TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, November 2, 2014

Dk Shein ashuhudia sherehe za KMKM Ushindi Misimu Miwili

unnamedRais wa Zanzibar na Mwenyekti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisaliniana na Mkuu wa KMKM KomodoreHaasan Mussa alipowasili katika sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali mbali zilizofanyika viwanja vya KMKM,[Picha na Ikulu.] unnamed1Rais wa Zanzibar na Mwenyekti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maaalum za SMZ Haji Omar Kheri katika sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali mbali zilizofanyika viwanja vya KMKM [Picha na Ikulu.] unnamed2Mshindi wa kwanza wa mbio za kilomita 10 Philip Jacob Mambo wa Mafunzo akifika mfundani kutoka Kibweni KMKM hadi viwanja vya Maisra Mjini Zanzibar palipofanyika   sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali  mbali  kutoka 2013-2014 mpaka 2014/2015,[Picha na Ikulu.] unnamed3Mshindi wa kwanza wa mbio za makundi maalum ya watu wenye Ulemavu Ali Abdalla kilomita 5 akifika mfundani kutoka Mtoni Mkapa Road hadi  viwanja vya Maisra Mjini Zanzibar palipofanyika   sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali  mbali  kutoka 2013-2014 mpaka 2014/2015,[Picha na Ikulu.] unnamed4Kamanda Haidari akiwa kama kocha kwa Timu yake ya Makamanda waliostaafu wa KMKM katika sherehe za  sherehe za KMKM kwa ushindi wa timu zake kushinda misimu miwili mfulizo michezo mbali  mbali  kutoka 2013-2014 mpaka 2014/2015,zilizofanikisha kwa mchezo wa kuvuta Kamba na hatimaye timu hii ya wastaafu iliwashinda Maofisa walio kazini kwa kuwatoa katika raund zote mbiliviwanja vya Maisara .[Picha na Ikulu.] unnamed5 Kundi la Watu wenye ulemavu wakiwa katika viwanja vya maisara katika kusherehekea Sherehe za KMKM kwa kushinda timu zake  misimu miwili  mfulizo michezo mbali  mbali  kutoka 2013-2014 mpaka 2014/2015,wakifuatilia kwa makini mwendelezo mzima wa sherehe hizo wakati mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ,[Picha na Ikulu.] unnamed6Miongoni mwa Askari wa KMKM waliohudhuria katika sherehe za Jeshi hilo kwa ushindi wa timu zake kushinda michezo mbali mbali katika kipindi cha mwaka 2013-2014 mpaka 2014/2015 katika viwanja vya maisara Mjini Unguja mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ,[Picha na Ikulu.] unnamed7 Mkuu wa KMKM Komodore Hassan Mussa akizungumza machache na kumkaaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein azungumze na wapiganaji katika sherehe za ushindi wa timu zake katika michezo mbali mbali kwa misimu miwili zilizofanyika  viwanja vya maisara Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu.] unnamed8 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na wapiganaji wa jeshi la KMKM katika sherehe za ushindi wa timu zake katika michezo mbali mbali kwa misimu miwili zilizofanyika leo viwanja vya maisara Mjini Zanzibar (kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maaalum za SMZ Haji Omar Kheri  ,[Picha na Ikulu.]

SUNDERLAND AFC NA SYMBION POWER WASHEREHEKEA UIDHINISHAJI WA UJENZI WA UWANJA MPYA WA MICHEZO YA UMMA JIJINI DAR-ES-SALAAM.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwaonyesha jezi yenye jina la Tanzania kwa wageni waalikwa pamoja na wananchi waliohudhuria hafla ya kutoa Kibali kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam. unnamed4Mkurugenzi wa Biashara wa Chama cha Michezo cha Sunderland, Bi. Gary Hutchinson akimkabidhi zawadi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla ya kutoa Kibali chake kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam. unnamed3Mkurugenzi wa Biashara wa Chama cha Michezo cha Sunderland, Bi. Gary Hutchinson akitoa maelezo machache kabla ya kumkaribisha rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kutoa hotuba pamoja na kutoa Kibali chake kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam. unnamed2Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Symbion Bwana Paul Hinks akitoa maelezo yake juu ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam. unnamed1Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Raymond Mushi akitoa maelezo machache kabla ya kumkaribisha rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Profesa Jakaya Mrisho Kikwete kwa ajili ya kutoa hotuba pamoja na kutoa Kibali chake kwa Chuo cha Michezo cha Sunderland kwa ajili ya ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Umma uliopewa jina la Rais Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park. Tukio hilo limefanyika leo 1 Novemba, 2014 eneo la Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam.
…………………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
01 Novemba, 2014.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prof. Jakaya Kikwete amevitaka Vilabu vya mpira wa miguu nchini kuwekeza katika timu za vijana wadogo walio chini ya umri wa miaka 18 ili viweze kuwa na mafanikio ndani na nje ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa na Rais Prof. Kikwete leo jijini Dar es saam alipokuwa akizindua ujenzi wa kituo cha michezo cha vijana wadogo waliochini ya miaka 18 kinachojengwa nchini eneo la Kidongo Chekundu manispaa ya Ilala.
“Katika nchi yetu, timu ya soka ya taifa haifanyi vizuri na michezo mingine nayo vivyo hivyo, vilabu mbalimbali vya michezo navyo havifanyi vizuri katika michezo yao ya ndani na nje” alisema Prof. Kikwete.
Prof. Kikwete aliendelea kusema “Kiini cha timu yetu ya soka ya taifa na vilabu vyetu kutokufanya vizuri katika mashindano, haviwekezi katika vijana wadogo”.
Katika kufanikisha adhima ya kuwa vilabu na timu ya taifa ya mpira wa miguu kuwa na mafanikio, Rais Kikwete amewaagiza viongozi Shirikisho la Mpira wa Miguu na wa vilabu vya mpira wa miguu nchini watekeleze majukumu yao ipasavyo ili soka la Tanzania liwe la mafanikio kwa wachezaji mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
Aidha, amelishauri Shirikisho la mpira wa miguu nchini liweke utaratibu ambao utailazimu kila timu kuwa na timu ya vijana wadogo kama ilivyo katika mataifa mengine duniani ambapo kwa mataifa hayo, suala la kuwa na timu ya vijana wadogo na uwanja wao sio la hiyari.
Kwa upande wake Kurugenzi Mtendaji wa Timu ya soka ya Sanderland ya nchini Uingereza ambao ndiyo watakaotoa wataalamu wa michezo watakaofundisha katika kituo hicho Bi. Margaret Byrne amesema kuwa kituo hicho kitakuwa na uwanja wa mpira wa miguu wa kisasa wenye ukubwa wa mita 100×60, viwanja viwili vya mpira wa kikapu, sehemu ya kuegesha magari 20 na kituo cha daladala, kiwanja cha kuchezea watoto.
 Bi. Margaret alisisitiza kwa ndani ya kituo hicho,  kutakuwa pia na jingo la utawala, vyumba vine vya wachezaji kubadilishia nguo vikiwa na vyoo na bafu, vyumba viwili vya wafanyakazi pamoja na chumba cha chakula ambacho kitaendana na madhari ya kituo hicho.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Symbion ya nchini Marekani Paul Hinks amesema kuwa kampuni yake iko mstari wa mbele na wataendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kukuza sekta ya michezo nchini kwa kujenga kituo cha soka kwa vijana wadogo.
Ujenzi wa kituo hicho ulizinduliwa na Rais Kikwete kwa kupanda mti wa mnazi ikiwa ni alama ya kuashiria kuanza ujenzi huo rasmi ambao unatarajiwa kukamilika mapema mwakani 2015 ambapo alibainisha kuwa kuwa siku ya Oktoba Mosi mwaka huu, imekuwa ni siku ya aina ya kipekee ambayo inafungua ukurasa mpya katika historia ya michezo nchini.

WAZIRI WA AFYA MH. SEIF RASHIDI AZINDUA RASMI GHETTO RADIO KATIKA HOSIPITALI YA TEMEKE JIJINI DAR.

Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid akiongea na Wauguzi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke, Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi Rasmi wa Radio hiyo, ambayo lengo lake ni kuwakomboa vijana wa Mtaani pamoja na vipindi vingine vya kuelimisha Jamii na Burudani, Pia amewashukuru kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali ambavyo vitasaidia katika Hospitali hiyo  Tarehe 1.11.2014
 Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm iliyo fanyika katika  katika Hosipitali Teule ya Mkoa wa Temeke Ambapo Ghetto Radio Imeweza kufunguliwa Rasmi Katika Mkoa huo nakuweza kutoa Msaada Vifaa Mbalimbali pamoja na Madawa Ambavyo Vyote kwa ujumla vimegharimu kiasi Cha Shilingi Milioni sita na Laki sita.
Mkurugenzi
wa Ghetto Radio Matt Brouwer akizungumza neno wakati wa uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Ambapo Bw.Brouwer Alisema kuwa Ghetto Radio ilianzishwa nchini Kenya Miaka Sita iliyopita nakuweza kuwasaidia vijana mbalimbali Hivyo wameweza kuingia Nchini Tanzania Ilikuendeleza kuwapa vijana Fursa Na elimu INayo Tolewa na Kituo Hicho Kwa Hapa Nchini
Mganga Mkuu wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke Amaani K. Malima akitoa neno la Shukurani kwa Timu nzima ya Ghetto Radio ya Sibuka Fm kwa kufanya uzinduzi wa Radio yao katika Hospitali hiyo pia kutoa Msaada wa vitu mbalimbali vitakavyo saidia katika eneo hilo.
 Meneja wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm  Edward  Lukaka  akitoa maelezo machache ya malengo ya Radio hiyo pia kueleza mikakati ya kuendelea kutoa msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba katika Vituo zaidi vya Afya.
 Mkurugenzi wa kituo cha afya cha Iran Nchini Tanzania Dkt. Farhad Arjomandi akiwashukuru Ghetto Radio ya Sibuka FM kwa kuanzisha Kituo hicho pia na wao wametoa vifaa vya matibabu kwa ajili ya kushiriki uzinduzi huo wa Radio
 Mwenyekiti wa Red Cross Mkoa wa Dar es salaam Leonard Masonu  akitoa neno la Shukurani
Hivi ni Baadhi ya vitu ambavyo vimetolewa na Ghetto Radio ya Sibuka Fm katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke wakati wa uzinduzi Rasmi wa Radio hiyo
 Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid akikabidhiwa Rasmi msaada wa Vifaa na Vitu mbalimbali vitakavyo tumika katika Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke kutoka kwa Ghetto Radio ya Sibuka Fm

Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid kushoto  Akishukuru kwa vifaa hivyo.
 Baadhi ya Wadau mbalimbali walioshiriki katika Sherehe hiyo ya Uzinduzi Rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
 Baadhi ya Wauguzi wakiwa katika uzinduzi huo Rasmi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm
 Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakijiandaa kuelekea kutoa Msaada wa vitu mbalimbali katika vyumba vya wagonjwa
  Wakiwa wanaelekea Wodini
 Kulia ni Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akiwa katika Wodi ya watoto kukabidhi zawadi za watoto na mama zao, katikati ni Mwanamuziki Mkongwe wa Bongo Flava Juma Nature ambaye ni Balozi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm

Balozi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Juma Nature akiwa anatandika Shuka moja wapo katika Wodi ya watoto kuashiria kukabidhi mashuka hayo.
Baadhi ya Timu ya wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm

SHUTUMA DHIDI YA TFF

index17
Oktoba 31 mwaka huu kupitia vyombo vya habari Wakili Damas Ndumbaro alitoa shutuma mbalimbali dhidi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Tunapenda kuuleza umma wa Watanzania yafuatayo;
1.Hukumu dhidi ya Wakili Ndumbaro ilitolewa na chombo halali kwa mujibu wa Katiba ya TFF. Hivyo, TFF inatoa tahadhari kwa wanafamilia wa mpira wa miguu kutomhusisha Wakili Ndumbaro katika masuala ya mpira wa miguu katika kipindi hiki anachotumikia adhabu.
2.Hadi sasa TFF haijapokea rufani yoyote kutoka kwa Wakili Ndumbaro. Hii ni kwa kuwa kupitia barua yake kwa TFF aliagiza asikabidhiwe nyaraka yoyote kutoka TFF hadi Oktoba 30 mwaka huu, hivyo hukumu ya Kamati ya Nidhamu dhidi yake alikabidhiwa Oktoba 30 mwaka huu. Alichokifanya Wakili Ndumbaro ni kuleta TFF barua ya kusudio la kukata rufani.
3.Tuhuma za ubadhirifu wa TFF zilizotolewa na Wakili Ndumbaro si za kweli. TFF inatafakari hatua za kisheria na kikanuni za kuchukua dhidi ya tuhuma hizi.
4.Mkataba wa TFF na TBL:
TFF inapenda kuwahakikishia wadau wa mpira wa miguu kuwa hakuna ubadhirifu wa aina yoyote katika matumizi ya fedha za mkataba wa TFF/TBL. TFF ingependa itoe kwa umma ufafanuzi wa vipengele vya mkataba huo na jinsi unavyoendeshwa lakini masharti ya mkataba huo (confidentiality clause) yanatuzuia kufanya hivyo.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi alikutana na klabu za Ligi Kuu na kuzielekeza zikae na kujadili kanuni za Ligi, kisha zipendekeze maboresho ili yajadiliwe katika kikao kijacho cha Kamati ya Utendaji.
TFF inapenda kuchukue fursa hii kusisitiza umuhimu wa kufuata mifumo tuliyojiwekea katika kutatua matatizo/kero zetu mbalimbali, utulivu ni muhimu katika kuendeleza mpira wa miguu.

TANZANIA NA BURUNDI ZA SAINI MKATABA WA MIAKA 50 KUSAFIRISHA UMEME KUTOKA MRADI WA RUSUMO

 Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania , Profesa, 
Sospeter Muhongo.
 Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, 
Come Manirakiza.
 Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania , Profesa, Sospeter Muhongo (kushoto) na Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, Come Manirakiza wakisaini mkataba huo.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospeter Muhongo (kushoto), akibadilishana hati na Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, Come Manirakiza, baada ya kutiliana saini mkataba wa miaka 50 wa  usafirishaji wa umeme kutoka Mradi wa Rusumo kwenda nchini humo katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam jana. Mradi huo unazihusisha nchi tatu za Tanzania, Rwanda na Burundi.
Hapa mkutano wa maofisa wa Tanaznia na Burundi ukiendelea.
 Maofisa wa Tanzania wakiwa kwenye hafla hiyo ya 
kusaini mkataba huo.
 Maofisa wa Burundi na Tanzania wakiwa katika 
hafla hiyo.
 Maofisa wa Burundi wakiwa kwenye sherehe hiyo.
 Maofisa wa Tanzania wakiwa kwenye tukio hilo.
 Wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
 Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania , Profesa, Sospeter Muhongo (kushoto) na Waziri wa Nishati na Madini wa nchi ya Burundi, Come Manirakiza wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa nchi hizo mbili wanahusika na wizara hiyo.
 …………………………………………………………………….
Dotto Mwaibale
 
 
SERIKALI ya Tanzania na Burundi zimesaini mkataba wa miaka 50 wamakubaliano wa mradi wa pili wa kusafirisha umeme utakaozalishwa kwenye kituo cha Rusumo.
 
TANZANIA NA BURUNDI ZA SAINI MKATABA WA MIAKA 50 KUSAFIRISHA UMEME KUTOKA MRADI WA RUSUMO
Awali Tanzania, Burundi na Rwanda zilisaini mkataba wa kwanza wa mradi wa kituo cha kuzalisha umeme cha rusumo chenye mega watt 80, kilichopo wilayani Ngara, Mkoani Kagera, mwaka 2013 ambacho kiligharimu takribani dola za kimarekani milioni 340 zilizotolewa na benki ya Dunia.
 
Akizungumza Dar es Salaam jana baada ya kusaini mkataba huo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospeter Muhongo, alisema mkataba huo umezihusisha nchi mbili ambapo alibainisha kuwa kupitia mradi huo ambao umeanza katika sehemu ya mwisho ya kutekeleza mradi wa kwanza ulioanza mwaka jana yapo baadhi ya maeneo nchini yatapata umeme.
 
Alisema kupitia mradi huo nchi itaweza kuimarisha grid ya Taifa na kupunguza tatizo la umeme kwenye maeneo mengi nchini.
 
Waziri Muhongo aliongeza kuwa pamoja na hatua hiyo pia kuitia mradi huo utaajiri wafanyakazi kutoka nchi zote tatu na hata wa mataifa mwengine ambapo alibainisha kuwa kwa sasa katika kituo cha mto rusumo wapo walioajiriwa kutoka nchi husika na miradi hiyo na mataifa mengine.
 
Kuhusu ujenzi wa mfumo wa usafirishaji umeme alisema kila nchi itajitegemea katika kusafirisha umeme na kubainisha kuwa Tanzania itajenga mfumo huo kuanzia miaka michache ijayo.
 
Hata hivyo Prof. Muhongo hakubainisha kiasi halisi kitakacho tumika kuendeshea mradi huo wa wamu ya pili

WAZIRI MKUU MIZENGIO PINDA KATIKA HAFLA YA KUCHANGIA MADAWATI

1Waziri Mkuu Mizengo Pinda wa tatu kutoka kulia akibonyeza namba ya simu kwa ajili ya kuchangia madawati 6000 ya wanafunzi wenye ukosefu  wa madawati nchini katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua vifaa hivyo  iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam. 3Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia ) akiangalia moja ya mfano wa dawati katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua  madwati 6000 kwa ajili ya wanafunzi  iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam.
4Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitoa hotuba yake  katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kuununua madawati 6000kwa ajili ya wanafunzi wenye ukosefu wa vifaa hivyo  iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam.
5Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Mahusiano na Utaratibu ,Stephen  Wassira  akitatangaza kiasi cha sh. milioni 17 kilichochangwa na wanabunda  ajili ya kuchangia madawati 6000ya wanafunzi wenye ukosefu  wa madawati nchini katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua vifaa hivyo  iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam. 6 Mke  wa Rais Mama Salma  Kikwetewa pili kutoka (kulia) akiingia katika ukumbi wa Diamond Jubilee kwa ajili ya kuhudhuria hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua  mawadati  6000  ya wanafunzi wenye ukosefu wa vifaa hivyo   iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam. Kulia wa kwanza ni Balozi  Mwanaidi  Maajar na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi. 6bMke  wa Rais Mama Salma  Kikwete wan ne kutoka (kulia)akiwa katika picha ya pamoja na  baadhi ya wadau   katika ukumbi wa Diamond Jubilee kwenye  hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua  mawadati  6000  ya wanafunzi wenye ukosefu wa vifaa hivyo   iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam. 7Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Christopher Majaliwa(kushoto) akifurahia jambo kwenye hafla hiyo na Mstahiki  Meya wa Manispaa ya Ilala ,Jerry Silaa.
9 Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenister Mhagama akitangaza wizara yake na taasisi zake ilivyochangia Sh.milioni 100. 12Waziri Mkuu Mizengo Pinda wa akizungumza jambo na  Jaji Mstaafu Joseph Warioba hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua vifaa hivyo  iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam kwa ajili ya kuchangia madawati 6000 ya wanafunzi wenye ukosefu  wa madawati nchini . 16Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria katika hafla hiyo 17Msanii Mwasiti Almasi akituimbuiza na wasanii wenzake kutoka THI kwenye  hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa  na Hassan Maajar Trust yenye lengo la kukusanya Sh. milioni 500 ili kununua  mawadati  6000  ya wanafunzi wenye ukosefu wa vifaa hivyo   iliyofanyika jana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dares Salaam.
PICHA ZOTE NA MAGRETH KINABO, MAELEZO