TAN

Bayport

Kikoa

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, October 23, 2014
KAMATI YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) YAJADILI HESABU ZA MWAKA WA FEDHA WA 31 DESEMBA, 2012 BAADA YA RIPOTI YA CAG, KWA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA (NIC)
2014 CNN – MULTICHOICE JOURNALIST AWARDS SHOWCASES TANZANIA DESPITE FAILURE TO WIN A SINGLE AWARD
By Victor Mlunde
Last
Saturday, the world witnessed a historic annual CNN-Multichoice
Journalist Award ceremony on the continent, hosted for the first time in
our commercial capital, Dar Es Salaam.
The
choice of Tanzania is not only an unprecedented honor to the great
peaceful nation on the continent, but a rare opportunity to showcase
Tanzania and open its market to the world.
I
congratulate the event organizers and His Excellency the President, Dr
Jakaya Mrisho Kikwete, for being the Guest of Honour, for his
outstanding economic diplomacy skills and unending efforts in showcasing
Tanzania to the world.
As usual, the president’s speech looked at quantity rather than quality, boasting to have more
media outlets in the country than neighbors – even with mounting
insecurity of media practitioners and existence of Draconian Newspapers
Act, 1976 and National Security Act, 1970 which limit press freedom as
we approach 2015 general elections, the standard rhetoric maintained
that the government will soon table the Freedom of Information and Media
Services Bills in parliament, a promise left unattended by the Ministry
of Information since begin of his second term in office back in 2006.
Despite
government’s slow pace in implementing commitments on free press, we
should acknowledge the fact that the head of state is at least committed
to transparency and open government more than his predecessors, at
least by signing international commitments and protocols on transparency
such as the Open Government Partnership, though more work needs to be
done in getting Media Freedom Bill and Services Act in place before busy
and tense election period comes in.
The
award categories covered economics and business, press freedom, culture,
sports, photo journalism, sports reporting and the environment. Others
included Portuguese and French stories awards. Winners wrote moving and
interesting stories. To mention a few; Bento Venâncio, Jornal Domingo,
Mozambique investigated how lack of transparency in procurement of
automobiles in Mozambique leads to fraud, Evelyn Watta, a sports
reporter from Kenya revealed the value of Senegal’s mythical Wrestling
heritage to the West African nation. The most touching of all was Press
Freedom Award handed to the wife of jailed Swazi journalist, Bheki
Makhubu who is facing sedition for penning columns supporting a state
clerk who was charged for trying to put right the system that allowed
judicial officers to misuse public cars.
My
sincere congratulations should go to the only brave Tanzanian nominee,
one Dickson Ng’hily whose Dar traffic jam story was a concern of all Dar
commuters; too bad the judges underestimated the significance of his
story in pushing authorities in fast growing African cities to expand
the road network.
However,
a question remains; where were the rest of Tanzanian journalists? it is
believed the majority did not submit their work for some reason –
probably due to the fact that everyone was very busy reporting on
“katiba” stunning headlines “serikali mbili au tatu” instead of simple
local stories that could create positive impact in the community! If the
awards had a politics category, I am sure we would have beaten the
Kenyans and West Africans for our genius in making stunning political
headlines.
Yes!
We would have defeated our neighbours in Kenya who have outperformed the
whole of East Africa in this year’s awards, yet again. In fact it is
not the first time; even in the prestigious annual Kili Marathon held in
Tanzania’s Kilimanjaro region, Kenyans end up winning more trophies
while we the hosts are reduced to mere spectators each year.
Overall winner
I was
personally moved by the story of the overall winner, Joseph Mathenge
and his son who convinced father to abandon his private photography
tender aimed at raising funds for son’s cancer treatment and instead
rushed to the Westgate Mall to capture the very first photos that
revealed the images of terror to the whole world.
Way forward
It is
high time Tanzanian journalists be proud of their work and confident to
present it in future awards, even when unsure of winning. More quantity
will help identify quality stories that will make all of us proud.
Organizers
should also add a social media category to honour and recognize
excellent work by social media which uses the internet and citizen
journalism to report sensational stories as they happen swifter than the
traditional media itself.
On
the other hand, award organizers should add a Swahili story category
alongside Portuguese and French story awards for it is an African Union
(AU) language widely spoken across East and Central Africa. Moreover, I
would like to advise CNN to introduce a CNN Swahili language service in
East and Central Africa, emulating BBC, Deutsche Welle, Radio France
International and VOA in giving local journalists in the broader Swahili
speaking East and Central African region to cover and explain local
stories to the world.
Victor Mlunde
is a Dar es Salaam-based Political and Development Consultant with
expertise in media, good governance, elections and conflicts resolution
in the Great Lakes region. He can be easily reached through +255 714
289428 and vicmlunde@yahoo.com
SWEDEN YATOA BIL. 42/- KUSAIDIA MIRADI UN
Na Mwandishi wetu
SWEDEN
imeyapatia mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo hapa nchini jumla ya
shilingi bilioni 42/- ili kusaidia katika miradi yake ya maendeleo
inayofanya nchiini Tanzania.
Makubaliano
ya fedha hizo yametiwa saini jana kati ya Balozi wa Sweden Lennarth
Hjelmaker na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania
Alvaro Rodriguez.
Fedha
hizo ambazo ni sawa na dola milioni 24, zitaelekezwa kwenye miradi ya
UNDAP inayoendana na sera za Sweden za kuwezesha masuala ya utawala
bora, ustawi wa jamii, wanawake na watoto na usawa wa kijinsia.
Kwa
mujibu wa Balozi wa Sweden, fedha hizo zitasaidia utekelezaji wa
Mkukuta, Mkuza na Matokeo makubwa sasa (BRN) mipango inayofadhiliwa na
mashirika ya Umoja wa Mataifa .
Alisema
ni matumaini yake kuwa fedha hizo zitaboresha hali ya kufanya biashara,
kuwekeza kwa lengo la kutoa ajira zaidi,kuwezesha uchaguzi huru,
kuimarisha huduma za jamii, kuimarisha mipango, uwajibikaji na
kuimarisha mawasiliano ya radio kwa ajili ya upashanaji habari vijijini
ili kusaidia maamuzi yenye mtazamo mpana zaidi miongoni mwa watu wa
vijijini.
Katika
hafla hiyo Balozi wa Sweden alisema pamoja na kutoa fedha hizo kwa
mashirika ya Umoja wa Mataifa, nchi yake itaendelea na makubaliano
yaliyofikiwa na serikali ya Tanzania na kuendelea kutoa misaada yake ya
kimaendeleo.
Akijibu
swali la kwanini wanatoa fedha kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa pekee,
na kama wameacha kutoa misaada ya moja kwa moja serikalini, Balozi huyo
alisema misaada ya taifa hilo imelenga kupata matokeo yanayotakiwa na
kwamba itaendelea kusaidia pia taasisi nyingine zisizo za kiserikali na
serikali yenyewe.
Aidha
Balozi Lennarth Hjelmåker alisema kwamba Tanzania imekuwa mfano bora
kabisa wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa kuwezesha ufanisi mkubwa wa
miradi ya maendeleo yaliyolenga kuwawezesha watanzania kupiga hatua
mbele na kuhakikisha kuwapo kwa amani.
Alisema
wanafurahia kusaidia masuala ya utawala bora, kazi kwa vijana, usawa wa
kijinsia na kuwapo kwa uchaguzi huru na wenye amani.
Sweden
imesema itaendelea kusaidia Umoja wa Mataifa nchini hasa inapotekeleza
mradi wake wa misaada kwa Tanzania (UNDAP) kama mashirika hayo
yalivyokubaliana na serikali ya Tanzania.
Naye Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez, ameishukuru Sweden kwa kuendelea kuwa mdau wa maendeleo.
Tanzania
na Umoja wa Mataifa wanatekeleza mradi wa miaka mitano wa UNDAP ambapo
mashirika ya UN yaliyopo nchini yanatoa kwa umoja wake huduma stahiki
ili kupata Matokeo Makubwa.
Rais azungumza na Balozi wa Marekani
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akifuatana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mark Bradley baada ya
mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ramadhan
Othman Ikulu.]
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akiagana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mark Bradley baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi,[Picha na Ramadhan Othman Ikulu.]
WAZIRI CHIKAWE AMKABIDHI MKUU WA WILAYA NACHINGWEA MABATI 2000 KWA AJILI YA UJENZI WA MAABARA SHULE ZA SEKONDARI
RAIS WA TOC KUFUNGA KOZI YA MAKOCHA
Ndugu Filbert Bayi (Katibu ) wa TOC
………………………………………………………………………………
Rais wa Kamati ya Olimpiki Tanzania
(TOC) Gulam Rashid kesho (Oktoba 24 mwaka huu) atafunga kozi ya makocha
ya Leseni C ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Hafla ya ufungaji kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 32 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
na kuandaliwa na TOC kupitia Olympic Solidarity kwa ushirikiano na
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) itafanyika saa 5 asubuhi
kwenye hosteli za TFF zilizopo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Kozi hiyo ya wiki mbili iliyoanza
Oktoba 12 mwaka huu iliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa
la Mpira wa Miguu (FIFA) Ulric Mathiot kutoka Shelisheli.
Makocha walioshiriki kozi hiyo ni Ahmed Suleiman Simba (Alliance),
Akida Saidi (Lindi), Ally Bushir Mahmoud (Zanzibar), Aloyce Akwilin
(Pwani), Amin Rashid Mdowe (Zanzibar), Augustino Dakto Damian (Katavi),
Athuman Bilal (Shinyanga), Bakari Shime (Tanga), Charles Mayaya
(Shinyanga) na Choki Abeid(Geita).
Wengine ni Edna Lema (Morogoro),
George Melchior (Kagera), Godfrey Kapufi (Katavi), Hamis Mabo (Kigoma),
Hawa Bajangero (TWFA), Ibrahim Mulumba (Geita), Jemedari Said (TAFCA),
Kenny Mwaisabula (TAFCA), Madenge S. Omari (Mara), Milambo Camil (Tabora) na Mohamed D (Ruvuma).
Pia wapo Mohamed Ismail Laiser
(Manyara), Mohamed Muya (Dodoma), Ngawina Ngawina (Mtwara), Nicholas
Kiondo (Ilala), Osuri Charles Kosuri (Simiyu), Rachel Palangyo (TWFA),
Salvatory Edward (Temeke), Seif Bausi Nassor (Zanzibar), Yusuf Macho
(Kigoma), Wilfred Mollel (Iringa) na Zacharia Mgambwa (Rukwa).
Makocha watakaofaulu kozi hiyo watapewa Leseni C za CAF wakati watakaoshindwa watapewa vyeti vya ushiriki tu.
Pata hapa nakala ya muswada wa Baraza la Vijana la Taifa; boresha tupate baraza bora
Narudia tena kuwashukuru vijana na wadau tulioshirikiana kuandaa muswada huo na naomba kuendelea kupata ushirikiano wenu wa karibu katika hatua zinazoendelea.
Kuanzia tarehe 21 Oktoba 2014 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii imeanza vikao vya kupokea maoni ya wadau kuhusu muswada huo. Nakala tete ya muswada huo inapatikana hapa, tafadhali pakua pitia na wasilisha maoni yako sasa.
Unaweza kuandika maoni yako kwenye mtandao wa http://mnyika.blogspot.com au kutuma kwa barua pepe kwenda mbungeubungo@gmail.com na nakala kwa Kamati husika ya Bunge kupitia tanzparl@parliament.go.tz.
Ikiwa unataka kutumia njia nyingine kuwasilisha maoni yako tafadhali wasiliana na Gaston Garubimbi 0715/0767-825025 kwa maelezo zaidi. Mdau wa masuala ya vijana zingatia kwamba zaidi ya miaka 18 ahadi za kukamilisha mchakato wa kuanzishwa kwa baraza la Vijana la Taifa zimekuwa zikitolewa bila utekelezaji kamili na wa haraka.
Baraza la Vijana la Taifa pamoja na malengo mengine litawezesha vijana kuanzia kwenye vijiji/mitaa mpaka taifa kuweza kuwa na vyombo vya kuwaunganisha vijana kwa kike na wa kiume kwa ajili ya maendeleo yao na ya taifa.
Aidha, Baraza hilo litafuatilia pia kwa karibu utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya vijana kwenye Halmashauri, Serikali kuu, katika vyombo mbalimbali vya maendeleo na wadau wa maendeleo.
Pia, Baraza la Vijana litafuatilia kwa karibu utendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kuhakikisha kwamba fedha zinatengwa za kutosha na kufika kwa walengwa kuwawezesha vijana kujiajiri, kukuza vipaji vyao na kushughulikia maendeleo yao kwa ujumla.
Kwa upande wangu nitashukuru ikiwa nitapokea maoni hayo kabla ya tarehe 28 Oktoba 2014, niweze kuyachambua na kutoa mrejesho mapema kuwezesha muswada kusomwa kwa mara ya pili Bungeni katika Mkutano wa 16 uliopangwa kuanza tarehe 3 Novemba 2014.
Kwa mujibu wa Hansard tarehe 21 Disemba 2013 baada ya Muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, Spika wa Bunge Anna Makinda alisema yafuatayo Bungeni “…muswada binafsi…. sasa utaanza kuwepo kwenye website ya Bunge na utakuwa public mpaka utakapopangiwa tarehe ya kujadiliwa na utapelekwa kwenye kamati zitakazohusika wakati muafaka”.
Majibu yanapaswa kutolewa na mamlaka husika ni kwanini toka wakati huo haukuwahi kuwekwa kwenye Tovuti ya Bunge pamoja na kukumbushwa. Hata hivyo nashukuru kuwa hatimaye sasa muswada huo umepelekwa kwenye Kamati, hivyo ni wakati muafaka kwa vijana na wadau wote kupata nakala ya muswada huo hapa na kutoa maoni ya kuboresha ili Baraza la Vijana la Taifa liweze kuundwa.
Kujadiliwa kwa muswada huo ni hatua ya pekee katika historia ya harakati za vijana nchini kwa kuzingatia kuwa Sera ya zamani ya maendeleo ya vijana ya mwaka 1996 ilitamka kwamba kutaanzishwa Baraza la Vijana na suala hilo kurudiwa katika Sera mpya ya mwaka 2007.
Hata hivyo Serikali imekuwa ikikwepa kuhakikisha kwamba matakwa hayo ya sera tajwa yanatekelezwa kwa wakati pamoja na kuwa suala hilo linahusu mustakabali wa maendeleo ya vijana nchini. Hivyo pakua nakala pekua toa maoni; boresha muswada tupate baraza bora.
Wenu katika uwakilishi wa wananchi,
John Mnyika (Mb)
23 Oktoba 2014
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA BALOZI WA BOTSWANA NCHINI TANZANIA IKULU DAR
Airtel yatatua changamoto za uhaba wa vitabu vya sayansi Katika shule ya Sekondari Mukulati Mkoani Arusha
……………………………………………………………….
Kampuni ya simu za mkononi ya
Airtel imeedelea kuungana na serikali katika kusaidia kuboresha
maendeleo ya sekta ya elimu nchini ambapo imetoa vitabu vya ziada na
kiada katika masomo ya sayansi kwa shule ya sekondari mukulati wilayani
Arumeru mkoani Arusha
Licha ya Kada ya sayansi kuwa ndio
chimbuko kubwa la wataalamu wengi katika fani mbalimbali bado
inatajwa kutofanya vizuri kutokana na uhaba wa miundombinu na vifaa
stahiki ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya kada hiyo.
Meneja wa Airtel mkoa wa
Kilimanjaro Paschal Mikomagu akizungumzia mchango wa kampuni hiyo
wakati wa mahafali ya 17 ya shule ya sekondari mukulati amesema Airtel
kwa kutambua changamoto mbalimbali ndani ya kada ya sayansi nchini
ikiwemo uhaba wa vitabu vya kujifunzia imeamua kuwa na utaratibu wa
kugawa vitabu hivyo. Leo tumehudhuria mahafali na kuchangia kutatua
moja ya kero zinazokumba sekta ya elimu na tuaamini kwa msaada huu wa
vitabu vitaongeza ufaulu wa wanafunzi na kusaidia shule kufanya vizuri
kitaaluma
Tutaendelea kutimiza dhamira yetu
kwa vitengo ya kusaidia kutatua changamoto mbalimbali mashuleni na
kuhakikisha tunaboresha uwiano wa vitabu kwa wanafunzi hadi kitabu
kimoja kwa mtoto moja au wawili.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya
Olkokola Joseph laizer leo ni sisi Airtel imetoa msaada huu wa vitabu
ambavyo vitasaidia shule hapa , lakini zaidi tunawaomba Airtel waendelee
kujitolea kushirikiana nasi na kutufadhili katika ujenzi wa maabara
katika shule hii ili kuweza kufikia malengo tuliyowekewa ya kuhakikisha
kila shule ya sekondari inajenga maabara kwa ajili ya mafunzo ya ziada
Akiongea mara baada ya kupokea
vitabu hivyo MkeeVitalisi Martine mkuu wa shule kwa msaada huu
umeongeza uwiano wa vitabu shule hapa ambapo kwa sasa kitabu kimoja
kitatatumika na wanafunzi wawili, napenda kuwhakikishia vitabu hivi
havitakaa kwenye kabati bali vitatumika kwa manufaa yaliyokusudiwa ili
atimaye watoto waweze kupata ujuzi kupitia vitabu hivi
Nao baadhi ya wanafunzi walito
maoni yao kuhusu mchango huu shule ni hapo ambapo Happy Lyimo alisema
natoa shukurani za dhati kwa niaba ya wanafunzi wenzangu kwa Airtel kwa
kutupatia mchango wa vitabu vingi vya sayansi. Nimatumaini yangu kuwa
vitabu hivi vitasaidia kuinua taaluma kwa wanafunzi na shule kwa
ujumla.
MAKAMU WA RAIS DKT. BIALA AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU MSTAAFU WA UBA TANZANIA GENERAL ROBERT MBOMA NA UJUMBE WAKE, IKULU DAR.
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
AJALI HIYO IMETOKEA MNAMO TAREHE
22.10.2014 MAJIRA YA SAA 22:20 USIKU HUKO MAENEO YA MWISHO WA WAYA, KATA
YA IYUNGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA
MBEYA/TUNDUMA.
AIDHA, WATU WATATU WALIJERUHIWA
KATIKA AJALI HIYO AMBAO NI 1. LAMECK LIMO 2. ANGOLISYE MWAKALOBO NA 3.
JOYCE ASAJILE AMBAO WAMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA
MATIBABU.
CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA
MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA
MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO IKIWA NI PAMOJA NA
KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI
ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
TAARIFA ZA MISAKO:
KATIKA MSAKO WA KWANZA, MTU MMOJA
MKAZI WA MKWAJUNI WILAYA YA CHUNYA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA PRISCA
SINKALA (31) ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA AKIWA NA
POMBE YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 05.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE
22.10.2014 MAJIRA YA SAA 18:00 JIONI HUKO KATIKA KITONGOJI CHA MAJENGO,
KIJIJI NA KATA YA MKWAJUNI, TARAFA YA KWIMBA, WILAYA YA CHUNYA, MKOA WA
MBEYA. MTUHUMIWA NI MUUZAJI WA POMBE HIYO, TARATIBU ZA KUMFIKISHA
MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
KATIKA MSAKO WA PILI, JESHI LA
POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA AITWAYE ISAYA DARON (27)
MKAZI WA SOWETO AKIWA NA POMBE KALI [VIROBA] ZILIZOPIGWA MARUFUKU AINA
YA BOSS PAKETI 30.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA MNAMO TAREHE
22.10.2014 MAJIRA YA SAA 14:00 MCHANA HUKO SOWETO, KATA YA RUANDA,
TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. MTUHUMIWA NI MUUZAJI WA POMBE
HIZO.
KATIKA MSAKO WA TATU, MTU MMOJA MKAZI WA AIRPORT JIJINI MBEYA
AITWAYE SALEHE SEKILE (32) ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA
AKIWA NA KETE 12 ZA BHANGI SAWA NA UZITO WA GRAMU 60.
MTUHUMIWA ALIKAMATWA KATIKA MSAKO
ULIOFANYIKA MNAMO TAREHE 22.10.2014 MAJIRA YA SAA 17:30 JIONI HUKO
MAENEO YA FOREST MPYA, KATA YA FOREST, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA
MBEYA. MTUHUMIWA ALIKUTWA NA KETE HIZO BAADA YA KUPEKULIWA KWENYE
MIFUKO YAKE YA SURUALI. AIDHA, MTUHUMIWA NI MTUMIAJI NA MUUZAJI WA
BHANGI HIYO.
KATIKA MSAKO WA NNE, JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI WAKAZI WA MANGA JIJINI MBEYA AMBAO NI 1. TERESIA MWAISAKILE (31) NA 2. ELIZABETH LONDELE (29) WAKIWA NA POMBE YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 01.
WATUHUMIWA KWA PAMOJA WALIKAMATWA
KATIKA MSAKO ULIENDESHWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA MNAMO TAREHE
22.10.2014 MAJIRA YA SAA 13:30 MCHANA HUKO MAENEO YA MANGA, KATA YA
MANGA, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. WATUHUMIWA NI WAUZAJI WA
POMBE HIYO, TARATIBU ZA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI ZINAENDELEA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA
MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL N. MASAKI ANATOA WITO KWA
JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA/POMBE YA MOSHI PAMOJA NA POMBE KALI
ZILIZOPIGWA MARUFUKU NCHINI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI
KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA, ANATOA WITO KWA WANANCHI KUTOA TAARIFA ZA
MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA UINGIZAJI/USAMBAZAJI NA UUZAJI WA POMBE KALI
NA POMBE YA MOSHI ILI WAKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI
YAO.
Imesainiwa na:
[BARAKAEL N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
[BARAKAEL N. MASAKI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Adha ya maji yaendelea kuwatesa wakazi wa Kijiji cha Songambele Halmashauri ya Nsimbo Wilayani Mlele.
Madiwani na watalaam wa Halmashauri ya Nsimbo wakijadili
mstakabali wa maendeleo ya Halmashauri yao Nsimbo,pamoja na kujadili
masuala ya elimu, Afya, Miundo mbinu ya barabara,utawala,na maengineyo
lakini suala la maji lilichukua nafasi ya kipekee katika kikao hicho cha
baraza la madiwani kilichomalizika mwishoni mwa wiki iiliyo
(Picha zote Kibada Kibada -Nsimbo Mlele Katavi).
Mama akisukuma maji kwenye
kisima kifupi kilichopo hapo huku akina mama wengine na watoto
wakisubiri zamu yao ifike ili waweze kuchota maji ambayo yanatoka
kidogokidogo kwenye kisima hicho hapo madumu yanaonekana hayana maji,
dumu moja kujaa inawachukua zaidi ya saa, hivyo kuwafanya watumie muda
mwingi kutafuta maji badala ya kufanya shughuli nyingine za maendeleo.
……………………………………………….
Na Kibada Kibada –Nsimbo Mlele
Wakazi wa Songambele Halmashauri
ya Nsimbo Wilayani Mlele wanakabiliwa na Changamoto ya uhaba wa maji
kufuatia visima vifupi vilivyopo kutokuwa maji ya kutosha.
Hali hiyo ya uhaba wa maji kwa
baadhi ya Vijiji vya Kata ya Nsimbo na maeneo mengine ya Halmashauri
hiyo inayowafanya akina mama na watoto kuamka kila siku alfajiri
majira saa kumi usiku kwenda kutafuta maji kwa au kusubiria maji
kwenye visim vifupi vilivyopo ambavyo navyo havitoi maji ya kutosha
hivyo kutumia muda mrefu kutafuta na kukosa muda wa kufanya shughuli
nyingine za maendeleo.
Akizungumzia hali ilivyotete
kuhusu upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Songambele na Kata ya
Nsimbo kwa ujumla Afisa Mtendaji wa Kata ya Nsimbo Wilbroad Milala
anasema kwa kweli hapo maji ni shida kubwa kwa wakazi wa hapo.
Milala anasema hata visima
vilivyopo havitoi maji ya kutosha wakati mwingine kama msimu huu wa
kiangazi maji hukata hata miezi miwili bila kutoa maji hali inayofanya
wakazi hao hasa akina mama na watoto kufuata maji kwenye mbuga umbali wa
takribani kilometa tatu hadi nne maji amabyo siyo safi wala salama.
Kufuatia kuwepo kwa changamoto
hiyo ya Maji wawakilishi wa wananchi ambao ni madiwani kupitia kwenye
vikao vya baraza la madiwani suala la maji lilionekana kuchukua nafasi
ya kipekee kuzungumzia ikiwa ni pamoja na kutafuta mbinu za kulipatia
ufumbuzi.
Akiongea katika kikao cha Baraza
la madiwani kwa nyakati tofauti Mjini Nsimbo Diwani wa Kata ya
NsimboMichael Kasanga, Diwani wa Kata ya Mtapenda Eliezer
Fyula,walieleza kuwa lazima hatua zichukuliwe kwa haraka ili kulipatia
ufumbuzi suala la upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Halamshauri hiyo
hasa maeneo yale yenye visima vifupi vichimbwe visima virefu.
Wakaeleza kuwa pia visima
vinapoharibika taarifa iwe inatolewa mapema kwenye Idara ya Maji ili
kuona namna ya kuweza kulipatia ufumbuzi pale panapo wezeakana kama
kununua vifaa vya ukarabati wa pump.
Awali Mwenyekiti wa Kamati ya
Elimu na Maji Raphael Kalinga akiwasilisha taarifa ya Kamati yake
alieleza mikakati inayochukuliwa na halmashauri ili kukabiliana na
changamoto ya uhaba wa maji ikiwa ni pamoja na kutenga fedha kupitia
bajeti zake na fedha kutoka kwenye mifuko ya maji ili kusaidia
upatikanaji wa maji ikiwa pia na kuomba ufadhili kutoka kwa wahisani
mbalimbali kusaidia suala la maji.
Aidha aliwashauri madiwani
kuwahamasisha wananchi kuanzisha kamati za mifuko ya maji ili fedha
inayopatikana iwe inasaidia katika matengenezo madogo madogo pindi pump
za visima vya maji vinapo haribika fedha hizo zitasaidia ukarabati mdogo
mdogo.
Katika hatua nyingine Baraza la
Madiwani la Halmashauri ya Nsimbo limemwagiza Kaimu Mhandisi wa Mji
katika Halmashauri Enock Msengi kuhakikisha anapoondoka awe anakaimisha
ofisi kwa mwenzake anayekuwa ofisini kuliko kuacha amefunga ofisi na
pia mali za ofisi inatakiwa awe anacha ofisi ikiwa wazi na awe
anaandika barua ya kukabidhi ofisi kuliko kijiondokea kama anavyofanya
kwa kuwa ofisi siyo mali yake bali ni mali ya Serikalai.
KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA AKABIDHI ZAWADI YA BASI DOGO BWAWANI SEKONDARI KATIKA MAHAFALI YA KUMI NA MOJA YA KIDATO CHA NNE YALIYOFANYIKA MKOANI PWANI
WAZIRI MKUU AZINDUA JARIDA LA FIRST JIJINI LONDON
*Ni Toleo Maalum la Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania
*Linatumika kuitangaza Tanzania kwa watu mashuhuri
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda
amezindua jarida la kimataifa la FIRST ambalo limesheheni taarifa za
kuitangaza Tanzania kwa wadau wa nchi mbalimbali duniani huku likielezea
hatua mbalimbali za ustawi kwa miaka 50 tangu nchi ipate uhuru.
Uzindusi huo ulifanyika kwenye
ofisi za ubalozi wa Tanzania jijini London, Uingereza ambako pia Waziri
Mkuu alikabidhiwa nakala ya kwanza ya toleo la sasa ambayo iliwekwa
kwenye jalada jekundu la ngozi (leather bound red cover).
Akizungumza katika uzinduzi huo,
Waziri Mkuu alisema Serikali ya Tanzania imepata fursa nzuri ya kujinadi
kwa watu maarufu na wafanyabiashara wa kimataifa duniani kupitia jarida
hilo na akataka uwekwe utaratibu wa kujinadi kisekta.
Alimtaka Balozi wa Uingereza, Bw.
Peter Kallaghe aweke mkazo na kusimamia suala hilo ili kuhakikisha
matoleo yanayofuata yanakuwa ya kisekta zaidi. “Balozi hapa umefanya
kazi nzuri sana ya kuinadi nchi yetu, wala usichoke. Tujitahidi sasa
kila mwaka waandike kuhusu fursa za uwekezaji kwa miradi ya kisekta kama
utalii, nishati, madini na kadhalika,” alisema.
Waziri Mkuu alimshukuru Mwenyekiti
wa taasisi ya First, Bw. Rupert Goodman kwa kazi nzuri aliyoifanya kwa
ajili ya Taifa la Tanzania. “Kazi uliyoifanya ni nzuri lakini katika
tolea lijalo tuangalie jinsi ya kuitangaza miradi ya uwekezaji ambayo
inauzika na iende sekta kwa sekta. Ukisirikiana na Balozo wetu hapa,
lazima utapata kitu kizuri,” alisema.
Mapema, akielezea kuhusu jarida
hilo la FIRST, Balozi Kallaghe alisema jarida hilo linasambazwa kwenye
mashirika mbalimbali ya ndege kama vile British Airways, Air Astana, Lufthansa, United Airlines, Gulf Air, American Airlines, South African Airways, Korean Airways, Etihad Airways, Qatar Airways na Continental Airlines.
“Siyo tu kwamba linasambazwa katika mashirika haya ya ndege, bali pia linawekwa kwenye vyumba vya kupumzikia (First Class and Business Class Lounges) abiria wa daraja la kwanza na la pili wa mashirika haya kwenye viwanja vingi vya ndege,” alisema.
Alisema hili ni toleo la sita
ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano na ofisi yake (Ubalozi wa Uingereza)
ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania lakini
pia ikilenga kutangaza fursa za uwekezaji lakini pia ikitangaza hatua
mbalimbali za maendeleo ambazo nchi hii imepitia.
Uzinduzi huo ulihudhuriwa pia na
Naibu Waziri wa Fedha, Bw. Mwigulu Nchemba; Naibu Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Mahadhi Maalim na Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Bw. Charles Kitwanga. Wengine ni Naibu Waziri wa
Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Said
Mwambungu ambao pia wamefuatana na Waziri Mkuu.
BONDIA THOMAS MASHALI AJIFUA KUMKABILI MKENYA HENRY WANDERA NOVEMBA MOSI FRENDS CORNE
…………………………………………………………………………. Na Mwandishi Wetu BON DIA Thomasi Mashali yupo katika maandalizi mazito ya kumkabili bondia kutoka kenya Henry Wandera Novemba mosi katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaam Akizungumza wakati wa mazoezi yake juzi Mashali amesema kuwa yupo fiti wakati wowote yeye kufanya kazi hivyo aofii ata kiogo mpambano huo na kuwataka mashabiki wake waje waone anavyo mgalagaza vibaya sana siku hiyo mkenya Wandera
Katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha kabisa kutokana na kujipanga vizuri katika swala hilo kingilio ni shilingi, 7000; kwa kila mtu mchezo huu utapambwa na burudani mbalimbali
MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE NA MATUKIO YA PICHA KATIKA ZIARA YA RAIS DR. JAKAYA KIKWETE NCHINI CHINA
PICHA NA JOHN LUKUWI.
Subscribe to:
Posts (Atom)