TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, February 12, 2014

TAHA yapata mwenyekiti mpya

IMG_8731
Na Mwandishi Wetu

TAASISI inayoshughulika na kilimo cha maua na mboga mboga nchini (

TAHA) imemteua Bw. Eric Ng’imaryo kama Mwenyekiti wake mpya kuchukua

nafasi iliyoaachwa wazi na Bw. Colman Ngalo, ambaye ameiendesha

taasisi hiyo kwa mafanikio kwa takribani miaka kumi ya utawala wake.

Sambamba na uteuzi huo pia Bw. Ng’imaryo, pia taasisi hiyo ilimpata
Makamu Mwenyekiti mpya pamoja na wajumbe nane wa Bodi ya TAHA pia
walichaguliwa katika Mkutano Mkuu wa TAHA (AGM) uliofanyika hivi
karibuni jijini Arusha.

Miongoni mwa wanaounda Bodi mpya ya taasisi ya TAHA ni pamoja na: Bi.
Fatma Riyami , Bw. Ravi Bhalerao, Bw. Herald Peeters , Bw. Juma
Lossini , Bw. Robert Daniel, Bw. Tjerk Scheltema na Bw. Adrian Moss.
Bw. Juma Ally Juma amechaguliwa kama mwakilishi kwenye taasisi ya Bodi
ya TAHA kutoka jimbo la uchaguzi Zanzibar.
Taasisi hiyo ya TAHA kwa sasa imekuwa ikikuza msendeleo ya wakulima
nchini ambayo hatua inayoonesha kujitolea katika kukuza maendeleo ya
sekta ya maua na mboga mboga nchini.

Kablya ya uteuzi huo, Bw. Ng’imaryo alikuwa Mwenyekiti wa Arusha
Blooms Company Limited, kampuni ambayo ni mwanachama wa TAHA na moja
ya wazalishaji wakubwa wa mboga mboga nje ya nchi na nchini. Bw.
Ng’maryo kitaalamu ni mwanasheria ambaye amekuwa akifanya kazi zake za
kisheria katika Tanzania tangu mwaka 1987. Hata hivyo, Mwnyekiti huyo
mpya ni mfanyabiashara, mkulima na mwandishi mahiri.

“Nimepata heshima kubwa na ya kipekee kabisa kuweza kuchaguliwa kuwa
Mwenyekiti mpya wa TAHA na niuangalia uteuzi huu kutekeleza wajibu na
majukumu kwa kufanya kazi na Bodi na Sekretarieti ili kuhakikisha
kwamba dira yetu inatekelezwa. Nami nitakuwa sehemu ya kuifanya
taasisi yetu ya TAHA kuwa na mafanikio zaidi katika siku zijazo.
Ninapenda pia kuwashukuru Bw. Colman Ngalo, Mwenyekiti anayemaliza
muda wake, kwa uongozi wake mzuri.

Bw. Ngalo amekuwa nguzo ya TAHA kwa miaka kumi iliyopita. “Bw.
Ng’imaryo pia alitoa shukrani zaidi kwa Bi. Jacqueline Mkindi ,
Mkurugenzi Mtendaji wa TAHA, samabmba na Sekretarieti nzima ya TAHA
kwa mchango wao mkubwa kwa taasisi na sekta nzima ya maua na mboga
mboga. “Jacqueline amekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa mfano. Utendaji wake
wa kazi umeijenga taasisi yetu uaminifu na heshima kutoka kwa Serikali
na Washirika wa Maendeleo.”

Katika hotuba yake, Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Bw. Ngalo
ameusifu uamuzi wa TAHA wa kuweza kumchagua Bw. Ng’imaryo ambapo
ameleelezea kuwa na imani na uongozi wake ambao utaleta mageuzi ya
kweli kwenye sekta ya maua na mboga mboga. “Kwa niaba ya Bodi ya TAHA
inayomaliza muda wake, napenda kumpongeza Bw.Eric kwa kuchaguliwa
kwake kuwa Mwenyekiti wa Bodi mpya ya TAHA na ni mategemeo yangu kuwa
tutaendelea kufanya kazi pamoja naye katika miaka ijayo.

Mchanganyiko wa ujuzi wake katika sekta ya maua na mboga mboga na
uzoefu mkubwa sambamba na utaalamu unafanya kuwa mtu bora kuchukua
nafasi ya Uenyekiti wa TAHA na sekta yenye maendeleo endelevu. Napenda
pia kuishukuru Sekretarieti ya TAHA na wanachama wake kwa ushirikiano
wao bora katika muongo uliopita. Kwa ushirikiano tumepata mafanikio
mkubwa. Mimi ninajisikia fahari kubwa kukabidhi taasisi hii yenye
mafanikio ambayo bado ina fursa kubwa kwa ukuaji zaidi katika TAHA na
sekta nzima kwa ujumla.”

TAHA ni taasisi ambayo ni mwanachama wa sekta binafsi ambapo imekuwa
ikishiriki kwa ufanisi katika kubadilisha kilimo cha sekta ya maua na
mboga mboga toka kuanzishwa kwake mwaka 2004.

Kutokana wa hatua za uwepo wa TAHA , sekta ya maua na mboga mboga
nchini na kufanikiwa kuvutia washirika mbali mbali kutoa misaada
mikubwa ikiwa ni pamoja na serikali ya Tanzania na Washirika kama vile
USAID, BEST- AC, Ubalozi wa Uholanzi , ITC, na Serikali Finland.

TAHA inatoa sapoti mbali mbali kwa wadau wa sekta ya maua na mboga
mboga ikiwemo kuwajengea uwezo kwenye majukwaa, kulinda na kukuza
maslahi ya watendaji katika sekta hiyo ya maua yaani wazalishaji ,
wauzaji, wasindikaji, na watoa huduma ya maua, matunda , mboga, viungo
, mimea na mbegu za maua.

============================================================= 

SUPER D AIPIGA TAFU GYM YA UHURU KARIAKOO VIFAA VYA NGUMI

=======================================================================
Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’ kushoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa masumbwi Gloves pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo kwa Kocha wa GYM ya Uhuru uwanja wa Basket, Kariakoo  Mohamed Chipota kwa ajili ya kuhamasisha mchezo  wa masumbwi katika eneo h ilo na kuwapa moyo wa kuendelea na mazoezi wanaoshuhudiatukio hilo wa pili kushoto ni Atanasi Kibwe,Omari Bai, Raymond Mbwago na Mussa Sindano Vifaa hivyo pamoja na DVD vina thamani ya shilingi laki mbili

Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’ katikati akiwa na baadhi ya mabondia wanaofanya mazoezi katika
GYM ya Uhuru uwanja wa Basket, Kariakoo kutoka kushoto ni
Atanasi Kibwe,Omari Bai, Raymond Mbwago ,
Mussa Sindano Vifaa na kocha wa GYM hiyo
Mohamed Chipota


Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’ kushoto akikabidhi vifaa vya mchezo wa masumbwi Gloves pamoja na DVD za mafunzo ya mchezo kwa Kocha wa GYM ya Uhuru uwanja wa Basket, Kariakoo  Mohamed Chipota kwa ajili ya kuhamasisha mchezo  huo wanaoshuhudia tukio hilo wa kutoka pili kushoto ni Atanasi Kibwe,Omari Bai, Raymond Mbwago na Mussa Sindano Vifaa hivyo pamoja na Dvd vina thamani ya shilingi laki mbili

Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’ kushoto akiwa katika picha ya pamoja  na baadhi ya mabondia wanaofanya mazoezi katika
GYM ya Uhuru uwanja wa Basket.
Na Mwandishi Wetu
KOCHA wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ ameipiga tafu 
GYM ya mchezo wa ngumi ya  Uhuru uwanja wa Basket, Kariakoo Dar es salaam kwa kuwapatia vifaa vya mchezo huo

akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo Super D alisema amevutiwa na uanzishwaji wa GYM hiyo ambayo ina uwezo mkubwa wa kuwatoa mabondia wazuri kipindi kijacho
aliongeza kwa kusema kuwa unajua hizi GYM za mtaani zipo chache sana na wana uhaba wa vifaa vya kufundishia hivyo mimi nimeamua kujitolea gloves mikono mitatu kwa kuanzia ili  wapate moyo wa kuendelea na mazoezi pamoja na kujipatia DVD za mafunzo maana ndiyo timu ambazo tunazitegemea kwa siku za usoni kutuletea mabondia wakali watakaoweza kutuletea medali na kutupa sifa nchi hii
Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo  Kocha wa GYM ya Uhuru uwanja wa Basket, Kariakoo  Mohamed Chipota amesema vifaa hivyo pamoja na DVD za mafunzo ya ngumi vimekuja wakati muafaka kwa kuwa kulikuwa nau uhaba wa vifaa kama hivi
hivyo tunaomba wadau mbalimbali wajitokeze kutupa sapoti kama alivyofanya Super D yeye ni kocha wa Mkoa wa Kimichezo Ilala sasa hapa kama amewekeza mabondia wa ilala sasa watatokea hapa kwa siku za usoni
tumeanza hivi karibuni lakini mategemeo yangu ni kuibua vipaji vipya kabisa vya mchezo wa masumbwi nchini alisema Chipota 
Super D ambaye anajihusisha na uuzaji wa DVD za mafunzo ya ngumi pamoja na vifaa vya mchezo huo zikiwemo, Gloves,Gum shit, Clip bandeji dambel,Protector,bukta, fulana na vifaa vyote vya mchezo wa masumbwi

No comments:

Post a Comment