TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, June 27, 2016

MKUU WA MKOA MJINI MAGHARIBI AKANUSHA TAARIFA YA WANYAMA KUCHINJWA MAISARA-ZANZIBAR




Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahamoud amekanusha uvumi wa baadhi ya wananchi kuwa wanyama walioshindwa kugombolewa ndani ya muda uliowekwa, kuchinjwa na kuuzwa kwa beinafuu Maisara.

Mkuu huyo alisema taarifa hizo hazina ukweli ukweli ni kwamba wanyama hao wataendelea kutunzwa na Serikali kwa kipindi kinachokubalika na kwa wale ambao watakaoshindwa kuwakombowa wanyama wao watataifishwa na kuwa mali ya Serikali.

Ameyaeleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Afisini kwake Vuga Mjini Zanzibari wakati akitowa taarifa maalumu kwa wananchi wa Mkoa Mjini Magharibi kuhusu Uthibiti wa wanyama kwenye maeneo yasio ruhusiwa.

Hata hivyo amewataka wafugaji kutokubali kutowa fedha kwa wahusika na ukamataji wa wanyama bila ya kupitia taasisi husika (Manispaa), kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na kuwataka wananchi kutoa taarifa kwa Masheha, Polisi au Manisipaa iwapo kutajitokeza hali hio ili kuzuia vitendo vya rushwa.

Aidha ameeleza katika utekelezaji wa zoezihilo kumejitokeza changamoto zikiwemo malalamiko kwa baadhi ya waumini wa dini ambao wanyama wao wanawatumia kwa ajili ya shughuli za ibada wamekamatwa.

Vilevile kumejitokeza kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaohusisha zoezi hilo na mambo ya kisiasa kwa kuwashajihisha wananchi kuvunja sheria kwa kupingana na utekelezaji wa zoezi hilo.


Alisisitiza kuwa zoezi hilo ni endelevu na Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi haitokuwa na muhali katika utekelezaji wa kazi zao na atakaekwenda kinyume na agizo hilo hatuwa za kisheria zitachukuliwa zidi yake.

Alifahamisha Utekelezaji wa sheria hizo umekuja kutokana na kukithiri kwa uvunjifu wa nidhamu kwa baadhi ya wafugaji katika maeneo mengi ya Mkoa wa Mjini Magharibi jambao ambalo linasababisha uchafunzi wa mazingira, ongezeko la ajali, kukuthiri kwa wizi, kuanza kwa migogoro baina ya wafugaji na wakulima, uharibifu wa miiundombinu pamoja na uhalifu wa kutumia mapanga. 

No comments:

Post a Comment