TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, April 5, 2016

HEKTA 5000 ZA ARDHI YA KIJIJI CHA LUHANGA WILAYANI MBARALI ZARUDISHWA KWA WANANCHI KUTOKA WAWEKEZAJI







SMZ KUTILIANA SAINI NA NORWAY MAKUBALIANO YA KUIMARISHA SEKTA YA UMEME







MKUU WA MKOA WA MWANZA JOHN MONGELLA AAMURU KURUDIWA KWA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA MKOA WA MWANZA







 
AFISA HABARI NA UHUSIANO OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA 04.April,2016

RAIS DK. SHEIN AKUTANA NA BALOZI MASILINGI

WAZIRI KITWANGA APIGA MARUFUKU KUCHEZA “POOL TABLE” WAKATI WA KAZI JIMBONI KWAKE










SHIRIKA LA EFG LAFANYA TAMASHA LA KUPINGA UKATILI WA JINSIA AWAMU YA PILI KATIKA SOKO LA MCHIKICHINI ILALA JIJINI DAR ES SALAAM

BENKI YA TADB YAINGIA MAKUBALIANO NA PASS KATIKA UCHOCHEAJI WA KILIMO CHENYE TIJA KWA WAKULIMA.









Monday, April 4, 2016

FEDHA ZA MAADHIMISHO YA MUUNGANO MWAKA HUU KUPANUA BARABARA YA MWANZA-AIRPORT.

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM WAKAMATA VITENGE NA PAMPERS ZISIZOLIPIWA USHURU

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii. JESHI la Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata Marobota 10 ya vitenge na Katoni 17 za Pampers  pamoja na Gari lililotumika kubebea hitu hivyo katika eneo ya Gezaulole lililopo pembezoni mwa ufukwe wa bahari ya Hindi.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa kukamatwa kwa gari lenye vitu hivyo ni mara baada ya kupewa taarifa na Raia wema kwa kuwa katika eneo hilo kunapitishiwa mali zisizotolewa ushuru.

Siro amesema kuwa Gari lililo kamatwa na Vitenge na Pampers ni aina ya Suzuki Carry lenye namba za usajili T490 CQB ambalo nalo linashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam.

Pia Sirro amesema kuwa mwananchi anaeona kuwa alitelekeza gari hilo lililo na vitu hivyo ajisalimishe Polisi ili apelekwe Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) akalipie ushuru wa vitu hivyo.

Katika Operesheni nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kukamata gari moja la wizi aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 314 DFH  ambapo kabla ya kuibwa lilikuwa na namba za usajili T 622 DDR  ikiwa gari hilo ni Mali ya Hellen Michael liliibwa maeneo ya Kitunda Kivule ambapo lililuwa limeegeshwa nyumbani kwake. Pia Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limkamata watu wawili wakiwa na Pikipiki mbili zenye namba za usajili MC343 ASL aina ya Boxer na MC 606 ex aina ya Fercon ambazo ni za wizi na watuhumiwa hao kukuli kuwa wameziiba Pikipiki hizo.

Mhe. Mhagama aagiza wamiliki wa vyombo vya usafiri kuzingatia mikataba ya kazi na ajira kwa madereva



Mhe mhagama alitoa agizo hilo wakati wa mkutano wake na Kamati hiyo uliofanyika Aprili 1, 2016 katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuangalia namna bora ya kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya usafirishaji. 

Katika kikao cha Kamati hiyo inayoundwa na Wamiliki wa malori, daladala, mabasi, vyama vya abiria, Idara ya Usafirishaji, Shirika la viwango, Wakala wa Vipimo, Jeshi la polisi, watu wa usalama barabarani, TANROADS  na Umoja wa Wasafirishaji Abiria Dar es Salaam (UWADAR) mhe. Mhagama alisisitiza kuwa Serikali haitawafumbia macho wamiliki wa vyombo vya usafiri ambao hawazingatii mikataba ya kazi kwa madereva. 
“Ninaagiza mikataba ya maderva iangaliwe upya na ikiwezekana yaainishwe majina ya wamiliki wa magari wanaokiuka haki na sheria zilizopo za kuwapa madereva mikataba na stahiki zao ili sheria iweze kuchukua mkondo wake,”alisema Mhagama 

Kutokana na changamoto mbalimbali za madereva zilizobainishwa wakati wa mkutano huo  Mhe.Waziri aliwataka wajumbe wote kuangalia namna nzuri ya kukabili changamoto hizo ili kuhakikisha malalamiko ya madeva yanaisha na kufanya sekta hiyo kuwa na  amani na utulivu. 

“Lengo kuu ni kuona sekta ya usafirishaji inakuwa salama na yenye amani kwani ikumbukwe sekta hii ni nyeti, inabeba roho za watu wengi kila iitwapo leo kwa kuwasafirisha mikoani na nje ya mikoa.” Alisisitiza Mhagama. 

Nae mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Leonard Chamuliho aliomba kamati kuyafikia maazimio ya muhimu yaliyojadiliwa na huku akisisitiza agizo la mhe. Mhagama la kuwataka wamiliki na waajiri wote kuzifuata na kuzitekeleza sheria za mikataba kwa waajiriwa wote. 

Rais Magufuli , Raila Odinga Kila Mtu Kivyake

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kuashiria kuagana na wageni wake, Raila Odinga pamoja na Mkewe Ida Odinga waliofika Chato juzi kwa ajili ya mapumziko na kumpongeza Mhe. Rais.
 Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiagana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita. Odinga alifika Chato juzi akiwa na familia yake kwa ajili ya kumpongeza Mhe. Rais pamoja na kushiriki pamoja Ibada ya jumapili ya pili ya Pasaka katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Raila Bi. Ida Odinga.
 Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiagana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita. 
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiagana na Mke wa Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga, Bi Ida Odinga katika katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Bi Ida Odinga, huku Raila Odinga akiagana na Mama Janeth Magufuli katika katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Raila Odiga, Ida Odinga pamoja na Mkewe mama Janeth Magufuli katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia watoto aliwakuta kwenye uwanja wa Mazaina Chato mkoani Geita. PICHA NA IKULU