TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, June 27, 2016

TASAF YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA.



Mfuko huo wa Maendeleo ya Jamii unaotekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini , unatoa huduma kwa Zaidi ya Kaya Milioni Moja na Lakini Moja nchini kote jukumu iliyopewa na serikali katika jitihada zake za kupambana na Umaskini nchini..
Imearifiwa katika kikao hicho kuwa mafanikio makubwa yameanza kujitokeza kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambapo wengi wao wameanza kujiwekea misingi ya kupunguza umaskini kwa kuwa na uwezo wa kusomesha watoto,kupata huduma za afya,kuwa na uhakika wa lishe na kuongeza uchumi wao.
Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pia umeanza kusisimua hamasa ya walengwa wa Mpango huo kuboresha maisha yao kwa kiwango cha kuanza kuboresha makazi yao kwa kujinunulia mabati na kuezeka nyumba,kuanzisha miradi midogo midogo kama ufugaji wa kuku wa kienyeji,mbuzi nahata nguruwe.
Akizungumza katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF bwana Ladislaus Mwamanga amesisitiza watumishi wa Mfuko huo kuendeleza jitihada za kuwahudumia wananchi na hususani walengwa wa Mpango kwa kuzingatia taratibu na kanuni za utumishi wa umma kama zinavyoelekeza.
Zifuatazo ni picha za watumishi wa TASAF wakiwa kwenye ukumbi wa mikutanowa taasisi hiyo maarufu kama “Mlimani City conference hall” ulioko makao makuu ya taasisi hiyo jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment