============================================
Serikali yapongezwa kwa kuwajali watu wenye mahitaji maalum
Wakonta
Kapunda akiwa katika picha ya pamoja na wazazi wake,Dada yake,
marafaiki zake aliosoma nao shule ya Sekondari Korogwe na mshiriki
mwenzake katika Shindano la uandishi wa Miswada lililofanyika mjini
Zanzibar leo Jijini Dar es Salaam. Picha Zote na: Frank Shija, MAELEZO.
Kutoka
kulia ni Wakonta Kapunda, Judith Assenga(dada yake na Wakonta), Mwajuma
Selkemani na Chritina Rubangula(waliokuwa wanafunzi wenzake na Wakonta)
wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Wakonta anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika baada
ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata mwaka
2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.
Baba
mzazi wa Wakonta (hayupo pichani) Bw. Brazilio Kapunda akifanya
mahojiano maalum na mwandishi wa Radio ya Kimataifa ya Ufaransa (Rfi)
wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es
Salaam.Mwenye brauzi nyekundu ni Mama wa binti huyo Bibi. Rahel
Lymo,Wakonta anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika
baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata
mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani
Waandishi
wa habari wakiwa wameshika karatasi lenye namba ambazo wadau wanaweza
kutumia kumchangia Wakonta Kapunda (aliyekaa kwenye kiti cha matairi)
ili apatae matibabu na hatimaye kutimiza ndoto zake za kwasaidia wengine
wenye matatizo kama yake leo jijini Dar es Salaam.Binti huyo amekusudia
kutumia kalama ya uandishi wa Filamu na kuanzisha Taasisi itakayo kuwa
msaada kwa watu wenye matatizo ya kupooza. Na: Frank Shija, MAELEZO
Msichana anayetumia Ulimi katika kuandika miswada ya Filamu amewashukuru wadau mbambali kwa misaada yao iliyomfanikisha kuweza kushiriki katika mashindano ya uandishi wa miswada ya Filamu yaliyofanyika mjini Zanzibar.
Shukuruani hizo amezitoa leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa anaongea na waandishi wa habari kuhusu malengo yake ya kuanzisha Taasisi itakayosaidia watu wenye matatizo kama yake.
Wakonta amesema kuwa kwa namna ya kipekee kabisa anaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kupitia kwa Bodi ya Filamu kumgharamia nauli iliyomsaidia kutoka kijijini kwa Kipili wilayani Nkasi mkaani Rukwa hadi kuanikisha ushiriki wake katika mashindano hayo.
“Ninaishukuru sana kwa kipekeke Serikali ya awamu ya Tano, kwani kupitia kwa KatIBU Mtendaji wa Bodi ya Filamu nimeweza kusaidiwa fedha iliyoniwezesha kushiriki katika mashindano ya Uandishi wa Miswada ya Filamu nashukuru sana”. Alisema Wakonta.
Aliongeza kuwa pamoja na Serikali kumpa msaada huo wapo baadhi ya wadau ambao nao wametoa michango yao katika kufanikisha Kampeni yake ambapo amewataja wadau hao kuwa ni Clouds Media waliomsaidia kuhabarisha umma, Joyce Kiria aliye safiri hadi kijijini kwao Kipili ili kumsaidia kupitia kipindi chake cha Wanawake Live.
Wengine ni pamoja na magazeti ya Mwananchi na Uwazi kupitia waliokuwa msaada kupitia habari zao, Fastjet waliomsaidia huduma ya usafiri kutoka Mbeya na Hoteli ya Serena waliomsaidia upande wa malazi wakati alipofika Dar es Salaam akitoea kijini kwao Kipili, Mkoani Rukwa.
Ametoa rai kwa wadau wenye nafasi zao kujitokeza na kushirikina naye katika kukuza kipaji chake ili aweze kukitumia katika kuleta tija kwa Taifa kwani kupitia Filamu unaweza kutangaza Utalii wanchi na ata biashara.
Wakonta alikuwa miongoni mwa washiriki 15 kutoka Afrika Mashariki katika Shindano la Uandishi wa Miswada ya Filamu la Maisha Scree Writer’s Laboratory Course lililofanyika mjini Zanzibar na huku yeye akiwa mshiriki pekee anayetumia Ulimi katika kuandika.
=============================================
Wakonta
Kapunda : Msichana mwenye umri wa miaka (22) akitumia ulimi kuandika
meseji kwenye simu yake ya Mkononi wakati wa mkutano wake na waandishi
wa habari leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Dada yake Bi. Judith
Assenga.Binti huyo ameanza kutumia kiungo hicho katika kuandika baada ya
kupooza sehemu ya mwili wake kutokana na ajali mbaya aliyoipata mwaka
2012 akiwa na wenzake tisa wakati wa Mahafali ya Kidato cha Sita katika
Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe Mkoani Tanga.
Msichana
mwenye umri wa miaka (22) Bi. Wakonta Kapunda akifanya mahojiano maalum
na mwandishi wa Radio ya Kimataifa ya Ufaransa (Rfi) wakati wa mkutano
wake na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Binti huyo
anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika baada ya
kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata mwaka 2012
akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.
Judith
Assenga(kushoto) dada yake na Wakonta Kapunda akimuelekeza jambo mdogo
wake wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Wakonta anatumia ulimi na simu aina ya Smart Phone katika kuandika
baada ya kupooza sehemu ya mwili wake kutoka na ajali mbaya aliyoipata
mwaka 2012 akiwa na wenzake tisa Korogwe Mkoani Tanga.



No comments:
Post a Comment