TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 20, 2013

NANI MTANI JEMBE!! KIVUMBI JUMAMOSI OKWI ATUA YANGA KUWAKABILI SIMBA


1 
Okwi katikati baada ya kuwasili JNIA akiwa na Katabaro kulia na Bin Kleb kushoto jioni hii na chini akionyesha jezi namba 25.

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
HABARI ya mjini kwa muda huu ni kwamba; mshambuliaji mpya wa Yanga, Emmanuel Anord Okwi amewasili alasiri  ya leo uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam tayari kwa kuanza kazi ya kuitumia klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.
Okwi ametia miguu Tanzania saa 9:30  kwa ndege na kulakiwa na viongozi wa Yanga ambao walikuwa na uchuku wa kupokea jembe lao la kazi.
Waandishi wa habari walikuwa na uchu wa kusikia kauli ya Okwi na ndipo muda ukafika baada ya nyota huyo kutoka nje ya uwanja wa JNIA ambapo alisema amekuja Yanga kufanya kazi.
Alipoulizwa sakata lake la usajili, Okwi alifungua mdomo wake kwa mara nyingine na kusema; “Mimi nimekuja kufanya kazi, hayo mengine hayanihusu, zipo mamlaka zinazohusika na zitajua la kufanya”.
Cha kufurahisha Okwi amewasili akiwa tayari ameshavalia jezi ya Yanga, namba 25 mgongoni.
Akizungumza uwanjani hapo, mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya Yanga, Abdallah Ahmed Bin Kleb amesema Okwi anakwenda moja kwa moja katika hoteli ya Protea kuungana na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya kesho kutwa ya Nani Mtani Jmebe dhidi ya Simba sc, uwanja wa Taifa.
Wakati Okwi akiwa amewasili, taarifa iliyopatikana kutoka mtandano wa MTNFootball.com  mchana wa leo imeeleza kuwa kaimu mkurugenzi wa mashindano wa shirikisho la soka nchini Uganda FUFA, Decolas Kiiza amethibitisha kuwa FIFA wamemruhusu Okwi kujiunga na Yanga.
“Ndiyo tuliandika barua FIFA na walisema mchezaji yuko huru kuuzwa”. Kiiza aliuambia mtandao wa MTNFootball.com.
Mapema wiki hii Mkurugenzi mkuu wa FUFA, Edgar Watson alisema wameiandika FIFA barua kuhitaji maelezo zaidi juu ya suala la Okwi.
Okwi aliuzwa na Simba katika klabu ya Etoile Du sahel ya Tunisia januari mwaka huu kwa kitita cha dola 300, 000 za kimarekani, lakini hakudumu katika klabu hiyo kwa madai ya kutolipwa haki zake na kuamua kurejea kwao Uganda.
Okwi baada ya kurejea kwao Uganda alikaa miezi sita bila kucheza na ndipo shirikisho la  kandanda la Uganda (FUFA) likasimama kidete kumpigania aruhusiwe kureja nyumbani na kujiunga na Sport Club Villa ya Uganda `Majogoo wa Kampala`  ili kulinda kiwango chake.
Kwa usajili wa Okwi, Yanga imetimiza wachezaji watano wa kigeni kwa maana ya washambuliaji Didier Kavumbagu, Khamis Friday Kiiza, beki Mbuyu Twite, kiungo Haruna Niyonzima.
Sakata la Okwi lilifikishwa FIFA na mpaka sasa Etoile Du Sahel hawajailipa Simba Sc fedha za mauzo ya mchezaji huyo.
Mchezaji huyo mwenye akili kubwa ya mpira na kasi alikuwa na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda katika michuano ya CECAFA Chellenge jijini Nairobi na kuonesha kiwango cha juu na sasa ametua Jangwani.
Yanga wamefanya usajili huo kwa lengo la kuimarisha kikosi chao kabla ya kuanza kampeni za ligi ya mabingwa barani Afrika mwakani.
Mpaka sasa wametangaza kumsajili Juma Kaseja, Hassan Dilunga na leo hii Okwi imetia nanga katika rada zao.

No comments:

Post a Comment