Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza (aliyesimama mbele) akielezea mchango wa
nishati ya umeme katika ukuaji wa uchumi wa mkoa huo, katika kikao
chake na Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles Kitwanga. Mhe. Kitwanga yuko ziarani mkoani humo ambapo anatembelea miradi ya umeme inayofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na kuzungumza na wananchi.
TAN

Bayport

Kikoa

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Saturday, October 18, 2014
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI- NISHATI MHE. CHARLES KITWANGA ATEMBELEA MIRADI YA UMEME INAYOFADHILIWA NA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA MKOA WA PWANI
Tanesco kuunganishia wateja wake wa umeme ndani ya siku moja
Naibu Waziri
wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Mhe. Charles
Kitwanga (katikati) akitoa maelekezo kwa wataalamu wa shirika la Tanesco
katika kituo cha Chalinze ya jinsi ya kuboresha hali ya umeme katika
mji wa Chalinze
……………………………………………………………………….
Na Greyson Mwase, Pwani
Ili kuhakikisha wananchi
wananufaika na nishati ya umeme na kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi,
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imeagiza Shirika la Umeme
Nchini (Tanesco) kufanya kazi kwa weledi na ufanisi lengo likiwa ni
kuwaunganishia wateja wake umeme ndani ya siku moja mara baada ya
kukamilika kwa taratibu za malipo.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Charles Kitwanga alipokutana na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza, watendaji wa Tanesco katika ziara yake ya kutembelea miradi ya umeme inayofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya pili.
Waziri Kitwanga alisema kuwa ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi, shirika la Tanesco linatakiwa litoe huduma kwa ubora wa hali ya juu, wa kuridhisha na kwa wakati.
“ Inabidi ifikie mahali iwapo mteja atalipia umeme kabla ya saa nne asubuhi na ambaye haitaji nguzo, basi aunganishiwe umeme ndani ya siku hiyo hiyo, na hili linawezekana.” Alisema Kitwanga.
Kitwanga aliendelea kusema kuwa kwa wateja wanaohitaji huduma ya nguzo za umeme, shirika linatakiwa liwe limewaunganishia umeme kwa kipindi cha siku tatu.
Waziri Kitwanga aliongeza kuwa shirika la Tanesco linatakiwa kuondoa mfumo wa wateja kulipa madeni yao kwa foleni badala yake, walipe kwa kufuata mfumo wa kielektroniki ili kurahisisha ulipaji wake na wananchi kupata huduma kwa wakati.
Aidha, Kitwanga aliongeza kuwa ili kuondokana na adha ya kukatika kwa umeme mara kwa mara kutokana na sababu za matengenezo ya miundombinu ya umeme, shirika la Tanesco linatakiwa kubuni mifumo mbadala ya kuwezesha huduma ya umeme kuendelea kupatikana wakati matengenezo yakiendelea pasipo kukwamisha shughuli za uchumi.
“ Inatakiwa ifike umeme uwe ni kama oksijeni katika mwili wa binadamu, mwili wa binadamu ukikosa oksijeni kwa muda mfupi unapoteza uhai, tukielewa umuhimu wa umeme kwa mantiki hii, zitatumika mbinu mbadala za kuzuia kukatika umeme wakati wa matengenezo hivyo kupelekea uchumi wa nchi kukua kwa kasi.” Alisisitiza Kitwanga.
Kitwanga aliendelea kusema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imejipanga kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inachangia katika kutimiza lengo la Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2025 ya kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025 nchi ya Tanzania inaondoka kwenye kundi la nchi masikini duniani na kuwa nchi ya kipato cha kati.
Alisema kuwa katika nchi nyingi zilizopiga hatua kubwa katika ukuaji wa uchumi wake, nishati ya umeme imechangia kwa kiasi kikubwa mno na kusisitiza kuwa Wizara ya Nishati na Madini imejizatiti kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakua kupitia mchango wa sekta ya nishati.
Wakati huo huo akielezea hali ya umeme katika mkoa wa Pwani, Meneja Mwandamizi wa Tanesco Kanda ya Dar es Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mugaya alisema kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Septemba mwaka huu Shirika la Tanesco lilifanikiwa kuwaunganishia umeme wateja 10, 100 katika mkoa wa Pwani na kufikisha asilimia 21.3 lengo likiwa ni kufikisha asilimia 30 ifikapo mwaka 2015.
Mhandisi Mahende aliongeza kuwa kwa sasa shirika la Tanesco linaendelea na zoezi la ukarabati wa miundombinu ya umeme iliyochakaa na kuongeza kuwa ifikapo Februari mwakani tatizo la kukatika umeme mara kwa mara litakuwa limekwisha kabisa.
Akielezea changamoto Shirika la Tanesco linalokumbana nazo katika shughuli zake katika mkoa huo, Mhandisi Mahende alitaja kuwa ni pamoja uchakavu wa miundombinu ya umeme na kusisitiza kuwa ukarabati bado unaendelea katika maeneo yaliyoathirika.
Mhandisi Mahende aliendelea kusema kuwa changamoto nyingine ni pamoja na madeni sugu kwa wateja na kuongeza kuwa hadi sasa Shirika linadai shilingi bilioni 16 wateja mbalimbali na kusisitiza kuwa Tanesco imepanga mikakati mipya ya ukusanyaji wa madeni hayo.
Alibainisha changamoto nyingine kuwa ni pamoja na wizi wa umeme, na madai ya fidia katika utekelezaji wa mradi wa umeme wa awamu ya kwanza uliokuwa unafadhiliwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) na kuongeza kuwa wananchi walidai fidia iliyokuwa kubwa kuliko gharama za mradi.
Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya nishati Charles Kitwanga alipokutana na mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantum Mahiza, watendaji wa Tanesco katika ziara yake ya kutembelea miradi ya umeme inayofadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya pili.
Waziri Kitwanga alisema kuwa ili kuendana na kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi, shirika la Tanesco linatakiwa litoe huduma kwa ubora wa hali ya juu, wa kuridhisha na kwa wakati.
“ Inabidi ifikie mahali iwapo mteja atalipia umeme kabla ya saa nne asubuhi na ambaye haitaji nguzo, basi aunganishiwe umeme ndani ya siku hiyo hiyo, na hili linawezekana.” Alisema Kitwanga.
Kitwanga aliendelea kusema kuwa kwa wateja wanaohitaji huduma ya nguzo za umeme, shirika linatakiwa liwe limewaunganishia umeme kwa kipindi cha siku tatu.
Waziri Kitwanga aliongeza kuwa shirika la Tanesco linatakiwa kuondoa mfumo wa wateja kulipa madeni yao kwa foleni badala yake, walipe kwa kufuata mfumo wa kielektroniki ili kurahisisha ulipaji wake na wananchi kupata huduma kwa wakati.
Aidha, Kitwanga aliongeza kuwa ili kuondokana na adha ya kukatika kwa umeme mara kwa mara kutokana na sababu za matengenezo ya miundombinu ya umeme, shirika la Tanesco linatakiwa kubuni mifumo mbadala ya kuwezesha huduma ya umeme kuendelea kupatikana wakati matengenezo yakiendelea pasipo kukwamisha shughuli za uchumi.
“ Inatakiwa ifike umeme uwe ni kama oksijeni katika mwili wa binadamu, mwili wa binadamu ukikosa oksijeni kwa muda mfupi unapoteza uhai, tukielewa umuhimu wa umeme kwa mantiki hii, zitatumika mbinu mbadala za kuzuia kukatika umeme wakati wa matengenezo hivyo kupelekea uchumi wa nchi kukua kwa kasi.” Alisisitiza Kitwanga.
Kitwanga aliendelea kusema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imejipanga kuhakikisha kuwa nishati ya umeme inachangia katika kutimiza lengo la Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2025 ya kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2025 nchi ya Tanzania inaondoka kwenye kundi la nchi masikini duniani na kuwa nchi ya kipato cha kati.
Alisema kuwa katika nchi nyingi zilizopiga hatua kubwa katika ukuaji wa uchumi wake, nishati ya umeme imechangia kwa kiasi kikubwa mno na kusisitiza kuwa Wizara ya Nishati na Madini imejizatiti kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakua kupitia mchango wa sekta ya nishati.
Wakati huo huo akielezea hali ya umeme katika mkoa wa Pwani, Meneja Mwandamizi wa Tanesco Kanda ya Dar es Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mugaya alisema kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Septemba mwaka huu Shirika la Tanesco lilifanikiwa kuwaunganishia umeme wateja 10, 100 katika mkoa wa Pwani na kufikisha asilimia 21.3 lengo likiwa ni kufikisha asilimia 30 ifikapo mwaka 2015.
Mhandisi Mahende aliongeza kuwa kwa sasa shirika la Tanesco linaendelea na zoezi la ukarabati wa miundombinu ya umeme iliyochakaa na kuongeza kuwa ifikapo Februari mwakani tatizo la kukatika umeme mara kwa mara litakuwa limekwisha kabisa.
Akielezea changamoto Shirika la Tanesco linalokumbana nazo katika shughuli zake katika mkoa huo, Mhandisi Mahende alitaja kuwa ni pamoja uchakavu wa miundombinu ya umeme na kusisitiza kuwa ukarabati bado unaendelea katika maeneo yaliyoathirika.
Mhandisi Mahende aliendelea kusema kuwa changamoto nyingine ni pamoja na madeni sugu kwa wateja na kuongeza kuwa hadi sasa Shirika linadai shilingi bilioni 16 wateja mbalimbali na kusisitiza kuwa Tanesco imepanga mikakati mipya ya ukusanyaji wa madeni hayo.
Alibainisha changamoto nyingine kuwa ni pamoja na wizi wa umeme, na madai ya fidia katika utekelezaji wa mradi wa umeme wa awamu ya kwanza uliokuwa unafadhiliwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) na kuongeza kuwa wananchi walidai fidia iliyokuwa kubwa kuliko gharama za mradi.
MISA TANZANIA YAKUTANA NA MAAFISA HABARI KUJADILI CHANGAMOTO ZA UTOAJI TAARIFA
Afrika(MISATAN) Bwana Andrew Marawiti akizungumza jambo wakati akifungua
kongamano na maafisa habari wa taasisi za serikali zilizofanyika jana jijini
Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu
Maafisa habari mbalimbali
kutoka wizara na mihimili tofauti ya nchi, jana walikutana katika hoteli ya JB
Belmont hapa Dar es Salaam kujadili changamoto wanazo kumbana nazo wakati kwa kutoa taarifa kwa wananchi.
kutoka wizara na mihimili tofauti ya nchi, jana walikutana katika hoteli ya JB
Belmont hapa Dar es Salaam kujadili changamoto wanazo kumbana nazo wakati kwa kutoa taarifa kwa wananchi.
Kongamano hilo linafuatia matokeo ya utafiti wa upatikanaji taarifa kwenye taasisi za umma uliofanywa na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) nakuzinduliwa rasmi siku ya tarehe 28 Septemba, ambayo pia ni Siku ya Kimataifa ya Haki ya Kupata Taarifa.
Miongoni mwa taasisi zilizoshiriki katika kongamano hilo ni Bunge, Mahakama, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Nishati na Madini, Idara ya Habari Maelezo, Mamlaka ya Taifa ya Vitambulisho (NIDA) na Idara ya Taifa ya Takwimu. Wizara za Afya na Mambo ya Nje hazikuweza kuwakilishwa licha ya kupata mwaliko.
Organization of Legal Assistance-nola) Bwana James Malenga akisisitiza
jambo alipokuwa anawasilisha mada yake kwenye kongamano hilo la maafisa habari
wa taasisi za kiserikali lililoandaliwa na Misa-Tanzania.
Gasirigwa akitoa ufafanuzi kwenye mada aliyokuwa anaiwasilisha kwenye
kongamano la maafisa habari wa taasisi za kiserikali(hawapo picha)
anazozipata anapokuwa anakwenda taasisi na idara mbalimbali za serikali
kupeleka barua ama maombi ya taarifa.
yake ilivyopokea Tuzo ya Kufuli na ambavyo imekuwa chachu ya mabadiliko katika
kutoa taarifa kwa umma.
Nyantori akielezea changamoto za utoaji taarifa katika taasisi na idara za
serikali.
Taarifa serikalini kutoka kwa mwanasheria wa kujitegemea Bwana James Marenga.
Bwana Andrew Marawiti akitoa shukrani wa wageni waliofika kwenye
kongamano hilo.
NHC yaelezea namna ilivyosaidia vijana kupitia mradi wa ufyatuaji wa matofali na ujenzi wa nyumba za gharama nafuu
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo, akimpa maelezo ya ujenzi wa
nyumba za gharama nafuu Mkuu wa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Bi Susan
Omari alipotembelea mradi huo ulioko eneo la Isikizya Wilayani Uyui
jana. (Picha kwa hisani ya Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa
Jamii cha Shirika la Nyumba la Taifa)
Mwonekanao wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Isikizya Mkoani Tabora.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo akiendelea kutoa maelezo ya mradi
kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Bi Susan Omari
Nyumba
38 zilizojengwa karibu kabisa na Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui eneo la
Isikizya. Nyumba zingine 12 zimejengwa upande wa pili wa barabara eneo
la Isikizya.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari akitoa maelekezo kwa Meneja wa Mkoa wa Tabora Bw. Chilambo
Msimamizi
wa mradi wa NHC isikizya Bw. Tokimu Mondo akitoa maelezo ya utekelezaji
wa mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya jana.
Sehemu ya nyumba zilizojengwa katika mradi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya Wilayani Uyui zinavyoonekana.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Chilambo akitoa maelezo kwa Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Bi. Susan Omari yanayohusu viwanja vya
Shirika vilivyoko eneo la Itetemia Manispaa ya Tabora.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo akielezea hatua mbalimbali
zilifikiwa na Mkoa huo za kutengeneza nyumba za Shirika. Hili ni
mojawapo ya jengo la Hoteli ya Golden Eagle baada ya kufanyiwa
matengenezo.
Sehemu ya mtaa wa Jamhuri/Shule wenye nyumba zilizofanyiwa matengenezo makubwa na NHC Mkoa wa Tabora
Mojawapo wa jengo lililofanyiwa matengenezo na NHC Mkoa wa Tabora linavyoonekana kwa sasa
Sehemu
ya Maafisa Vijana wakisikiliza mada iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari (hayuko pichani)
alipoelezea mpango wa NHC wa kugawa mashine kwa ajili ya kusaidia vijana
kwenye Halmashauri zote za Wilaya hapa nchini. Jumla ya mashine 656
zimeshambazwa kwa ajili hiyo.
Washiriki wa semina iliyotolewa na NHC wakisikiliza mada kwa makini
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari
akitoa mada juu ya mpango wa NHC wa kusaidia vijana mashine za
kufyatulia matofali katika Halmashauri zote za Wilayanchini.
MKURUGENZI MKAZI WA UNESCO AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA
SSRA yajipanga kuboresha Sekta ya Hifadhi ya Jamii.
Mkoa wa Katavi kuzindua kampeni ya kutokomeza magonjwa ya surua rubella
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt
Rajabu Rutengwe akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake hawapo
pichani wakati akielezea mkoa kufanyakuzindua kampeni ya chanjo ya
magonjwa ya surua na Rubella kuzinduliwa leo nchini ambapo mikoa 16
inshiriki na katavi ikiwemo,katika mkoa wa Katavi zinafanyika
Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo.
………………………………………………………………
Na Kibada Kibada-Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt
Rajabu Rutengwe amesema Mkoa wa Katavi kupitia mpango wa Taifa wa
chanjo na wadau mbalimbali utaendesha kampeni shirikishi ya
chanjo dhidi ya Surua Rubella, matone ya vitamin A, utoaji wa dawa za
minyoo na kinga dhidi ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele.
Akizungumza katika mkutano wa
Waandishi wa Habari Dkt Rajabu Rutengwe ameeleza kuwa katika kampeni
hiyo chanjo ya surua-rubella itatolewa kwa watoto wote wenye umri kati
ya miezi tisa hadi miaka mitano.
Matone ya Vitamini A’yatatolewa
kwa watoto wenye umri kati ya miezi sita na miaka mitano, dawa dhidi ya
minyoo itatolewa kwa watoto wenye umri kati ya mwaka mmoja na miaka
mitano, kinga tiba dhidi ya matende, mabusha au ngiri maji na usubi kwa
wenye umri wa miaka mitano na kuendelea.
Mkuu wa Mkoa alisema Kampeni ya
Chanjo ya surua inaendeshwa ikiwa ni muendelezo wa utaratibu wa kufanya
kampeni kila baada ya miaka mitatu, utaratibu huu unaotokana na ukweli
kwamba baadhi ya watoto hukosa chanjo ya surua katika utaratibu wa
kawaida ,pia watoto 15 kati ya 100 wanaopewa chanjo ya surua
hawajijengei kinga ya mwili ya dhidi ya surua, hali hii husababisha
kutokea milipuko ya surua.
Amesema Wizara ya Afya na
ustawi wa Jamii kupitia Mpango wa Chanjo imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa
ugonjwa wa surua,kila mtu anayejitokeza na dalili za surua sampuli
huchukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara,sampuli huchukuliwa kwa
ajili ya uchunguzi wa kimaabara, Sampuli nyingi zilizochukuliwa
zilithibitika kuwa ni ugonjwa wa Rubelle .
Akaongeza kuwa ugonjwa wa
Rubella una dalili zinazofanana na surua ingawa husababishwa na vimelea
tofauti, njia za kuthibiti magonjwa haya mawili zinafanana ,kwa
kuzingatia haya shirika la Afya ulimwenguni (WHO) liliamua kuunganisha
chanjo ya surua na Rubella ili kuongeza ufanisi wa rasilimali na pia ni
mkakati wa kidini kutokomeza surua na Rubella kwa pamoja ifikapo mwaka
2020.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa
Mkoa wa Katavi Dkt Yahaya Husein anaeleza kuwa lengo kuu la kufanya
kampeni hii ni kudumisha upungufu wa magonjwa ulemavu na vifo
vinavyotokana na surua na Rubella,pamoja na kutoa matone yaVitamini A’na
dawa ya kukinga ugonjwa minyoo tumbo,usubi,mabusha na matende,ngirimaji
ili kutibu maradhi na kuimarisha afya.
Naye Katibu Tawala mkoa wa
Katavi Mhandisi Emmanuel Kalobelo ameleza kuwa katika kampeni hiyo Mkoa
wa Katavi umelenga kutoa chanjo ya surua –Rubella kwa watoto wapato
392,174,walengwa wa matone ya vitamin A’watoto 107,609,walengwa,wa kinga
tiba dhidi ya magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni watu
451,683,na walengwa wa dawa dhidi minyoo ni 95,652.
Huduma hizi zitatolewa katika
vituo maalum ambavyo vitahusisha vituo vya kutolea huduma za Afya ,Shule
za Msingi,Sekondari na maeneo mengine yaliyopangwa.
Subscribe to:
Posts (Atom)