TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 26, 2014

JE, KWA HAYA BADO KUNA SERIKALI INAYOMILIKIWA NA WANANCHI, ILIYOTOKANA NA WANANCHI, KWA AJILI YA KUTIMIZA MATAKWA YA WANANCHI TANZANIA (DEMOCRACY)?.

JE, KWA HAYA BADO KUNA SERIKALI INAYOMILIKIWA NA WANANCHI, ILIYOTOKANA NA WANANCHI, KWA AJILI YA KUTIMIZA MATAKWA YA WANANCHI TANZANIA (DEMOCRACY)?.
(Ni ndefu lakini tumia muda wako kwa kutulia na kusoma)
Ndugu Watanzania wenzangu popote mlipo, nimshukuru mwenyezi Mungu aliyetupa uhai mpaka muda huu tunasherekea sikukuu ya Noeli na namuomba Mungu muweza atupe uhai tuuone mwaka mpya. Kwa wale waliotutoka kipindi chote cha mwaka au siku za mwisho kuelekea kuumaliza mwaka, Mungu aziweke roho zao mahala pema peponi. Amen...!
Nachukua fursa hii adhimu ya kuelekea mwisho wa mwaka kuakisi tulikotoka, kuangalia tulipo na kuchungulia (forecast) tuendako kama taifa la Tanzania na mustakbali wa nchi yetu.
Ukweli ni kuwa niwe mimi, wewe na yule hakuna sababu ya kunyamaza kama kuna jambo tunaweza kusema likaisaidia nchi kwa ajili ya kizazi chetu na kijacho. Najua kuna watu (wepesi wa kukata tamaa na kutotaka kuthubutu, wapendao business as ussual) wataniuliza "wangapi wamepita wakashindwa kuibadilisha nchi hii, wewe ndo uweze?". Ninachoamini ni kuwa wale wote wanaothubu kuongea kwa ajili ya ustawi wa taifa letu kuna waliotangulia walipanda mbegu ya mawazo hayo ndani yao, nao wasipofanikisha leo kuleta mabadiliko watoto wao wajukuu watayaleta kwa sababu ya msingi wa mabadiliko unaojengwa leo. Vinginevyo watoto na wajukuu wasingeyaleta kwa sababu wangeanza na msingi wenyewe.
Baada ya utangulizi huo bila kukuchosha, fuatana nami hatua kwa hatua kwa nilichokuandalia leo.
Kimsingi kukua au kutokua kwa nchi yoyote kiuchumi, kisiasa na kijamii kunategemea dira, sera na usimamizi wa serikali husika iliyopo madarakani.
Dira ni mwongozo wa taifa lolote ambayo kwayo, kila serikali inayoingia madarakani lazima itengeneze sera zitakazosaidia kufikia dira ya taifa. Dira ya taifa hulenga mipango ya muda mrefu kama taifa (kama miaka 50 na zaidi) ambayo kwayo hujipambanua kwa mataifa mengine. Mfano; enzi za Mwalimu, dira ya Tanzania ilikuwa ni kutengeneza jamii yenye ujamaa na usawa inayojitegemea (kiuchumi na kijamii) ndiyo maana katiba yetu ya 1977 ibara ya kwanza 3(1) inasema wazi kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa, isiyofungamana na dini yoyote na inayofuata demokrasia ya vyama vingi. Hili pekee linaipambanua Tanzania vilivyo.
Sera ni mipango ya serikali iliyopo madarakani (yenye dola) ambayo kwayo serikali iliyopo madarakani inatekeleza mipango ya kutekeleza dira ya taifa. Wakati wa Mwalimu alitengeneza sera ya vijij vya ujamaa ili watu wakae pamoja, wakizalisha na kugawana walichozalisha kwa umoja.
Kwa sasa, kila mwenye akili za kawaida anatambua kuwa taifa letu linaenda "bora liende" kama vile trekta lisilo na taa na dreva wake analala usingizi wa pono kwenye usukani. Najua tuna watu wazuri ndani yake ila "trekta” lilipopoteza mwelekeo linawapeleka msobemsobe.
Vyanzo vikuu vya hayo matatizo ni viwili.
1. Nchi kutokuwa na dira ya kufuata.
2. Kukosa viongozi wakuu bora ambao wapo tayari "ku-take risk" kwa lengo la "ku-reshape" nchi.
Wengi hawajui kuwa kama nchi sasa hatuna dira tunayofuata ili kuweka wigo njia kwa kila mwananchi kwa kila anachokifanya kilenge kutufikisha tunakotaka kama taifa. Tunajua sera ya Mwalimu ilikuwa ya ujamaa na kujitegemea na aliibaini hivyo kwenye katiba. Sera hiyo iliposhindwa, mambo yalianza kubadilika pole pole kuuelekea ubepari mpaka sasa ubepari umekomaa labda muda si mrefu tutaingia ubeberu, lakini viongozi wetu "kwa kumuogopa marehemu Mwali Nyerere" wameshindwa kuweka wazi kwenye katiba kuwa nchi yetu inafuata misingi ya kibepari. Athari ya kutoliweka wazi hili ni mvutano unaofanya tusinie mamoja kama taifa kuanzia kwa wananchi mmoja mmoja mpaka viongozi wetu. Hivyo wakati wengine wanapambana kuleta maendeleo kijamaa, wengine wanapambana kuleta maendeleo kibepari hivyo ni mgongano mkubwa. Ukitaka kuamini kuhusu hili, wafuate wabunge tofauti (rondom sampling) 5, waulize "Hivi Tanzania tunafuata sera gani? Ya ujamaa au ubepari? Majibu usinipe kwa sababu nayajua! Matokeo ya nchi kutokuwa na dira ya maendeleo ya nchi, inaanza kuongozwa kwa sera tu (mipango ya aliyshika dola kwa kipindi ambacho atakuwa madarakani). Akaja mtawala fulani akasema haoni umuhimu wa masomo ya sayansi katika kuendeleza taifa hili na badala yale tuwe na taifa la wacheza ngoma pekee, yanafutwa masomo ya sayansi na kubaki na masomo ya kucheza ngoma pekee mashuleni ili kuzalisha wacheza ngoma tu. Lakini nchi ingekuwa na dira, mfano: tunataka Tanzania iwe nchi ya kijamaa inayoendeshwa na uchumi wa viwanda (msingi wa maendeleo duniani kote) tungefanya "elimu hitajika" ndiyo nguzo pekee nchini. Siyo kilimo ni uti w mgongo, siasa ni kilimo wala kilimo kwanza kwa sababu nchi ikiwekeza katika elimu sahihi kwa watu wake ndipo maendeleo katika nyanja zote yanawezekana. Kinachobakia baada tu ya kuwapa elimu, ni kuwatengezea mazingira mazuri kila mwananchi mwenye ujuzi wa anachokijua kukifanya "precisely". Tukajifunze kwa Rwanda ( mhh..! Najua watawala hawaendi kuisikia kauli hii).
Shida kubwa ya pili tulionayo ni UONGOZI.
Taifa likifika lilipofikia hakuna tena kitakacholibadilisha mpaka mfumo wa viongozi wote waliopo watoke, waingie wengine ambao watakuwa tayari "ku-take highest risk ku-reshape" nchi. Si rahisi hata kidogo.
Umuhimu wa "ku-reshape" unatokana na;
1. Kukithiri kwa rushwa
Tumeshuhudi skendo za rushwa zinazovunja rekodi tangu nchi hii kupata. Shida ni kuwa rushwa hiyo inapita mpaka kwa wanaotakiwa kukemea rushwa, matokeo yake serikali nzima inamezwa mifukoni mwa mafisadi.
2. Kuzeeka kwa mawazo ya kiongozi.
Miaka 50 ni mingi sana kwa chaki kimoja kutawala nchi. Inafika wakati hakuwi mawazo mapya ya kuiongoza nchi ilihal ili uongozi uwe bora mawazo mapya na ubunifu vinahitajika. Kwa msingi huo, nawahakikishia Watanzani kuwa tungeanza kuonana maendeleo Tanzania kama upinzani ungechukua nchi 2015 kisha 2020 tena ichukue Ccm na baadaye kila anayeharibu angejua hachaguliwi tena. Matokeo yake ni maendeleo kwa wananchi.
3. Nepotism/ undugulism
Hili ni tatizo kubwa. Nenda kila sehemu, idara za serikali, vyombo vya dola kwenye vyama vya siasa nk utakuta zile krimu zote ni za vigogo wa serikali. Sisemi wao hawana uwezo na haki ya kufanya huko, laaah! Bali fuatilia CV zao na fanya ulinganifu na kipindi cha Nyerere. Inamaana nyerere watoto wake walikuwa mbumbumbu sana ukilinganisha leo ambapo mfano; baba mNEC, mama mNEC, mtoto mNEC, mkwe mNEC, shemeji mNEC, wakurugenzi wote BOT wenyewe, TISS wenyewe, nk.
4. Kushindwa kusimamia mipango yao na kila mtu kuwa na ya kwake serikalini.
Kuna suala la pembejeo na ununuzi wa mahindi napenda kulichukulia kama mfano wangu halisia wilayani kwetu Mbozi.
Kwanza serikali ilitangaza kununua mahindi wilayani Mbozi na kwingineko kwa kupima na kuyahifadhi ghalani huku ikizuia wafanyabiashara kupeleka mahindi nje ya nchi. Tangu serikali imepima mahindi hayo, wakulima/wafanyabiashara hawajalipwa pesa zao hadi leo. Kwa kweli watu sasa wanaamini shughuli ya kilimo ni biashara kichaa kwa sababu watu wapata mavuno na kupata neema ya soko zuri nje, mipaka huzuiwa kuwa serkali itayanunua na malipo yenyewe ndo huwa hivi. Mbons hatujasikia wafanyabiashara wa vinyago, nguo, cement nk wakipata soko zuri wakizuiliwa mipaka? Tunahisi kamfumo haka kamelenga kuwafanya wakulima watumwa wa kudumu kwa sababu hawana haki kabisa ya kupata bei nzuri ya mazao yao. Badala yake, mh. Godfrey Zambi aliwawezesha watu wake wa tatu wa karibu kisiasa ndiyo wakalipwa.
Zaidi ya hapo, naibu waziri wa kilimo na ushirika akijibu swali la Mh David Silinde mbunge wa Momba alimwambia mbolea ipo inakuja, lakini alipokuja mkurugenzi wa pembejeo alisema hazitakuwepo. Kwa sababu hiyo, tutegemee balaa la njaa mwakani.
For all those, lazima tuunganishe nguvu zetu kulinusuru taifa letu kwa kuiambia serikali ya CCM 2015 kapumzike uje tena kuomba 2020.
Nawatakia msimu mzuri wa sikukuu. Mungu awabariki.

PATCHO MWAMBA AKANUSHA KUFUMANIWA, KUPIGWA

Patcho Mwamba akiwa katika ofisi za Global Publishers Ltd leo.
Picha ya Patcho iliyozua utata mitandaoni.
MWIGIZAJI na mwanamuziki wa Bendi ya FM Academia, Patcho Mwamba hivi punde ameibuka katika ofisi za mtandao huu na kukanusha vikali taarifa zilizozagaa katika mitandao ya kijamii kuwa amefumaniwa akiwa na mke wa mtu na kupokea kipigo.
Akiongea na Full Utamu, Patcho amesema picha iiliyozagaa mitandaoni aliipost mwenyewe juzi baada ya kupata aleji ya macho kwa lengo la kutafuta uumbuzi wa kupata dawa kwa watu watakaokuwa na dawa za hilo tatizo na kwamba baada ya kufanya hivyo ametokea Mtu mmoja akumtaja jina ambaye ni Mdada aliyeiweka kwenye mitandao baada ya kukurupuka bila kusoma maelezo aliyokuwa ameyasema katika kuomba msaada huo kwa watu wanaofahamu dawa za aleji ya namna hiyo.
Mdada huyo ambaye kwa namna ingine patcho anasema imemshangaza sana kutokana na kuweka habari ambazo zilikuwa hazina ukweli wowote. ambapo baadaye ilisambaa mitandaoni ikidaiwa kuwa kapigwa baada ya fumanizi.
"Unajua nina aleji na pombe pamoja na vumbi, nikitumia tu pombe lazima macho yangu yavimbe
juzi nilikunywa Windhoek mbili na usiku hali yangu ikabadilika na macho kuvimba, baada ya tukio hilo niliamua kujipiga picha na kuipost katika mtandao wa Instagram na hapo ndipo balaa likazuka" Alisema Patcho akiwa katika ofisi za mtandao huu zilizopo Mwenge-Bamaga, Dar.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWAAGA WATOTO WENYE MATATIZO YA MOYO KWENDA KUTIBIWA INDIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi mtoto, Nabil Hahya (4) kutoka Jijini Dar es Salaam, mmoja kati ya watoto 55 wa awamu ya kwanza kati ya 104 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo wanaokwenda kutibiwa nchini India, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto hao iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mama wa motto huyo, Amina Yahya.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ya kuwaaga jumla ya watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, waliofadhiliwa na Lions Club ya jijini, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ya kuwaaga jumla ya watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, waliofadhiliwa na Lions Club ya jijini, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Rais wa Lions (Host) Club ya Dar es Salaam, Mathew Levi, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na mmoja kati ya watoto wanaokwenda kutibiwa nchini India, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto hao wenye matatizo ya ugonjwa ya moyo iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akivishwa Beji ya miaka 50 ya Lions Club na Makamu wa Gavana wa Club hiyo, kwa nchi za Tanzania na Uganda, Hyderali Gangji, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo wanaokwenda nchini India kutibiwa. Hafla hiyo ilifanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi mtoto, Nabil Hahya (4) kutoka Jijini Dar es Salaam, mmoja kati ya watoto 55 wa awamu ya kwanza kati ya 104 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo wanaokwenda kutibiwa nchini India, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto hao iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mama wa motto huyo, Amina Yahya.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya wadau wa Lions Club, baada ya hafla fupi ya kuwaaga watoto hao.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi mtoto, Hyria Ally (miezi 9) Kutoka Zanzibar, mmoja kati ya watoto 55 wa awamu ya kwanza kati ya 104 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo wanaokwenda kutibiwa nchini India, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto hao iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mama wa motto huyo, Zulekha Said.
Badhi ya watoto hao wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo, wakiwa na mama zao wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya wadau waliohudhuria hafla hiyo. Picha na OMR
 

MLIPUAJI WA MABOMU SONGEA AJIKUTA AKILIPUKIWA YEYE NA KUPOTEZA MAISHA


Kamanda wa polisi Mkoa wa Ruvuma Mihayo Msikhela akitoa
maelezo kwa DCP Diwani Athumani ambaye aliwasili mkoani humo jana
kwaajiri ya bomu la kutengenezwa kienyeji ambalo askari wa doria
walinusurika kurushiwa na kumlipukia mlipuaji wa bomu hilo ambaye
alifariki papo hapo.

Askari WP Mariam mwenye namba 8616 akiwa amelazwa wodi ya
majeruhi hospitali ya Mkoa baada ya kujeruhiwa mkono wa kushoto kwenye bega baada ya vipande vya bomu kumfikia akiwa na askari wenzake kwenye doria siku ya sikukuu ya krisimas.
  Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akiuangalia mwili wa
mtuhumiwa wa ulipuaji wa bomu ambaye alitaka kuwarushua askari wa
doria wakati wa sikukuu ya krismas kwenye chumba cha kuhifadhia maiti. (PICHA NA AMON MTEGA ,SONGEA)
-----------------------------------------

 NA AMON MTEGA,SONGEA
 
JESHI la Poilisi mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na timu ya makachelo
toka makao makuu ya jeshi hilo wanawasakaka watu watatu ambao wanasadikiwa kujihusisha na ulipuaji wa mabomu huku mwenzao mmoja
akiwa amefia katika eneo la tukio baada ya kutaka kufanya jaribio la
kuwatupia  bomu askari waliyokuwepo doria katika sikukuu ya Krisimas ambalo lilimshinda na kumlipukia mwenyewe na kusababishakupoteza maisha papo hapo huku utumbo ukiwa umemwagika nje na  mkonowake wa  kushoto ukiwa umekatika kabisa na vipande vyake hajijulikanivilipo. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ukumbi wa mikutano wa
jeshi la polisi Mkoa wa Ruvuma Naibu Kamishna wa jeshi la Polisi,
kaimu mkurugenzi wa upelelezi wa Makosa ya Jina nchini (DCP)  Diwani
Athumani alisema kuwa tukio hilo limetokea jana majira ya saa 1.30
usiku huko katika mtaa wa Kotazi uliopo kata ya Majengo manispaa ya
Songea ,timu ya askari wakiwa doria kulitokea mlipuko wa kitu
kinachozaniwa kuwa ni bomu ambalo limetengenezwa kienyeji  nakusababisha kuwajeruhi  askari wawili .
DCP Athumani aliwataja askari waliojeruhiwa kuwa ni PC Mselem mwenye
namba G 7903 ambaye alijeruhiwa mkono wake wa kushoto na alitibiwa na kuruhusiwa na  mwingine PC Mariam mwenye namba WP. 8616 ambaye
amejeruhiwa kwenye bega la mkono wa kushoto na amelazwa katika hospitali ya Mkoa Songea(HOMSO)akiendelea kupata matibabu.
 Alisema kuwa timu ya makachelo toka makao makuu wakishirikiana na
tatu kwa mwaka huu. 
 
DCP Athumani alieleza zaidi kuwa wahalifu hao watakamatwa kirahisi
kutokana na tukio walilolifanya baada ya mwenzao kulipukiwa na bomu
hilo na kusababisha kifo chake walijaribu kutorosha mwili wa mwenzao
ili kupoteza ushahidi lakini ilishindikana baada ya askari polisi
doria wengine kuwahi eneo la tukio na wahalifu hao waliacha mwili wa
mwenzao na kutokomea kusikojulikana.
“Wahalifu hao waliuvuta mwili wa mwenzao kutoka katika eneo la tukio
kwa umbali wa mita zisizopungua 80 na 90 kwa lengo la kutaka kupotezausahidi  lakini waliwahiwa na askari wengine wa doria na kuuacha mwilina kutokomea kusikojulikana” alisema DCP Athumani.
Hata hivyo amewaomba wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini,wanasiasa,wazee, makundi mbalimbali  ya kijamii pamoja na
waandishi wa habari kuwa kitu kimoja katika kuwafichuwa waharifu hao
ili matukio hayo yasiweze kujirudia tena hususani Mkoa wa Ruvuma.
 Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu aliyetembelea
eneo la tukio na kuzungumza na waandishi wa habari kwa masikitiko
makubwa alisema kuwa waharifu hao wanaishi kwenye jamii inayotuzunguka hivyo ni vyema kila mmoja akaliona jambo hili kwa umuhimu wake wapekee kulipa uzito na kuwafichuwa wahalifu ili Mkoa uendelee kuwa naamani kwani linaleta taharuki kwa jamii jambo ambalo linarudisha nyumashughuli za maendeleo.
 Naye Mganga Mkuu mfawidhi Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma Dkt. Benedkto
Ngaiza amethibitisha kupokea mwili mmoja  wa mtu ambaye amekufa ukiwautumbo umetoka nje na  majeruhi wawili ambao ni askari na kwambaaskari mmoja alitibiwa jana na kuruhusiwa huku mmoja akiwa amelazwawodi ya majeruhi namba mbili  akiendelea kupatiwa matibabu na haliyake inaendelea vizuri.

HOTUBA YA RAIS KIKWETE NA WAZEE WA DAR ES SALAAM - 12/22/2014

PESA ZA ESCROW SI ZA UMMA, ASEMA RAISI KIKWETE,
-ANADAI SERIKALI HAIKUPATA HASARA YOYOTE KUTOKANA NA SAKATA HILI,
-ATENGUA UTEUZI WA PROF TIBAIJUKA KWA KUKUBALI KUWEKEWA PESA KWENYE AKAUTI YAKE BINAFSI.
-AMUWEKA KIPORO PROF MUHONGO,WAKATI UCHUNGUZI BADO UNAENDELEA,AKIPATA MAJIBU ATATOA UAMUZI.
-APANGUA BAADHI YA MAPENDEKEZO YA BUNGE.
-ADAI CCM WALIKUWA IMARA KWENYE SAKATA LA ESCROW
-AWATAKA CCM NAO WAKAWAAMBIE WANANCHI KUHUSU ESCROW
-AKIRI KUWA UJAMAA USHAKUFA KITAMBO
,huu ndi mchanganuo wa aliyoyasema rais  kikwete kuhusu ESCROW.
i) AMEKIRI KUWA TANESCO ILIKUWA INAIBIWA NA IPTL
ii) TRH 5.7.2006 NDIYO ACCOUNT YA TEGETA ILIFUNGULIWA NA KUFIKIA TAMATI TRH 5.9.2013 MAHAKAMA ILIAMURU SHUGHULI ZOTE ZA TANESCO ZIKABIDHIWE KWA IPTL HUKU KUKIWA HAKUNA KESI ILIYOFUNGULIWA ACHILIA MBALI ILE YA MWANZONI YA MALALAMIKO YA TANESCO KUWA WANAIBIWA KUPITIA CAPACITY CHARGE
iii). PESA ZILIKAAKWENYE ACCOUNT YA ESCROW KWA MIAKA 7.
iv) .Wakati CAG anakagua kulikuwa na shilingi 202 Bilioni nukta tisa.
v) Kama Tanesco wangeli tozo za uwekezaji,akaunti hii ingekuwa na shilingi Bilini 306.7,kutokana na Tanesco kutolipa ilibaki na madeniya shilingi Dola Bilioni 33.6 na IPTL.
vi) .Account ya Ecsrow haikuwa na Bilioni 306,bali zilikuwemo Bil 202 pekee ambazo IPTL ilikuwa inaidai Tanesco.
vii).Amesema kuwa kutoka na hali ya mgogoro ulivyokuwa pesa zilizokuwa ndani ya akaunti ya ESCROW SI ZA UMMA BALI NI ZA IPTL kwani ndiyo mlipwaji kutokana na madeni ambayo IPTL inaidai TANESCO kutokana na tozo za uwekezaji.
vii).Kuhusu majibu ya CAG,kuhusu pesa ni za nani?raisi amesema kama Tanesco wangeshinda mgogoro wao na IPTL basi pesa hizo zingekuwa za UMMA kama ilivyokuwa kwenye kesi yao ya mwaka 2001,ila kwa sababu Tanesco walishindwa,pesa hizi ni za IPTL na si UMMA(PUBLIC)
viii),KUHUSU KUWEMO KWA KODI ZA SERIKALI NDANI YA ESCROW ACCOUNT KIASI CHA BILIONI 21 NA MILIONI 700,AMESEMA PAP WALIPELEKEWA DENI LA KODI YA SERIKALI,AMESEMA CAG ALIKAGUA NA KUSEMA PESA ZILIZOKUWEMO KWENYE AKAUNTI YA ESCROW HAZIKUWA NA SIFA ZA KUITWA PESA ZA UMMA.
ix).Trh 15.9.2013 mahakama kuu ya Tanzania ulifanya uamuzi wa maombi ya kampuni ya VIP kuomba kusimamisha mchakato wa kuuza hiza za IPTL wakilumbana juu ya hisa,uamuzi wa mahakama ulikuwa PAP wapewe hisa 30 NA WAKANUNUA HISA 70 na waliandikisha hisa 70 Brela,mahakama ikaamua hisa zikabidhiwe PAP ambao ndiyo mmiliki halali wa IPTL.,Uamuzi huu wa mahakama ulimaanisha kuwa PAP wanatakiwa kumiliki mpaka pesa za ESCROW kwa PAP,umauzi ambao ulizuia malumbano serikalini juu ya akauniti ifungwe ama isifunwe,pesa zitoke ama zisitoke.
x).Wizara ya nishati na madini waliamu kuomba ushauri kwa mwanasheria mkuu juu ya pesa,AG alielekeza kuwa pesa zilipwe kama mahakama ilivyotaka,benki kuu waliuliza maswali haya,na AG akaelekeza walipe kwa PAP na hakuna kodi,ushsuri wa AG uliitoa nafasi ya akaunti kufungwa na kugawanywa rasmi na baadae kuingia barabarani.
xi).Maamuzi yote yaliyofanyika yalifanyika kwa maelekezo ya mwanasheria mkuu,umuzi huu wa mwansheria kuu umeibua mjadala mkuu kuwa kuna rushwa kubwa,watu wamemegewa mshiko,kila mtu kaongea.
xii).Amekanusha kuwa kufungwa kwa akaunti ya ESCROW hakukuwa na msukumo kutoka kwa maafisa wa serikali,amesema serikali ilifanya juhudi kubwa kwenye sakata hili.
xii).Amesema mwanasheria mkuu alimwambia hakukuwa na makosa yeyote kwenye maamuzi ya mahakama,na pia hakuna hasara ambayo serikali imepata kutokana na sakata hili la ECSROW kwa sababu pesa hizo zilikuwa ni deni ambalo Tanesco ilikuwa inadaiwa na IPTL.
xiii).Kuhusu kuwa PAP walinunua hisa za PIPAL LINK huku kikuwa na amri ya mahakama ya kutouza hisa,amesema bado vyombo vya mamlaka vinachunguza
xiv).Kuhusu uuzwaji wa hisa,amesema napo kunahitaji uchunguzi zaidi hasa bei ya hizi hisa.
xv).Amesema Rugemalira alilipa kodi aliyokuwa anadaiwa kiasi cha shilingi Bilioni 38,RUGEMALIRA hana makosa kwenye hili,Alilipa kodi zote.
xvi).KUHUSU MAPENDEKEZO CAG ameelekeza taaifa zile zipelekwe PCCB.
xvii).Kuhusu waliomegemewa pesa na RUGEMALIRA,amesema Takukuru na tume ya maadili ya watumishi wa umma wanachunguza na kushuhulika na watumishi wa umma wote waliopewa pesa,amesema tume ya maadili ya umma itawahoji wote waliopewa pesa.
KUHUSU MAZIMIO YA BUNGE
i.Amesema serikali imeyapokea maazimio na itayafanyia kazi
ii.Kuhusu kutaifisha mitambo ya IPTL,amesema si sawa kutaifisha sababu kutafukuza wawekezaji
iii.Kuhusu uwazi wa mikataba,amesema serikali itafanya mapitio ya mikataba,amesema kuna haja ya serikali na bunge kukaa pamoja na kuzungumza,kwa sababu kuna makampuni yanataka usiri wa mikataba(company secret)
iv)Kuhusu PCCB,na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vichukue hatua,amesema tayari utekelezaji ueanza.
v).Kuhusu kuwavua vyeo wenyevitio wa kamati amesema bunge ndilo litekeleza.
vi).Kuhusu kuundwa kwa tume ya kijaji kuwachunguza majaji waliohusika na sakata la ESCROW,amesema itabidi kuzingatia utaratibu wa kikatiba na sheria,amese suala hili linatakiwa kuanzia kwenye mahakama,halianzii kwa raisi wala bungeni,Amemuachia Jaji mkuu alishughulikie na kumpelekea mapendekezo raisi.
vii).Kuhusu mamlaka husika za kifedha na kiuchunguzi ziitaje Stanbic bank na benk zilizohusika zitangazwe kuwa taasisi zinazotakatisha fedha amesema uchunguzwe na mamlaka husika.
viii).Kuhusu serikali iandae na kuwasilisha marekebisho ya sheria ya uundwaji wa rushwa kubwa,amesema hilo ni wazo zuri,na serikaliimekuwa inaifanyia marekebisho taasisi ya kuzuia rushwa tangia mwaka 2008
ix).Kuhusu kuwavua nafasi zao watumishi wa umma wakiwemo mawaziri waliotajwa,raisi Kikwete amesema,Bodi ya Tanesco imeshamaliza muda wake,hili lishajifuta,kuhusu katibu mkuu Maswi amesema mamlaka zinazohusika zianze ushunguzi wa kuchunguza tuhuma zake,mwanasheria mkuu ameshajiuzulu,kuhusu mawaziri(TIBAIJUKA) amesema wamezungumza nae na wamekubaliana aachie ngazi,kuhusu Prof Muhongo amemuweka kiporo..

AJALI YAUWA WAWILI NZEGA TABORA

 Ajali iliyohusisha magari mawili imesababisha waliokuwa kwenye gari dogo kupoteza maisha maeneo ya Nzega, inaasemekana chanzo cha ajali ni speed ya gari dogo na mvua kubwa iliyokuwa inanyesha eneo hilo.

Askari watatu wa AU wauawa Somalia

Askari wa Somalia wakiangalia mabaki ya magari katika moja ya mashambulio ya kigaidi mjini Mogadishu, Somalia.
Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Afrika nchini Somalia limesema askari wake watatu na kandarasi raia wameuawa katika shambulio lililofanyika katika makao yake makuu mjini Mogadishu.
Taarifa ya Umoja wa Afrika imesema wapiganaji wa al-Shabab waliingia katika kambi wakivalia sare kama askari wa jeshi la serikali ya Somalia.
Taarifa hiyo imesema washambuliaji watano waliuawa na wengine kadha kukamatwa. Pamoja na kutoa eneo hilo kuwa makao makuu ya majeshi ya kulinda amani ya AU nchini Somalia, eneo hilo lililoimarishwa pia makao ya balozi za Uingereza na Italia.

Indonesia wakumbuka Tsunami

Wanawake eneo la Aceh wakifanya sala ya kukumbuka maafa makubwa yaliyosababishwa na tsunami miaka kumi iliyopita nchini Indonesia
Wananchi wa Indonesia wameanza kuadhimisha mwaka wa kumi tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi lililosababisha mawimbi makubwa katika bahari ya Hindi, tsunami na kusababisha vifo vya watu zaidi ya watu laki mbili na elfu ishirini katika eneo kubwa.
Umati wa watu umekusanyika karibu na jengo la makumbusho la tsunami katika eneo la Banda Aceh katika kisiwa cha Sumatra.
Mji huo ulisambaratishwa kabisa na tetemeko kubwa la ardhi na mawimbi ya tsunami. Makamu wa Rais wa Indonesia(Jusuf Kalla) anaongoza maadhimisho hayo na atawashukuru wafanyakazi wa kujitolea katika eneo hilo na duniani kote kwa kulisaidia eneo la Aceh kurejea katika hali ya kawaida baada ya mkasa huo.

Boti yazama na watu 36 DRC

Boti yazama DRC pamoja na watu 36 
 
Ripoti kutoka kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo zinasema kuwa mashua moja iliyokuwa imebeba bidhaa na abiria imezama na karibu watu 36.
Maafisa wanasema kuwa zaidi ya watu 100 wamenusurika.
Inaripotiwa kuwa ajali hiyo ilitokea siku ya Jumatatu umbali wa kilomita 30 kutoka mji wa kisangani na kusababisa maandamano yaliyofanywa na vijana wenye hasira kwenye mji wa Isangi ambapo mashua hiyo ilikuwa ikielekea
Nyumba kadha za serikali zinaripotiwa kuchomwa.

Sudan yawatimua maafisa wa UN

Mshirikishi mkuu wa utoaji msaada Ali Al-Zatariv
Umoja wa mataifa unasema kuwa Sudan imewafukuza maafisa wake wawili wakuu kutoka nchini humo.
Katibu mkuu wa umoja wa mataifa, Ban Ki-moon, amelishutumu taifa hilo kwa kumfurusha mshirikishi mkuu wa utoaji msaada Ali Al-Zatari, na mkurugenzi mkuu wa mpango wa maendeleo wa Umoja wa mataifa Nchini humo Yvonne Helle.
Haijafahamika ni kwa nini wawili hao wamefurushwa.
Uhusiano kati ya Umoja wa mataifa na serikali ya Sudan umekuwa m'baya tangu walinda amani wa umoja wa Afrika kuchunguza ripoti ya ubakaji ulioendeshwa na wanajeshi wa taifa hilo katika eneo la Darfur mwezi uliopita.

NHC yakabiliana na tatizo la moyo nchini kwa kusaidia matibabu ya watoto 53 nchini India

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ya kuwaaga jumla ya watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, waliofadhiliwa na Lions Club ya jijini, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.

=======================================================
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limechangia kiasi cha takribani shilingi milioni 29 katika kuokoa maisha ya watoto wenye maradhi mbalimbali ya moyo nchini ambao wanaondoka leo kwenda India kwa upasuaji. Watoto hao 53 wameagwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal.
  Rais wa Lions (Host) Club ya Dar es Salaam, Mathew Levi, akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo. 
Akizungumza na wazazi wa watoto hao waliofika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Dk Bilal alililipongeza Shirika la Nyumba la Taifa pamoja na wadau mbalimbali waliojitolea kuhakikisha wanakabiliana na tatizo la moyo ambalo linaongezeka kwa kasi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akivishwa Beji ya miaka 50 ya Lions Club na Makamu wa Gavana wa Club hiyo, kwa nchi za Tanzania na Uganda, Hyderali Gangji, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo wanaokwenda nchini India kutibiwa. Hafla hiyo ilifanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
“Kama Serikali hatuwezi kukabiliana na tatizo hili peke yetu hivyo nawapongeza wadau mbalimbali binafsi na taasisi zilizojitolea kwaaajili ya kuokoa maisha ya Watanzania wenzao, ni jambo linalotia faraja na ni desturi ya Watanzania kusaidiana,”alisema.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na
Makamu wa Gavana wa Club hiyo, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.
Alisema Serikali inaendelea na jitihada mbalimbali za kukabiliana na tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kujenga taasisi za kukabiliana na tatizo hilo nchini ili kusudi hudma ziweze kuwafikia Watandania wengi zaidi.
Naye Mratibu wa magonjwa ya moyo katika Klabu ya Lions ya Dar es Salaam, Dk. Rajni Kanabar, alisema wagonjwa hao watatibiwa katika hospitali mbalimbali nchini India.
Alisema safari ya wagonjwa hao imeratibiwa kwa pamoja na Klabu ya Lions ya Dar-es-Salaam (Host), Regency Medical Centre na Wizara ya Afya ya Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam ya kuwaaga jumla ya watoto 55 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo kati ya 104, waliofadhiliwa na Lions Club ya jijini, kwa ajili ya kwenda kutibiwa nchini India. Watoto hao 55 wa awamu ya kwanza wanaanza kuondoka nchini leo.
Alisema katika kundi hilo, watakuwamo wauguzi wawili na madaktari wawili na wanatarajiwa kurudi nyumbani baada ya wiki nne zijazo.
Dk. Kanabar alisema wagonjwa 15 watatibiwa katika hospitali ya Jaypee Health Care Heart Institute iliyoko mji wa New Delhi na wengine 27 watatibiwa katika taasisi kubwa ya Fortis Escorts Heart iliyoko New Delhi, India.
  Badhi ya watoto hao wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo, wakiwa na mama zao wakati wa hafla hiyo.
“Watafanyiwa upasuaji ambao utagharimu Dola 2,500  za Marekani kwa kila mgonjwa na watapewa Dola  500 kwa ajili ya kujikimu wakiwa huko,” alisema Dk. Kanabar ambaye pia ni Mwenyekiti wa Hospitali ya Regency Medical Centre.
 Badhi ya watoto hao wenye matatizo ya ugonjwa wa moyo, wakiwa na mama zao wakati wa hafla hiyo.
Alisema hospitali ya  Escorts ni miongoni mwa hospitali kubwa duniani kwa matibabu ya moyo na imekuwa ikiwafanyia upasuaji wagonjwa wa moyo kutoka Tanzania kwa punguzo kubwa la gharama za matibabu hayo.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi zawadi mtoto, Nabil Hahya (4) kutoka Jijini Dar es Salaam, mmoja kati ya watoto 55 wa awamu ya kwanza kati ya 104 wenye matatizo ya ugonjwa wa Moyo wanaokwenda kutibiwa nchini India, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga watoto hao iliyofanyika leo Desemba 26, 2014 kwenye Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mama wa motto huyo, Amina Yahya.
Aliishukuru Wizara ya Afya ya Zanzibar kwa kuchangia nauli za ndege kwa wagonjwa 33 na kutoa Dola 500 kwa kila mgonjwa na Ubalozi wa India ambao viza za bure kwa wagonjwa wote kupitia balozi wa nchi hiyo hapa nchini, Debnath Shaw.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiinua glasi juu kumtakia heri Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa Lions Club, baada ya hafla fupi ya kuwaaga watoto hao. 
Dk. Kanabar aliwataja wengine waliochangia kuwa ni Bank M  iliyochangia Dola 10,000 gharama za upasuaji wa wagonjwa wanne, Shirika la Nyumba la Taifa limechangia shilingi milioni 29
na Klabu ya Lions Dar es Salaam (Host) Dola 16,500,  Pradeep Kumar wa Bengaluru, India Dola 16,400,  Regency Medical Centre Dola 12,500, wanafunzi wa British Columbia University Vancouver, Canada na Jumuiya ya  Theosophical ya Dar es Salaam Dola 10,000.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa Lions Club, baada ya hafla fupi ya kuwaaga watoto hao. 
Wengine ni Riyaz Hassan Ali wa Karim Foundation Marekani Dola 9,000, Familia ya Mohamed Gulam Dewji Dola 5,000, Africarriers Dola 5,000, Lakhan Pal wa Dar es Salaam Dola 2,500, Nashrin Sarkai wa Marekani Dola 5,000, Hazi Abbas wa Dar es Salaam Dola 2,500, Lion Siraz Jessa wa Dar es Salaam Dola 2,500,  Lion Mohamed Laljee, Lion Yusuf Dalal, Lion Karim Meetha, Lion Nazmu Dola 3,500, Guru Sikh Sabha wa Dar es Salaam Dola 5,000, Harun Zacharia, Salim Turkey Dola 5,000, Dk.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa Lions Club, baada ya hafla fupi ya kuwaaga watoto hao.
Kiran Nad Pallavi Patel wa Global Foundation Marekani Dola 10,000, Habib African Bank ya Dar es Salaam Dola 3,000 na Prem Kapoor & Family ya Mwanza Dola 3,000 na Gavana wa District 411B.