TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, February 15, 2014

CHADEMA YALE YALE YAMPIGA CHINI MSHINDI WA KURA ZA MAONI, WAWEKA MBEBIZ KWENYE UBUNGE

Wajumbe  wa  mkutano  mkuu  wa uchaguzi  jimbo la Kalenga  walivyompongeza Sinkala Mwenda  siku ya  kura za maoni  baada ya  kushinda wenzake 13.
KAMATI kuu   ya  chama cha  Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) imemteua aliyekuwa  mshindi  wa  pili  wa  kura  za maoni katika zoezi la kura  za maoni Bi Grace Tendega kupeperusha bendela ya Chadema katika uchaguzi mdogo  jimbo la Kalenga.

Habari za uhakika  kutoka ndani ya  kamati  kuu ya  Chadema iliyoketi  jijini Dar es Salaam leo zinadai  kuwa  aliyekuwa mshindi   wa  kura za maoni  mwanasheria  Sinkala Mwenda  hajateuliwa na kamati  kuu  hiyo mbali ya  kuongoza kwa kura  kura 132 dhidi ya kura 122 alizopata mpinzani  wake wa karibu Grace Tendega 

Katibu  wa  Chadema wilaya  ya  Iringa vijijini Felix  Nyondo ameuthibitishia  mtandao  huu  wa www.matukiodaima.com  kuwa amepata  taarifa  hizo  za  kuteuliwa Bi Grace  Tendega  kuwa  mgombea wa Chadema  jimbo  hilo la Kalenga .

Hata  hivyo  alisema anapongeza maamuzi ya kamati  kuu na  kuwataka wana Chadema Kalenga kujiandaa kwa   kampeni  za uchaguzi huo na kuanza  kumnadi  mgombea  wao ili  kuweza kushinda  uchaguzi  huo mdogo.

Kutokana na uteuzi sasa Tendega  atavaana  Godfrey Mgimwa wa  CCM katika uchaguzi  huo   ili kuziba nafasi iliyoachwa  waziri na aliyekuwa mbunge wa  jimbo la Kalenga marehemu Dr Wiliam Mgimwa aliyefariki mwanzoni mwa  mwaka  huu.

Hata  hivyo  duru  za kisiasa kutoka ndani  ya  Chadema  zinadokeza  kuwa sababu ya kuachwa kwa mgombea  huyo aliyeshinda kura za maoni mwanasheria Mwenda ni kutokuwa na mtaji wa  watu  kwa maana ya  kutokubalika ndani na nje ya  chama hicho hivyo  Chadema  kuona kumsimamisha Mwenda ni kulipoteza jimbo  hilo.

Huku kwa upande wa mteule  wao Bi Tendega  amekuwa na sifa ya  kugombea  katika  jimbo hilo kupitia chama cha Jahazi Asilia na kufanya vema  japo si kwa  kushinda hivyo nin imani  yao kupitia Chadema  anaweza  kufanikiwa  kushinda.

No comments:

Post a Comment