TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Tuesday, April 5, 2016
MKUU WA MKOA WA MWANZA JOHN MONGELLA AAMURU KURUDIWA KWA UHAKIKI WA WATUMISHI HEWA MKOA WA MWANZA
Monday, April 4, 2016
JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM WAKAMATA VITENGE NA PAMPERS ZISIZOLIPIWA USHURU
Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
JESHI
la Polisi kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekamata Marobota 10 ya
vitenge na Katoni 17 za Pampers pamoja na Gari lililotumika kubebea
hitu hivyo katika eneo ya Gezaulole lililopo pembezoni mwa ufukwe wa
bahari ya Hindi.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa kukamatwa kwa gari lenye vitu hivyo ni mara baada ya kupewa taarifa na Raia wema kwa kuwa katika eneo hilo kunapitishiwa mali zisizotolewa ushuru.
Siro amesema kuwa Gari lililo kamatwa na Vitenge na Pampers ni aina ya Suzuki Carry lenye namba za usajili T490 CQB ambalo nalo linashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam.
Pia Sirro amesema kuwa mwananchi anaeona kuwa alitelekeza gari hilo lililo na vitu hivyo ajisalimishe Polisi ili apelekwe Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) akalipie ushuru wa vitu hivyo.
Katika Operesheni nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kukamata gari moja la wizi aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 314 DFH ambapo kabla ya kuibwa lilikuwa na namba za usajili T 622 DDR ikiwa gari hilo ni Mali ya Hellen Michael liliibwa maeneo ya Kitunda Kivule ambapo lililuwa limeegeshwa nyumbani kwake. Pia Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limkamata watu wawili wakiwa na Pikipiki mbili zenye namba za usajili MC343 ASL aina ya Boxer na MC 606 ex aina ya Fercon ambazo ni za wizi na watuhumiwa hao kukuli kuwa wameziiba Pikipiki hizo.
Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, amesema kuwa kukamatwa kwa gari lenye vitu hivyo ni mara baada ya kupewa taarifa na Raia wema kwa kuwa katika eneo hilo kunapitishiwa mali zisizotolewa ushuru.
Siro amesema kuwa Gari lililo kamatwa na Vitenge na Pampers ni aina ya Suzuki Carry lenye namba za usajili T490 CQB ambalo nalo linashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam.
Pia Sirro amesema kuwa mwananchi anaeona kuwa alitelekeza gari hilo lililo na vitu hivyo ajisalimishe Polisi ili apelekwe Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) akalipie ushuru wa vitu hivyo.
Katika Operesheni nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam lilifanikiwa kukamata gari moja la wizi aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 314 DFH ambapo kabla ya kuibwa lilikuwa na namba za usajili T 622 DDR ikiwa gari hilo ni Mali ya Hellen Michael liliibwa maeneo ya Kitunda Kivule ambapo lililuwa limeegeshwa nyumbani kwake. Pia Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limkamata watu wawili wakiwa na Pikipiki mbili zenye namba za usajili MC343 ASL aina ya Boxer na MC 606 ex aina ya Fercon ambazo ni za wizi na watuhumiwa hao kukuli kuwa wameziiba Pikipiki hizo.
Jeshi la
Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam kwa kipindi cha wiki moja
limefanikiwa kukamata Pikipiki 519 katika Operesheni ya ukamataji wa
Pikipiki kwa makosa mbalimbali operesheni hiyo ilifanywa katika mikoa ya
Ilala piki[iki 183,Kinondoni pikipiki 139 na Temeke pikipiki 197.

Mhe. Mhagama aagiza wamiliki wa vyombo vya usafiri kuzingatia mikataba ya kazi na ajira kwa madereva
Mhe mhagama alitoa agizo hilo wakati wa mkutano wake na Kamati hiyo uliofanyika
Aprili 1, 2016 katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dar es
Salaam kwa lengo la kuangalia namna bora ya kukabiliana na changamoto
zinazoikabili sekta ya usafirishaji.
Katika kikao cha Kamati hiyo inayoundwa na Wamiliki wa malori, daladala,
mabasi, vyama vya abiria, Idara ya Usafirishaji, Shirika la viwango, Wakala wa
Vipimo, Jeshi la polisi, watu wa usalama barabarani, TANROADS na Umoja wa
Wasafirishaji Abiria Dar es Salaam (UWADAR) mhe. Mhagama alisisitiza kuwa
Serikali haitawafumbia macho wamiliki wa vyombo vya usafiri ambao hawazingatii
mikataba ya kazi kwa madereva.
“Ninaagiza mikataba ya maderva iangaliwe upya na ikiwezekana yaainishwe majina
ya wamiliki wa magari wanaokiuka haki na sheria zilizopo za kuwapa madereva
mikataba na stahiki zao ili sheria iweze kuchukua mkondo wake,”alisema Mhagama
Kutokana na changamoto mbalimbali za madereva zilizobainishwa
wakati wa mkutano huo Mhe.Waziri aliwataka wajumbe wote kuangalia namna
nzuri ya kukabili changamoto hizo ili kuhakikisha malalamiko ya madeva yanaisha
na kufanya sekta hiyo kuwa na amani na
utulivu.
“Lengo kuu ni kuona sekta ya usafirishaji inakuwa salama na yenye amani kwani
ikumbukwe sekta hii ni nyeti, inabeba roho za watu wengi kila iitwapo leo kwa
kuwasafirisha mikoani na nje ya mikoa.” Alisisitiza Mhagama.
Nae mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Leonard Chamuliho aliomba kamati kuyafikia
maazimio ya muhimu yaliyojadiliwa na huku akisisitiza agizo la mhe. Mhagama la
kuwataka wamiliki na waajiri wote kuzifuata na kuzitekeleza sheria za mikataba
kwa waajiriwa wote.
Rais Magufuli , Raila Odinga Kila Mtu Kivyake
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono
kuashiria kuagana na wageni wake, Raila Odinga pamoja na Mkewe Ida Odinga
waliofika Chato juzi kwa ajili ya mapumziko na kumpongeza Mhe. Rais.
Waziri
Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiagana na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Shule ya
Sekondari ya Chato mkoani Geita. Odinga alifika Chato juzi akiwa na
familia yake kwa ajili ya kumpongeza Mhe. Rais pamoja na kushiriki
pamoja Ibada ya jumapili ya pili ya Pasaka katika Kanisa la Bikira Maria
Parokia ya Chato mkoani Geita. Wengine katika picha ni Mke wa Rais Mama
Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Raila Bi. Ida Odinga.
Waziri
Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiagana na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika katika uwanja wa
Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita.
Mke
wa Rais Mama Janeth Magufuli akiagana na Mke wa Waziri Mkuu mstaafu wa
Kenya Raila Odinga, Bi Ida Odinga katika katika uwanja wa Shule ya
Sekondari ya Chato mkoani Geita.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na
Bi Ida Odinga, huku Raila Odinga akiagana na Mama Janeth Magufuli
katika katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani Geita.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa
katika picha ya pamoja na Raila Odiga, Ida Odinga pamoja na Mkewe mama
Janeth Magufuli katika uwanja wa Shule ya Sekondari ya Chato mkoani
Geita.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia watoto
aliwakuta kwenye uwanja wa Mazaina Chato mkoani Geita. PICHA NA IKULU
Subscribe to:
Posts (Atom)














