TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, March 24, 2016

Wafanyabiashara wa soko kuu Mkoa wa Lindi watoa malalamiko kuhusu changamoto wanazokutana nazo katika biashara zao.


sokoni
Mmoja wa wafanyabiashara hao aliyejitambulisha kwa jina la Maria Mahenge ameeleza moja ya changamoto katika soko hilo ni udogo wa Soko hilo kwani wafanyabiashara wamekuwa ni wengi na kupelekea bidhaa zao kuweka msongamano unaopelekea mzunguko wa hewa ndani ya soko hilo kuwa mdogo hivyo kupelekea bidhaa zingine kuharibika hasa ukizingatia badiliko la Tabia nchi, kwani hivi sasa kunajoto kali sana.
Kwa upande wa Ndg Shaibu Ramad Langa ambaye naye ni mfanyabiashara wa soko hilo aliweza kuelezea changamoto ambazo amekumbana nazo ameeleza kuwa mzunguko wa pesa ni mdogo hivyo kupelekea mauzo kuwa hafifu.
Aidha Makamu mwenyekiti wa soko hilo naye ameeleza kuwa soko kuu kwa sasa ni dogo kwa kuwa watu ni wengi na hawana kazi zingine za kufanya tofauti na biashara hivyo inapelekea kujazana katika soko hilo, hali hiyo inatokana na mkoa kukosa viwanda vidogo vidogo na vikubwa, hivyo inawalazimu wananchi kufurika sokoni kuja kutafuta riziki.
Pia aliweza kutoa rai kwa mamlaka husika iweze kupanua soko hilo kwani kwa sasa soko hilo ni dogo na halitoshi kwa sasa.

No comments:

Post a Comment