TAN

Bayport

Kikoa

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Saturday, March 22, 2014
USAID yatoa elimu ya lishe Zanzibar
TASWIRA ZA RAIS KIKWETE BAADA YA KUHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA MJINI DODOM MACHI 21, 2014
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongozwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
Katiba Mhe Samuel Sitta mara baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa
mjini Dodoma Machi 21, 2104
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
Katiba Mhe Samuel Sitta mara baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa
mjini Dodoma Machi 21, 2104
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akipewa pongezi kwa hotuba nzuti na Makamu
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Samia Suluhu Hassan mara
baada ya kulihutibia Bunge hilo Ijumaa mjini Dodoma Machi 21, 2104
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar Dkt Mohamed Ali Shein,
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe Samuel Sitta na Makamu
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Suluhu Samia Hassan
wakifurahia jambo mara baada ya Rais kulihutibia Bunge hilo Ijumaa
mjini Dodoma Machi 21, 2104
PICHA NA IKULU
MATEMBEZI YA UVCCM KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO YAZINDULIWA
WANAFUNZI WANAWAKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DAR WAWEKA HISTORIA, WAANZISHA MFUKO WA KUWAKOMBOA KIELIMU
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO
…………………………………………………………………………………………….
Na Aron Msigwa – MAELEZO, Dar es salaam.
Wanafunzi wanawake wa Chuo cha
Elimu ya Biashara Dar es salaam (CBE) wamezindua mchakato wa kuanzisha
mfuko wa Jumuiya ya wanafunzi wa kike wenye lengo la kumkomboa na
kumwezesha mwanafunzi wa kike kujitambua, kielimu, kisiasa na
kiutamaduni.
Akizungumza na jumuiya ya
wanafunzi wa kike wa chuo hicho wakati wa uzinduzi wa mfuko huo leo
jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Wizara ya
Viwanda na Biashara Dkt. Mery Mwangisa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika
hafla hiyo amesema kuwa kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni ishara ya umoja
na mshikamano wa wanafunzi wa kike chuoni hapo.
Amesema kuanzishwa kwa mfuko
huo kunatokana na kuongezeka kwa changamoto mbalimbali zinazowakabili
wanawake pia kukosekana kwa mifuko ya aina hiyo katika taasisi nyingi
za elimu ya juu hapa nchini.
Ameeleza kuwa malengo ya
mfuko huo ni kumwezesha mwanafunzi wa kike wa CBE kujitambua kielimu,
kisiasa na kiutamaduni na kuongeza kuwa yamekuja wakati muafaka
kufuatia mabadiliko yaliyopo sasa ya kiuchumi, kisiasa, kijamii na
kiutamaduni.
Amefafanua kuwa mfuko huo
ulioanzishwa katika chuo hicho ni fursa pekee ya kuwawezesha wanafunzi
wa kike kunufaika kwa kupata elimu bora bila vikwazo.
“Napenda kutumia fursa hii
kuushukuru uongozi wa chuo hiki kwa kuonyesha njia ya kuwajali wanawake
na pia katika kuweka taratibu nzuri za kulinda maadili, katika maisha
yangu sijawahi kusikia chuo kikuu chochote kimezindua jukwaa la wanawake
lenye malengo mazuri kama yenu” Amesema Dkt. Mwangisa.
Ameeleza kuwa kwa muda mrefu
wanawake kote nchini wamekuwa na juhudi mbalimbali za kujikomboa
kiuchumi pamoja na kulitumikia taifa kwa kushika nyadhifa mbalimbali
serikalini kwa ufanisi mkubwa na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa
bidii pindi wanapokabidhiwa madaraka.
“Ninapowaangalia ninyi nafarijika maana naona viongozi wakuu wa serikali, naona marais na pia wakurugenzi wa biashara”
Akizungumza kuhusu kuanzishwa
kwa mfuko huo na mafanikio yake Dkt. Mwangisa amesema kuwa atatoa
ushirikiano kwa wanafunzi hao ili kuhakikisha kuwa mfuko huo unajengewa
uwezo wa kusimama na kuwanufaisha wanawake wanaokumbwa na changamoto
zinazokwamisha maendeleo yao ikiwemo ukosefu wa fedha.
Amesema kuwa kukamilika kwa
taratibu za jumuiya hiyo ikiwemo maandalizi ya katiba ya jukwaa hilo
kutaliwezesha jukwaa hilo kupanga, kuandaa na kutekeleza mikakati
mbalimbali ya kujiendesha ili kuwawezesha wanafunzi hao kutatua
changamoto zinazowakabili kwa kulinda heshima yao katika jamii.
Kwa upande wake mjumbe wa Bodi
ya Taaluma ya Chuo hicho Dkt. Ellen Oturu Okoedion amesema kuwa
wanafunzi wa kike wa chuo hicho wanahitaji msaada kupitia mfuko huo
utakaowawezesha kupambana na wimbi la wanafunzi wa kike kushindwa
kumaliza masomo yao kwa kushindwa kumudu gharama za masomo.
Amewataka wanafunzi wa kike wa
chuo hicho kutumia ipasavyo taaluma wanayoipata kusaidia mfuko huo
kupata fedha ili uwe endelevu kwa maendeleo ya wanawake na chuo hicho.
“Ninyi mnasoma elimu ya
biashara na ndio watalaam wenyewe sitarajii mfuko wenu ukose uwezo,
naamini mtatumia taaluma yenu mnayoipata hapa chuoni kutafuta fedha kwa
kuwa mnao uwezo huo” Amesisitiza Dkt. Ellen.
Naye Waziri wa Wanawake wa
Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Bi. Mwajuma Sangali ameeleza kuwa
wanawake kote nchini wana jukumu la kuandaa kizazi cha watu wenye
upendo, uzalendo, kupenda kazi na maendeleo.
Amesema kuanzishwa kwa chombo hicho kunalenga kuboresha maisha ya wanawake hasa katika masuala ya elimu,jamii,uchumi na siasa.
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KULIHUTUBIA BUNGE MAALUM LA KATIBA, TAREHE 21 MACHI, 2014, DODOMA
Mheshimiwa Samuel Sitta, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar;
Mheshimiwa Balozi Seif Ali Iddi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Mheshimiwa Anne Semamba Makinda; Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano;
Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, Spika wa Baraza la Wawakilishi na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba ;
Mheshimiwa Rashid Othman Chande, Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Othman Makungu, Jaji Mkuu wa Zanzibar;
Viongozi Wakuu Wastaafu;
Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba;
Waheshimiwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana;
Pongezi
Nakushukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti kwa kunipa fursa ya kuja
kuzungumza na Waheshimiwa Wajumbe wa Bunge letu Maalum la Katiba katika
siku hii muhimu na ya kihistoria kwa nchi yetu. Nimekuja kuwatakia heri
na naungana na Watanzania wenzetu wote kuwaombea baraka za Mwenyezi
Mungu, ili muweze kuifanya kazi yenu kwa utulivu, hekima, umakini mkubwa
na kuimaliza kwa salama na kwa mafanikio yanayoyatarajiwa na
Watanzania.
Natoa
pongezi nyingi kwako na kwa Makamu wako kwa kuchaguliwa kwenu kuongoza
Bunge hili maalumu na la kihistoria. Ushindi mkubwa mliopata ni
kielelezo tosha cha imani kubwa na matumaini waliyonayo Wajumbe wenzenu
kwenu. Matumaini yao ndiyo matumaini ya Watanzania wote, kwamba
mtaliongoza vizuri Bunge hili, ili liweze kutimiza kwa ufanisi mkubwa
jukumu lake muhimu sana katika historia ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti;
Niruhusu
pia niwapongeze kwa dhati Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba kwa
bahati ya aina yake waliyopata ya kutunga Katiba mpya ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania. Fursa hii hutokea mara chache sana katika
historia ya nchi yo yote na watu wake. Mkifanikiwa kuipatia nchi yetu
Katiba nzuri majina yenu yataandikwa kwa wino wa dhahabu, katika
kumbukumbu za historia ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ni
matarajio ya Watanzania kuwa mtatunga Katiba itakayokubalika na wengi.
Katiba inayotekelezeka. Katiba itakayoimarisha Muungano wetu kwa
kuondoa changamoto zilizopo sasa. Katiba itakayoipa nchi yetu mfumo
bora wa kuongoza na kuendesha mambo yetu. Katiba itakayoimarisha umoja,
upendo, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Tanzania,
licha ya tofauti zao za asili za upande wa Muungano na maeneo watokako,
au tofauti za jinsia, rangi, kabila, dini na ufuasi wa vyama vya siasa.
Katiba itakayodumisha amani, usalama na utulivu nchini. Katiba
itakayostawisha zaidi demokrasia, haki za binadamu, utawala wa sheria,
utawala bora na kudhibiti maovu. Na, mwisho ingawaje siyo mwisho kwa
umuhimu, Katiba itakayoweka mazingira mazuri kwa uchumi wa nchi kukua,
na wananchi wengi kunufaika sawia na maendeleo yatayopatikana
www.baloziwademokrasiatanzania.blogspot.com
Rais Dkt. Jakaya Kikwete azindua rasmi Bunge Maalum la Katiba.
![]() |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea salama ya heshima kutoka Jeshi la Polisi kabla ya hotuba ya uzinduzi wa Bunge maalum la Katiba leo mjini Dodoma. |
![]() |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride liliandaliwa na Jeshi la Polisi kabla ya hotuba ya uzinduzi wa Bunge maalum la Katiba leo mjini Dodoma. |
![]() |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutuba Bunge Maalum la Katiba wakati wa sherehe za uzinduzi wa Bunge hilo leo mjini Dodoma. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya Pamoja na Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Leo Mjini Dodoma. |
(Picha na Idara ya Habari-MAELEZO)
Posted By Blogger to THE GOVERNMENT OFFICIAL BLOG
MKUU WA WILAYA YA NKASI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA INJINIA STELLA MANYANYA AFUNGUA RASMI KAMPENI YA TOHARA KWA WANAUME MKOANI RUKWA
Mkuu
wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kimanta akihutubia katika hafla fupi ya
uzinduzi rasmi wa kampeni ya Tohara kwa wanaume Mkoani Rukwa
iliyofanyika kimkoa katika Tarafa ya Challa Wilayani Nkasi. Akihutubia
katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Injinia Stella Manyanya
Mkuu huyo wa Wilaya amesema hadi kufikia mwezi wa tisa mwaka huu 2014
Mkoa wa Rukwa unatakiwa uwe umeshafanya tohara za wanaume 22, 000 ikiwa
ni agizo la kitaifa ambapo hadi sasa jumla ya wanaume 7,000
wameshafanyiwa tohara.
Kwa
mujibu wa mratibu wa zoezi hilo Mkoani Rukwa tangu kampeni hiyo ianze
tarehe 17 Machi 2014 hadi jana tarehe 20 Machi 2014 jumla ya wanaume 583
wameshafanyiwa tohara ndani ya siku 4 katika kituo kilichopo tarafa ya
Challa. Kampeni hiyo inaenda sambamba na zoezi la upimaji wa VVU ambapo
kati ya wananchi 699 waliopimwa ni mmoja tu amekutwa na maambukizo ya
virusi hivyo katika tarafa hiyo ya Challa.
Akizungumzia faida za tohara kwa wanaume amesema husaidia kupunguza uwezekano wa akinamama kupata kansa ya kizazi pamoja na kusaidia kuepusha uwezekano wa maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 50%.
Katibu
Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa akiwasalimia wananchi wa
tarafa ya Challa waliojitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa Kampeni
hiyo.
Mganga
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Daktari John Gurisha akizungumza katika hafla
hiyo. Akizungumzia juu ya zoezi hilo la tohara amesema tohara kwa
wanaume husaidia kuepusha uwezekano wa maambukizi ya virusi vya ukimwi
kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 50%.
Zoezi la Tohara likiwa linaendelea katika zahanati ya Challa.
Mkuu
wa Wilaya ya Nkasi Iddi Kimanta akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa wa
Rukwa Ndugu Smythies Pangisa awasalimu wananchi wa Challa.
Katibu
Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa (wa nne kulia) akiwa katika
picha ya pamoja na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. John Gurisha
(watatu kulia), Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa Albinus Mugonya
(wa tano kulia) na watumishi wa Idara ya Afya katika Hospitali Kuu ya
Mkoa wa Rukwa (kulia) mara baada ya uzinduzi wa kampeni hiyo.
(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)
SERIKALI KUTOA RUZUKU KWA WAVUVI ILI KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI NCHINI
Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa wamefika kwenye kisiwa cha Bongoye.
Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na baadhi ya waandishi wa habari, wakielekea kwenye sehemu ya kufanyia mkutano.
Msemaji
wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Mohammed Bahari akizungumza na
waandishi wa habari juu ya ruzuku kwa wavuvi.Katikati ni Afisa Habari wa
Idara ya Habari (MAELEZO) Frank Mvungi na mwisho ni Mkurugenzi Msaidizi
wa Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi.
Meneja
Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk.
Milali Machumu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo
pichani).Katikati ni Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Mohammed
Bahari na mwisho ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank
Mvungi.
Mkurugenzi
Msaidizi wa Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi,
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu ruzuku kwa
wavuvi.Katikati ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Frank
Mvungi na mwisho ni Msemaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk. Mohammed
Bahari.
Baadhi
ya waandishi wa habari wakimsikiliza Msemaji wa Wizara ya Mifugo na
Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Mohammed Bahari akizungumza na
waandishi wa habari juu ya ruzuku kwa wavuvi.
Baadhi
ya Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na waandishi wa habari,
wakiteremka kutoka kwenye Boti baada ya kuwasili kwenye hoteli ya Sea
Cliff wakitokea kisiwa cha Bongoye ambako ndiko kulikofanyika mkutano na
waandishi wa habari. Picha zote na Hussein Makame
………………………………………………………………………….
Frank Mvungi- Maelezo
SERIKALI
imetenga Shilingi Bilioni 1.9 kwa ajili ya ruzuku kwa wavuvi katika
kipindi cha mwaka wa Fedha 2013/14 ili kusaidia kukuza sekta ya uvuvi
hapa nchini
Hayo
yamesemwa na Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt.
Mohammed Bahari wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar
es salaam.
Dkt
Bahari amesema kuwa ruzuku hiyo itatolewa kwa kuzingatia vigezo ikiwemo
waombaji kuwa na vyama vya ushirika na vilivyosajiliwa kisheria.
Alitaja
vigezo vingine kuwa ni chama cha ushirika kiwe kinafanya kazi za uvuvi
kufuatana na sheria ya uvuvi na 22 ya mwaka 2003 na kanuni za uvuvi za
mwaka 2009 na miongozo mbalimbali.
Aliongeza
kuwa chama hicho kiwe na akaunti benki iliyo hai na kithibitishe kuwa
na uwezo wa kuchangia asilimia 40% ya gharama ya mradi husika, ambapo
Serikali itachangia asilimia 60% ya gharama ya mradi husika.
“Chama
husika kitapitisha maombi yao kwa Mkurugenzi wa Halmashauri husika kwa
ajili ya kupitia maombi hayo na kuona kama yanakidhi vigezo viliwekwa na
baada ya hapo kuwasilishwa Wizarani” alisema Dk. Bahari.
Alisema
miradi itakayofadhiliwa ni pamoja na ununuzi wa boti za uvuvi, injini
na vifaa vingine vitakavyowawezesha wavuvi kuongeza tija katika shughuli
za uvuvi
Dkt
Bahari alifafanua kuwa ruzuku hiyo kwa wavuvi itakuwa na manufaa
makubwa kama vile kuongeza mapato ya wavuvi na wafanyabiashara wa mazao
ya uvuvi.
Aliongeza
kuwa ruzuku hiyo pia itaongezeka maduhuli ya Serikali, kupunguza
vitendo vya uvuvi haramu,kuimarika kwa biashara ya mazao ya uvuvi na
kuongeza ajira katika sekta ya uvuvi.
Naye
Mkurugenzi Msaidizi Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi, Baraka Mngulwi
alitoa wito kwa wale wote wanajihusisha na vitendo vya uvuvi haramu
kuacha tabia hiyo mara moja kwa kuwa Serikali imeimarisha doria katika
maeneo yote .
Aliongeza
kuwa kwa wale wanatumia nyavu ambazo zimepigwa marufuku nao waache
mara mara moja tabia hiyo na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa
wale wote watakaokwenda kinyume cha sheria ya uvuvi na. 22 ya mwaka 2003
na kanuni zake za mwaka 2009.
Alizihimiza
Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa sheria za uvuvi na kanuni zake
zinazingatiwa kikamilifu na kuwa uvuvi haramu na biashara ya samaki
wachanga vinadhibitiwa katika maeneo yao.
HOTUBA YA KIKWETE WAPINZANI WAISASAMBUA
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu. mchimati@gmail.com au
Dodoma.
Wenyeviti
wa vyama vya Upinzani vya Chadema, Chama cha Wananchi (CUF) na Chama
cha NCCR-Mageuzi, jana usiku walikutana ili kutoa kauli ya pamoja,
kutokana na hotuba ya ufunguzi wa Bunge kwa maelezo kuwa tayari Rais
amevuruga mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya.
Wakati
viongozi hao wakikutana, Mwenyekiti wa Chama cha DP Mchungaji,
Christopher Mtikila alisema, Rais ameingilia mchakato na kutoa maelezo
jinsi ya kuandika Katiba.
Wakizungumza
na wanahabari wa Full Utamu mara baada ya hotuba hiyo, Freeman Mbowe, James
Mbatia na Profesa Ibrahim Lipumba, walisema wameipokea kwa masikitiko
makubwa hotuba hiyo.
“Tunakwenda kujadili hotuba ya Rais na tutatoa msimamo wetu,” alisema Mbowe.
Awali
Katibu wa muda wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Julius Mtatiro
alisema Rais Jakaya Kikwete amevuruga mchakato wa Katiba, kwani
walitarajia angetumia mamlaka yake kama Rais kuwaunganisha.
“Rais
tulitarajia angeongea kama mkuu wa nchi, lakini amezungumza kama
Mwenyekiti wa CCM na kutoa msimamo juu ya muundo wa Muungano jambo
ambalo hatukulitegemea,” alisema Mtatiro.
Alisema kwa Rais kutoa msimamo ni sawa na mwongozo jambo ambalo limevuruga mchakato mzima.
Hofu ya kuvunjika Bunge
Wakizungumza nje ya Bunge, baadhi ya wajumbe wameeleza kuwa hotuba ya
Rais Kikwete kama ikitekelezwa uwezekano wa kupata Katiba Mpya utakuwa
mgumu.
Mjumbe
Luhaga Mpina alisema kwa jinsi rasimu ilivyoandikiwa na kama muundo wa
serikali mbili ukipita basi rasimu ya Katiba itabidi iandikwe upya.
“Rasimu yote imetengenezwa kwa mfumo wa serikali tatu sasa hapa kuna hatari ya Bunge kukwama ,” alisema.
Mtatiro
kwa upande wake alisema sasa kuna hofu ya kushindwa kupatikana Katiba
Mpya kwani Rais amewachanganya wajumbe na kama watapitisha maoni yake
itabidi rasimu kuandikwa upya.
Mjumbe Mustapha Akoonay, alisema upatikanaji wa katiba upo shakani kwani sasa upinzani utakuwa mkubwa juu ya muundo wa muungano.
“Kwa sasa nadhani itabidi turudi upya kwa wananchi kupata kura ya maoni juu ya muundo wa muungano,” alisema.
Lucy
Owenya alisema Rais amegeuza mkutano wa Bunge kuwa ni mkutano wa Chama
Cha Mapinduzi, kwani ameshindwa kabisa kutoa mwelekeo wa nchi na badala
yake ametoa msimamo wa CCM.
“Kutokana
na hili, naamini kabisa Bunge halitakuwapo na ni bora iwe hivyo kwa
kuwa amejibu hotuba ya Warioba na kwa maana hiyo amepingana na mawazo ya
wananchi.”
Godbles Lema alisema kuwa Rais hakuja kuhutubia taifa bali alikuja kufanya semina na kujibu hotuba ya Warioba.
Mjumbe
huyo ambaye ni mbunge wa Arusha Mjini alionyesha shaka kuwa baada ya
muda wa wiki tatu hakutakuwa na Bunge la Katiba kwa kuwa wako baadhi ya
watu ambao hawatakubali kilichofanywa na Rais Kikwete.
“Waliochukua
fedha ni vyema wakaenda kumalizia nyumba zao kwa kuwa kiongozi wetu
amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwafurahisha wanaCCM lakini kwa
Watanzania hatutakubali,” alisema Lema.
John
Cheyo alisema, “Mimi ninachokiona ni maridhiano tu, suala la kufumua
rasimu halinipi shida kwa kuwa vitu vyote vinavyoletwa bungeni huwa ni
mali ya Bunge na hivyo tutafanya tunavyoona sisi inafaa.”
Mchungaji
Peter Msigwa, alisema kuwa kosa kubwa ambalo lilifanywa na upinzani ni
kukubali na kuruhusu Jaji Warioba atangulie kuwasilisha rasimu yake
akasema hilo ndilo lililowagharimu.
Alitaka
Bunge livunjwe mara moja ili warudi kwa wananchi wakaamue na kuwahukumu
kutokana na kile ambacho walikifanya katika Bunge ambalo kwa maoni yake
wamekula fedha za walipa kodi bure.
Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa aliipongeza hutuba ya Rais Jakaya Kikwete ya uzinduzi wa Bunge la Katiba.
Lowassa
ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge la Katiba, alisema kwa kifupi hotuba ya
Rais Kikwete ni nzuri. Lowassa alitoa kauli hiyo, wakati akitoka nje ya
Bunge, muda mfupi baada ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza hotuba ya
uzinduzi wa Bunge hilo.
Naye Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Mchungaji Ernest Kadiva, alisema hotuba ya Rais imetoa mwanga kwa wajumbe.
“Rais
ameonyesha upungufu wa hoja mbalimbali hasa katika mfumo wa serikali
tatu na sasa ameacha kazi ya kuamua tuwe na mfumo wa serikali mbili au
tatu ni ya wajumbe,” alisema Mchungaji Kadiva.
Hata
hivyo, mjumbe mmoja ambaye hakupenda kutaja jina lake alisema Rais
alizungumza kama si mkuu wa nchi bali Mwenyekiti wa CCM kwa sababu
amesimamia hoja za chama chake.
Alisema
hata kama mapendekezo ya Rais Kikwete yatatekelezwa, kamwe hayatakuwa
mwarobaini wa muungano. Mbunge wa Mwibara, Khangi Lugora alisema hotuba
hiyo waliitarajia na ndio maana kulikuwa na ubishi wa nani atangulie
kati ya Jaji Joseph Warioba na yeye kwa mujibu wa kanuni.
“Hotuba
ilikuwa ikijaribu kumjibu Jaji Warioba na kwangu mimi nilikuwa naona
kuwa Rais naye alikuwa anachangia katika kuitunga Katiba kwa kupitia
hotuba yake hiyo. Tumeyasikia na sisi tutakwenda kutafakari katika
kutunga Katiba ambayo itakuwa ya Watanzania wote,” alisema.
Kwa
upande wake Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) Mkiwa Kimwanga, alisema
kilichofanyika ni Rais kwenda kutoa uamuzi juu ya mchakato uliokuwa
ufanywe na Bunge hilo.
Kwa
upande wake, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema hakuitendea haki Tume ya
Mabadiliko ya Katiba na kwamba Bunge hilo haliwezi kutengeneza Katiba
ambayo inalenga katika mfumo wa serikali la mbili.
“Itakuwa
ni vigumu zaidi kupata Katiba Mpya, alikuwa anapinga mambo ya msingi
yaliyoelezwa katika rasimu ya kwanza. Hayo angeyaeleza katika hatua ya
awali ili rasimu hiyo ibadilishwe na si katika hatua hii ya mwisho kabla
ya kwenda kupigiwa kura na wananchi,” alisema.
Alisema
ndani ya siku 70 haiwezekani kubadili rasimu hiyo ambayo imejikita
katika muundo wa serikali tatu kwenda katika muundo wa serikali mbili.
Ezekiah Olouch alitahadharisha wajumbe wenzake kutodharau maoni ya wananchi waliyoyatoa katika rasimu hiyo ya pili.
Alisema
haiwezekani tume zote ambazo zimeundwa kuangalia aina ya muundo wa
serikali zije na jibu moja kuwa namna ya kuimarisha muungano ni kuwapo
kwa serikali tatu.
Jussa Ismail Ladu alisema kwa ufupi kwamba hotuba ya Rais Kikwete imekuwa yenye sura ya CCM zaidi.
Naye
Mbunge wa Lulindi, Jerome Bwanausi, aliielezea hotuba ya Rais kuwa
imeibua mambo mengi ambayo baadhi ya watu walikuwa wakiyaelewa tofauti,
hivyo imeweka uelewa mzuri katika baadhi ya maeneo.
Profesa Costa Mahalu alisema ni hotuba ambayo imewaachia changamoto,
hasa katika eneo la muungano kwa sababu wanahitajika kuunda muungano
usiotetereka.
Chanzo: Mwananchi.
Subscribe to:
Posts (Atom)