kisha kuhojiwa na Polisi na alikubali kuhusika katika tukio hilo na askari waliongozana naye hadi nyumbani kwake Kiwalani Migombani ambapo alikutwa na silaha ambayo ni bastola aina ya REVOLVER No.BDN 6111 pamoja na risasi 21 za bastola hiyo ikiwa ni mali ya Dkt.Mvungi,"alisema Kova.
Pia katika upekuzi uliofanywa na Jeshi la Polisi katika chumba cha mtuhumiwa vilipatikana baadhi ya vifaa vya mlipuko vya aina tofauti vikiwemo,baruti aina ya Explgel, Tambi mbili ambazo ni viwashio vya baruti pamoja na mlipuko.
Aliongeza kuwa mtuhumiwa alipohojiwa kuhusu umiliki wa silaha hiyo alikiri kuwa hana kibali cha kumiliki silaha. Alisema silaha hiyo ni miongoni mwa vitu vilivyoibwa kwa Dkt. Mvungi.

Posted: 13 Nov 2013 10:43 PM PST

 Na Mwajuma Juma, Zanzibar
  Kontena lililobeba meno ya tembo limekamatwa katika bandari ya Malindi mjini Zanzibar ambalo lilikuwa linasubiri kusafirishwa jana.Kamishna wa Polisi Zanzibar, Musa Ally Musa, alithibitisha kukamatwa kwa kontena hilo jana lililokuwa na magunia 98 yaliyowekwa meno ya tembo tayari kwa kusafirishwa.

  "Ni kweli tumekamata kontena lililobeba meno ya tembo ila mpaka sasa bado hatujafahamu uzito na idadi ya meno yaliyokuwemo ndani ya magunia yaliyokuwa na idadi tofauti ya meno hayo kwani ukaguzi unaendelea," alisema Kamishna Musa Ally Musa.
  Kamishna Musa Ally Musa alisema hadi sasa wanawashikilia watu wawili kwa mahojiano ili kufahamu kama wanahusika na mzigo huo na wapi mzigo huo ulikuwa unapelekwa .Aliongezea kwa kusema taarifa kamili juu ya kontena hilo zitatolewa baada ya kupakuliwa na kufahamu uzito na idadi ya meno hayo.
Posted: 13 Nov 2013 10:49 PM PST

 Na Rachel Balama
   Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, inatarajia kufanyia mapitio ya uamuzi wa kutupilia mbali ombi la upande wa utetezi la kutaka kufutwa kwa shtaka la kutotii amri halali ya mahakama linalomkabili Shekhe Ponda Issa Ponda.

   Ombi hilo lilitupiliwa mbali na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, Richard Kabate. Mapitio hayo yanatarajiwa kufanyika Novemba 18, mwaka huu.
   Mawakili wa Ponda wakiongozwa na Juma Nassoro, waliiomba mahakama hiyo kupitia uamuzi huo uliotolewa Oktoba mosi, mwaka huu na hakimu huyo.
  Hakimu Kibate alitupilia mbali ombi la upande wa utetezi uliokuwa ukiomba mahakama hiyo kuondoa shtaka hilo la kutotii amri halali linalomkabili mteja wake au lifutwe akidai kuwa ilitolewa na Mahakama ya Kisutu.
  Wakili Nassoro alidai kwamba amewasilisha ombi hilo baada ya kubaini kuwa mahakama hiyo ya Morogoro haina uwezo kisheria kusikiliza shtaka hilo, vinginevyo lifunguliwe katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambayo ilitoa hukumu hiyo.
  Hata hivyo, Hakimu Kibate alitupilia mbali ombi hilo na kusema kuwa kwa mujibu wa vifungu mbalimbali vya sheria vya uendeshaji wa kesi za jinai, shtaka hilo dhidi ya Ponda la kudaiwa kutokutii amri halali ya mahakama litaendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo na sio kuhamishiwa Kisutu.
  Alizitaja sababu za shtaka hilo kuendelea kusikilizwa katika mahakama hiyo kuwa ni mshtakiwa huyo kutenda kosa hilo eneo la Kiwanja cha Ndege la Manispaa ya Morogoro.
  Hakimu huyo alisisitiza kuwa hakuna sababu ya kuhamishiwa shtaka hilo katika Mahakama ya Kisutu.Sababu nyingine ni mshtakiwa huyo kuvunja amri halali iliyotolewa na Mahakama ya Kisutu na sio sharti kama ambavyo upande wa utetezi ulidai na kufafanua kuwa hata kama mahakama hiyo ilitoa sharti, kisheria sharti linalotolewa na mahakama yoyote ni amri.
   Sheekhe Ponda anakabiliwa na mashtaka matatu anayodaiwa kuyatenda kwenye mhadhara huo. Ilidaiwa mahakamani kwamba aliwaambia Waislamu wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti kwani zimeundwa na ambao ni vibaraka wa CCM na serikal
Posted: 13 Nov 2013 10:58 PM PST

 Na Darlin Said
  Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umekanusha vikali kauli iliyotolewa na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kwa kuhusisha umoja huo na picha zinazomdhalilisha mbunge huyo kwenye mitandao ya kijamii.

  Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Idara ya Hamasa na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Paul Makonda, alisema UVCCM haihusiki na tukio hilo, hivyo alimtaka Lema atafute mchawi wake.
  Alisema watu waliofanya tukio hilo ni wale ambao amewatengeneza yeye mwenyewe katika mikutano yake ambao aliwahamasisha kutokuwa na nidhamu na kutotii sheria na taratibu za nchi."Sasa anamtafuta mchawi kwa kuishutumu UVCCM wakati hao waliofanya hivyo ndiyo matunda yake mwe n y ewe , " a l i s ema Makonda.
  Makonda alisema CHADEMA kila kinapopatwa na changamoto kinaishutumu CCM wakati hivi sasa ndani ya chama hicho hali sio shwari."Hivyo wasimtafute mchawi kwani bundi ameshatua,kazi ya UVCCM ni kuwatetea vijana, hatuna muda wa kumtafuta Lema," alisema Makonda.
  Makonda aliongezea kwa kusema kuwa Serikali imekuwa mstari wa mbele kusimamia amani,utulivu pamoja na watu kutii sheria na taratibu za nchi, lakini vyama vya upinzani vimekuwa vikitaka wananchi kutotii sheria.
  Alisema kilichomkuta Lema ni matunda yake mwenyewe, hivyo atambue hilo na si kuichafua UVCCM kama anavyodai.Lema juzi aliutuhumu uongozi na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Khamisi, kuwa alishiriki kumchafua kwa kusambaza picha katika mitandao ya kijamii zinazoonesha akidhalilishwa.
  Kutokana na tukio hilo, Lema alimtaka Spika wa Bunge, Anne Makinda achukue hatua kwa kuwa ushahidi wa jambo hilo upo hadharani.
Posted: 13 Nov 2013 10:53 PM PST

 Na Faida Muyomba, Geita
  Mwanamke mjamzito mkazi wa kijiji cha Nyamalembo wilayani Geita, Magdalena Kyaruzi (26) , ameuawa kikatili nyumbani kwake kwa kukatwa panga shingoni na mtu anayesadikiwa kuwa mgeni.

Mwanamke huyo alikuwa na ujauzito wa miezi minne, ambapo mumewe ni mfanyakazi wa kampuni ya Moolman, inayojishugulisha na uchimbaji dhahabu katika mgodi wa Geita (GGM).
Kamanda wa Polisi mkoani Geita , Leonard Paulo , alithibitisha kutokea kwa tukio hilo. "Ni kweli tukio hili lipo na lilitokea juzi saa 3:30 asubuhi, ambapo mtu ambaye hadi sasa hajulikani jina wala sura yake alifika nyumbani kwa mama huyu kisha kufanya ukatili huo wakati mumewe akiwa kazini,"alisema.
  Alisema muuaji huyo kabla hajafanya ukatili huo, alifika nyumbani hapo na kubisha hodi alipokaribishwa ndipo alianza kumkata mapanga sehemu ya kisogoni, kichwani na kufa papo hapo.
Alisema, mara baada ya kutimiza azma yake hiyo, muuaji huyo alitoweka na simu ya marehemu, na kuwa taarifa za kiintelijensia zinaeleza kuwa mtu huyo aliwahi kufika nyumbani hapo mwezi mmoja uliopita.
"Uchunguzi wetu wa awali umebaini kuwa mwezi mmoja uliopita wakati mumewe akiwa hayupo, alifika hapo na kufanya mazungumzo naye jambo linaloonesha kuwa walikuwa wanafahamiana," alisema.
   Alisema, jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi zaidi kubaini chanzo chake na kwamba hakuna mtuhumiwa anayeshikiliwa kutokana na mauaji hayo.
Posted: 13 Nov 2013 11:01 PM PST

 Na Esther Macha, Rungwe
  Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imewahukumu kunyongwa hadi kufa watu wawili waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya mauaji dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja.

  Watuhumiwa hao wawili ni kati ya watuhumiwa wanne waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo.
  Hukumu hiyo ilitolewa jana katika Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, iliyokuwa ikiendesha vikao vyake katika Mahakama ya Wilaya ya Rungwe chini ya Jaji Samweli Karua.
  Awali kabla ya kusomwa kwa hukumu hiyo mwendesha mashtaka wa Serikali, Archiles Mulisa, aliwataja watuhumiwa wanne kuwa ni Hakimu Mwakalinga, Daudi Mwasipasa, Obote Mwanyingili na Kelvin Myovela ambao wanatuhumiwa kumuua kwa makusudi aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, John Mwankenja.
  Alisema watuhumiwa hao waliokuwa wakikabiliwa na kesi namba 131/2012 walitenda kosa hilo Mei 19, 2011 katika Kijiji cha Mpandapanda, Kata ya Kiwira Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
  Mulisa aliyekuwa akisaidiwa na Wakili wa Serikali Lugano Mwakilasa kwa upande wa mashtaka huku watuhumiwa wakitetewa na mawakili wawili ambao ni Victor Mkumbe na Simon Mwakolo.
  Alisema katika kutetea hoja zao upande wa mashtaka ulileta mashahidi 11 ambao wote kwa pamoja wakiongozwa na shahidi namba moja waliwatuhumu washtakiwa kuhusika na tukio hilo.
  Jaji Karua alisema pamoja na ushauri wa wazee wa baraza la mahakama ambao pia wanawatuhumu washtakiwa hao kuhusika na tukio hilo naye alikubaliana nao lakini siyo kwa watuhumiwa wote.
  Waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa ni Hakimu Mwakalinga na Daudi Mwasipasa, huku wengine wakihukumiwa adhabu ya kwenda jela miaka saba. Mtuhumiwa huyo ni Mwanyingili ambaye alipatikana na kosa la kumhifadhi mtuhumiwa aliyehusika kufanya mauaji hayo.
  Kwa upande wa mtuhumiwa Myovela alitiwa hatiani kutokana na kuhifadhi silaha iliyotumika katika mauaji hayo ingawa hakuhusika na kitendo hicho moja kwa moja.
  Alisema kutokana kosa hilo mtuhumiwa huyo atatumikia kifungo jela miaka saba ingawa pia tayari alikuwa amehukumiwa kifungo jela cha miaka 20 kwa kosa la kukutwa na silaha kinyume cha sheria.
Posted: 13 Nov 2013 11:05 PM PST

 Na Elizabeth Mayemba
  Uongozi wa klabu ya Simba umesema kuwa usajili wake katika kipindi hiki cha dirisha dogo watafanya kimyakimya kwa ajili ya kukwepa hujuma, kwani kuna klabu zinasubiri klabu hiyo itangaze nia ya kusajili mchezaji fulani ili wavuruge.

Akizungumza na gazeti hili jana mmoja wa wajumbe wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba ambaye hakutaka kuandikwa jina lake gazetini, alisema watamtangaza mchezaji pale tu watakapoingia naye mkataba.
"Sisi hatusajili kwa kutangaza nia, tutakapomhitaji mchezaji fulani tutakubaliana naye na kuingia naye mkataba ndipo tutakapomtangaza rasmi katika vyombo vya habari," alisema Mjumbe huyo.
Alisema kuna klabu zinasubiri kuona Simba inamnyatia mchezaji gani ili nao waingilie kati, lakini kwa staili hiyo safari hii hawawapati na badala yake watasikia tu washamsainisha mchezaji wanayemtaka.
  Mjumbe huyo alisema timu yao inamapungufu katika kila idara, hivyo watatafuta wachezaji ambao wataondoa tatizo hilo kwa lengo la timu yao kutwaa ubingwa msimu huu tofauti na watu wanavyofikiria.
  Alisema kuwa inashangaza kuona baadhi ya watendaji ndani ya Simba wanathubutu kusema kuwa Simba haichukui ubingwa, hali ambayo inaonesha ni kuwakatisha wachezaji tamaa na wakati nafasi waliyonayo wana nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa huo.
  Kiongozi huyo alisema kwa sasa mengi yatasemwa kuhusu timu yao, lakini wao wanaamini kwamba ubingwa watauchukua na wale wanaotamba mapema kabla ya mzunguko wa pili haujaanza wataishia kuumbuka.
  Simba wamemaliza ligi hiyo wakiwa na pointi 24 na kushika nafasi ya nne, huku vinara wa ligi hiyo wakiwa Yanga wenye pointi 28 ikifuatia Azam FC wenye pointi 27 sawa na Mbeya City
Posted: 13 Nov 2013 11:20 PM PST

  Timu ya Future Taifa Stars jana imewaadhiri Taifa Stars katika mechi ya kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Karume Dar es Salaam, anaripoti Fatuma Rashid .

  Mechi hiyo ni maalumu kwa Kocha Mkuu wa Stars, Kim Poulsen kwa ajili ya kuchagua wachezaji wengine 10 watakaoungana na timu hiyo ambayo itakwenda jijini Arusha kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Kenya 'Harambee Stars', ambayo ipo kwenye kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (F IFA).
  Katika mchezo huo Future ndiyo walioanza kupata bao dakika ya 40 kupitia kwa mchezaji wao Elias Mguli baada ya kutumia udhaifu wa beki wa Stars,Kelvin Yondan.
  Katika mechi hiyo Future walionekana kuutawala mchezo zaidi na kukosa nafasi nyingi za kufunga , ambapo dakika ya 26, Ramadhani Singano 'Messi'aliachia shuti kali lililotoka nje ya lango.
 Taifa Stars ilionekana kupotea na kutokana na kasi ya vijana wa Future kufanya mashambulizi mfululizo huku kiungo wake, Salum Abubakari akipoteza mipira mingi na kuwafanya Future kuendelea kutawala mchezo huo.
  Dakika ya 31 Taifa Stars ilizinduka na kufanya shambulizi kali langoni mwa Future lakini shuti la beki wake Erasto Nyoni liliokolewa na mabeki wa Future Taifa Stars. 
  Kipindi cha pili timu zote ziliingia uwanjani zikiwa na uchu wa kutak a kufunga mabao lakini mabeki wa pande zote walikaa imara ya kuon doa hatari zote zilizoelekezwa langoni.

No comments:

Post a Comment