TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, March 18, 2015

KITABU KIPYA CHA MHAMASISHAJI MAHIRI ZAIDI AFRIKA, ERIC SHIGONGO KUINGIA MTAANI MEI 1, 2015

Rais Kikwete afungua Kituo Cha Taifa Cha Kumbukumbu Dodoma

001
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Kituo cha Taifa Kumbukumbu huko kisasa mjini Dodoma leo.Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, watatu kushoto ni Mwenyekiti wa BungeMh. Zungu na kulia ni Waziri wan chi Ofisi ya Rais Utawala BoraMh.George Mkuchika.
002
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa katika jiwe la msingi kufungua rasmi Kituo cha Taifa Cha Kumbukumbu kilichopo Kisasa mjini Dodoma leo.
003
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia jalada la mwaka 1940 ambapo alisoma utendaji kazi wa Babu yake Chifu  wa Kabila la Wakwere Mrisho Kikwete wakati huo.Jalada hilo ni moja ya majalada ya zamani yaliyohifadhiwa kutumia teknolojia ya kisasa katika Kituo Cha Taifa Cha Kumbukumbu kilichopo Kisasa mjini Dodoma.Katika hotuba yake wakati wa ufunguzi wa kituo hicho Rais Kikwete ametoa agizo la kuanzishwa maktaba za Viongozi wa kitaifa hususan marais wastaafu ili kuhifadhi vyema historia ya nchi.
(picha na Freddy Maro)

MATUKIO KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO.

6
7
1
3
4
5

ZANZIBAR YAADHIMISHA SIKU YA KISWAHILI DUNIANI


imagesNa: Ali Issa  Maelezo- Zanzibar

Hakuna sababu itayoifanya Zanzibar kushindwa kuitumia lugha ya Kiswahili katika kufundishia wanafunzi Skuli kwani Zanzibar inahazina kubwa ya watalamu na  ndio chimbuko la   Kiswahili katika Nchi za Afrika na Dunian kwa ujmlai.

Hayo yamesemwa leo huko Eacrotanal Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Mohamed Seif Khatib  wakati wa ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Kiswahili Duniani yalio fanyika hapo.

Amesema inawezekana kabisa na frusa hiyo ifanyiwekazi kwa kukaa pamoja Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar pamoja  na Wizara ya Habari UtAMADUNI Utalii na Michezo Zanzibar kuzipitia sera zilizo tangulia kulipatia mamuzi suala hilo. Amesema kunanchi nyingi tu duniani ambazo zinasomeshwa kwakutumia lugha zao na haijawa tatizo katika nchihizo.
“Kuna nchi kama China,Uholazi na nyengnezo wanatumia furusa ya kusomeshea wanafunzi kupitia lugha zao,”

Nae Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khadija Bakar na Naibu Katibu Mkuu Wiara ya Habari, Utamaduni,Utalii na Michezo Zanzibar Issa Mlingoti alisema watakaa pamoja na wizara zao kulijadili suala hilo kwani hadi sasa kuna sera mbilizo pingana.
Wamesema wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wao wamelikubali hilo kuwa wanafunzi wafundishwe kupitia lugha ya Kiswahili la kini Wizara ya Elimu wao wanalipinga,hivyo watakaa pamoja na kusawazisha ili waendesambamba na wezao wa Tanzania Bara.

Nae Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) pia mjumbe wa baraza la kiswahili Zanzibar Mmanga M. Mjawiri amesema kuna umuhimu mkubwa wanafunzi Skuli wafundishwe kupitia lugha yao ya kishwahili kwani kiengereza Tanzania bado kikwazo. Hakuna masiliano mazuri kati ya walimu na wanafunzi wakati wa kufundisha hivyo Kiswahili ndio suluhisho la wanafunzi kumuelewa mwalimu.

KUMBUKUMBU ZA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE.


VICHEKESHO NA WASANII WA COMEDY KIVUTIO CHA MITANDAO YA JAMII



HII NDIYO NYUMBA YA SANAA KATIKA WASANII


ANGALIA MAAJABU YA YA ULIMWENGU HAPA:



CHUO CHA TAKWIMU MASHARIKI MWA AFRIKA KUTILIANA SAINI YA MKATABA WA MAKUBALIANO YA MAFUNZO YA WATALAAM WA TAKWIMU NA CHUO CHA TAKWIMU CHA INDIA.

Na: Veronica Kazimoto,  Dar es Salaam,
17 Machi, 2015.
Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) kimekamilisha maadalizi ya kutiliana saini ya mkataba wa makubaliano ya mafunzo ya Watalaam wa Takwimu na Chuo cha Takwimu cha nchini India.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo cha EASTC Prof. Innocent Ngalinda amesema mkataba huo utasainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
“Maandalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu na Chuo cha Takwimu cha nchini India yamekamilika kwa kiasi kikubwa na ndio maana hapa mbele yenu mnamuona Naibu Balozi wa Ubalozi wa India hapa nchini amefika kwa ajili ya kujirizisha”, amesema Prof. Ngalinda.
Prof. Ngalinda amesema kuwa mkataba huo una manufaa makubwa kwa kuwa utasaidia kuongezeka kwa wataalam wengi katika tasnia ya takwimu hapa nchini.
Pamoja na ongezeko la watalaam wa takwimu hasa wakufunzi, kutakuwa na ukarabati wa miundombinu katika chuo hicho ambapo mabweni ya wanafunzi pamoja na ofisi za chuo hicho zitakarabatiwa.
Prof. Innocent Ngalinda amefafanua kuwa katika mkataba huo, kutakuwa na mpango wa kubadilishana wanafunzi katika vyuo hivyo viwili ili kupanua uelewa wa wanafunzi ikiwa ni pamoja na kuongeza ujuzi zaidi katika masuala ya kitakwimu.

Kwa upande wake Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal amefurahishwa na maandalizi yaliyofanyika na kusema kuwa nchi yake iko tayari kutiliana saini ya mkataba wa makubaliano ya mafunzo ya Watalaam wa Takwimu kutoka chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na chuo cha Takwimu cha nchini India.
“Nimefurahishwa na maandalizi yaliyofanyika katika chuo hiki na sasa tunamsubiri Waziri wa mambo ya Nje wa nchini India kwa ajili ya kutiliana saini ya mkataba huu ifikapo tarehe 28 Machi, 2015,” amesema Naibu Balozi Humpal.
Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika kilichopo Changanyikeni jijini Dar es Salaam na chuo cha Takwimu cha India vimekuwa vikishirikiana tangu mwaka 2012 lakini ushirikiano huo haukuwa rasmi hivyo vyuo hivyo vimeamua kusaini mkataba wa makubaliano kwa ajili kufanya ushirikiano huo kuwa rasmi.
==================================================================
Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) Prof. Innocent Ngalinda akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu kukamilika kwa maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa chuo hicho na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal akiwaelezea Waandishi wa Habari jinsi alivyofurahishwa na maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal akimsalimia mwanafunzi wa Udhamili katika Takwimu Rasmi Happiness Katuma wakati akikagua baadhi ya vitu  mbalimbali kama maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal akipitishwa katika maeneo mbalimbali ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika kama maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa chuo hicho na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal akiangalia vitabu mbalimbali vilivyopo katika maktaba ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika wakati wa kuangalia maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal akisoma moja ya vitabu kilivyopo katika maktaba ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika wakati wa kuangalia maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015.
Mkuu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC) Prof. Innocent Ngalinda akimwelezea Naibu Balozi wa India nchini Balvinder Humpal kuhusu chumba cha kompyuta kilichopo chuoni hapo wakati wa kuangalia maadalizi ya kutiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano ya Mafunzo ya Watalaam wa Takwimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika na Chuo cha Takwimu cha nchini India utakaosainiwa tarehe 28 Machi, 2015. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO)