| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:10 AM PST 
 
  
  
 
- ALIKUWA KWENYE MATIBABU AFRIKA KUSINI
 
- NCCR- MAGEUZI KUZUNGUMZIA MSIBA  
 
 
Aliyekuwa
 Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Sengondo Mvungi, amefariki
 dunia jana alasiri nchini Afrika Kusini, katika Hospitali ya Milpark, 
Johannesburg. 
   
Dkt.
 Mvungi ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha 
NCCR-Mageuzi na Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria Chuo Kikuu cha Bagamoyo 
(UB), alipelekwa nchini humo baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa usiku wa 
kuamkia Novemba 3 mwwaka huu akiwa nyumbani kwake, Kimbamba Msakuzi.  
 
Chama
 cha NCCR-Mageuzi, kimethibitisha juu ya kifo hicho na kuongeza kuwa, 
taarifa kamili zitatolewa leo Makao Makuu ya chama yaliyopo Ilala, 
kuanzia saa tatu asubuhi.  
 
Mtoa
 habari hizo ndani ya chama ambaye hakutaka jina lake liandikwe 
gazetini, alisema marehemu Dkt. Mvungi alikuwa kiongozi mkubwa ndani ya 
chama na ametumia fursa hiyo kukifanya chama hicho kiwe na wanachama 
wengi.  
 
Dkt.
 Mvungi baada ya kujeruhiwa kwa mapanga, alikimbizwa katika Hospitali ya
 Rufaa Tumbi, iliyopo Kibaha, mkoani Pwani na baadaye kuhamishiwa katika
 Hospitali ya Taifa Muhimbili, Kitengo cha Wagonjwa Wanaohitaji 
Uangalizi Maalumu (ICU).  
 
Kutokana
 na hali yake kutoimarika vizuri akiwa hospitalini hapo, Novemba 7 mwaka
 huu, Dkt. Mvungi alisafirishwa kwa ndege ya kukodi ya Shirika la Ndege 
la Flightlink, kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi hadi mauti 
yalipomkuta wakati madaktari wakiendelea kuokoa maisha yake.  
 
Msemaji
 wa Kitengo cha Taasisi ya Mifupa (MOI), Bw. Jumaa Almas, alisema 
walilazimika kumsafirisha Dkt. Mvungi kutokana na afya yake kutoimarika 
vizuri.  
 
Dkt.
 Mvungi alipata majeraha makubwa kichwani ambapio katika msafara wake, 
aliongozana na Daktari Bingwa wa Upasuaji Ubongo na Mishipa ya Fahamu 
Dkt. Clement Mugisha na Muuguzi, Bi. Juliana Moshi.  
 
Juzi
 Jeshi la Polisi nchini kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. 
Emmanuel Nchimbi, alisema watu tisa ambao walihusika kumpiga, kumjeruhi 
na kuiba vitu mbalimbali vya marehemu Dkt. Mvungi, tayari wamekamatwa.  
 
Dkt.
 Nchimbi alisema watu hao walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya Dar es
 Salaam kwa nyakati tofauti ambapo awali walikamatwa sita na juzi 
kufikia tisa.  
 
Kamanda
 wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, 
ambaye alikuwepo katika mkutano huo, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni 
Msigwa Mpopela (30), Shabago Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu 
'Hatibu'.  
 
Wengine
 ni Zakaria Raphael (dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa, Juma Hamisi, 
Longisho Semeriko (muuza ugolo), Paul Jeirosi na mwingine aliyemtaja kwa
 jina moja la Kilimimazoka, ambao wote ni wakazi wa Dar es Salaam  
 
"Watuhumiwa
 hawa walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vimethibitika kuwa vilitumika
 katika tukio hilo, pia walikutwa na simu ya mkononi mali ya Dkt. 
Mvungi," alisema.  
 
Kamishna
 Kova alisema, katika mahojiano ya awali na watuhumiwa, walikiri 
kuhusika na tukio hilo na ushahidi umekamilika kwa asilimia 80. 
 
"Watuhumiwa wote wamekiri kosa hivyo tunakamilisha upelelezi ili wafikishwe mahakamani mara moja," alisema.  
 
Marehemu Dkt. Mvungi, aliwahi kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2005 kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi 
  
 
   
   
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:16 AM PST 
  
 
-  ACHAFULIWA MTANDAONI, AITUHUMU UVCCM TAIFA
 
 
Queen Lema, Arusha na Mariam Mziwanda, Dar  
 
  Katika
 hali isiyo ya kawaida, Mbunge wa Arusha Mjini, Bw. Godbless Lema, 
ameutuhumu uongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), 
Taifa kwa mada ya kusambaza picha zinazoonesha akiingiliwa kinyume na 
maumbile katika mitandao ya kijamii.  
  
  Mbali
 ya uongozi huo, Bw. Lema pia alimtuhumu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Bw. 
Sadifa Juma Khamis, kwa kushiriki kumchafua hivyo amemtaka Spika wa 
Bunge, Bi. Anne Makinda, achukue hatua na kudai ushahidi wa jambo hilo 
upo hadharani.  
 
  Bw.
 Lema aliyasema hayo Mjini Arusha jana alipokutana na waandishi wa 
habari ili kuzungumzia jambo hilo na kusisitiza kuwa, suala hilo 
limemsikitisha sana. “Ushahidi wa namba za simu zilizohusika kusambaza 
picha hizo upo, Khamis (Mwakilishi Jimbo la Donge, Zanzibar), anahusika 
na udhalilishaji uliofanywa na vijana wa UVCCM Taifa,” alisema Bw. Lema.
  
 
  Alisema
 picha hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii na watumiaji wa simu
 za mkononi zikiwa na ujumbe unaodai Lema akilawitiwa na wanaume 
wenzake.Aliongeza kuwa, Oktoba 29 mwaka huu, mkewe aliyemtaja kwa jina 
la Bi. Neema Lema, alipata picha hizo zilizotumwa moja kwa moja katika 
simu yake zikiwa na ujumbe usemao “Hiyo ndiyo kazi anayoifanya mume 
wako”.  
 
   Bw.
 Lema alisema, suala hilo halikuishia hapo kwani picha hizo zilitumwa 
kwa mama mkwe wake na kusababisha familia ya mke wake na wazazi wake 
kukosa amani “Mke wangu alitumiwa picha hizi katika mtandao wa WhatsApp 
na baadaye ilisambazwa zaidi hadi kwa wapigakura wangu jimboni na kudai 
ndiyo kazi inayofanywa na Mbunge wao,” alisema.  
 
  Aliongeza
 kuwa, uchafu huo ulikuwa ukifanyika wakati akiwa bungeni Dodoma ambapo 
Bw. Khamis, alionekana akisambaza picha hizo kutoka kwenye kompyuta yake
 (mpakato), kuwapa wabunge jambo ambalo lilichangia amani ya bunge 
kuharibika siku hiyo.  
 
 “Wakati
 picha hizi zikisambazwa, nilijulishwa suala hili na wabunge wanawake wa
 CCM, ilibidi niende kwa Spika ambaye alikiri picha hizo zimesababisha 
akose morali ya kuendesha vikao. “Pia nilizungumza na uongozi wa Bunge 
nikilalamikia kudhalilishwa kwa kutengenezewa picha zinazoonesha 
nikiingiliwa na wanaume wenzangu... Spika aliahidi kulishughulikia,” 
alisema Bw. Lema.  
 
  Bw.
 Lema alisema, kutokana na picha hizo, bado hazimnyimi kinga ya 
kuendelea kusema ukweli juu ya jambo lolote badala yake ataendelea 
kupambana ili kuwatetea wanyonge.“Kamwe siwezi kuwatafuta waliotengeneza
 picha hizi na kuzisambaza kwenye mitandao na simu za watu bali 
atawasaidia viongozi wa UVCCM kuzisambaza kwenye Makanisa, Misikiti, 
mikutano ya hadhara ili kuwaonesha wananchi ukatili dhidi yake 
unavyozidi kushika kasi asiwe na sauti ndani ya nchi,” alisema.  
 
  Wakati huo huo,
 Mke wa Mbunge huyo, Bi. Neema, alisema hicho ni kitu kidogo sana dhidi 
ya mumewe na waliofanya vitendo hivyo walilenga kuvunja ndo yake lakini 
haitatokea. Sadifa azungumza  
 
  Akijibu
 tuhuma hizo akiwa njiani kwenda nchini Ethiopia, Bw. Khamis alisema 
jumuiya hiyo au yeye mwenyewe hawezi kutumia cheo chake kufanya vitendo 
hivyo.  
 
  “Mimi
 na Mheshimiwa Lema wote ni wabunge, tofauti yetu ipo katika vyama na 
majimbo...tomefahamiana bungeni na wala simjui kwa undani, tuhuma dhidi 
yangu si za kweli kwani siwezi kufanya kitendo hicho ambacho si cha 
kibinadamu hata kama tuna tofauti za kisiasa.  
 
 “Mimi
 ni Muislamu na dini yangu hairuhusu kufanya hivyo, binafsi sijui 
kutumia kompyuta na Mheshimiwa Lema analijua hilo...hivi sasa Ofisi ya 
Bunge imeanza kutoa mafunzo kwa wabunge wasiojua kutumia kompyuta, nami 
najifunza,” alisema.  
 
  Alisema
 simu anazomiliki ni mbili, moja ni Nokia ya tochi na nyingine ya 
kichina yenye laini tatu na hajui kama simu hizo zina mitandao na 
hajawahi kujaribu.Bw. Khamis aliongeza kuwa, hulka yake hayupo karibu na
 makundi yanayoweza kumuingiza au kumshawishi afanye vitendo hivyo hivyo
 yupo tayari kukutana na Bw. Lema kwa amani ili wazungumze na kuwasaka 
waliofanya vitendo hivyo ambavyo si vya kistaarabu.  
 
“Mheshimiwa
 Lema akinitafuta nitampa ushirikiano, ninachokijua mimi, mwenzangu 
ananitafutia umaarufu kwa sababu pamoja na vyeo nilivyonavyo bado 
sifahamiki sana.  
 
  “Natumia
 cheo changu ndani ya UVCCM kuijenga jumuiya na CCM... kwanza namuomba 
radhi kwa sababu tayari ana imani potofu dhidi yangu, pili namshauri 
afanye utafiti,” alisema.  
 
Alisema
 imani yake ni kwamba, tofauti zao kisiasa haziwezi kumshawishi afanye 
vitendo hivyo kwani ipo siku Bw. Lema anaweza kurudi CCM na kufanya naye
 kazi pamoja.  
 
  Aliongeza
 kuwa, umefika wakati wa Bw. Lema kukumbuka kuwa, tofauti za kisiasa 
zilizopo ndani ya chama chao pia zinaweza kutumika kumchafua katika 
mitandao 
 
  
     
   
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:25 AM PST 
  
 Rais Jakaya Kikwete, amerudisha zawadi ya dhahabu safi gramu 227 aliyopewa  na Kampuni ya Nyamigogo Grand Vezir Holdings ya mkoani Geita na kutaka itumike kuwasaidia watoto yatima, anaripoti Mwandishi Wetu 
. Zawadi
 hiyo alikabidhiwa juzi katika sherehe ya uzinduzi wa Mgodi wa Uchenjuaj
 iDhahabu wa kampuni hiyo uliopo nje kidogo ya Mji mdogo wa Kharuma 
ambako ndiko Makao Makuu ya Wilaya Mpya  ya Nyang’hwale,mkoani humo.  
 
 
 Dhahabu hiyo ina thamani ya sh. milioni 16 kwa bei ya sasa katika soko 
la dhahabu duniani ambapo baada ya kukabidhiwa, Rais Kikwete aliuliza; 
“Sasa nifanye nini na zawadi hii, naomba kuirudisha hii dhahabu muiuze 
popote, fedha ambayo itapatikana tutawapa watoto yatima,” alisema.  
 
 
 Akizungumza na wananchi katika mgodi huo, Rais Kikwete aliupongeza 
uongozi wa mgodi na kusema umeongeza thamani ya dhahabu na ya maisha ya 
wananchi katika eneo hilo.Aliushauri
 uongozi wa mgodi huo, kufanya jitihada za kuboresha teknolojia 
inayotumika. “Mgodi huu ni mradi wa maana sana kwani umeongeza thamani 
ya dhahabu na kuboresha maisha ya wananchi katika eneo hili, ubunifu huu
 unastahili pongezi.   
 
 “Lazima tuboreshe teknolojia, ile inayotumika katika mgodi huu ni ya 
zamani kidogo, hii ni sawa na hadithi ya mtu mwenye chongo katika jamii 
ya vipofu watupu, yeye anaonekana kama mfalme,” alisema Rais Kikwete.  
 
 
 Mgodi wa Nyamigogo ni wa marudio kwa maana ya kuzalisha dhahabu 
kutokana na mchanga ambao awali ulifukuliwa ili kutoa dhahabu na 
ulianzishwa mwaka 2011 ambapo hadi sasa, sh. bilioni 1.6 zimewekezwa 
katika uendelezaji wa mgodi huo.  
 
 
 Katika risala ya uongozi wa mgodi huo, ilisema mgodi huo unazalisha 
kati ya gramu 500 na 600 kwa mwezi na umeajiri watu 45 wakiwemo wanawake
 10.Tangu
 kuanzishwa kwake, umekuwa unaunga mkono shughuli za jamii inayouzunguka
 kwa kujenga zahanati na madarasa ya shule katika vijiji viwili.   
 
 Rais Kikwete amezindua mgodi huo kama sehemu ya kukagua na kuzindua 
miradi ya maendeleo akiwa katika ziara yake rasmi ya kikazi mkoani humo 
ambao ni miongoni mwa mikoa minne aliyoianzisha mwaka 2012.  
 
 
 Ziara hiyo imemalizika jana kwa kupokea ripoti ya maendeleo ya Wilaya 
ya Nyang’hwale na kuhutubia wananchi katika mkutano wa hadhara 
uliofanyika katika Mji Mdogo wa Kharuma 
 
  
 
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:29 AM PST 
 
 Frank Monyo na Daniel Samson  
 
  Naibu
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 
(TAMISEMI), Zuberi Samatabe, amewahimiza walimu wa shule za msingi 
kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kujisomea vitabu ili kuongeza uelewa 
katika masomo yao. 
 
Aliyasema
 hayo katika uzinduzi wa tovuti ya kufuatilia mgawo wa vitabu vya chenji
 ya Rada uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.  
 
Lengo
 la tovuti hiyo ya www. pesptz.org ni kutoa taarifa kwa wadau wa elimu 
pamoja na wanafunzi juu ya vitabu vinavyosambazwa katika shule za msingi
 kwa kutumia chenji hiyo.  
 
Alisema,
 Serikali ya Uingereza iliamuru fedha zilizotumika vibaya katika 
manunuzi ya Rada zirudishwe kwa Watanzania na zitumike katika manunuzi 
ya vitabu na madawati kwa shule za msingi.  
 
"Fedha
 za chenji ya Rada sh. bilioni 72 zilizorudishwa ziliingizwa katika 
mpango wa manunuzi ya vitabu na madawati katika shule za msingi na 
asilimia 75 zimetumika katika manunuzi ya vitabu vya wanafunzi na vya 
mwongozo wa walimu kufundishia," alisema Samatabe.  
 
  Kwa
 upande wake Meneja Takwimu wa Kampuni ya Data vision International, 
William Kihula alisema Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kupitia Shirika la 
Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza (DFID) iliwapa jukumu la kutengeneza
 tovuti kufuatilia mgao wa vitabu vya chenji ya Rada, ili kuwezesha 
ushirikishwaji wa wadau wa elimu na wananchi katika kufuatilia 
usambazaji wa vitabu shuleni.  
 
  Alisema
 hatua hii itawezesha serikali kuendelea kutembelea katika maeneo yake 
na kuwa na uendeshaji wa uwazi ndio maana wamejenga mfumo huu katika 
namna ambayo itaweza kutumika na wizara hata baada ya mradi huo wa mgawo
 wa vitabu vya chenji ya rada kuisha.  
 
"Tovuti
 hiyo ndio pekee inayoweka mtandaoni majina yote ya shule za hapa nchini
 wilaya na mikoa iliyopo hii itatoa mwanga wa kuanzia katika ufuatiliaji
 wa maendeleo ya mwanafunzi mmoja mmoja," alisema Kihula.  
 
  Aliongeza
 kuwa, kuwepo kwa jitihada za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi 
kuanza kutumia mfumo mpya wa kupima ufaulu wa wanafunzi kwa kuhusisha 
"Continous Assessment" kwa kuanza na shule za sekondari.  
 
  "Katika
 hili Datavision tupo kwenye hatua za mwisho za kutengeneza mfumo wa 
teknolojia itakayowezesha kupatikana na kutunza taarifa za maendeleo ya 
mwanafunzi shuleni kwa wakati," alisema Kihula. 
  
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:32 AM PST 
  
 Penina Malundo na Maua Mashu  
 
  Wafanyakazi
 wakiwemo vibarua zaidi ya 200 wa Kampuni ya STRABAG inayojenga barabara
 ya mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam wamegoma.  
  
Mgomo
 huo ulianza jana jijini humo kwa madai ya kutaka kulipwa stahiki zao za
 zamani kabla ya kampuni hiyo kuingia mkataba na kampuni nyingine.  
 
Wakizungumza
 kwa nyakati tofauti jana na waandishi wa habari, wafanyakazi wa kampuni
 hiyo walisema kuwa, wameingia katika kampuni hiyo kwa sheria zote na 
wengi wao wameweza kufanya kazi zaidi ya mwaka mmoja, hivyo wanapaswa 
kulipwa madai yao kabla ya kuvunja mkataba na Kampuni ya STRABAG.  
 
Walisema
 kuwa, mgogoro mkubwa uliibuka kati ya vibarua hao na kampuni iliyoingia
 mkataba na Strabag ijulikanayo kama Laba Constractors juu ya malipo 
watakayolipwa kuwa madogo tofauti na malipo ya Kampuni ya Strabag.  
 
"Jumamosi
 tulikaa kikao na viongozi wa Laba Constractors wakatueleza kuwa kuanzia
 siku ya Jumatatu (juzi), malipo yetu yatakuwa chini yao, kwani 
wameingia mkataba na Kampuni ya Strabag kwa ajili ya kulipa wafanyakazi 
wake na vibarua, jambo la kushangaza sisi hatujapata taarifa yoyote 
kutoka kwa Strabag juu ya mkataba huo walioingia na Kampuni ya Laba 
Constractors," alisema mmoja wa vibarua hao ambaye hakutaka kutaja jina 
lake.  
 
Alisema
 kuwa, Kampuni ya Strabag ingefanya utaratibu maalumu wa kumaliza madai 
yote ya msingi kwa vibarua wake na hapo ndipo wangeweza kuanza kuingia 
mkataba na kampuni nyingine.  
 
"Mpaka
 sasa hatujui hatma yetu, sisi tumekaa hapa toka saa 12 asubuhi na 
tutaendelea kukaa mpaka kieleweke hadi tupatiwe haki yetu, malipo yetu 
tupewe ndiyo kampuni nyingine ianze upya na sisi, kwani tumeshakaa zaidi
 ya mwaka mmoja, kisheria sisi tayari ni wafanyakazi halali," alisema.  
 
Naye
 Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi katika Kampuni ya STRABAG (TAMICO),
 Abdullah Rukusa alisema kuwa, Kampuni ya Strabag ilikuwa inawalipa 
vibarua hao malipo ya sh. 12,500 kwa siku huku malipo ya posho yakiwa 
sh. 4,800 kwa saa za ziada.  
 
Alisema
 kuwa, Kampuni ya Laba Contractors inataka kuwalipa vibarua hao kiasi 
cha sh.10,000 kwa siku hali itakayofanya kampuni hiyo kuwanyonya 
wafanyakazi hao pindi wanapoanza kazi saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni.  
 
Kwa
 upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Laba Contractors, Emanuel 
Mshana alisema kuwa, mkataba kati yao na Kampuni ya Strabag ulisainiwa 
Jumamosi iliyopita na kazi rasmi ilianza kufanyika juzi huku tayari 
akidai wamekutana na wafanyakazi hao kwa mazungumzo.  
 
Alisema
 kuwa, vibarua 95 waliopewa na Kampuni ya Strabag kati yao 45 ndio 
walioanza kufanya kazi nao juzi na kampuni yao kuongeza vibarua 28 kwa 
siku, kwa ajili ya kufanya kazi.  
 Juhudi
 za kumtafuta Mkurugenzi wa Kampuni ya Strabag ziligonga mwamba baada ya
 kugoma kuzungumza na waandishi wa habari huku geti likizuiliwa na mawe 
makubwa ya barabaran  
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:39 AM PST 
  
 Na Grace Ndossa  
 
   Mkurugenzi
 Mkuu wa Shirika la Nyumba (NHC), Nehemia Mchechu ametunukiwa tuzo ya 
uongozi bora pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake mkubwa katika 
jamii na ndani ya shirika hilo.  
  
  Tuzo
 hiyo ilikabidhiwa jana jijini Dar es Salaam na Rais wa Rotary Klabu ya 
Mzizima, Ambrose Nshala ambapo alieleza kuwa Mkurugenzi huyo amekuwa 
kiongozi bora na amethubutu kufanya kazi kwa ujasiri na kuonesha ndoto 
za kufika mbali.  
 
  Alisema
 kuwa, Mkurugenzi huyo ni kijana mdogo, lakini ameonesha uthubutu wake 
katika kufanya kazi na mageuzi ndani ya shirika, hali ambayo imeonesha 
hatua kubwa kiuchumi na kazi anazofanya zitalifikisha mbali shirika.  
 
  Alisema
 kuwa, Rotary klabu inathamini mchango wake na kutambua kazi aliyofanya 
kwa jamii kwani ni kubwa hivyo wametoa tuzo hiyo na cheti kwa ajili ya 
kuongeza hamasa kwa viongozi wengine kuiga mfano wa mkurugenzi huyo ili 
nchi iweze kupata maendeleo.  
 
  Kwa
 upande wake, Mchechu alisema kuwa, tuzo hiyo itasaidia kuongeza hamasa 
zaidi katika kufanya kazi ili nchi iweze kupata maendeleo.  
 
  Alisema
 kuwa, sera za Tanzania ni nzuri ila tatizo liko kwenye utekelezaji 
kwani viongozi wengi wanathamini maneno kuliko vitendo, hivyo ndiyo 
vinavyofanya mambo mengi kukwama.  
 
  Pia
 alisema, sera nyingi hapa nchini nyingi huishia kwenye karatasi na nchi
 nyingi huiga sera za Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali 
ndiyo maana zimepiga hatua 
  
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:36 AM PST 
  
 Na Mwandishi Wetu  
 
  Imeelezwa
 kuwa kuanzishwa kwa kampuni huru za minara ya mawasiliano ya simu, 
kunaweza kupunguza gharama za uendeshaji kwa kampuni za simu za mkononi 
nchini, hivyo kuweza kusaidia kuleta ahueni kwa watumiaji wa simu hizo.  
  
Kabla
 ya hapo kampuni zote za simu za mkononi nchini kila moja ililazimika 
kujenga mnara wake ambao unahitaji kiasi kikubwa cha uwekezaji ikiwa ni 
pamoja na matumizi ya jenereta, ulinzi na gharama nyingine za 
uendeshaji.  
 
Hayo
 yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya 
Helios Towers, Michael Magambo wakati akizungumza na waandishi wa habari
 jijini Dar es   Salaam.  
 
"Hapo
 ndipo kampuni huru za minara zinapoingia. Humiliki, husimamia na 
huendesha minara, inayoweza kutumiwa na kampuni nyingi za simu kwa 
wakati mmoja na pia hata matangazo ya Tv, redio na mawakala wa hali ya 
hewa," alisema.  
 
  Alisema,
 matumizi ya mnara mmoja huondoa mzigo wa gharama za uwekezaji wa 
miondominu pamoja na shughuli nyingine kwenye eneo la mnara.  
 
  Pia
 alisema, kampuni za simu zinapata nafasi ya kuelekeza nguvu zaidi 
katika eneo wanaloliweza zaidi kutoa huduma za sauti na 'data' kwa 
Watanzania.  
 
 "Wengi
 hawaufahamu mchango wetu katika kupanua huduma za simu Tanzania na 
Afrika kwa ujumla. Helios Towers ni kampuni kubwa ya minara huru nchini,
 ikiwa imejenga zaidi ya minara 1,000 ya Tigo Tanzania mwaka 2010, kisha
 ikajenga minara mingine 250 na inatarajia kuongeza mingine 150 ifikapo 
Desemba mwaka huu," alisema Magambo.  
 
  Aidha,
 alisema kwa miaka miwili iliyopita, maeneo ya Helios yanayotumiwa kwa 
pamoja na kampuni za simu ni asilimia 53 kwa sasa na ni asilimia 60 ya 
maeneo mapya kwa nchi nzima huku ikisubiri uthibitisho wa serikali wa 
kuchukua minara ya Vodacom Tanzania.  
 
"Tumekuwa tukisikia wakosoaji wakidai kwamba, kampuni kama Helios hayana ushindani kwa kuwa yamekamata soko kubwa.  
 
  "Hii
 si kweli. Uhakika ni kwamba Helios imekuwa chachu ya kuwapo kwa 
ushindani kwenye soko la huduma za simu, ikiruhusu wageni kuingia kwenye
 soko na kuwapa nafasi watoa huduma kupeleka vijijini bila wasiwasi.  
 
  "Mwishowe
 ni walaji ndio hufaidika zaidi kwa kupunguziwa bei za simu na kuchagua 
mtandao wanaoutaka. Ukweli ni kwamba tunafungua zaidi soko," aliongeza 
Magambo.  
 
  Hata
 hivyo, katika kupunguza changamoto za kupeleka huduma maeneo ya 
vijijini yasiyo na huduma za simu, awali Serikali ilitoa gari 
lijulikanalo kama Universal Communication Action Fund (UCAF) 
linalosaidia kupunguza gharama na kuwahamasisha watoa huduma kwenda 
kwenye soko la vijijini.  
 
  Hatua
 hiyo ilitokana na Sheria ya Upatikanaji wa Mawasiliano ya mwaka 2006 
yenye lengo la kukuza maendeleo ya kijamii na uchumi mijini na vijijini 
kupitia TEKNOHAMA.Mbali na hayo Kampuni ya Helios iko mbioni kuweka 
mitambo 27 chini ya UCAF 
   
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:42 AM PST 
  
 Na Mwandishi Wetu  
 
  Kampuni
 ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imeamua kupambana na changamoto 
zinazoikabili sekta ya elimu nchini kwa kuzisaidia shule mbalimbali za 
sekondari kupata miundombinu ya kufundishia na vifaa vya kujifunzia. 
   
  Pia
 kampuni hiyo kupitia mradi wake wa Shule Yetu imewanufaisha wanafunzi 
wa Shule ya Sekondari Chalinze iliyopo mkoani Pwani baada ya kukabidhi 
vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya sh. milioni tano kwa 
shule hiyo.  
 
  Akizungumza
 wakati wa kukabidhi vitabu hivyo, Meneja Masoko wa Airtel Kanda ya 
Kusini na Mkoa wa Morogoro, Aminata Keita alisema vitabu hivyo 
vitatumika katika kuongeza kiwango cha uelewa na kukuza ufaulu kwa 
wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na tatizo la uhaba wa vitabu.  
 
  "Vitabu
 hivi...vitatumika kukuza ufaulu kwa wanafunzi maana wanafunzi wataweza 
kujisomea kwa urahisi na kufuatilia masomo kwa ukaribu zaidi," alisema 
Aminata.  
 
  Aliongeza
 kuwa, msaada huo wa vitabu ni sehemu ya mpango mkakati wa kuzisaidia 
shule za kata zinazolalamikiwa kufanya vibaya katika mitihani yao ya 
kitaifa.  
 
  "Tumetoa
 vitabu vya masomo ya sayansi tukijua kabisa wanafunzi wengi hushindwa 
masomo hayo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo upungufu wa zana za 
kujifunzia ila nina imani mradi huu wa Shule Yetu utaziwezesha shule za 
kata kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa," alisema Aminata.  
 
  Kwa
 upande wake mkuu wa shule hiyo, Emmanuel Kahabi alisema, upatikanaji wa
 vitabu utarahisisha kazi ya ufundishaji kwa wanafunzi na pia wanafunzi 
wataweza kuelewa kiurahisi maana zana za kufundishia zinapatikana 
  
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:49 AM PST 
  
Neema Ndugulile  
 
  Timu
 ya Mbeya City imepigwa faini ya sh. 500,000 na Bodi ya Ligi Kuu 
Tanzania (TPL Board) na kupewa onyo kali kwa timu yake ya U20 kutocheza 
mechi ya utangulizi walipocheza na Yanga. 
   
  Akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa Shirikisho la
 Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu wa 
shirikisho hilo, Boniface Wambura alisema pia Mbeya City wanatakiwa 
kulipa gharama za uharibifu, baada ya mashabiki wao kuvunja kioo cha 
basi la Yanga, baada ya gharama hizo kuthibitishwa na bodi hiyo.  
 
  "Pia
 Mbeya City imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa mashabiki wake kushambulia
 basi la wachezaji wa Tanzania Prisons, baada ya mechi dhidi yao na 
kulipa gharama za uharibifu baada ya kuthibitishwa na Bodi ya Ligi," 
alisema Wambura.  
 
  Alisema
 Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za 
mashabiki wake ilipocheza na Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani ambapo 
mwamuzi msaidizi, Hassan Zani alishambuliwa kwa mawe na kujeruhiwa 
mkononi na kichwani, tukio lililosababisha mchezo kusimama kwa dakika 
tatu.  
 
  Wambura
 alisema beki wa Coastal Union, Hamad Khamis amepigwa faini ya sh. 
500,000 kwa kumpiga kichwa kwa makusudi Kipre Tchetche wa Azam. "Kitendo
 hicho kilisababisha refa amtoe nje kwa kadi nyekundu, hivyo atakosa 
mechi tatu zinazofuata za timu yake.  
 
  "Nayo
 Simba wamepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za mashabiki 
wake wakati wa mechi dhidi ya Kagera Sugar," alisema Wambura.  
 
  Alisema
 adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa kanuni. Pia Bodi ya Ligi 
imeahirisha kufanya uamuzi wa mechi kati ya Stand United na Kanembwa JKT
 iliyochezwa Uwanja wa Kambarage, ili kukusanya taarifa zaidi. Mechi 
hiyo haikumalizika. Bodi ya Ligi itakutana tena Jumapili. 
   
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:46 AM PST 
 
Na Fatuma Rashid  
 
  Bodi  ya
 Ligi Kuu Tanzania (TPL Board), imefungia viwanja saba vilivyokuwa 
vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza
 (FDL), hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi 
za mpira wa miguu.  
  
Akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa Shirikisho la
 Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema uamuzi huo 
umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika juzi
 ambapo pamoja na mambo mengine, kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL
 katika mzunguko wa kwanza.  
 
  Alisema
 viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza, 
ili viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa
 yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji) na Uwanja wa 
CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo 
(dressing rooms) havina hadhi.  
 
  Wambura
 alisema Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea-pitch ni 
mbovu), Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha (sehemu ya kuchezea ni
 mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia kutumika 
kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea (pitch ni 
mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu).  
 
  Wambura
 ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, alisema klabu ambazo timu zake 
zinatumia viwanja hivyo zimeshataarifiwa rasmi juu ya uamuzi huo, ambapo
 ama vinatakiwa kuwasiliana na wamiliki wa viwanja hivyo, ili wafanye 
marekebisho au kutafuta viwanja vingine vya kuchezea mechi zao.  
 
  Wakati huo huo, timu
 za Taifa za Future Taifa Stars na Taifa Stars zinacheza leo. Mechi hiyo
 ya kirafiki itafanyika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam kuanzia 
saa 10 kamili jioni.  
 
  Mechi
 hiyo ni maalumu kwa Benchi la Ufundi la Taifa Stars linaloongozwa na 
Kim Poulsen, kuangalia wachezaji kumi kutoka Future Taifa Stars 
watakaoongezwa katika Taifa Stars, tayari kwa mechi ya kirafiki ya 
kimataifa itakayochezwa Novemba 19, mwaka huu jijini Arusha.  
 
  Watazamaji
 300 tu wataruhusiwa kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 5,000. 
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imeingia kambini
 jana. Miongoni mwa wachezaji wanaotarajia kuripoti ni kipa Ivo Mapunda 
wa Gor Mahia.  
 
 | 
| 
 
Posted: 13 Nov 2013 12:57 AM PST 
  
Na Fatuma Rashid  
 
  Kocha mpya wa timu ya Azam Fc anatarajiwa kutua katika kikosi hicho mapema, kabla ya wachezaji wa timu hiyo kurudi kambini.  
Akizungumza
 na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Msemaji wa timu hiyo, Jaffer 
Iddi alisema wachezaji wote wamepewa likizo ya wiki mbili, hivyo uongozi
 upo katika mchakato wa kutafuta kocha atakayerithi mikoba ya aliyekuwa 
kocha wa timu hiyo, Mwingereza Stewart John Hall.  
  
Msemaji
 huyo alisema kocha mpya atakapowasili, ndipo atakapojua ni mchezaji 
gani atataka aanze naye na yupi amalize naye, kwani yeye ndiye atakuwa 
akiufahamu uwezo wa wachezaji kuanzia mazoezini hadi katika mechi.  
  
Akizungumzia
 katika mechi ya mwisho ya mzunguko wa kwanza ya michuano ya Ligi Kuu 
Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City, Iddi alisema ilikuwa nzuri kuliko 
nyingine kwani wote walikuwa wazuri na walipigana kutafuta nafasi nzuri 
katika kumalizia mzunguko huo.  
  
  Alisema
 timu yake kwa sasa ipo mapumziko na itarudi kambini baada ya wiki 
mbili, ili kujipanga zaidi kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo na michuano
 ya kimataifa.  
  
  Aliongeza
 kuwa, katika mzunguko wa pili anaimani timu yake itakuwa vizuri zaidi 
kutokana na kuona pamoja na kupima uwezo wa kila timu shiriki za Ligi 
Kuu, ambazo uwezo wake wameshauona, hivyo anaona timu itajifunza 
kutokana na walichokiona katika mzunguko wa kwanza.  
  
  Kocha
 Hall aliwaaga wachezaji na benchi la ufundi, mara tu baada ya mchezo wa
 mwisho wa mzunguko wa kwanza dhidi ya Mbeya City uliomalizika kwa sare 
ya mabao 3-3 kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam.   
 
 | 
 
No comments:
Post a Comment