TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, December 29, 2011

Gari likiwa limeacha njia na kutumbukia mtaroni kutokana na Mvua zilizonyesha Mwishoni wa juma

Gari aina ya Scania lenye namba za Usajili T 143 ADJ , ambalo lilikuwa likitoka Morogoro kuelekea Dar es Salaam, baada ya kutumbukia katika Mtalo Eneo la Mbezi Magari Saba(Picha na Shaaban Mpalule)

SAFARI YA ERASMUS LUNAGA-WAKATI WA MAZIKO YAKE NA JINSI ALIVYOWAACHA WATU KATIKA MAJONZI

 Hii ni Familia yake,
 Getruda Mongela akiweka udongo wakati wa salamu za mwisho
 Kaka wa Marehemu Erasmus Lunaga akiweka Udongo
 Mke wa Marehemu, Mama Lunaga akiweka Udongo wakati wa maziko
Mke wa Marehemu, Mama Lunaga akiweka Udongo wakati wa maziko
 Mtoto wa Marehemu, Richard Lunaga(kati) na ndugu yake Rede Mkama  wakati wakiwa kanisani
 Baadhi ya watu waliofika kuaga Mwili wa Mpendwa wetu, Baba yetu Erasmus Lunaga
Mke na Watoto wa Marehemu Erasmus Lunaga wakati wa maombezi katika kanisa la Roman Mbezi

Sunday, December 25, 2011

ZULU PARADISE CLUB ILIVYOPAGAWISHA GONGO LA MBOTO



Hii ni katika Moja na mbili kusherehekea Siku Kuu ya Chrismass, Ukumbi wa Zulu Paradise-Gongolamboto Mtu wangu Hapatoshi, Si Disco Toto wala Watu wazima, Nyomi, Wameanza watoto katika shoo yao ya kutafuta wakali watoto wanaocheza kuliko wengine, Watoto kibao, kama hivyo- Chrismas hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee- Yesu Kazaliwa Upya, je  wewe upo nafasi ipi? au ndo umalaya, Uzinzi, Fitina, Wivu, Husda, Kiburi, Mnyimi, Mwizi, usali, ufanyi mazoezi, usaidii wenzako, unajitenga, mlevi, dhulumati, fisadi, tapeli, msengenyaji, mlawiti, mchawi, kidokozi, mvivu, na mto tii Amri za Mungu? Watoto kama unavyojua wao ni furaha tu.

Sunday, December 18, 2011

KAFULILA ATIMULIWA NCCR..POSHO MPYA HATAIFAIDI TENA




Mbunge wa Kigoma Kusini, David kafulia

CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimemfukuza uanachama Mbunge wa Kigoma Kusini, David kafulia na wajumbe wengine sita akiwamo aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, Hashim Rungwe.Uamuzi huo ulitolewa kwenye kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu (Nec) ya chama hicho kilichofanyika katika Ukumbi wa Poroin jijini Dar es Salaam jana, ambao ulitawaliwa na vurugu mpaka polisi wakaitwa ili kuongeza ulinzi.
Baada ya uamuzi huo kutolewa Kafulila alikwenda kupiga magoti mbele ya Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia huku akibubujikwa machozi na kuomba radhi akisema: “Naomba radhi, nimekosa mnisamehe...”
Baada ya hapo Mbatia alisimama na kumwombea msamaha kwa wajumbe wa kikao hicho, lakini walikataa na kumweleza (Mbatia) kuwa akisamehewa watarudisha kadi zao za uanachama.“Hatutaki, Kafulila hatufai anakiharibu chama na akisamehewa sisi tutarudisha kadi zetu za uanachama ili ubaki naye kwenye chama...,” walisikia wajumbe hao wakisema kwa sauti ya juu.Wanachama wengine waliofukuzwa ni, Ally omari, Mbwana Hassan, Josam Rugugila, Lucy Kapya, Jamwe Batifa na Hashim Rungwe ambao walikuwa viongozi wa chama hicho.


Dalili za Kafulila kufukuzwa zilijionyesha wazi juzi baada ya wazee wa chama hichi kupitia kwa Katibu wao wa Taifa, Ernest Mwasada kuitaka Nec kumfukuza (Kafulila kwa kuwa ndiye chanzo cha migogoro yote inayoendelea ndani ya chama.
“Hizi vurugu zinachochewa na Kafulila ambaye ndiyo mfadhili na kiongozi wa waasi wa uchochezi huu. Menejimenti inapaswa kumwangalia sana, huyu ni hatari ndani ya chama hastahili kabisa kukaa na jamii yoyote inayopenda amani,” alisema Mwasada.
Hata hivyo, Kafulila juzi alikanusha akisema kuwa madai hayo ni ya uongo na kwamba, Katibu wa Taifa wa chama hicho anateuliwa na Katibu Mkuu ambaye amekosana naye.
“Ni hivi, Katibu wa Wazee wa Chama anateuliwa na Katibu Mkuu ambaye hatuelewani na juzi alifanya kikao kilichoeleza mambo mengi mabaya dhidi yangu," alisema Kafulila na kuongeza.
“Huyo Katibu wa Wazee amelishwa maneno na Ruhuza kwani ndiye mwajiri wake ambaye anafanya kazi maalumu ya kumchafua Kafulila na alifanya hivyo kwenye semina ya wenyeviti na makatibu wa chama 19 iliyomalizika jana (juzi) jijini Dar es Salaam.”
Kafulila alisema kazi ya Ruhuza ni kuwanywesha sumu viongozi wa chama kuwa yeye (Kafulila) ni mkorofi badala ya kuendesha semina kuhusu mambo ya msingi ya kukijenga chama.

HUU NDO UJIO WA SHINDANO LA MISS DEMOKRASIA TANZANIA.

 Kwa nini Tanzania kumsaka Miss DEMOKRASIA? 
 Miss Demokrasia Nigeria akiwa katika pozi
 
Demokrasia katika kumsaka Miss wa Tanzania wa Demokrasia shindano litokanalo na maono linafanyika ikiwa ni  motomoto juu ya imani yetu kwamba wanawake na vijana wetu ambao walikuwa awali kushoto nje ya utaratibu wa mambo, wana majukumu makubwa ya kucheza katika kuchagiza agenda yetu ya kisiasa, ikiwa ni katika  kuimarisha demokrasia yetu kujitokeza na actualizing Tanzania bora. Demokrasia katika kumsaka Miss Demokrasia Tanzania ikiwa pia  ni maadhimisho ya demokrasia yetu changa.

Utangulizi 
Miss Demokrasia Tanzania 2010, Rebeca Mdamu.
 
Muongo mrefu ya utawala wa kidikteta chini mbalimbali imekuwa kikwazo kikubwa kwa actualization ya demokrasia ya kweli. Nguvu chini ya utawala wa kijeshi, na katika Mtutu wa bunduki. Kwa kweli, ya kijeshi na tabia yake, ni ya mamlaka ya serikali zilivyo , syndrome na maadili vimekuwa adui wa utawala wa kidemokrasia katika mbalimbali. si wakati wa kihafidhina, kimabavu ni wakati wa marekebisho na ukombozi.

Haki za binadamu, hasa haki za wanawake na  nafasi ya ushiriki wa wanawake katika serikali. haki za binadamu pamoja na utamaduni wa kisiasa na kijamii ya Serikali. Kati ya 50 miaka, ikiwa pia ni maadhimisho ya Miaka ya Uhuru kwa Tanzania,

Demokrasia kama falsafa ya kisiasa ni lengo la maendeleo ya binadamu, ni kushukuru thamani ya mtu binafsina kutaka crystallize katika kipengele chochote cha jamii ya binadamu kwa njia ya kidemokrasia ya maisha.Yoyote ya mfumo wa kisiasa kuwa haina kusaidia mtu katika kufikia yake aliyopewa na Mungu tamaa namalengo hawezi kuwa imara.

Demokrasia ya kudumu huja wakati wananchi wana uwezo wa kutambua matarajio yao. Demokrasia yakweli lazima kuhakikisha uhuru hasa kutoka katika utumwa, aibu ubaguzi, na mambo hayo yote kudhoofishamaendeleo ya wanawake, pamoja na kutoa fursa kwa ajili ya utekelezaji binafsi.


Haki ya kushiriki katika mipango ya  kisiasa maana zaidi ya uchaguzi huru na wa haki. pia inahusu ushiriki nataarifa za wasichana ambao mara nyingi kushoto nje ya kutengeneza sera. Utulivu wa kisiasa ni hali ambayo inawezesha MENA na wanawake wa taifa kufikia kwa wenyewe, malengo ya busara na maadili kwa ajili yaambayo wao kuwa na sababu ya kushirikiana na kila mmoja. Ni katika mawazo ya haya kwamba "EditionMaiden ya kumsaka Miss Demokrasia Tanazania" ilikuwa mimba.


Malengo ya kumsaka Miss Demokrasia Tanzania:

-Kujenga uelewa mkubwa wa dhana na kutekeleza demokrasia

  miongoni mwa wanawake na vijana.
-Ili kuongeza ushiriki wa wanawake vijana katika michakato ya

  kisiasa.
-Wanawake vijana kutoa sauti katika kuunda mazingira ya kisiasa ya

  Tanzania
-Kuandaa wanawake vijana kwa ajili ya uongozi baadaye makini
-Kuchunguza vipaji, ubunifu na ubunifu wa wanawake vijana.
-Kutoa mazingira mazuri kwa ajili ya kujieleza binafsi na utambuzi

   wa ndoto ,Zinazozalishwa kwa ujasiri na  kujiamini katika
   wanawake vijana kuwa hamu ya kukabiliana na changamoto ya
   kuongea mbele ya umma.
-Kuendeleza roho ya urafiki na uzalendo miongoni mwa wanawake

   vijana.
-Kuendeleza mabadiliko chanya katika hali ya hewa ya kisiasa ya

   Tanzania
-Kuhifadhi na kutunza demokrasia yetu kujitokeza.
-Ili kuimarisha demokrasia yetu na kujenga utulivu wa kisiasa.


Miss Demokrasia Tanzania ni Mkakati na  moja ya kuimarisha Utawala kila Mwaka

Malkia wa Demokrasia Tanzania, watakuchukua Utekelezaji na  baadhi ya miradi ambayo ni pamoja na:
 * Safari nchini kote kwa lengo la  kushirikina na umma na kufanya
     mahojiano na vyombo vya habari
     * Kufanya ziara ya utetezi kwa viongozi wa jamii na bunge

        katika ngazi zote za serikali.
     * Kushirikiana na Wakala za Serikali, Mashirika ya Ushirika,

        Banks, Makanisa, Balozi, NGOs, CBOs, nk kutekeleza baadhi
        ya miradi ya maendeleo ya jamii na matendo ya upendo.
     * Kufanya ziara ya watoto yatima.
     * Kuandaa warsha ya wanawake na vijana uwezeshaji
     * Kuandaa mipango ya kuwawezesha makundi chini priviledged

        na wanyonge katika jamii
     * Kufanya mipango ya kutetea wanawake zaidi kushiriki katika 

        utawala.
Miss Demokrasia Malkia itakuwa na Golden Jubilee Press Mkutano wa Demokrasia Endelevu, Utawala Bora na Maendeleo ya Uchaguzi wa Mwaka 2015. Maelezo yanakuja hivi karibuni!

WEMA V/S JOKETI=PILATO

KWA HADITHI ILIYOTUFIKIA MUDA MFUPI FROM NOW NIKWAMBA KUNA MANENO ZIKO CHINI YA SAKAFU ETIIII!JOKETH ANAJIPANGA KUMBURUZA WEMA SEPETU MAHAKAMANI KWAA KUMCHAFUA...
NI vurugu mechi kati ya Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu (pichani) na namba mbili
wake, Jokate Mwegelo, mtifuano ni mzito lakini habari mpya ni kwamba sakata hilo linahamia kwenye mkondo wa kisheria.
Wema anamtuhumu Jokate kutoka kimapenzi na aliyekuwa mchumba wake, Naseeb Abdul ‘Diamond’, kitu ambacho kimesababisha wamwagane.
Kwa mujibu wa rafiki wa Jokate, Wema atasimamishwa kortini siku chache zijazo kujibu tuhuma za kumchafua mrembo huyo.
THAT KUTOKA KWA bongo codes

Mr Blue Afiwa na Mama yake Mzazi.


Mr Blue Akiwa Unguja , Dakika 30 Baada Ya Kushuka Kwenye Stage Apata Taarifa Mama Yake Mzazi Amefariki .
Nikiwa kama (mdau) nawapa pole, Mr.Blue na familia yake na wapa pole kwa kuondokewa na mama ke Mr.blue,R.I.P!Mungu watie nguvu.
Pole Sanaa Ma Friend Mr. Blue.

Saturday, December 10, 2011

HAYA NDIYO MATENDO YA CHIPS WA MISS UTALII TANZANIA

 WALAKA HUU NI BAADA YA KUMSIKIA AKIJITETEA KUPITIA KIPINDI CHA AMPLIFIRE, CLOUDS FM 

 Chips baada ya kura Uroda na kufanya uchafuzi wake


 Huyo mshiriki ni wa kati mbele( Irene Richard)
hapa huyo mshiriki anaonekana anekaa
Habari yako Ayo, mimi kwa ujumla sijambo sana, na pia nimatumaini yangu kuwa wewe na wenzako kina wasiwasi,kibonde,paul,babla,michuzi jr,lwambano,pamoja na wakuu wako wa kazi kina kaka zangu Ruge, charles, Kusaga.
Kwanza kabisa nimesikia kwamba ulinitafuta wakati wa mazungumzo yako na yule mwendesha shindano la Utalii, pengine ukuwa na namba yangu ya simu au ukutaka tu kunitafuta, kwani naamini kuwa namba yangu hapo ofisini kwenu wanayo watu wengi.

Na kama ni kuhusiana na suala langu na huyo kiepe, kwa kweli ni inshu ndefu sana, kwani pamoja na wingi wa maneno yake ya uongo kwako juu yangu pia nataka uamini kwamba huyo kiumbe ana tofauti na shetani.

Kwanza kitendo cha kuvuta Sigara muda wa masaa 24 kila sekunde, changanya na Pombe anazoongezea utagundua kwamba karibia Dunia yetu hii takatifu tutamkosa, maana hata huo mdomo wake kwa sasa ni sawa na tanuru la Mavi kwa kuwa nahisi linanuka kwa huo mchanganyiko wa bidhaa haramu ambayo aikuwekwa tuitumie na mkuu wa mbingu na Ardhi kwa kuwa ni dhambi.

Kitu cha msingi ambacho bila shaka unataka kukisikia kutoka kwangu ni kuhusu ukweli, juu ya kile alichokueleza na pia kuhusu shindano lake la Utalii kwa kuwa naamini kwamba wewe unatambua kwamba mimi ni mtu pekee ninayemfahamu kuliko mtu mwingine yeyote.

Ni kama historia vile pamoja na kwamba sikupenda kuyaweka wazi maneno haya, lakini kwa kuwa amenilazimisha kufanya hivyo, nami sina budi kuuweka wazi uaribifu, ujinga, ushenzi, wizi, utapeli, udanganyifu, ulaghai, uzinzi, ubakaji, uongo, unyonyaji, wivu, na utumwa wake.

1-uharibifu- nasema huyo jamaa ni mwaribifu kwa maana pamoja na kuwatumia wasichana wetu wa kitanzania kwa lengo la kujenga misingi ya jina la kampuni yake, pia uwaharibu kisaikorojia, kimwili  kutokana na matendo yake ya:-
(a)- kuwapotezea muda wao mwingi wawapo kwenye shughuli yake bila kupata manufaa
na maendeleo yoyote,
(b)- uwaharibu kimwili kwa kuwa utumia fulsa hiyo kuwalala kimwili kwa
kuwadanganya kwamba watapata nafasi za kwenda kushiriki nje ya nchi ama
kuwapa  maksi za ushindi ama kuwapa zawadi ya gari na mengine ya uongo kama
huo.
©- ni mjinga kwa kuwa uhamini sana Ushirikina, kwani tangu nimemfahamu huyo jamaa anaishi kwa kutegemea nguvu za giza, ana waganga si chini ya 100 hapa nchini, na uwezi kuhamini kwani pamoja na yote anadiriki pia kuwadanganya waganga wake, kuwanyima haki zao, pamoja na kugombana nao mara kwa mara kutokana na kutotimiza masharti wanayompa, hivyo yawezekana wao pia wakachangia kumfanya huyo bwege kuwa mwendawazimu ama nahisi tayari kichaa kimemuanza.
i-                  waganga wake watano wanapatikana eneo la Kigogo hadi mabibo, watatu wapo Vingunguti kiembe mbuzi, kwa simba mmoja, banana wawili, madafu 1, mwenge 2, kijitonyama 1, ubungo maziwa 3, kisukuru ya tabata 1 huyo sidhani kama ni mganga bali ni mchawi kutokana na maelezo yake wakati nikijaribu kumfahamu vizuri, maana huwa nawahoji kuhusiana na kazi zao hizo za nguvu za giza, tegeta 2, mwembe chai 1, mapipa 1, bagamoyo huko ndiko usiseme maana huwa wananichanganya sielewi huyu ni yupi na yule kwa kuwa unipeleka usiku na hata maeneo wanamofanyia kazi zao sidhami kama ni miliki zao, kwa kuwa wanapatikana kwenye magofu ya majengo ya kale yaliyojengwa na wakoloni, ni pachafu ukiingia, na hata ukiambiwa kesho yake uende mchana unaweza kushindwa kuingia kwenye majengo hayo, nahisi hata serikali haitambui uwepo wa wafanyabiashara hao haramu ndani ya majengo hayo ya kumbukumbu ya makumbusho, wakati mwingine nilihisi kuwa alikuwa akinipeleka kuzungumza na majini maana sidhani kama ni watu.
ii-               Wengine wanapatikana Miono kati kati ya Bagamoyo na Tanga, ambako pia hawapunguwi 5,  kati kati ya Bagamoyo na Dar es Salaam pia yupo mmoja, njia ya Kilwa yupo eneo la ikwiriri, na hapo sijaweka wa kijijini kwao ambako akunipeleka, je we uoni kama ni hatari mtu mmoja kuwa na waganga wa idadi kama hiyo? Je mtu kama huyo utamwina nani kama si Shetani? Na je mtu kama huyo kweli anayomatumaini ya kutenda mema kwa binadamu wenzie wakati yeye tayari amekwisha jiondoa kwenye njia nyoofu ya Mungu? Je unategemea mtu kama huyo asiwe mwizi, dhuruma, muongo, Tapeli, Mzinzi, mlaghai, ama mbakaji? Kubaka si lazima utumie nguvu, hata kumwingilia binti mwenye umri wa miaka 18 kwa uraghai, kumdanganya, ama kumfungia ndani kasha kutenda bila yeye kuwa ni hiyari, na angali umri wake na hao watoto anaowafanyia hayo, si Ubakaji kweli huo?
iii-            Je unahitaji niwataje watoto ambao nawafahamu ambao tayari walitendewa hivyo kwa nyakati tofauti iwe kwa hiyari yao ama kufungiwa vyumbani? Maana nina uhakika wazazi wa watoto hao baada ya kuwataja hakika watakwenda na mapanga, shoka, kumtoa roho, yawezekana hata wewe nduguyo kama aliwahi kujiingiza kushiriki hilo utalii lake akawemo, je wewe nduguyo kama alikuwa ni miongoni mwa hao nitakaowataja utachukua uhamuzi gani? Inasikitisha na ni hatari sana na ndiyo maana nilitumia busara ya kuwa msiri nikiwa na lengo la kumbadilisha tabia kitu ambacho nimeshindwa kutokana na akili yake kuwa imedidimizwa na nguvu za giza(Amekaliwa na Shetani),
iv-            Kati ya Ushenzi ambao sikutaka tena uendelee ndani ya Utalii wake huo wa kipumbavu ni kile kitendo cha kuwadhurumu Zawadi washindi wanaopatikana, uliza ni mrembo yupi kwenye huo utalii wake aliwahi kupewa zawadi kulingana na makubaliano? Je unazotaarifa kwamba Gari la zawadi ya Mshindi wa Mwaka 2011/12 ameliweka leani kwa mtu, baada ya kumtapeli huyo mrembo wa Utalii kwamba anakwenda kulipeleka kwenye matengenezo? Kama aliweza kuweka gari yake (Pajero) leani angeshindwa nini kuweka ya huyo Binti? Na kwa kuwa huyo binti masikini wa baba yangu kama si tajiri, baada ya kutumiwa kimwili yawezekana anaogopa kumfuata kwa kuwa anaweza kufungiwa tena geto na kuendelea kuharibiwa umalkia wake, fanya utafiti kwa huyo Binti, gari yake hiyo kwa nini amdhurumu? Na siku zote anapowapa ushindi hao warembo wake wa kwanza uwadanganya na kuwaraghai kuwa atamuoa, na kwamba yeye huyo ndiye chaguo lake, hivyo hata kama kuna mchumba wake aachane naye, lengo lake likiwa ni kama hivyo kwamba binti baada ya kuliwa sana uroda, atoweza kuthubutu kudai chochote hata kama ni zawadi ana kulalamikia vitendo vyovyote viovu anavyovifahamu kutoka kwa huyo mshenzi wa Utalii.
v-               Alianza na witi wa mwaka 2005, baada ya kuchezewa sana, baadae yule binti aliamua kuachana kabisa na kubadili namba kwa kuwa hakuna alichopewa pamoja na ahadi nyingi alizohaidiwa, je jiulize, ilikuwa witi awe mshindi wa Dunia wa Utalii akitokea Ardhi yetu kasha awe ni mtu asiyetambulika tena kwa watu hadi sasa hakuna anayemtambua, aonekani, hana kitu masikini wa Mungu, au Sashi anazowavalisha ndo zawadi za kuwa Hela wakiziomba, kwa hiyo waziabudu Sashi siyo eh?
vi-            Mwaka uliofuata vile vile niambie yuko wapi na nini alipata yaani 2006,
vii-         2007 hakukuwa na mashindano pamoja na kwamba yeye utamsikia eti mshindi wa 2007 ni Fulani na alikwenda uturuki shindano la dunia, uturuki ipi hiyo, au kijijini kwao kwa waganga wake wa nguvu za Kiza?
viii-      2008 hiyo ndo ilikuwa ya hatari sana, maana si mimi tu aliyenichefua, bali hata waziri wa maliasili na Utalii-Mh. Maige, Muulize- baada ya hapo maige hataki hata kusikia jina la Chips, ulikuwa ni utumbo mtupu, TBC Ndo waliokuwa wadhamini wa matangazo, walikuwa wameingia mkataba wa kifedha baada ya onyesho wakitaraji kupata angalau kurejesha baadhi ya matumizi,Utumbo mtupu maana baada ya onyesho walisikika wakisema huu ni wizi na utapeli, hatutaki tena ututafute wewe mpuuzi, kwanza umetupotezea muda wetu, pili umeendesha shindano hadi majira ya asubuhi, je uliona wapi shindano likaendeshwa masaa kumi na mbili ya Usiku, watu wasilale jamani mambo gani hayo? Au kwa kuwa yeye amezoea kuwanga na hao waganga wake ndo anafikiri ni kila mtu ana usingizi? Hakuna shindano la Utalii lililofana na kumalizika saa saba usiku kama ilivyo kwa mashindano mengine ya Urembo kama la Lundenga(ON Time), Uliza wandishi waliofika siku hiyo pale Mwalimu Nyerere Cinema Mwenge, walikasirika sana, na hata baada ya siku ile hakuna ambaye utamwambia njoo Kwenye Utalii wa Gideon Naye hakaja, zaidi anaweza kukutukana, pamoja na kupewa mialiko lakini walijuta, kwa kushindishwa na njaa na kisha kunyimwa usafiri wa kuwarejesha maofisini mwao.
ix-            Kilichotokea baada ya Onyesho hilo ni Aibu, kwani uwezi amini nikikwambia kwamba Hoteli tuliyokuwa tumepewa hifadhi ya kukaa vyumba bure, baada ya muda kumalizika pale LAMADA Hoteli, aliendelea kuishi Pale akiwa na Makusudi ya kumtaka Yule Binti (Violeth Timoth), ambapo pamoja na kuwaondoa washiriki wengine bila kuwapa zawadi kama ilivyokawaida yake, alimfungia yule binti chumbani na kumzuia kuondoka kwa wiki mbili, wakati huo alikuwa akiagiza chakula cha jiko la hoteli kwa bili ambayo baada ya kutimiza lengo lake la kumfanyia ushenzi na ukatili mkubwa binti yule, tuliondoka pale hoteli kwa kutoroka kwa kuwa deni lilikuwa kubwa la chakula, Vocha na Internet, tulipitia mlango wa Nyuma na Funguo zao(Kadi) baada ya hapo hatukuonekana tena pale hadi leo hakuna mahusiano mazuri kati yake na Mmiliki wa Lamada(James), Dada wa Yule Binti alilalamikia sana ile hali ya mdogo wake kutembea na Chips, lakini chips akajidai eti amemuchagua awe mke wake wa ndoa hivyo hakuwa na lengo la kumharibu tu, ilibidi yule dada akubari akidhani ni kweli mdogo wake kapata mume, kishingo upande kwani hata amngekataa pia isingekuwa na maana , maana kama ni kuliwa alishariwa uroda, tena mimi nasema siyo uroda bali Alimbaka yule binti, kwani baada ya hapo yule binti alinielezea jinsi alivyofanyiwa na kwa kweli binti yule hakupendezewa na ule unyama, na kwa kuwa yeye ndo alikuwa Mrembo wa Utalii hakuwa na namna ya kujifichia siri yake pamoja nami kuuficha uovu ule, nikitarajia siku moja anaweza kubadilika, na baada ya hapo aliendelea kumliwadha yule binti kwa kumpelekea fedha ambazo alikuwa akizichukua kwa Msofe, na waheshimiwa Wabunge ususani Idd Azan,  baada ya hapo hakukuwa na mahusiano tena ya Kikazi, Urafiki, wala Ujamaa kati yake na Yule Binti(Mrembo wake), je ungekuwa wewe ungeendelea kuwa karibu na huyo Shetani kama Mungu angekuwa amekuumba Msichana na umekuwa ndo umefanyiwa vile? Namba ya huyo Binti hiyo ongeeni naye-0713261262
x-               Na unapomuuliza kwamba ni kwa nini warembo wake hawatumikii taifa kwa shughuli za jamii atakachokwambia ni uzushi tu, zaidi ya kuwasingizia watoto wa watu ambao wanakuwa wameshindwa kuvumilia tabia zake, maana wakiwa karibu yake wanabakwa so, wafanye nini zaidi ya kujitenga na Maumivu Moyoni? Yule Binti wa 2008 baada ya kukabidhiwa gari yake, kulikuwa na mkakati wa muipora ile gari ili airejeshe kwenye miliki yake kisha kuiuza ama kuiweka laani kama alivyofanya kwa mwaka huu, maana hata kadi ya gari kama unakumbuka yule binti alikwenda kushitaki hadi BASATA, akidai kadi, zilikuwa ni porojo nyingi tu, mara kadi anayo james mmiliki wa Lamada, ambaye ndiye aliyekuwa amenunua ile Gari, eti hakumpa kadi, ingewezekana wapi mtu kama yule(Tajiri) kajitolea kununua gari na kuwapa kisha awanyime Kadi?Matokeo yake BASATA walitangaza kumfungia, wakidai Ripoti ya mashindano, lakini hata hivyo, sina uhakika na Maafisa wanaoongoza Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) kama kweli wanachotenda pale ndicho wanachotakiwa kutenda, kwani wakumbuke kwamba BASATA siyo mali yao, ni mali ya wananchi, ususani wasanii wenyewe kwa maana ipo kwa ajili ya kulinda, kudhibiti, kusaidia, watanzania, Wasiifanye mali yao eti hapo, au nao tayari wamekwishajijengea majengo ndani ya Ofisi hizo za Basata? Kumbe hayo majengo tunayoyaona si mali ya Serikali, kwa nini wasituambie kwamba Basata ni Mali ya watu na si mali ya Umma, ili tusipoteze muda wetu kwenda pale kufikisha Haidia zetu, na kupeleka malalamiko juu ya Tabia kama hizo za huyo Shetani, nahisi pale yupo kama siyo wapo, wanaokula, ama kunywa, na kushiriki na uharibifu wa Mabinti wale, kama si kupewa Hongo basi kuna namna ingine ambayo wamefanyiwa ikiwemo kuchawiwa, viongozi gani tangu wamesikia shutuma, malalamiko, Ubabaishaji, kutoka kwa huyo Chips na wasichukue hatua, ndiyo kwanza akienda mtu mwingine anataka kusajili shindano lolote lisilofanana na Miss Utalii ila la Urembo, watakataa, je BASATA wapo kwa ajili ya kukataa fikira na mawazo ya watu wenye nia ya kuleta mabadiliko au kupokea aidia na kuzisimamia? Nyinyi Basata kwa nini mnakataa kusajili mashindano ya Urembo, ndiyo kazi yenu hiyo, ndicho kilichowaweka hapo BASATA? Au mnataka nini? Je nyinyi mnatazamia kuishi Milele hapo BASATA siyo, au mnataka kupageuza BASATA kuwa sehemu ya Malumbano na Wananchi kama vilivyo vyama vya siasa? Au mnataka siku maandamano yaje hapo yakipinga mtu, au jambo Fulani?sina maana ya kuwatukana ila kuwaeleza ukweli kutokana na Tabia mnazoonyesha za kutotenda haki Mahala hapo, Badilikeni sasa maana watanzania wanahitaji mabadiliko, wamechoshwa na matendo kama hayo, kama vipi Mjiudhuru hizo nyazifa zenu mfungashe vilago muondoke hapo, kazi imewashinda, msing’ang’anie madaraka kama wanavyoendelea kung’ang’ania wenye vyeo wengine, Tokeni waingie wenye uwezo wa kutenda haki ati eh, tabia gani hiyo, hata aibu kweli, ninaamini mtafanya maamuzi sasa na mtatenda ipasavyo.
xi-            Baada ya Fainali zile za 2008 mwaka uliofuata hakukuwa na shindano kutokana na kukosa muelekeo, 2009 na 2010, lakini leo hii utamsiki chips akisema eti washindi walipatikana na walikwenda kuiwakilisha Tanzania kimataifa, weeeee, mataifa gani walikwenda hao wasioonekana? Au wamekuwa upepo sasa Miss Utalii inatumia Hewa? Au wanga, sisi tusiwaone lakini walikwenda kuwakilisha Tanzania, Tanzania ipi hiyo au kwa babu na bibi zake kuzimu? Au kijijini kwao kuna nchi inaitwa Tanzania tusiyoiona kwa macho ya kibinadamu? 2009 eti alikwenda Jamaica, weeeee Jamaica ya wapi hiyo? Au kwa wavuta Bangi vijiweni na kwa masela? Vijiweni na kwa masela watuta Bangi siku hizi limekuwa Taifa siyo, walibebeshwa bendera ipi au Moshi wa Sigara zake anazokesha usiku na mchana akipuliza ndo ukipeperuka anaona kama ni taifa la Jamaica na bendera ya Tanzania ni Moshi wa Sigara? 2010 eti alikwenda Takei na wa kipaji alikwenda Uturuki, weee sheteni Chips, hiyo takei au uliwapeleka kwa wachina waliokuwa wakijenga Uwanja wa Taifa wakati huo kuwauza Kingono mabinti uliowadanganya kwamba wanakwenda kuwakilisha nchi, maana kwenye Utalii wake pia kumbukeni kuwa kuna Soko la Utumwa wa Watu kuuziwa Warembo wa kwenda kustarehe nao, ntawataja waliouziwa mabinti yaani walionunua na waliouzwa, nawafahamu sanaaaa, siku zao tu bado za kuwekwa wazi mbona, maana safari hii nimekuja kwa lengo la Ukombozi wa Watu wote wanaodhalilishwa na kuonewa, ntakufa kwa ajili ya haki siku zote, na nimejiweka wakfu kwa Roho, kwa ajili ya Utukufu wa Mbinguni.
xii-         Baada ya kukwama miaka hiyo miwili maana wakati huo mimi nilimkimbia baada ya kuona matendo yake yamenikera, nilikwenda kuitumia ajira yangu, baada ya kutoka TIMES FM RADIO, nilikwenda MLIMANI REDIO, na baadae- PRAISE POWER RADIO, kisha nikaamia Gazeti la Tanzania Daima nikiwa kama mwandishi na Mpiga Picha, hivyo nilikuwa nikimfuatilia kwa makini sana bila yeye kutambua kutokana na kazi yangu ya kutaka haki.
xiii-      Mwaka 2011 ndo akatokea sijui wapi huko, baada ya kunitafuta kwa muda mrefu sana na kutafuta namba yangu ya simu, aliamini kuwa naweza kuendelea kumsaidia shughuli zake, sikuwa na tatizo baada ya kuniomba sana nirejee na kunihakikishia kuwa tayari kishabadilisha tabia zake, maana wakati naachana naye kati ya vitu nilivyombambia ni pamoja na Ubaya wa tabia zake kwamba sijazipenda, hivyo sikuwa tayari kuendelea kuzivumilia, so baada ya kudai kishabadilika kitabia, nilikwenda kwake wakati huo alikuwa akiishi chumba cha kupanga Tabata Segerea, ambapo hata hivyo kwa taarifa tu ni kwamba mwisho wake na bosi wake haukuwa mzuri, maana alifurumushwa kwenye chumba hicho baada ya kukosa fedha za kuendelea kumiliki chumba chake, matokeo yake alikwenda kuishi Gest inayopakana na Rufita Bar, ambako pia baada ya kuishi kwa takribani miezi miwili mitatu hivi alijikuta anadaiwa deni kubwa ambalo alikimbia usiku wa manane na kutoroka, na hata leo hii bado anadaiwa pale ni Kimeo Tabata. Ambapo baada ya kutoroka alikwenda kuomba makazi kwa mmoja wa waganga wake kama nilivyokwambia, alijidai anamatatizo na mama mwenye nyumba wake, eti anamuwangia hivyo mganga naomba niwe kwako kwa kipindi cha mwezi, yule mganga jina lake mr Kalonga, yupo Kigogo na nyumba yake, alikubali, maana uwezi kumfukuza mteja wako, aliendelea kuishi pale kwa udanganyifu siku zikisonga mbele hadi alipogombana na huyo Kalonga namba za kalonga za simu ni hizi-0715228163, kwa hivyo kwa sasa hana makazi maana baada ya kugombana na kalonga alinipigia simu na kunitaka nimsindikize kwa mganga wake mwingine Bagamoyo, niliendesha gari usiku wa manane hadi bagamoyo, siku ya pili niliendesha gari hadi Miono, na baada ya Miono tuliporejea Dar ndipo aliponituma mimi kwenda Dodoma kuandaa shoo iliyomalizika kwa yeye Kugombana ikiwa ni kutaka kumuingiza Binti ambaye alidai ameachwa na majaji kwenye Tano bora, je kazi ya majaji ni nini? Si waliteuliwa kwa ajili ya kufanya kazi zao, ilikuwaje yeye aingilie matokeo ya majaji?
xiv-       OK- Nimeruka mbali- hili la mwaka 2011 lilinikera kuliko kifani kwa kweli, naomba unielewe na unisikilize kwa makini sana, alinipigia simu akiwa tayari amekusanya mabinti wengine wakiwa kweli wametoka mikoani, lakini wengine hawakuwa wametoka mikoani zaidi ya kukutana nao tu mitaani kisha kuwaomba wakaongeze wingi wa washiriki, ilikuwa ni KIROMO Hoteli ambako nilifika na kukutana na Mwandishi mwenzangu kwa jina anaitwa Mwinyi , mhariri wa gazeti la Sani namba yake pia ni hii kama ukitaka maelezo zaidi kuhusu ushahidi huu ninaokwambia-0713552211, pamoja na kwamba mwinyi aliondolewa ofisini na kuhaidiwa kupewa malipo ya shilingi milioni moja baada ya kazi yote, aliambulia elfu 30 tu kwa kipindi cha miezi mitatu, hivi siku 90 unaweza kumpa mtu malipo ya kiasi hicho cha fedha kama siyo wizi na unyonyaji ni nini? Tulisafiri na huyo mwinyi pamoja na Paulo Siboka namba yake hii 0715094209 na ya mke wake ambaye pia alikopwa milioni moja lakini alirejeshewa laki tano na kudhulumiwa lakini tano ambazo alitusaidia kwa ajili ya kuweka mafuta kwenye magari aliyokuwa amekodo kwa ajili ya safari ya Mikumi na Udzungwa mkoani Morogoro, namba ya huyo Dada ni-0655429569, haya mwingine ambaye sidhani kama alipewa fedha zake za kukodishiwa basi lake ni huyu mama namba yake ni hii-0715-270634 maana nakumbuka alipata usumbufu sana katika kudai malipo yake, huko Safarini hapakuwa salama hata kidogo, kwanza safari haikuwa na mpangilio, pamoja na kwamba tulifika salama Mikumi kisha Udzungwa, ila tatizo la kwanza ilikuwa ni Mafuta ya kuweka kwenye magari, yeye wakati tunaondoka alidai kuwa TANAPA wangeweza kumuingizia fedha za udhamini kwenye akaunti tutakapoianza tu safari, lakini hadi tunataka kuondoka Mikumi hatukuwa na mafuta kwenye Gari kitendo kilichotulazimu kupoteza muda(TUKIZUGA) ndani ya Hifadhi kwa madai eti tulipanga kuwafanyia shoo wakazi na wafanyakazi wa ile HIFADHI, tulipomaliza kufanya onyesho la uzushi aliniagiza niende nionane na MHIFADHI UTALII WA HIFADHI YA TAIFA YA MIKUMI- niombe mafuta(DIESEL) namba ya Mhifadhi yule ni hii 0712491316 anaitwa APAIKUNDA , ambayo kwa kweli kwa kuwa kwenye  Hifadhi nyingi kuna Visima vya mafuta waliweza kutusaidia kwa kuzingatia tuliwapa burudani, tulipewa mafuta ya kutufikisha Udzungwa, tulipofika Udzungwa kwa kuwa pale Udzungwa kuna Hoteli na Vyumba Vingi, baada ya kutelemka Mlimani, walituandalia chakula na kwa kuwa mfumo wa Onyesho tuliubuni tukiwa Mikumi, alionelea tufanye na Udzungwa, ambako ilitulazimu kulala pale hivyo usiku baada ya chakula warembo walifanya onyesho ambalo yeye aliwadanganya kuwa wanatafutwa mabalozi wa hifadhi watakaofanya kazi ndani ya Hifadhi hizo baada ya kuchaguliwa, nitakupa namba za simu za Waliochaguliwa wote kwenye Hifadhi wawaambie ni lini na wapi walikwenda kufanya kazi au hata kuitwa tu kwa kuwa wao ni mabalozi wa hizo hifadhi? Hakuna hata mmoja, lakini kibaya pale Udzungwa ndipo alipoanzia ushenzi wake wa kuwataka kipapenzi washiriki, maana siku hiyo hakulala na mimi pia alinipa usumbufu mkubwa maana alikuwa akiangaika na pia akiniangaisha hata mimi kunituma mara kwa binti huyu mara yule wanaitwa chumbani kwake, siku hiyo hakuna aliyemkubali maana nilikuwa namwaga sumu kwa wale watoto, wasijekuthubutu kukubali, na kweli wengi wao hadi inafika asubuhi hakuna aliyekubali, Asubuhi yake baada ya chai ambayo tulipewa bure(OFA) hatukuwa na mafuta mengi na tulitakiwa kuwa siku hiyo Mkomanzi Tanga, haikuwa hivyo maana tuliangaikia mafuta hadi tulipopata msaada wa fedha za kukopa kutoka kwa warembo wenyewe ambao walidanganya familia zao na hivyo kadhaa wakatumiwa hela ambazo waliokoa jahazi kisha kuondoka.
xv-          Tukiwa safarini kuelekea ARUSHA maana tayari tulishapoteza ahadi ya MKOMANZI hivyo hatukwenda, na nasikia Mkomanzi walikuwa wameandaa Chakula na walitumia gharama kwa ajili ya maandalizi ya Miss Utalii, je uoni kama aliwasababishia kama si kuchangia kuisababishia Wizara ya Maliasili na Utalii(SERIKALI) hasara?
xvi-       Wakati huo huo Arusha alikuwa amefanya matayarisho ya kuwepo kwa shindano la Fainali za Kipaji siku hiyo, ilikuwa ni aibu maana wakati sisi tunaondoka Udzungwa ilikuwa yapata saa 7 mchana, na Arusha shoo ilipangwa kuanza saa tatu usiku, Mgeni Rasmi Arusha alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, ambaye yeye pamoja na viongozi wengine na watazamaji waliokuwa wameingia ukumbini, sidhani kama tena wakisikia shoo ya Miss Utalii wanaweza kwenda, walisubiri hadi saa sabaaa Usiku bila kuona Miss wala Chips, ilipofika saa nane Usiku ndo sisi tukaingia Ukumbini, hatukukuta Mgeni Rasmi wala wageni waalikwa na hata waliokuwa wamelipa viingilio vyao pia walishasamee, walibaki walinzi wa ukumbi, wauza bar pamoja na Mwandaaji ambaye namba yake ni hii-0755975454 anaitwa Upendo ambaye kiujumla alishushiwa matusi, zarau, na kejeli nyingi kutoka kwa mashabiki, alikoma tangu siku hiyo, alivyokuwa akinieleza kwa uchungu hadi machozi yalikuwa yakimtoka kutokana na kujivunjia Heshima yake ambayo watu wengi walikwenda kwa kuwa waliamini Pendo kazi zake upendeza tofauti na siku hiyo(AIBUUUUUU), Dada Pendo ameapa kutoshirikiana tena na Miss Utalii, si hilo tu, tukiwa hapo Arusha hatukuwa na Senti hadi muda huo, ambapo alimuomba jamaa mmoja Musa Mwandishi wa Mwananchi Gazeti kwa upande wa Arusha namba yake ni 0754296503 kumsaidia kutafuta Hoteli ya Mkopo kwa madai wangelipwa siku mbili kwa cheki baada ya kuomba msaada kutoka kwa Maafisa wa TANAPA makao makuu, ambao hata hivyo baada ya siku mbili tukiwa hatuna mwelekeo baada ya kupoteza ratiba waliyokuwa wamepanga TANAPA ya kuwatembeza hao warembo kwenye hifadhi kama alivyokuwa ameomba, tuliondoka na kumwachia Deni Muss ambalo alikuja kulipa baada ya kupigia kelele pia ilikuwa aibu kwa Mussa.
xvii-    mhasibu wa TANAPA, alikubali kutoa fedha zake mfukoni ili kumkopesha na kwa kuwa alikuwa ameomba udhamini TANAPA, aliahidi kulipa mara tu itakapotoka cheki yake, mkopo wa kwanza ulikuwa ni Milioni mbili ambazo zililipa Hoteli pamoja na kuweka mafuta hadi Tarangire, ambako walitupokea kwa shingo Upande lakini hata hivyo Tarangire walikuwa na hamu ya kuwaona warembo maana walikuwa wakiwasikia tu, hivyo haikuwa tabu kupokelewa, tulipata hifadhi za kulala na tabia yake ikawa kama ilivyokuwa Udzungwa, pia niliwakataza wale mabinti, kwani tukiwa Arusha mimi nay eye tulilala chumba kimoja kutokana na kubana bajeti ya vyumba hivyo hakusumbua kuwataka watoto wa watu.
xviii- Tulifanikiwa kuondoka vyema Tarangire na kuelekea Arusha National Park, ambako pia tuliondoka, na kwenda Serengeti , kisha kurejea Ngorongoro, lakini wakati huo wote tulishapoteza ratiba ya TANAPA, isipokuwa walikuwa wakikubali kuwapokea wale mabinti kwa maana waliamini kuwa walikuwa wakiteseka hivyo hawakuwa tayari kuwa kati ya watesaji, maana tulifika kwenye hizo hifadhi kama wakimbizi.
xix-       Lakini wakati tunakwenda Ziwa Manyara, Mhifadhi wa Manyara kwa kuwa alifuata sheria za kazi hakuweza kukubali kutupokea na waliturudisha tukiwa geti la kuingilia hifadhini, kwamba siku mliyotakiwa kufika ni juzi iweje mje leo, hakuna bajeti ya kulala wala kula, na chakula chenu kilitupwa asubuhi ya jana baada ya kukosa walaji, hasara ingine kwa SERIKALI.
xx-          Ilibidi kulala gesti mbovu sijawahi kuona, maana siku hiyo wezi waliiba ikiwemo simu yake chips iliibiwa, Tulisota sana pale maana hatukuwa na hela ya kujikimu, hivyo ilibidi tu kesho yake kubembeleza makao makuu TANAPA watoe hidhini ya sisi kulala Hosteli za  Hifadhi, ambao ilibidi wakubali, lakini siku hiyo ndo alinikera sana, maana hatukuwa na hela hivyo mabinti wengi walitumia fedha zao kutoka kwenye Tigo ama Mpesa, lakini ndugu yangu maana pale tulikaa siku tatu, watoto wale walito………yaani walibakwa kwa zamu, nitawataja siku ikiitajika, na eneo alilofanyiwa ushenzi, ila mwingine alitendewa Chooni na hata washiriki wenzake wanajua, mwingine kwenye Basi, Mwingine pembeni ya Ukuta ikiwa ni baada ya kuwanunulia vilevi  vikali, siku hiyo walilewa sana, nilikuwa na kazi ya kuwaokota kuwaweka kwenye room zao, na vile wengine walikuwa wakifuata mkumbo hawakujua ukali wa zile Pombe ndugu, ilikuwa ni Aibu sana. Lakini yeye alifanikiwa kuwachafua wote aliokuwa amepanga kufanya hivyo, kilichowashangaza wengi uusani wale madereva ni kitendo cha kuwafukuza madereva na waandishi wa habari wasiwepo eneo hilo na badala yake walitafutiwa gest za kulala eneo la mjini, walijiuliza sana wakati eneo la hosteli kulikuwa na vitanda vingi tu, baada ya kuwapeleka madereva wa basi mimi ndiye niliyeendesha basi hilo, hadi Hosteli kwani baada ya kuwateremsha tu madereva, tulipita eneo la vinywaji vikali kisha kununua na kwenda navyo, waliulizwa kwa mtego wa mabinti, eti, je mnataka leo tufanye kasherehe kidogo tujipongeze kwa hii safari yetu, wote walikubali kwa maana hawakujua kinachokwenda kufanywa, je ninunue pombe gani mnakunywa, wengine Bia, Wengine, konyagi, wengine whisk, wengine value, na kila aliyesema bia alipatiwa hadi kusaza, konyagi ukiomba ndogo unapewa kubwa, whisk kadhalika na Value, yaani watoto ilikuwa ni aibu hata kusema kwa watu waliyotendewa siku hiyo, majina ninayo na siyo siri maana warembo wote baada ya matendo ya siku ile kesho yake yalikuwa yakizungumzwa, wanafahamu kama ni ushahidi upo, na wapo watakaokuwa tayari kuyasema hayo. Namba za simu za waandishi wa Star Tv ni hizi maana waliyasikia hayo yaliyotendeka na pia walishangaa ni kwa nini walitakiwa kutolala na sisi yaani mimi na chips t undo tulilala eneo hilo la warembo-0685358942/ 0713168889 anaitwa mpangala, na 0784888844/0655368848 anaitwa Salim Mlege(Prof). na namba za Madereva wa mabasi tuliyokuwa nayo ni hizi hapa 0715285277(Moshi) na 0715073382(Ustadhi).
xxi-       Iliniuma sana tena sana, na wote aliotembea nao siku hiyo ya Manyara ndo aliwaweka kwenye nafasi za mwanzo 1-5.
xxii-    Sidhani kama kweli eti walikuwa na vigezo halisi vya kutwaa nafasi hizo kwa maana siku ya fainali wenye sura zao na akili zao, maumbile yao hawakuambulia chochote, kuna binti mmoja YAKOBA alikuwa ni Mshiriki pia, baada ya shindano aliyaweka maneno haya TBC, lakini wengi walidhani kwamba ilikuwa ni kushindwa kwake hivyo hakuwa na jipya, no yule binti alikuwa sahihi kabisa namba yake ni hii 0716078488, na mwingine aliyekerwa na yaliyotokea Manyara na pia amekuwa ni kati ya wanayoweka wazi ni huyu mwenye namba hii 0718933720 Ritha Mvungi, mwingine ambaye alitakiwa kimapenzi na baada ya kukataliwa akatimuliwa ni mwenye namba hii 0655432394/ 0654817418 anaitwa Rebeca Mdamu wa Morogoro,
xxiii- Je unafahamu kwamba anapokuwa kwenye maandalizi ya onyesho lake anawapiga mateke, ngumi, na makofi washiriki ikiwa ni pamoja na kuwashika makalio au maziwa kwa makusudi wale ambao wanakuwa na msimamo kuhusu kutoruhusu miili yao aichezee, piga namba hii ya mshiriki ambaye alijiengewa baada ya kushikwa nna kisha kupigwa 0659-402339 anaitwa Ester George mwanafunzi wa chuo cha Biashara CBE- Dodoma Cumpas. Mwingine ni Kibibi Amani namba zake ni 0755-441296 na 0713400791.
xxiv- Na ndiyo maana sikuona tatizo kuondoka alipoanza tena tabia yake ya kuwalewesha mabinti na tayari alishamtenda IRENE RICHARD (ngono) ni kama alimbaka maana yule binti wa watu na hali ya ukata wa fedha dodoma unadhani angefanyaje?
xxv-    Ananishangaza anapokwambia kwamba zile picha nilizomvizia akiwa na yule binti zilikuwa ni Tangazo la Hoteli, hii ni namba ya mwenye hoteli yaani msimamizi atueleze kama ni kweli walikubaliana hivyo-0713266366 anaitwa Alex,
xxvi- Na je unatambua kwamba Dodoma kwa sasa anadaiwa na watu wengi na hana fedha za kuwalipa, usishangae ukisikia kwamba yupo Lumande kwa kukosa fedha, na kati ya maeneo anayodaiwa ni pamoja na NAM HOTEL ni zaidi ya Milioni mbili sasa, KITOLI HOTELI namba zao ni  0655201660, Side Way 0653333997, ROYAL VILLAGE namba ya Merley sikuiona ila anadaiwa laki nne na 65, VETA HOTEL laki 7, Dodoma Hotel pia, CF Communications, amekodi gari dodoma kwa siku anatakiwa alipe 20,000/= ana zaidi ya mwezi sasa, kuna hela ambazo anaendelea kukopa kwa Emmanuel pamoja na Mtoto wa Mzee Shayo anaitwa Babu, tena huyo ndo mzazi wake akijua itakuwa kasheshe maana amekabidhiwa duka la jumla, na anachukua mahesabu ya baba yake akitarajia kuja kurejeshewa, itakuwa aibu huko Dodoma,
xxvii-          Hapa kati alikamatwa na Polisi na kufikishwa Mahabusu kwa Deni la Kitoli Hoteli ambalo aliweka LapTop yake Leani kwa laki 2, kupunguza deni na bado anadaiwa na huyo kitoli maana hakumaliza deni,
xxviii-       Hapa Dar es Salaam ndo kabisaaaaaaaaaaaaaaa sijui nikwambieje , maana hata Ruge inawezekana anamdai, Wasiwasi anamdai, alikuwa MC wa shoo moja kinondoni na yule dada wa hapo Clouds fm, anadai, CXC TOURS & Safari mr Charles Hamka anadai hela nyingi tu na huyo ndo hataki hata kumsikia, Msofe kisha mchoka maana kishauziwa hao watoto hadi wengine anapelekewa akiwa hawapendi, utasikia huyu simtaki,
xxix- Ninayo mengi tu sanaaaaaaaaa na baada ya kujibu haya nitakuletea mengine ikiwemo ambalo ameuzia na kuwashawishi wabunge wetu, kumbe mnawalaumu bure waheshimiwa eti posho ni nyingi, sasa kama kuna watu kama Chips wanawapelekea usumbufu na ndama wao wakiwauza, je wafanyeje jamani?
xxx-    Safari ya Bungeni nilipokwenda nae utacheka sana nikikusimulia, ni aibu
KWA LEO NAISHIA HAPA, SI KWAMBA YAMEISHA BUT NAMUWEKA KIPO………………………si ni bingwa wa kuongea na kujitetea haya………….

Friday, December 9, 2011

KWA MARA YA PILI MATOKEO YA UCHAGUZI CONGO DRC, YAAHIRISHWA TENA!

kongo 1


Tume huru ya uchaguzi katika Jamhuri ya Demokrasia ya Congo imeahirisha kwa mara ya pili kutangaza matokeo ya uchaguzi wa urais ambapo mkuu wa tume ya uchaguzi amesema kuwa yatatangazwa leo Ijumaa.
Tayari asilimia 90 ya kura zimehesabiwa na rais Joseph Kabila anaongoza kwa asilimia 49 huku mpinzani wake mkuu Etienne Tshisekedi akimfuata kwa asilimia 33, huku Polisi wa kupambana na fujo mjini Kinshasa walipambana na wafuasi wa upinzani ambao wanadai uchaguzi ilikuwa na udanganyifu.
Kulingana na kiongozi wa tume ya uchaguzi Daniel Ngoy Mulunda, wana kibarua kigumu kuhakikisha kuwa matokeo yote yamethibitishwa kabla ya kutangazwa ambapo Tume ya uchaguzi pamoja na magavana wa mikoa wametoa wito kwa watu kutulia lakini mwandishi wa BBC amesema bado kuna shaka kuhusu matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo.
Kulitokea shambulio katika mojawapo wa vituo vya kuhesabu kura katika eneo la Fizi mashariki mwa nchi ambapo Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Umoja wa Mataifa, Okapi, kilitangaza kuwa matokeo ya mojawapo ya vituo thelathini katika mji wa pili kwa ukubwa Lubumbashi yamepotea. Inadaiwa kuwa fujo za baada ya uchaguzi ndio zilizosababisha kupotea kwa matokeo hayo.

WEZI WALICHOMFANYIA DIAMOND!



.
EXCLUSIVE: usiku wa kuamkia jana, Wezi wameruka ukuta na kuingia kwenye nyumba anayomiliki mwimbaji DIAMOND Sinza na kufanikiwa kumuibia vitu kibao vikiwemo vifaa vya gari.
wakati wanaiba, DIAMOND hakushtukia chochote, baadae usiku ndio jirani yake akamuamsha akamwambia jamaa wamemuibia na kusepa.
vifaa vya gari alivyoibiwa thamani yake ni milioni 1.9! na ndani ya gari kulikua kuna nguo alizozitumia kushoot video yake mpya ambayo bado hajamaliza kuishoot na aliakiwa kuwa na nguo hizo hizo kwa ajili ya muendelezo wa SCENES.
kwenye gari pia kulikua na pete, saa 2, 1 ya rolex aliyonunua SOUTH AFRICA, cheni ya gold, viatu,mikanda na headphones za DR DRE ambavyo vyote wezi wamevibeba na mpaka sasa hajafaham ni watu gani waliohusika.
mlinzi alikuepo lakini walimteka na kumpiga, DIAMOND kuamka anakuta wamemfunga na gunia na damu kibao.

MASTAA WAANGUA VILIO KUTOKANA NA MSANII WA ZE COMEDY VENGU HALI YAKE KUENDENDELEA KUWA TETE



Na Joseph Shaluwa
WINGU zito limetanda kwa mastaa nchini wakionesha majonzi makubwa juu ya afya ya staa mwenye uzani wa juu Bongo, Joseph Shamba a.k.a Vengu (pichani) ambaye hali ya afya yake ni tete, kalamu ya Risasi Mchanganyiko inaandika kwa simanzi.

Vengu ambaye ni mchekeshaji wa Kundi la Orijino Komedi linalorusha michezo yake kupitia Kituo cha Runinga cha TBC1 cha jijini Dar es Salaam, kwa muda mrefu sasa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akiendelea na matibabu huku ugonjwa unaomsumbua ukiwa siri.

Habari ambazo zimepatikana mpaka sasa, zinaeleza kwamba Vengu anasumbuliwa na maradhi ya kichwa bila kufafanua zaidi aina ya tatizo alilonalo kichwani.

Kwa nyakati tofauti, mastaa wameonesha vilio vyao juu ya staa mwenzao huyo kwa kile walichoeleza kuwa wanafichwa maradhi yanayomsumbua, lakini pia hawapati taarifa rasmi kutoka kwa watu wa karibu na msanii huyo ili nao waweze kuonesha undugu wao kama familia moja katika fani.

Mastaa waliopata fursa ya kuzungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, juzi Jumatatu na kutoa maoni yao ni Vincent Kigosi ‘Ray’, Ruth Suka ‘Mainda’, Maimartha Jesse, Aunt Ezekiel, Mhe. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Ambwene Yesaya ‘AY’ na Jacqueline Wolper.
Ray, Mainda, Aunt na Wolper ni wasanii wa filamu, Maimartha ni mtangazaji, AY ni mwanamuziki wa Bongo Fleva wakati Sugu ni Mbunge wa Mbeya Mjini huku akiendeleza harakati zake katika muziki wa kizazi kipya.

RAY
“Kaka kwenye hili suala (la Vengu) fedha si tatizo, tatizo ni usiri wa kinachomsumbua ndugu yetu. Hata sisi wasanii wenzake tukiuliza, hatupewi ushirikiano mzuri.

“Kwa mfano ni juzi tu, nilimpigia Masanja (Emmanuel Mgaya) na kumuuliza kuhusu tatizo la Vengu, hakusema chochote zaidi ya kuniambia anaumwa tu. Ugonjwa unafichwa. Jambo lingine ni utaratibu wa kumuona, sisi wasanii nadhani tungepewa kipaumbele kwenda kumuona mwenzetu, maana ICU (Chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum) hawaruhusu watu kuingia hovyo.

“Hata hivyo, siamini kama Komedi wameshindwa kumsaidia kama anahitaji usaidizi. Unajua Vengu anafanya kazi TBC1, televisheni ambayo ipo chini ya serikali, nini kinashindikina?” alisema na kuongeza:
“Huu ni wakati wa wasanii wote nchini kushikamana. Kwa kufanya hivyo tutaonesha umoja wetu.”

AY
“Najua kwamba jamaa anaumwa, lakini sijapata details (maelezo) zaidi ya kusikia anaumwa kichwa. Inauma sana kwa kweli, unajua Vengu ni msanii mwenzetu na katika kipindi kama hiki anahitaji sana faraja yetu.

“Kiukweli bado sijaenda kumuona, lakini nitajipanga nikamuone. Kama kutakuwa na harambee ya kumsaidia, nipo tayari muda wowote kutoa kile nitakachojaliwa.”

MAIMARTHA
“Maradhi hayana hodi. Leo kwa Vengu kesho kwa mwingine. Mastaa tuoneshe mshikamano katika kumsaidia mwenzetu. Nilipata bahati ya kwenda kumuona Muhimbili siku kama sita zilizopita, hali yake ni mbaya...
“...maskini! Haongei...hajitambui. Tunapaswa kuchangishana tumsaidie. Sisi ndiyo ndugu zake. Nashukuru sana kwa kutukumbusha na ninawaomba mastaa wenzangu tumkumbuke jamani.”

SUGU
“Kiukweli sijapata nafasi ya kwenda kumuona, majukumu yamenibana sana, lakini najipanga niende. Kwa mara ya kwanza nilisoma taarifa za kuugua kwake kwenye gazeti, tena nilimuona Mhe. Rais (Dk. Jakaya Kikwete) naamini atakuwa amemsaidia.

“Unajua rais ndiyo kila kitu katika nchi, kwa hiyo kama alikwenda kumuona, nina imani ikiwa Vengu anahitaji msaada wowote, basi ni lazima atakuwa amepatiwa. Juzi tu, nimesoma kwenye gazeti, serikali imewapeleka watoto kama 20 hivi India kwa matibabu, naamini kwa Vengu ambaye ni msanii na ana mchango kwa taifa ni rahisi zaidi.

“Sema kuna tatizo la taarifa. Washkaji zake (Orijino Komedi) hawajajipanga vizuri kuhusu kutoa taarifa. Ukiachana na hao, kuna vyama vya wasanii, nadhani walipaswa kutoa maelekezo vizuri kwa wasanii badala ya kuona na kusikia kutoka kwenye vyombo vya habari.”

MAINDA
“Nilisoma kwenye gazeti, lakini kiukweli inaumiza sana. Kuna umuhimu wa Kundi la Orijino Komedi kutoa taarifa rasmi kwa wasanii, maana tupo gizani. Mimi nilisikia juujuu kuwa anaumwa, lakini nilipoona kwenye gazeti ndiyo nikashtuka. Sikujua kama yupo serious (amezidiwa) vile. Namuombea kwa Mungu ampe afya.”

WOLPER
“Ndiyo kwanza nasikia habari hizi kutoka kwako, nipo busy namuuguza mama yangu ambaye ni mgonjwa sana. Enhee... amelazwa wapi ili nikitoka hapa nikamuone?”
Risasi Mchanganyiko lilimtajia wodi na hospitali aliyolazwa ili akamtembelee kama alivyosema mwenyewe kwamba hana taarifa zozote!

AUNT
“Sikuwa najua chochote kuhusu Vengu, nilisoma tu gazetini. Kinachoonekana ni kwamba, haya mambo yanapelekwa kimyakimya sana. Sisi kama wasanii wenzake tuna haki ya kupata taarifa ya moja kwa moja juu ya afya ya mwenzetu lakini pia tuna wajibu wa kumsaidia.

“Wasanii hatuna umoja wa kweli, nashauri tuitane, tuketi na kujadiliana namna ya kumsaidia. Ni kweli Kibongobongo wasanii hatuna uwezo kivile wa kumsaidia kifedha, lakini kwa sababu tuna wadau wapenda burudani wanaweza kutupa support kama sisi tukianza. Wasanii tuamke, tushikamane tumsaidie mwenzetu.”

KALAMU YA RISASI
Hakuna jambo gumu linaloshindikana kwa Mungu, Vengu kwa sasa ni mgonjwa lakini kwa maombi yetu Watanzania, siku moja ataamka na kuendelea kutoa burudani kwa jamii. Tunamuombea kwa Mungu apone haraka– MHARIRI.

DIAMOND AMWAGA WEMA SEPETU


Musa Mateja na Imelda Mtema
“Washikaji, nimewaita hapa nifunguke mbele yenu kuwa nimemmwaga rasmi yule demu (Wema) kwa sababu hapatani na mama yangu (Sandra Sammy).

ALINILAZIMISHA NITENGANE  NA MAMA
“Kwanza Wema amekuwa akinilazimisha nitengane na mama yangu, yaani nimrudishe kule Tandale tulipokuwa tukiishi mwanzo , halafu mimi na yeye tuishi Sinza (Madukani), jambo ambalo sipo tayari kulifanya.
“Mimi na mama tumetoka mbali, hakuna kama yeye, alikuwa akishinda njaa ili mimi nisome, alinilea kwa shida sana, hata siwezi kuelezea kwani nikikumbuka huwa natokwa machozi, kwa hiyo siwezi kumtelekeza kwa sababu ya Wema.
“Hata katika muziki, nakumbuka nilishamuibia pete yake ya dhahabu nikaenda kuiuza ili nirekodi muziki na alinivumilia.
NI WAKATI WA MAMA ‘KUINJOI’
“Piga ua, huu ni wakati wa mama yangu kula na ‘kuinjoi’ matunda ya mwanaye, mapenzi hayawezi kusababisha nimtende vibaya. Natamka rasmi huyu demu nimemmwaga bwana.”
SWALI LA MWANDISHI WA IJUMAA
“Mlianza mapenzi muda mrefu na ni wiki mbili tu zimepita tangu ulipomvisha pete ya uchumba, je, hukujua kwamba mambo kama haya yangetokea?
DIAMOND AKAJIBU
“Sikuligundua hilo mapema na pia si unajua mambo ya ujana tena? Ukweli ni kwamba tukio hili limenikumbusha kuwa ujana ni jalala linalotupwa kila aina ya takataka.”
UPANDE WA WEMA
Baada ya Diamond kumwaga unga na ishu hiyo kuwa gumzo jijini Dar usiku kucha, kama ilivyo desturi ya gazeti hili namba moja kwa habari za mastaa nchini, asubuhi na mapema (Jumatano), mapaparazi wake wa kuheshimika walimsaka Wema ili kupata mzani wa habari hiyo.
NDANI YA HOTELI YA LAMADA
Kutokana na uzito wa habari yenyewe, Ijumaa lilisaga lami hadi Hoteli ya Lamada Ilala, chumba namba 35 flati ya Mikumi ambapo Wema alikuwa kambini kwa ajili ya kurekodi filamu.
HALI ILIKUWA HIVI
Baada ya kubisha hodi, ‘mkaribisha wageni’ alikuwa  Elizabeth Michael ‘Lulu’, alifungua mlango ambapo Wema alishuhudiwa akinyanyuka na kwenda kuosha uso, aliporejea na kuwaona ‘polisi’ wa Ijumaa wakifunga ‘makamera’ yao alipaza sauti na kufuatiwa na kilio: “Maweee! Nimeachwa? Nyiii….nyiiiii.”
Lulu: Nyamaza Wema usikie kilichowaleta.
Ijumaa: Mambo vipi Wema?
Wema: Hata salamu yenu sitaki, niambieni nimeachwa?
Ijumaa: Poa, ili mgonjwa apone lazima achomwe sindano inayouma au ameze vidonge vichungu. Iko hivi Wema; jana pale Lion Hotel, Sinza,  Diamond alitangaza rasmi kukutema kwa sababu eti umekuwa ukimlazimisha kumtenga mama yake ili muishi peke yenu, yeye hayupo tayari kufanya hivyo, je, hili unalizungumziaje?
Wema: (kilio) siko tayari kuzungumza chochote.
Ijumaa: Tafadhali waambie mashabiki wako umeipokeaji taarifa hii?
Wema: Amenidhalilisha, nitaweka wapi uso wangu? Anyway, niacheni nitawatafuta baadaye niongee.
Lulu: Dada Wema, funguka tu kile unachokijua, itakusaidia watu wajue ukweli.
Wema: No, please. Waondoke tu nitawatafuta baadaye.
UTABIRI
Ili kuthibitisha kuwa kile kinachoandikwa na Magazeti Pendwa ya Global Publishers kina uhakika asilimia zote, wakati hayo yanatokea, tayari gazeti tumbo moja na hili, Risasi Mchanganyiko toleo namba 844 la Jumatano wiki hii lililokuwa na kichwa cha habari: WEMA, DIAMOND HAKUNA NDOA, lilitabiri na kuweka vigezo kuwa Wema na Diamond hawatadumu.
Aidha, Gazeti la Risasi Jumamosi iliyopita, ukurasa wa 16 kulikuwa na habari yenye kichwa; ETI WEMA, MAMA MKWE WAKE HAWAIVI.
Diamond alionesha kutokubaliana na madai hayo, lakini yaliyotokea yameweka wazi.
WADAU WANASEMAJE?
Kwa mujibu wa wadau walioinyaka habari hiyo walilieleza Ijumaa kuwa haijawahi kutokea Wema akamwagwa na midume kwani yeye ndiye huwa anawamwaga.
“Ama kweli mtenda akitendewa…safari hii kaachwa yeye!” alisema mmoja wa wadau hao.
ANATAMANI DUNIA IRUDI NYUMA
Uchunguzi wa Ijumaa ulibaini kuwa usiku wa kuamkia Jumatano wiki hii, Wema hakupata usingizi kwa kuwa alishanusa dalili za tukio hilo.
“Ukweli Wema hakulala kabisa, alikuwa akijigeuza mara kwa mara na kutaja jina la Diamond huku akilia, alipoulizwa kulikoni alijibu: “Natamani dunia irudi nyuma ili lile tukio la kuvishwa pete ya uchumba pale New Maisha Club wiki mbili zilizopita lifutike,” alisema mmoja wa wasanii aliyekuwa naye kambini hapo.