TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, May 6, 2015

WANANCHI NA TAASISI WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI WANAPOTAKA KUPIMA MAENEO YAO YA ARDHI KUEPUKA KUTAPELIWA.

Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani vijijini wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Bw. Huruma Lugalla (kushoto) akitoa maelekezo kwa wataalam wa Upimaji na Ramani wa wizara hiyo  wakati wa uhakiki wa moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze, Bagamoyo mkoani  Pwani iliyopimwa na Kampuni ya Intergrated Property Consultancy and Services (IPCS) ya Morogoro na kubainika kuwa chini ya kiwango.
Wataalam wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakifanya uhakiki wa moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze, Bagamoyo mkoani Pwani lililopimwa chini ya kiwango. Katikati (aliyesimama) ni Bw. Bernard Malugu, Mkurugenzi wa Kampuni ya Intergrated Property Consultancy and Services (IPCS) ya Morogoro iliyoifanya kazi hiyo chini ya kiwango.
Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani vijijini wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Bw. Huruma Lugalla (kushoto) akifuatilia moja ya eneo ambalo lilitakiwa kuwa na  alama ya mpaka ambalo halikuwa na alama yoyote wakati wa uhakiki wa moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze, Bagamoyo mkoani  Pwani iliyopimwa na Kampuni ya Intergrated Property Consultancy and Services (IPCS) ya Morogoro ambayo ilibainika kuwa chini ya kiwango. Kulia ni Bw.Allex Kachoka Mpima Ardhi wa wizara hiyo.
Moja ya alama ya mpaka ya ambayo iligundulika kujengwa chini ya kiwango wakati wa uhakiki uliofanywa na wataalam wa Wizara ya Ardhi kwenye moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze, Bagamoyo mkoani  Pwani.Kampuni ya Intergrated Property Consultancy and Services (IPCS) ya Morogoro ambayo ilipewa kazi ya Upimaji wa eneo hilo  imeifanya kazi hiyo chini ya kiwango.
Wapima Ardhi na Mipaka wa  Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiendelea na zoezi la uhakiki wa alama za mipaka kwa kutumia kifaa kiitwacho Hand Heled GPS kwenye moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze,Bagamoyo Pwani.(Picha zote na Aron Msigwa).
===========================================================


Na. Aron Msigwa –MAELEZO.


Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeto tahadhari kwa Taasisi na wananchi wanaotaka kupimiwa maeneo yao ya ardhi kuhakikisha kuwa wanafuata sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia masuala ya upimaji wa ardhi ili kuepuka kupata hasara na kuingia kwenye migogoro ya ardhi isiyo ya lazima kutokana na kutumia watu au makampuni yasiyosajiliwa kishera.
Hatua hiyo imekuja kufuatia baadhi ya makampuni yanayojishughulisha na upimaji wa Ardhi na ramani kugundulika kufanya kazi za wateja wao chini ya viwango kufuatia ramani zilizowasilishwa na makampuni  hayo  wizarani hapo kwa ajili ya kuidhinishwa kukosa sifa pindi zinapofanyiwa uhakiki na wataalam wa wizara hiyo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani vijijini wa wizara hiyo Bw. Huruma Lugalla akizungumza mara baada ya timu ya wataalam wa wizara hiyo kufanya uhakiki wa moja ya ramani ya eneo linalopaswa kuwa la makazi ya watu na taasisi nje kidogo ya mji wa Chalinze, Bagamoyo mkoani  Pwani ambalo  upimaji wake umekiuka kanuni na taratibu amesema Serikali haitayafumbia macho makampuni yote yanayochukua fedha za wananchi na Taasisi na kisha kufanya upimaji usiokidhi viwango vilivyowekwa na wizara hiyo kwa mujibu wa Sheria.
Amesema wizara hiyo itaendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuyafungia   makampuni yote yanayobainika kufanya kazi chini ya kiwango, kukiuka kwa makusudi taratibu za upimaji wa ardhi na kufanya uzembe wa kushindwa kuweka mipaka na alama sahihi za maeneo wanayoyapima jambo linalochangia mivutano na migogoro pindi maeneo husika yanapogawiwa kwa wananchi.
“Nawaomba wananchi na Taasisi mbalimbali zinazotaka kupimiwa maeneo yao kwa kutumia makampuni kuwa makini na kuchukua tahadhari ili kuepuka hasara ya kulipa gharama za upimaji mara mbili, msichukue watu wa kati au kampuni zisizosajiliwa kisheria  ambazo haziko kwenye orodha ya Katibu wa Baraza la Taifa la Wapima Ardhi” Amesisitiza.
Bw. Lugalla ameeleza kuwa Kampuni ya Intergrated Property Consultancy and Services (IPCS) kutoka Morogoro iliyohusika na  zoezi la upimaji na ramani katika eneo hilo haikufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa sheria kufuatia ramani iliyowasilishwa na Mkurugenzi wake Bw. Bernard Malugu wizarani hapo kushindwa kukidhi vigezo vya ubora unaotakiwa mara baada ya kuhakikiwa na wataalam wa Upimaji na ramani wa Wizara.
Amesema wataalam wa upimaji na ramani wa Wizara hiyo mara baada ya kufanya  uhakiki wa eneo hilo wamebaini   ukosefu wa alama (bikoni) za baadhi viwanja, kukosekana kwa pini za kugawa viwanja na tofauti umbali wa eneo la kiwanja kimoja hadi kingine iliyokuwepo kwenye ramani ambayo haikuendana na uhalisia wa eneo husika wakati wa zoezi la uhakiki.
 Aidha, amebainisha kuwa ramani ya eneo hilo ilisainiwa kimakosa na Mkurugenzi wa Kampuni hiyo kufuatia kampuni yake  ambayo imesajiliwa kisheria dhamana  kuamua kumtafuta mtu wa kati wa kuifanya kazi hiyo badala yake na kisha Mkurugenzi wake Bw. Bernard Malugu kuidhinisha ramani hiyo kwa kuisaini huku ili ipelekwe wizarani kupatiwa kibali huku akijua wazi kanuni na taratibu zinazosimamia sekta hiyo hazimruhusu kutoa kazi kwa mtu au kampuni nyingine.
“Ili kuepusha migogoro ya ardhi inayoweza kutokea katika eneo lile taratibu zitafuatwa ili kampuni hiyo iifanye kazi ile upya kwa gharama zake na kisha kuwaita wataalam wa wizara kufanya uhakiki upya ili kujiridhisha kabla ya kutoa kibali cha viwanja hivi, Sisi kama wizara hatutakubali kuendelea kulaumiwa na wananchi kwa uzembe unaofanywa na makampuni haya” Amesisitiza.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya IPCS iliyopewa kazi ya kupima eneo hilo akitoa utetezi kwa kampuni yake mara baada ya kufanyika kwa uhakiki huo alikiri kuwa kampuni yake imefanya  makosa na kukiuka sheria, miiko na maadili yanayosimamia shughuli za upimaji na ramani nchini.
Amesema  yeye kama Mkurugenzi wa kampuni hiyo alisaini ramani ya eneo hilo Machi 19, 2015 kimakosa hivyo kampuni yake  imeonyesha uzembe na udhaifu wa usimamizi ikiwemo yeye mwenyewe kutomfahamu mtu wa kati aliyeifanya kazi hiyo.
Aidha, amesema kampuni yake iko tayari kuyabeba mapungufu yote yaliyojitokeza na kukubali kurudia kazi ya kupima na kuweka mipaka iliyokosekana endapo itaruhusiwa na wizara hiyo kufanya hivyo


Friday, May 1, 2015

WAKUU WA TAASISI ZA TAKWIMU WA NCHI ZA AFRIKA WAKUTANA JIJINI DAR !

 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) nchini Tanzania Dkt.Albina Chuwa akifungua Kongamano la Kimataifa kuhusu Uongozi na utawala la wataalam na Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi za Afrika zinazozungumza lugha ya Kiingereza na Kifaransa leo jijini Dar es salaam. Kongamano hilo la siku 2 linajadili namna Bora ya uendeshaji wa Taasisi za Takwimu na namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za masuala ya Takwimu Barani Afrika.
(Picha Zote na: Aron Msigwa –MAELEZO
 Mtendaji Mkuu wa  Taasisi ya  Takwimu ya Bara la Afrika Bw. Joseph ILboudo akizungumza na watalaam na wakuu wa Ofisi za Takwimu Kongamano la Kimataifa kuhusu Uongozi na utawala lililowahusisha wataalam na Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi  za Afrika zinazozungumza lugha ya Kiingereza na Kifaransa leo jijini Dar es salaam.
 Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Takwimu Barani Afrika (AFRISTAT) pia mtaalam wa Takwimu kutoka nchini Cameroon Bw. Martin BALEPA akiwasilisha mada kuhusu namna nchi za Bara la Afrika zinavyoweza kukabiliana na changamoto mbalimbali kwa kutumia takwimu sahihi.
 Bw. Andry Andriantseheno kutoka UNECA akiongoza kongamano hilo la siku 2 la  watalaam na wakuu wa Ofisi za Takwimu wa nchi za Afrika linalojadili masuala ya Uongozi na utawala na leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Dkt. Albina Chuwa, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu kutoka Tanzania wenyeji wa mkutano huo.
 Baadhi ya watalaam na wakuu wa Ofisi za Takwimu kutoka katika nchi mbalimbali za Bara la Afrika wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa kongamano la Kimataifa kuhusu Uongozi na utawala linaloendelea jijini Dar es salaam.
Watalaam na wakuu wa Ofisi za Takwimu kutoka katika nchi mbalimbali za Bara la Afrika wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa kongamano la Kimataifa la siku 2 linalojadili masuala ya Uongozi na utawala wa taasisi za takwimu Barani Afrika linaloendelea jijini Dar es salaam.