(Photos by Freddy Maro)
TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, October 23, 2014
President Kikwete inaugurates African Cultural Centre in Beijing
MAOFISA WA UN WAHAMASISHA WANAFUNZI WA JANGWANI KUTEKELEZA AJENDA ZA UMOJA WA MATAIFA
on October 22, 2014
Shamrashamra za maadhimisho ya miaka 69 toka Umoja wa Mataifa uanzishwe zimeanza nchini, na leo jumatano maofisa waandamizi wa UN walitembelea shule ya sekondari ya Jangwani na kuwahabarisha wanafunzi hao juu ya shughuli za Umoja wa Mataifa hapa nchini.
Mjadala kati ya maofisa hao Phillemon Mutashubirwa, Programme Manager wa UN Habitat, Usia Nkhoma Ledama, Afisa habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(UNIC), Albert Okal (ILO),Greta Sayungi (UNICEF), ulijikita katika masuala ya HIV/AIDS, EBOLA, Usafi na umuhimu wakuosha mikono ili kujikinga na maradhi, elimu ya ujasiriamali, ajira kwa vijana, kazi za kujitolea, malengo ya Milenia na malengo ya Umoja wa Mataifa kwa ujumla wake.
Ijumaa wiki hii Umoja wa Mataifa utaadhimisha mkiaka 69 toka uanzishwe na kilele cha maadhimisho hayo yatafanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Bi. Usia Nkhoma Ledama akifafanua jambo wakati akizungumza na wanafunzi wa shule yasekondari Jangwani jijini Dar. Kutoka kushoto ni Phillemon Mutashubirwa (UN Habitat), Greta Sayungi (UNICEF) pamoja na Dr Bwijo Bijo (UNDP)
=============================================
Rais Kikwete akutana na Mabalozi wa Afrika nchini China
on October 22, 2014
================================================
Shirika la ndege la Flydubai lenye makao yake makuu Dubai lazindua njia mbili mpya za ndege
on October 22, 2014
Makamu
wa Rais mwandamizi katika shughuli za kibiashara wa shirika la ndege
la FlyDubai ,Bwa.Sudhir Sreedharan akizungumza mbele ya wageni waalikwa
mbalimbali wakiwemo wana habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo
pichani) katika hafla fupi ya uzinduzi wa njia mbili mpya za shirika la
ndege hiyo kutoka Dubai kuja jijini Dar es salaam na Zanzibara (nchini
Tanzania). Bwa.Sudhir amesema kuwa shirika hilo la Flydubai liliingia
katika soko la kibiashara kuanzia mnamo mwaka 12009,ambapo mpaka sasa
wamefanikiwa kuongeza njia mpya sita (six new routes ) .
Mgeni
rasmi,Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano,Mh Samia Suluhu
akizungumza mapema leo katika uzinduzi wa njia mbili mpya za ndege ya
FlyDubai aina ya Boieng 737-800,uliofanyika katika uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini Dar.
Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo wa njia mpya ya shirika la ndege la Flydubai lenye makao yake makuu Dubai..
Wageni waalikwa wakishangilia jambo.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye tukio hilo .
========================================================
========================================================
PUSH MOBILE MEDIA LTD, PARTNERS WITH APALYA TECHNOLOGIES FOR OTT VIDEO STREAMING TECHNOLOGY
on October 22, 2014
By Our Reporter
Dar es Salaam. Tanzania’s
leading interactive mobile communications technology provider, Push
Mobile has partnered with Apalya Technologies, South Asia’s leading
technology platform provider to enhance mobile video and live TV
streaming experience in Tanzania and into other markets across the
region.
Freddie Manento, Push Mobile
Managing Director, speaking at the signing ceremony held at Push Mobile
offices said the partnership serves to cement Push’s vision and mission
of being the mobile communications market leader in East Africa and the
international sphere and a provider of high quality products and
services.
“Our partnership with Apalya
Technologies is in line with our strategy to expand our video and Live
TV streaming technology to new markets around the region and they are
the right technology partners to take us there.” said Manento.
On his part Rishabh Gunjal,
Apalya Technologies’ AVP – International Business said “Apalya
Technologies is excited to partner with Push Mobile in their drive to
provide best-in-class mobile video solutions across East and Central
Africa. Apalya’s leadership across the emerging markets of India and
South Asia as well as their 8 year track record in working with some of
the biggest global telecom brands will be a great leverage in helping
Push Mobile serve the growing mobile market in this region.”
He said that the firm
partnership promises the best platform in terms of technology and
content offering providing an opportunity to mobile network operators to
monetize their mobile data network with best possible consumer
experience.
Television stations and
production houses can use this platform to create new revenue stream in
digital media space. Consumers will also have access to best of local
and international content at an affordable price across all video
streaming supported devices like feature phones, smart phones, tablets
and PCs.
========================================================================
NHIF NA MPANGO WA KUPELEKA MADAKTARI BINGWA MIKOANI
on October 22, 2014
Pamoja na kutekeleza mpango wa kusogeza huduma karibu na wanachama na wadau kwa maana ya kufungua ofisi mikoani, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeanzisha mpango wa kupeleka huduma za Madaktari Bingwa mikoani.
Mpango huu unawahusisha Madaktari Bingwa ambao ki-ukweli ni wachache kutoka katika hospitali zifuatazo:-
- Hospitali ya Taifa ya Muhimbili;
- Taasisi ya Mifupa MOI;
- Hospitali ya Bugando.
Madaktari hao ni mabingwa wa:-
- Magonjwa ya Moyo
- Magonjwa ya Wanawake
- Magonjwa ya Watoto
- Upasuaji na
- Mabingwa wa Dawa za Usingizi.
- LENGO LA KUANZISHA MPANGO HUO:
- Kuwapeleka Madaktari Bingwa katika mikoa yenye uhaba mkubwa wa madaktari bingwa na kuwatumia wataalamu hao wachache kitaifa;
- Kuwapunguzia wananchi gharama za usafiri kufuata huduma za madaktari bingwa katika miji mikubwa;
- Kurahisisha utaratibu wa kumwona daktari bingwa ambao wanaonwa kwa ahadi maalum;
- Kuwapa fursa ya kujifunza na kuwajengea uwezo wa kiutendaji madaktari walioko kwenye hospitali za mikoa hiyo.
Mpango wa kupeleka Madaktari Bingwa mikoani umekuwa na mafanikio makubwa kwa maana ya kuwafikia walengwa ambao wana mahitaji makubwa ya huduma za madaktari hao. Maisha ya watanzania yameokolewa kwa huduma zitolewazo na Madaktari Bingwa unaofadhiliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Mikoa ya Lindi, kigoma, Katavi na Rukwa imeshafikiwa na mpango huo na idadi ya wananchi waliopata huduma hiyo ya madakatari bingwa ni kama ifuatavyo:-
| SN | MKOA | WAGONJWA WALIOONWA | WALIOFANYIWA OPERESHENI |
| 1 | Lindi | 258 | 6 |
| 2 | Kigoma | 754 | 37 |
| 3 | Katavi | 1276 | 37 |
| 4 | Rukwa | 1410 | 18 |
| Jumla | 3,698 | 98 |
5.0 RATIBA YA MIKOA INAYOFUATA
Mikoa inayofuatiwa kupelekewa huduma hii ya madaktari bingwa ni Mara,Tabora, Manyara na Mtwara.
| MKOA | TAREHE | MAHALI HUDUMA ZITAKAPOTOLEWA |
| Mara | 3/11/2014-8/11/2014 | Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara |
| Tabora | Mipango ya maandalizi inaendelea (wanachi watajulishwa) | |
| Manyara | Mipango ya maandalizi inaendelea (wanachi watajulishwa) | |
| Mtwara | Mipango ya maandalizi inaendelea (wanachi watajulishwa) | |
- CHANGAMOTO ZA MPANGO WA KUPELEKA MADAKTARI BINGWA MIKOANI:
- Idadi ndogo ya Madaktari Bingwa ikilinganishwa na wananchi wanaohitaji huduma hizo.
- Uhaba wa vifaa tiba vya kisasa, kama vile vipimo katika hospitali za mikoa ya pembezoni na
- Uhaba wa vitendea kazi na madawa ili kufanikisha zoezi hili.
6.0 MIPANGO YA BAADAYE YA MFUKO.
Mfuko utaendelea kupeleka Madaktari Bingwa katika maeneo mbalimbali ya nchi baada ya kufanya upembuzi wa mahitaji ya huduma na utaalamu katika maeneo husika.
Kauli mbiu yetu ni “ Afya Bora Ndiyo Mambo Yote.”
======================================================================
Mahakama ya Tanzania imedhamiria kutekeleza dira yake ya haki sawa kwa wote
on October 22, 2014
Kaimu Mkurugenzi, Kurugenzi ya Usimamizi na Uendeshaji wa Mashauri kutoka Mahakama ya Tanzania Bw. John Kahyoza akiwaeleza waandishi wa (hawapo pichani) mikakati iliyoweka iliyowekwa na Mahakama ya Tanzania ili kutekeleza dira yake ya haki sawa kwa wote na kwa wakati kwa vitendo, kwa kuhakikisha inapunguza muda wa mashauri kukaa mahakamani, wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Habari wa Mahakama ya Tanzania Bi. Mary Gwera. Picha na Hassan silayo-maelezo
………………………………………………………………………………..
Na Georgina Misama-MAELEZO.
Mahakama ya Tanzania imedhamiria kutekeleza dira yake ya haki sawa kwa wote ili kuhakikisha inapunguza muda wa mashauri na rufaa kukaa Mahakamani kwa muda mrefu. Hayo yamesemwa na Afisa Habari wa Mahakama ya Tanzania Bi Mary Gwera wakati wa mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Akizitaja hatua zilizochukuliwa na Mahakama Bi Mary alisema, kuboresha bajeti ya kushughulikia mashauri kupitia mfuko wa mahakama toka bilioni 57 kwa mwaka 2012/13 mpaka bilioni 88 mwaka 2014/15, Idadi ya vikao vya Mahakama ya Rufani vimeongezeka kutoka 26 mwaka 2012 hadi 34 mwaka 2013/14. Aidha, Bi Mary alisema kuwa hatua nyingine ni pamoja na kuanzisha kitengo cha Mahakama Kuu Dar es Salaam kitakachoshughulikia masuala ya utatuzi wa mashauri kwa njia ya suluhu muafaka, pia uundwaji wa kamati ya kanuni za Mahakama itakayosaidia kutunga au kurekebisha kanuni ili kuhakikisha kuwa kanuni zinazotumika Mahakamani si chanzo cha kuchelewa mashauri Mahakamami Naye, Kaimu Mkurugenzi, Kurugenzi ya Usimamizi na Uendeshaji wa Mashauri kutoka Mahakama ya Tanzania Bw. John Kahyoza alisema kuwa Mahakama imeanza kuchukua hatua za kuimarisha ukaguzi wa shughuli za Mahakama na maadili ya watumishi kwa kuanzisha kurugenzi ya ukaguzi na maadili. Aidha, Bw Kahyoza alivitaja viwango ambavyo kila hakimu au Jaji anatakiwa kuvitimiza kwa mwaka na muda ambao mashauri yanatakiwa kuwa Mahakamani kuwa ni Mh. Jaji wa Mahakama Kuu analenga kumaliza kesi 220, Mahakimu wa Mahakama za Wilaya na Hakimu Mkazi kesi 250 na Mahakimu wa Mahakama za mwanzo kesi 260 Mahakama Kuu inatoa rai kwa Watanzania kufika Mahakamani kwa Tarehe zinazopangwa ili kuisaidia Mahakama kuhakikisha inapunguza muda wa mashauri kukaa Mahakamani.
=======================================================================
Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania imeanzisha masomo ya jioni ya diploma ya ukutubi
on October 22, 2014
Mkuu wa Kitengo cha Mipango kutoka Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Bw. Comfort Komba akiwaeleza waandishi wa habari(hawapo pichani) Kuhusu mafanikio yaliyofikiwa na Ofisi hiyo ikiwamo ujenzi wa majengo ya chuo cha ukutubi na uhifadhi wa nyaraka kilichopo Bagamoyo na uzinduzi wa maktaba za wilaya za Kibaha, Chunya, Ruangwa, Ngara, Rulenge, Masasi na Mbulu, wakati wa Mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari(MAELEZO) Bi. Georgina Misama.
………………………………………………………..
Na Hassan Silayo-MAELEZO Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania imeanzisha masomo ya jioni ya diploma ya ukutubi katika Kampasi ya Dar es Salaam katika mwaka wa masomo 2014/2015. Hatua hiyo inatokana na kuongezeka kwa maombi ya wanafunzi wanaohitaji kuendelea na masomo baada ya kuhitimu mafunzo ya cheti. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Mipango kutoka Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania Bw. Comfort Komba wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam. Comfort alisema kuwa masomo hayo kwa awali yalikuwa yakitolewa katika kampasi ya Bagamoyo lakini kutokana na kuongezeka kwa uhitaji wa masomo hayo ambapo mpaka sasa kuna wanafunzi wapya 130 “Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania imeamua kuanzisha masomo ya jioni ya diploma ya ukutubi katika Kampasi ya Dar es Salaam katika mwaka wa masomo 2014/2015 na utaratibu huu tunautekeleza kutokana na kuwepo kwa ongezeko la uhitaji wa wanafunzi” Alisema Comfort. Aidha Comfort alisema kuwa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania kwa kushirikiana na halmashauri za Wilaya na Mikoa imefanikiwa kuanzisha maktaba katika wilaya mbalimbali ikiwemo Kibaha, Chunya, Ruangwa, Ngara, Rulenge, Masasi na Mbulu. Akizungumzia kuhusu uhufadhi wa machapisho ya kitaifa, Comfort alisema kuwa Ofisi hiyo imefanikiwa kuhifadhi jumla ya vitabu 1,300,000 pamoja na majarida 950,000 tangu Bodi hiyo ilipoanzishwa katika ngazi ya Mikoa, Wilaya hadi Tarafa. Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania ni Shirika la umma lililopo chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
==============================================================
Chanjo ya ugonjwa wa Surua na Rubella Manispaa ya Ilala yavuka lengo.
on October 22, 2014
Manispaa ya Ilala imevuka lengo la kutoa chanjo ya ugonjwa wa Surua na Rubella kwa watu 468,297 ambapo awali lengo lao lilikuwa kutoa chanjo hiyo kwa watu 445,801 wakati wa wiki ya kutoa chanjo hiyo nchini. Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Manispaa ya Ilala Dkt. Willy Sangu leo jijini Dar es salaam alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya zoezi la chanjo hiyo linalofanyika nchi nzima. Dkt. Sangu alisema kuwa zoezi la kutoa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Surua na Rubella linaendelea vizuri katika Manispaa ya Ilala kama ilivyopangwa ambapo linafanyika kwa muda wa wiki moja katika kote nchini. “Ninawaomba watu wote ambao hawajajitokeza kupata chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Surua na Rubella, wafike kwenye vituo vya kutolea chanjo hiyo ili kuokoa maisha ya watoto, akina mama wajawazito, akiba baba na vijana” alisema Dkt. Sangu. Dkt. Sangu alisema kuwa idadi ya watu walioitikia wito wa kupata chanjo hiyo imekuwa kubwa katika Manispaa ya Ilala suala ambalo linawapa faraja ambapo watu wa rika zote wamejitokeza kupata huduma. Ili kutoa huduma ya chanjo kwa wakati kulingana na ratiba, Dkt. Sangu amesema kuwa imewalazimu kuongeza vituo 30 ambapo timu ya wahudumu kutoka kwenye vituo mama inatoka ili kuwafuata wananchi waliko. Awali Manispaa ya Ilala ilitenga vituo 236 vya kutoa chanjo hiyo kwa wananchi ndani ya Manispaa hiyo. Dkt. Sangu amesema kuwa mafanikio idadi kubwa hiyo ya mwitikio wa watu kupata chanjo katika manispaa ya Ilala yanatokana na sifa ya kuwa katikati ya jiji ambapo watu wengi hupata huduma mbalimbali za kijamii. Kwa upande wake Afisa Muuguzi Hospitali ya Mnazi Mmoja iliyopo Ilala Queen Lutufyo amesema kuwa mwitikio wa watu kuja kupata chanjo ni mzuri na hawajakosa wateja muda wote wakati wa kutoa huduma hiyo kituoni hapo. Aidha, katika zoezi la kutoa chanjo hiyo magonjwa ya Surua na Rubella wahudumu pia wanatoa dawa za magonjwa ya matende, mabusha, minyoo na matone ya vitamin ‘A’. Muda wa kutoa huduma hiyo ya chanjo vituoni ni kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni licha ya kwanba wakati mwingine huduma hiyo hutolewa hadi saa 1:00 usiku kulingana na idadi ya wateja waliopo katika kituo wakati huo kuanzia Oktoba 18 hadi 24 mwaka huu. Zoezi la kutoa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Surua na Rubella nchini linaongozwa na kauli mbiu inayosema “Linda, Okoa, Zuia ulemavu- Kamilisha Chanjo” na kusimamiwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ufadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Kusaidia Watoto (unicef), Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Misaada la Marekani (UNSAID) na Muungano wa watoa chanjo duniani (Gavi).
================================================================
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
on October 22, 2014
TUKIO HILO USIKU WA KUAMKIA LEO MAJIRA YA SAA 00:51 HUKO KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MKOA WA MBEYA, KATA NA TARAFA YA SISIMBA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, WANANCHI HAO WAISHIO KATIKA ENEO LA FOREST MPYA NYUMA YA HOSPITALI YA MKOA WA MBEYA WALIWAKAMATA WATU HAO WAKIWA NA VIFAA VINAVYOTUMIKA KUVUNJIA VIKIWEMO NONDO, PLAIZI PAMOJA NA MISUMARI NA NDIPO WALIAMUA KUWASHAMBULIA KWA KUWAPIGA SEHEMU MBALIMBALI ZA MIILI.
WATU HAO WALIFARIKI DUNIA WAKIWA NJIANI KUPELEKWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA NA ASKARI WA KIKOSI CHA KUZUIA NA KUPAMBANA NA UJAMBAZI CHA WILAYA YA MBEYA, JUHUDI ZA KUWATAFUTA WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI ZINAENDELEA. MIILI YA MAREHEMU IMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA UCHUNGUZI WA KITABIBU NA UTAMBUZI.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA WANANCHI KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA BADALA YAKE WAWAFIKISHE WATUHUMIWA WANAOWAKAMATA KWA TUHUMA MBALIMBALI KATIKA MAMLAKA HUSIKA KWA HATUA ZAIDI ZA KISHERIA.
KATIKA TUKIO LA PILI:
MTU MMOJA MKAZI WA KIJIJI CHA KANGAGA WILAYANI MBARALI AITWAYE FUNGO KIFANGA (50) ALIUAWA KWA KUPIGWA NA KITU KIZITO SEHEMU ZA KICHWANI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 21.10.2014 MAJIRA YA SAA 19:00 JIONI HUKO KATIKA KIJIJI CHA KANGAGA, KATA YA MAWINDI, TARAFA YA RUJEWA, WILAYA YA MBARALI, MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, CHANZO CHA MAUAJI HAYO NI UGOMVI WA ARDHI KATI YA MAREHEMU NA WATU HAO AMBAO BADO KUFAHAMIKA. AIDHA, WATU WATATU WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA MAHOJIANO ZAIDI KUHUSIANA NA TUKIO HILO AMBAO NI 1. CLEMENCE KIBIKI, (28) MKAZI WA KANGAGA 2. IMANI KIBIKI (23) MKAZI WA KANGAGA NA 3. FIDELIS KIBIKI (34) MKAZI WA KANGAGA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MBARALI KWA UCHUNGUZI WA KITABIBU.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA WANANCHI KUTATUA MIGOGORO YAO KWA NJIA YA AMANI NA UTULIVU ILI KUEPUKA MADHARA YANAYOWEZA KUEPUKIKA.
KATIKA TUKIO LA TATU:
MTU MMOJA MKAZI WA KIJIJI CHA MBIGILI WILAYA YA RUNGWE AITWAYE AMANI LIKENEME MWAKYOMA (50) ALIUAWA KWA KUKATWA NA KITU CHENYE NCHA KALI SEHEMU ZA KICHWANI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 20.10.2014 MAJIRA YA SAA 23:00 USIKU HUKO KATIKA KIJIJI CHA MBIGILI, KATA YA RWANGWA, TARAFA YA BUSOKELO, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA.
CHANZO CHA MAUAJI HAYO BADO HAKIJAFAHAMIKA, JUHUDI ZA KUWATAFUTA WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI ZINAENDELEA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA RUNGWE.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI ALIPO/WALIPO WATU WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA KWA HATUA ZAIDI ZA KISHERIA. Imesainiwa na: [BARAKAEL N. MASAKI – ACP] KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
=====================================================================
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA RAIS WA MMI BINGWA WA MASUALA YA UTAWALA NA UONGOZI KUTOKA BAHAMAS, DKT. MYLES MUNROE
on October 22, 2014
=======================================================================
SOS VILLAGES IKISHIRIKIANA NA MONTAGE INAWALETEA CHAKULA CHA HISANI
on October 22, 2014
SOS VILLAGES IKISHIRIKIANA NA MONTAGE INAWALETEA CHAKULA CHA HISANI KATIKA KAMPENI YAO YA ‘NIJALI, MCHANGO WAKO TUMAINI LA MAISHA YANGU’ KWA AJILI YA WATOTO WA SOS VILLAGES ITAKAYOFANYIKA TAREHE 24/10/2014 PALE HOTEL YA SERENA MJINI ZANZIBAR KUANZIA SAA MOJA USIKU
MGENI RASMI ATAKAWA MHESHIMIWA MAKAMU WA RAISI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DR MOHAMMED GHARIB BILAL, TICKET ZINAUZWA SHILLING LAKI MBILI ZA KITANZANIA AU SHNG MILION MBILI KWA MEZA YA WATU KUMI, PIGA SIMU NO 0756-860231 AU 0715-003355 UNAWEZA PIA CHANGIA KWA KUPITIA EASY PESA NO 0774 022270 AU TIGO PESA 0652 475847
==============================================
Chuo Kikuu Ardhi kutatua tatizo la udhibiti wa maji taka na taka ngumu
on October 22, 2014 in
INDA AZINDUA TOLEO LA JARIDA LA FIRST LINALOINADI TANZANIA
on October 21, 2014
===================================================================
Waajiriwa wapya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo watakiwa kuwa waadilifu
on October 21, 2014
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akiongea kwa msisitizo kuhusu maadili ya Utumishi wa Umma wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa waajiriwa wapya wa Wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam.
APIGWA FIMBO NA KUTEKETEZWA KWA MOTO MKOANI KATAVI
on October 21, 2014
Na Kibada Kibada-Katavi
Siku za hivi karibuni kumekuwa na matukio ya mauaji Mkoani Katavi vitendo vinavyoashiria kuwepo ukiukwaji wa sheria na kujichukulia sheria mkono kinyume na taratibu za sheria. Matukio hayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara Mkoani Katavi,mwishoni mwa wiki Mkazi wa kijiji Nsemlwa Mathias Kameme (35)mkulima aliuwawa kwa kupigwa na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha mwili wake kuchomwa moto na kuteketea kabisa. Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Kamishina Msaidizi wa Polisi Dhahiri Kidavashari anaeleza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kuwa wananchi wasiojulikana waliamua kujichukulia sheria mikononi kwa tuhuma za wizi wa ng’ombe. Kamanda Kidavashari alieleza kuwa tukio hilo lilitokea mnamo oktoba 17 majira ya saa mbili usiku kitongoji cha malebwe kijiji cha mnyamasi Kata ya Ugalla Halamsahuri ya Nsimbo Wilayani Mlele. Akaeleza kuwa siku ya oktoba 16 mwaka huu majira ya mchana marehemu aliondoka nyumbani kwake na kuelekea na kuelekea kusikojulikana na alirejea oktoba 17 majira ya saamoja mke wake aitwaye Fotonatha Raphael miaka (26)mkazi wa Nsemlwa alimuuliza marehemu unatoka wapi muda huo .marehemu alijibu kuwa yeye ni mwanamke hapaswi kumuhoji. Ilipofika majira ya saa mbili usiku wakiwa ndani wamelala walisikia vishindo vya watu wengi wakiizunguka nyumba huku wakisema MATHIAS toka nje na alipotoka nje walianza kmsahambulia huku wakimuuliza nyama ya ng’ombe aliyoiba na kuchinja ipo wapi?. Kamanda akaeleza kuwa ndipo marehemu alimuelekeza mke wake ilipo na aliifuata nyama hiyo nyuma ya nyumba na alipoileta ndipo watu hao wasiofahamika walikotoka waliendelea kumshambulia hadi kufa na kisha mwili wake kuuchoma moto na kutokomea kusikojulikana. Hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo na Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini na kuwatia nguvuni wale wote waliohusika katika mauaji hayo kisha kuwafikisha mbele ya mahakamani ili kujibu tuhuma hizo na sheria ichukue mkondo. Katika tukio jingine huko wilayani mpanda Kijiji cha Mpandandogo Tarafa ya Kabungu mtoto mwenye umri wa miaka mitano jina linahifadhiwa alinajisiwa na mtu anayejulikana kwa jina la Rashidi Mbogo (62) na kumsababishia maumivu makali, mtuhumiwa huyo yuko chini ya ulinzi wa polisi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kujibu tuhuma hizo. Katika hatua nyingine Kamanda Kidavashari ametoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkono na badala yake wajenge tabia ya kutoa taarifa za matukio katika mamlaka husika za kisheria ziweze kuchukua nafasi yake.Akashukuru wananchi wanaoendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika mapambano dhidi ya uharifu kwa kuwataka waendelee na moyo huo huo ili Mkoa uwendele kuwa salama na Taifa kwa ujumla.
===============================================================
MILIONI 16/- ZATOLEWA NA CIP TRUST UJENZI WA MADARASA
on October 21, 2014
Na Nathaniel Limu, Singida
SHIRIKA lisilo la kiserikali la Community Initiatives Promotion Trust Fund (CIP Trust), limetumia zaidi ya shilingi 16 milioni, kugharamia ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu, katika shule ya msingi Kinyamwenda kata ya Itaja.
Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa shirika la CIP Trust,Affesso Ogenga,wakati akitoa taarifa ya ujenzi huo kwenye hafla ya kukabidhi vyumba hivyo na ofisi ya walimu ambayo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi.
Alisema fedha hizo zimetolewa na serikali ya Austria kupitia asasi ya Sister Cities Singida Salzurg (SCSS).
Ogenga alisema asasi yao iliombwa na uongozi wa shule ya msingi Kinyamwenda kusaaidia kukamilisha mradi huo ambao tayari wananchi waliisha changia nguvu kazi.
Mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,akiwa amevikwa nguo na kukabidhiwa zana za ushujaa na wananchi wa kijiji cha Kinyamwenda,kwa kile kilichodaiwa kuwa ni mchapa kazi wa kupigiwa mfano katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.
“Tunatarajia kwamba baada ya uzinduzi wa majengo haya, tatizo la msongamano wa wanafunzi darasani,litakuwa limepungua kwa kiasi kikubwa.Pia walimu watakuwa na ofisi nzuri kwa ajili ya kazi zao za kila siku”,alifafanua Ogenga.
Kwa upande wake mgeni rasmi katika makabidhiano hayo,mkuu wa wilaya ya Singida,Queen Mlozi,aliwapongeza wananchi wa kijiji cha Kinyamwenda chini ya mwenyekiti wao na madiwani wa kata ya Itaja kwa kuupokea mradi huo na kuchangia nguvu kazi.
“Nitumie fursa hii kuipongeza asasi ya CIP Trust kwa msaada wao wa kuijengea shule ya msingi Kinyamwenda vyumba viwili vya madarsa na ofisi ya walimu.Hongereni sana kwa kuiunga mkono serikali katika juhudi zake za kuboresha sekta ya elimu”,alisema Mlozi.
Aidha,DC huyo aliangiza uongozi wa serikali ya kijiji kumaliza uhaba wa madawati 25 kabla ya januari mwakani.
Dc Mlozi aliendesha harambee kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa maabara ya sekondari ya kata ya Itaja na kufanikiwa kukusanya shilingi 450,000.Fedha hizo zilitumika kununulia mifuko 25 ya saruji.
============================================================
South Sudan’s SPLM warring factions ink CCM-brokered framework agreement to address conflict causes
on October 21, 2014
Factions
of the ruling party in South Sudan, the Sudan Peoples’ Liberation
Movement (SPLM), on Monday 20th October, 2014 signed a framework
agreement aimed at addressing root causes of the conflict that erupted
in mid-December and plunged the country into violent crisis.
The
signing ceremony, held at the Ngurdoto Mountain Lodge in the outskirts
of Arusha, was witnessed by the two principal rival leaders – President
Salva Kiir Mayardiit, Chairman of SPLM in government and Mr. Riek
Machar Teny, former vice president and leader of the SPLM-in-Opposition,
as well as the SPLM faction of former detainee, who also participated
in the talks.
The
Chairman of the Tanzania’s ruling party, Chama Cha Mapinduzi (CCM),
President Jakaya Kikwete, CCM Secretary General Mr Abdulrahman Kinana,
Tanzania Minister for Foreign and Internationa Relations Mr Bernad
Membe, and Former Tanzania Vice President and Prime Minister Mr John
Samwel Malecela, who chaired the talks, also witnessed the occasion.
Delegates
of the three rival groups of the South Sudanese ruling party met in
Arusha from 12th to 18th of this month to try to come up with the
framework of the intra-SPLM dialogue which is being facilitated by CCM.
However, it said the process is distinct from the peace talks which take place in Addis Ababa, Ethiopia.
“The
parties recognize that the Arusha process is essentially an intra-SPLM
dialogue and is separate and distinct from the IGAD mediated peace talks
among South Sudanese stakeholders.
“Yet
the parties are fully aware that the two processes, although separate,
are mutually interdependent and reinforcing,” partly reads a
communiqué.
It further calls for “unity of SPLM as a safeguard against fragmentation of the country along ethnic and regional fault lines.”
“Initiate
measures to stop the war, lead the government and the people of South
Sudan towards peace, stability and prosperity,” it further urges.
Both leaders expressed their commitment to the intra-party dialogue that would reunite the divided historical party.
The
document was signed by senior officials of the rival factions, namely
Daniel Awet Akot, Peter Adwok Nyaba and Pagan Amum Okech, representing
SPLM in government, SPLM-in-Opposition and SPLM former detainees,
respectively.
The governance crisis within the
SPLM gave birth to the 15 December violence which has unfortunately
plunged the country into the current national crisis or civil war.
The
intra-party dialogue provides a supplement to the peace talks in Addis
Ababa to try and address the root causes of this conflict within the
ruling party.
The
framework agreement has also recognized the need to “revitalize,
reorganize, strengthen and restore the SPLM to its vision, principles,
political direction and core values.
Analysts
say the dialogue, could provide an avenue for progress on key issues,
including deep divisions between South Sudanese party leaders, if
respected.

CCM
Chairman President Jakaya Mrisho Kikwete walks to the conference hall
with the two principal rival leaders – President Salva Kiir Mayardiit,
Chairman of SPLM in government and Mr. Riek Machar Teny, former vice
president and leader of the SPLM-in-Opposition, ready for the Monday
20th October, 2014 ready for the signing ceremony of the framework
agreement aimed at addressing root causes of the South Sudan conflict
that erupted in mid-December and plunged the country into violent
crisis.

CCM
Chairman President Jakaya Mrisho Kikwete leads to the high table the
two principal rival leaders – President Salva Kiir Mayardiit, Chairman
of SPLM in government and Mr. Riek Machar Teny former vice president and
leader of the SPLM-in-Opposition

CCM
Chairman President Jakaya Mrisho Kikwete and CCM Secretary General
Abdulrahman Kinana at the high table with President Salva Kiir
Mayardiit, Chairman of SPLM in government and Mr. Riek Machar Teny

Mr Pagan Amum Okech, representing SPLM in government, makes his opening remarks

Part of the conference hall during the ceremony

Malecela, who chaired the talks, is introduced

A
relaxed atmosphere as the CCM Chairman President Jakaya Mrisho Kikwete
and CCM Secretary General Abdulrahman Kinana engage in pep talks before
the start of the proceedings at the high table with President Salva
Kiir Mayardiit, Chairman of SPLM in government and Mr. Riek Machar Teny
as Former Tanzania Vice President and Prime Minister Mr John Samwel Malecela, who chaired the talks

A
relaxed atmosphere as the CCM Chairman President Jakaya Mrisho Kikwete
and CCM Secretary General Abdulrahman Kinana engage in pep talks at
the high table with President Salva Kiir Mayardiit, Chairman of SPLM
in government and Mr. Riek Machar Teny as Former Tanzania Vice President and Prime Minister Mr John Samwel Malecela, who chaired the talks

Mr. Pagan Amum Okiech of the SPLM-in-Opposition makes his remarks

Mr. Pagan Amum Okiech of the SPLM-in-Opposition makes his remarks

Mr Daniel Awek Okot of the SPLM-in-Government delivers his statements

Tanzania Minister for Foreign and Internationa Relations Mr Bernad Membe steers the meeting

CCM Secretary General Mr Abdulrahman Kinana makes his statements

CCM Secretary General Mr Abdulrahman Kinana addresses the delegates

CCM Secretary General Mr Abdulrahman Kinana speaks on
STATE HOUSE PHOTOS.
====================================================
NI SHIDAAAA: WAKIMBIZI WAGONJWA KUTOKA CONGO DRC WATELEKEZWA DAR ES SALAAM,WAKOSA CHAKULA WAANZA KUNYONYOKA NYWELE, SHIME WATANZANIA TUJITOKEZE KUWASAIDIA
on October 21, 2014
Mgonjwa,
Mwalihoba Nyasa, anaye sumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya titi, sasa
ameanza kunyonyoka nywele zake kwa madai ya kukokosa chakula kutokana na
kutumia dawa kali lakini hapati chakula.
Mtoto
Josephiner Obeid aliyepooza miguu ni miongoni mwa wagonjwa hao
wanaoteseka katika nyumba ya kulala wageni ya Bosco iliyopo Ilala
Mchikichini jijini Dar es Salaam kwa kukosa chakula kwa madai ya
kutelekezwa na Taasisi ya Redeso.
Mtoto
Maulid Yunus anayesumbuliwa na ugonjwa wa kukatika vidole na vidonda
miguuni ni miongoni mwa wagonjwa walio katika adha hiyo ya kukosa
chakula.
Mtoto
Lucy Angela ambaye anajisaidia kwa kutumia mpira baada ya kutobolewa
tumboni naye ni miongoni mwa wagonjwa hao wanaoteseka katika nyumba hiyo
ya wageni kwa kukosa chakula ‘hakika ukikutana na ndugu zetu hawa
unaweza kutokwa na machozi kwani inauma na kutia uchungu’
Mama huyu naye yupo katika mateso hayo, hakika inaumiza.
Watoto hawa nao hawajui cha kufanya wapo katika mateso.
| Dada huyu ambaye ni mgonjwa hana la kufanya zaidi ya kumuachia mungu. |
…………………………………………………………………………………..
Dotto Mwaibale
WAKIMBIZI zaidi ya 100
wanaokabiliwa na magonjwa mbalimbali, wametelekezwa na Taasisi ya Msaada
na Mandeleo ya Jamii (Redeso) ambayo ni wakala wa Shirika la Kuhudumia
Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), baadhi yao wameanza kunyonyoka
nywele kutokana na kukosa chakula, kwa muda wiki moja sasa.Mtandao wa www. habari za jamii.com leo ulifanikiwa kuwatembelea wakimbizi hao ambao wapo katika Hotel mbalimbali zilizopo Ilala na Kinondoni katika nyumba za wageni Eritex na Bosco ambapo wamehifadhiwa hapo wametokea Kambi ya Nyarugusu Mkoani Kigoma kwa lengo la kupatiwa matibabu katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Wakiongea kwa nyakati tofauti na mtandao huo wakimbizi hao ambao ni wagonjwa walisema wamekuwa wanateseka kwa muda sasa jambo ambalo wanaliona kuwa linahatarisha maisha yao.
Walisema pamoja na kutoa taarifa kwa wahusika ambao ni Redeso hadi sasa hawajapatiwa msaada wowote hivyo kujikuta wakinywa dawa bila kula chakula hali ambayo inawaletea madhara.
Mgonjwa, Mwalihoba Nyasa, anaye sumbuliwa na ugonjwa wa kansa titi alisema ameanza kunyonyoka nywele zake kwa madai ya kukokosa chakula kutokana na kutumia dawa kali.
“Hii si afya yangu na sikuwa hivi siwezi kubeba chochote na afya yangu imeendelea kuteteleka na nywele zangu zimeanza kunyonyoka kutokana na kukosa chakula” alisema Nyasa.
Mmoja wa wakimbizi hao alisema baadhi yao wanamagonjwa ya kansa, kupoza, ukoma na magonjwa mengine ambayo ni hatari iwapo hakutakuwa na utaratibu mzuri wa kuwapatia chakula ili dawa ziweze kufanya kazi.
Baadhi ya wakimbizi hao ambao ni wagonjwa ni Sango Nyasa (36), Josephiner Obeid (15), Kashindi Alfan (47), Andhurin Elisha (5), Muhambo Msana (7), Maulid Yunus (5), Jane Kabeza (30), Lucy Kashindi (11) na Mwalihoba Nyasa (37) ambaye anasumbuliwa na kansa ya titi.
“Jamani tunaomba msaada kwani hali zetu ni mbaya mmoja wetu ameshapoteza maisha kutokana na tatizo hilo tunaomba msaada hata kwa serikali ya Tanzania,” alisema.
Aidha alisema wanawaomba wasamaria wema wengine kujitokeza kuwasaidia msaada wa chakula kwani kwa sasa hawakopeki kutokana na kukosa fedha.
Alisema wanapaswa kupata shilingi elfu 70 kila mmoja kwa wiki kwa ajili ya chakula lakini hali hiyo imekuwa kinyume kwa takribani wiki nzima.
Mkimbizi huyo alisema iwapo hakuna juhudi ambazo zitachuliwa upo uwezekano mkubwa wakimbizi hao kupoteza maisha.
Akizungumza kuhusu jambo hilo mmoja wa maofisa wa Taasisi ya Redeso, Neema Malulu alisema yeye sio msemaji na kumtaka mwandishi awaulize UNHCR kwani wao ndio wanatoa fedha.
“Mimi sio msemaji, kazi yangu ni kuwapatia fedha wakimbizi hao baada ya kupewa na UNHCR hivyo ni vema ukawaulize wao,” alisema Malulu.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Pereira Ame Silima alisema mimi ndio nampa taarifa hizo na kudai kuwa suala hilo linawahusu UNHCR hivyo waulizwe wao.
“Upo uwezekano wa kuwepo hapa kama ulivyosema ila wanao husika na watu hao ni UNHCR nadhani itakuwa vema ukiwauliza wao kwanini hawawapatii chakula wakimbizi hao,” alisema Silima.
Jitihada za kuwapata watu wa UNHCR kwa ufafanuzi ziligonga ukuta kwani kila simu yao ilipokuwa ikipigwa walikuwa wahawapokei simu.
Ndugu zetu hawa katika kupigania maisha yao awali walikuwa wakienda kukopa vyakula katika maduka ya jirani na wanapoishi lakini baada ya kuona hawalipi wenye maduka hayo wamesitisha kuwasaidia ambapo baadhi yao wanadaiwa kuanzia shilingi 45,000 hadi 50,000.
Ndugu wasomaji wa mtandao huu wa www. habari za jamii.com kwa yeyote atakayeguswa na kupenda kuwasaidia ndugu zetu hawa ambao licha ya kuwa katika hali ya ugonjwa hasa hao watoto ambao wanapita katika kipindi kigumu kutokana na taasisi hiyo kushindwa kuwapatia chakula kwa wakati unaweza kwenda katika nyumba ya kulala wageni ya Bosco wanapo jihifadhi kwa ajili ya kupeleka chochote ulichonacho iwe matunda, nguo, unga, sabuni, mafuta ya kula na vitu vingine ambavyo utaona vinafaa kwani kutoa ni moyo na si utajiri. Okoa maisha ya wapendwa wetu hawa kwa kutoa ulichonacho kwani mpendwa wao mmoja aitwaye Maua tayari ametangulia mbele za haki kwa kile walichodai ni kukosa chakula. Kama utapenda kupata maelezo zaidi wasiliana na Mwandishi wa mtandao huu, Dotto Mwaibale kwa namba ya simu 0712-727062,0786858550 na 0754-362990.
====================================================================
Mbunge wa Jimbo la TemekeMh.Abbas Mtemvu azindua vicoba
on October 21, 2014
Mbunge
wa Jimbo la TemekeMh.Abbas Mtemvu alipowasili katika Viwanja vya TCC
Club, Dar es Salaam, (kushoto ni) Naibu meya na Diwani wa Miburani Juma
Mkenga, na kulia ni Mwenyekiti wa Temeke Jogging, Mussa Mtulya.(PICHA NA
KHAMISI MUSSA)
Baadhi
ya wanachama wa Vilab kumi vya Jogging Jimbo la Temeke wakimsikiliza
Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu wakati alipofanya kazi ya
kuzindua Vikoba katika viwanja vya TCC Club jijini Dar es Salaam na
kuchangisha zaidi ya shilingi milioni 1.8.
Mbunge
wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu, akizindua vikoba na kupitisha
Harambee ambapo zaidi ya Sh. milioni 1.8 zilipatikana katika harambe
hiyo
Mbunge
wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu, kulia na Mwenyekiti wa Temeke Jogging,
Mussa Mtulya , wakati mbunge huyo alipokuwa akizindua vikundi zaidi ya
kumi vya Vicoba.
Pendo
Masigati , alipofunguwa kinywaji cha Shampeni katika hafla hiyo ya
uzinduzi wa Vikoba hivyo katika Viwanja vya TCC Clob ,Dar es Salaam
Mbunge
wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu (kulia), akimkabidhi Sh. Laki moja ,
Mwenyekiti wa Jogging Sports Club ya Mikocheni Dar es Salaam, Muhamed
Husseni kwa ushiriki wao baada ya kukubali mwaliko bila kujali umbali,
wanao shuhudia katikati kushoto ni Diwani Hamisi Mzuzuri na anayefuatia
ni Naibu meya na Diwani wa Miburani Juma Mkenga
Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu, akiongea na wana Habari baada ya uzinduzi wa Vicoba.
=====================================================
TANZANIA KUANIKIZA MAFANIKIO YA LFI KWA MATAIFA 8
October 21, 2014
Na Mwandishi wetu
MATAIFA manane yaliyopo katika nchi zinazoendelea zitaanikizwa mafanikio ya Tanzania katika utekelezaji wa programu ya Jitihada za Mahalia za Utafutaji Fedha (LFI) inayosimamiwa na Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF).
Pamoja na upelekaji wa maarifa yaliyopatikana nchini Tanzania katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mradi huo ambao ulianza mwaka 2012 na kumalizikia 2015, Watanzania ndio watakaotumika kupeleka maarifa mapya.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa ushauri wa ufundi wa UNCDF, Peter Malika wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu warsha ya siku tatu inayofanywa na UNCDF iliyolenga kuwaelimisha wadau mbalimbali wanaohusika na programu hiyo.
Wadau hao ni waandaaji wa miradi, watoa fedha na wasimamizi wanaofanya maamuzi.
Alisema baada ya mafanikio ya mradi huo, UNCDF imemua Tanzania kuwa makao makuu ya LFI na kwamba watanzania baada ya kuonesha uwezo wa dhana za LFI, mafanikio hayo katika mataifa mengine.
Mataifa yaliyoelezwa kupelekewa utaalamu wa watanzania kuanzia awamu ya pili inayotarajiwa kuanza mwakani hadi mwaka 2017 ni Uganda, Benin, Senegal na Bangladesh.
Alisisitiza kwamba program ya LFI inatekelezwa kwa kushirikiana na serikali na hapa Tanzania inafanyika kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI).
Katika utekelezaji wa program hiyo LFI imesaidia miradi kadhaa yenye kipaumbele inayogusa miundombinu ya nishati, kilimo na mawasiliano.
Kwa mujibu wa Malika kuna miradi 25 yenye maslahi kwa umma ambayo imewezeshwa kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Akifafanua zaidi alisema miradi hiyo 25 ya miundombinu iliyoanzishwa na wawekezaji wa umma na binafsi iko katika hatua mbalimbali za uendelezaji.
Aidha alisema miradi hiyo imetawanyika katika sekta mbalimbali zikiwemo za usindikaji bidhaa za kilimo, nishati, miundo mbinu ya utoaji huduma za jamii, mawasiliano na uzalishaji viwandani katika mikoa 10 kote nchini.
Hadi kufikia Septemba mwaka huu miradi mitano iliyopiga hatua kubwa zaidi ilitarajiwa kufikia kikomo cha bajeti yake katika miezi sita hadi tisa ijayo ambapo dola milioni 26 za mtaji wa ndani katika muundo wa mkopo na misaada ipatayo dola milioni 3 ilihamasishwa.
Msaada wa LFI kwa miradi iko katika muundo wa utaalamu wa kiufundi, kutoa amana, misaada ya kifedha na aina nyingine ya mikopo ambayo inahitajika sana kwa miradi midogo na ya kati ya miundombinu ili ivutie uwekezaji.
LFI imeundwa kuhamasisha ukuaji endelevu, jumuishi na wenye usawa kwa kufungua fursa za uwekezaji ili kuleta mabadiliko chanya na kusaidia miradi kupata fedha kupitia sekta binafsi na hasa masoko ya mitaji.
UNCDF yenye jukumu la pekee kuhusiana na fedha katika mfumo wa Umoja wa Mataifa, shirika hili limelenga kutoa msaada wa mtaji wa kuwekeza na wa kiufundi katika seklta ya umma na binafsi.
Aidha imepewa uwezo wa kutoa fedha za uwekezaji katika muundo wa misaada, mikopo na uwezeshaji wa ukopaji na utaalamu wa kiufundi katika kuandaa taarifa ya mradi kuhusu uendelevu na kujenga uwezo wa kuondoa hatari ya kuporomoka.
Na katika hilo Malika alisema lengo kuu ni kuhakikisha kwamba miundombinu hasa ya maeneo ya vijijini ambayo haiwezi kupata kirahisi ridhaa ya taasisi za kifedha au utekelezaji wa serikali kuu inawezeshwa kwa kuitafutia andiko madhubiti na kuelekeza namna ya kupata fedha za utekelezaji.
“Kwa maneno mengine, miradi ile ambayo pengine isingekopesheka athari zake zinapunguzwa na kuingizwa katika hatua ya kuwa tayari kupokea uwekezaji ambapo inaadaliwa ili ipate mtaji wa kibiashara” alisema Malika.
Matokeo ya jumla ya LFI, kwa mujibu wa Malika ni kuongezeka kwa ufanisi wa rasilimali fedha kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi ya hapa nchini kupitia uhamasishaji kwanza kabisa wa mtaji binafsi kutoka nchini na masoko ya mitaji ili kuwezesha na kuhamasisha maendeleo ya mahalia yaliyo jumuishi na endelevu.
Akizungumzia warsha hiyo ya siku tatu ambayo imeanza leo, Malika alisema kwamba zaidi ya watu 120 watashiriki wakiwamo waandaaji miradi na taasisi za kifedha.
Mafunzo ya leo ambayo yalihusu waandaaji miradi waliwezeshwa na mtaalamu nishati mbadala Michael Feldner ambaye pia ni mshauri wa masuala ya kifedha wa UNCDF.
Mtoa mada huyo aliainisha zana za ubunifu zikiwemo masuluhisho wakati wa uhaba wa fedha , mkakati ya kukabili athari, mtiririko wa uandaaji mikataba na masharti na kanuni za msingi zinazoweza kujitokeza katika kila mkataba.
Mafunzo mengine yatagusa watu wa fedha wanaopokea maandiko na kuyafanyia tathmini, ambayo yatafanyika kesho na kuishia na watoa maamuzi katika taasisi hizo kuhusu mikopo iliyoombwa.
====================================================================
RITA YAFANIKIWA KUSAJILI WANAFUNZI ELFU 15 MANISPAA YA ILALA.
on October 21, 2014
Picha na MAELEZO.
……………………………………………….
Na Fatma Salum- Maelezo Jumla ya wanafunzi 15,120 wa shule za Msingi na Sekondari katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam wameweza kusajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa kupitia Mkakati wa Usajili na Kutoa Vyeti vya Kuzaliwa unaotekelezwa na Wakala wa Usajili,Ufilisi na Udhamini (RITA). Hayo yamesemwa na Meneja Masoko, Mawasiliano na Elimu kwa Umma kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Bw. Josephat Kimaro wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. “Mkakati huu umeonesha mafanikio makubwa kwani mpaka sasa wanafunzi 15,120 wamepata vyeti vya kuzaliwa wakiwemo wasichana 7,712 na wavulana 7,408 kutoka shule 201 za Manispaa ya Ilala ambapo 201 ni shule za Msingi na 96 ni Sekondari.” Alisema Kimaro. Akifafanua zaidi kuhusu mkakati huo uliozinduliwa mwezi Aprili mwaka huu Kimaro alisema umelenga kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwapatia wanafunzi vyeti vya kuzaliwa wakiwa shuleni badala ya wazazi kuvifuata kwenye Ofisi za RITA. Aidha umesaidia kuongeza uelewa kwa wanafunzi, wazazi na walezi kuhusu umuhimu wa cheti cha kuzaliwa kwani wazazi wengi wameshawishika kufanya usajili na kupata vyeti kwa ajili ya familia nzima. Pia Kimaro aliongeza kuwa baada ya mkakati huo kufanikiwa katika Manispaa ya Ilala RITA inatarajia kuendeleza katika Manispaa za Temeke na Kinondoni mnamo mwezi Januari 2015 zikifuatiwa na Manispaa nyingine za Tanzania Bara. Akitoa wito kwa wazazi na walezi Kimaro amewataka kutumia fursa hiyo kuwapatia vyeti watoto wao wanaosoma katika shule ambazo program inatekelezwa kwani hutumia mfumo rahisi kwa gharama nafuu na mtoto hupata cheti halisi.
Subscribe to:
Posts (Atom)