MATUKIO YA UNGENI LEO.
Mwenyekiti
wa Kamati maalum ya maandalizi ya mechi ya kati ya wabunge ambao ni
wapenzi wa timu yaSimba na wapenzi wa timu ya Yanga Mhe. John Kadutu
akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo mjini
Dodoma uliolenga kuhamasisha wadau mbalimbali kujitokeza kuunga mkono
juhudi za Serikali katika kutatua tatizo la madawati ambapo kamati hiyo
inaratibu maandalizi ya mechi kati ya wabunge ambao ni wapenzi wa timu
hizo itakayofanyika mwezi Agosti 2016 kwa lengo la kukusanya madawati
yatakayo pelekwa katika Halmashauri zote nchini, kushoto ni Mwenyekiti
wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club) Mhe. William Ngeleja.
========================================
WAZIRI MKUU MAJALIWA AMUWAKILISHA RAIS DKT MAGUFULI MKUTANO WA SADC NCHINI BOTSWANA
===============================================
RC MAKALLA AIOMBA BENKI KUU IFANYE UTAFITI KUHUSU UNUNUZI WA MAZAO YAKIWA SHAMBANI.
| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla akizungumza na viongozi na wafanyakazi wa benki kuu ya Tanzania (BOT)tawi la Mbeya mara baada ya kufanya ziara katika kwa engo la kujitabulisha . |
| Baadhi ya viongozi wa benki hiyo wakimsikiliza kwa makini Mkuu huyo wa Mkoa wa Mbeya Amosi Makalla mara baada ya kufanya ziara katika benki hiyo June 28 mwaka huu. |
=============================================
Waziri Nape Nnauye akutana na Wanachama wa Shirikisho la kazi za Sanaa za Ufundi Tanzania.
==================================================
NAIBU KATIBU WAKUU WAAPISHWA LEO ZANZIBAR
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed
Shein akimuapisha Dk.Islam Seif Salum kuwa Naibu Katibu Mkuu ,Mifugo
na Uvuvi katika Wizara ya Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi, katika
hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed
Shein akimkabidhi hati ya kiapo Dk.Islam Seif Salum baada ya
kumuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu ,Mifugo na Uvuvi katika Wizara ya
Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi, katika hafla iliyofanyika leo ukumbi
wa Ikulu Mjini Unguja.
====================================================
SHAMO WORLD FOUNDATION YATOA MSAADA KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA MAUNGA JIJINI DAR LEO.
WATEJA WA SIMBA CEMENT KUNUNUA KUNUNUA SARUJI KWA M PESA
===============================================
















Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya
Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora akizungumza na ujumbe kutoka Kampuni
ya Oracle Afrika (hawapo pichani) walipomtembelea ofisini kwake kwa nia
ya ushirikiano katika kulinda miundombinu na mifumo ya TEHAMA.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya
Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi
mtendaji wa Kampuni ya Oracle Afrika Bw. Cherian Varghese (katikati)
akielezea nia ya Kampuni yao katika ushirikiano wa kulinda miundombinu
na mifumo ya TEHAMA hapa nchini.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia
sekta ya Mawasiliano Dkt. Mhandisi Maria Sasabo (wa kwanza kushoto)
akizungumza na ujumbe kutoka Kampuni ya Oracle Afrika walipotembelea
sekta ya Mawasiliano na kueleza nia yao ya ushirikiano katika kulinda
miundombinu na mifumo ya TEHAMA. 






Mwananchi
akiangalia moja ya bidhaa zinazotengenezwa na kikundi cha African
Flowerless fashion cha Arusha kinachouza bidhaa zake nje ya nchi.Kulia
ni Afisa wa kikundi hicho Bi.Suzana Mwalongo. 
No comments:
Post a Comment