TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, March 24, 2016
DKT. KASHILILAH AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA BUNGE LA ISRAEL
TANZANIA NA SAUDIA ZASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA UCHUMI NA UWEKEZAJI.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
pamoja na wajumbe wa Serikali zote mbili wakishuhudia uwekwaji saini wa
mkataba kuhusu Ushirikiano kati ya Tanzania na Saudi Arabia katika
nyanja za Uchumi, Biashara, Uwekezaji, Ufundi, Vijana na Michezo. Kwa
upande wa Tanzania mkataba ulisainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje,
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine
Mahiga (kulia) na Serikali ya Saudi Arabia iliwakilishwa na Waziri wa
Mambo ya Nje, Mhe. Adel Al Jubair.
MANYARA YAPITISHA BAJETI YAKE
Mkuu wa mkoa wa Manyara Joel Bendera Na Woinde Shizza,manyara
Mkoa wa Manyara unatarajia kutumia sh202.1 bilioni kwa ajili ya mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2016/2017, ambapo mishahara itakuwa ni sh5.5 bilioni, matumizi ya kawaida sh2.1 bilioni na sh2.7 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Katika mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 mkoa umekadiriwa kukusanya mapato ya ndani ya sh18 bilioni ambapo sh17.9 bilioni ni kwa ajili ya serikali za mitaa na sh192 milioni ni za sekretarieti ya mkoa.
Akisoma mpango wa bajeti ya mkoa huo juzi, Katibu Tawala wa mkoa huo Eliakim Maswi alisema kijiografia Manyara yenye kilomita za mraba 50,921 ni kubwa kuliko baadhi ya mikoa, hivyo inahitaji gharama kubwa za uendeshaji.
Maswi alisema katika mpango huo wa bajeti, Babati mjini wanatarajia kutumia sh25 bilioni, Babati vijijini sh37 bilioni, Hanang’ sh33 bilioni, Kiteto sh30 bilioni, Mbulu vijijini sh38 bilioni, Mbulu mjini sh6 bilioni na Simanjiro sh19 bilioni. “Pia tunakabiliwa na changamoto ya kuchelewa au kutopatikana kwa fedha za ruzuku za matumizi ya kawaida na ruzuku ya miradi ya maendeleo, ufinyu wa bajeti wa kuboresha na kujenga miundombinu ya zahanati na shule,” alisema.
Alisema umbali kutoka makao makuu ya halmashauri ya wilaya hadi makao makuu ya mkoa ambapo ni lazima upitie wilaya nyingine kama Kondoa, Monduli na Arusha ili ufike mkoani wakati wa kufuata huduma mkoani pia ni kikwazo.
Hata hivyo, mkuu wa mkoa huo Dk Joel Bendera alizitaka halmashauri zote saba kuhakikisha zinachangia bajeti zao kwa asilimia 60 ya mapato ya vyanzo vya ndani kama serikali kuu ilivyoagiza ili kutekeleza miradi ya maendeleo yao.
Sunday, March 20, 2016
OLE SENDEKA ATANGAZWA RASMI LEO KUWA MSEMAJI WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimtangaza Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Christopher Ole Sendeka kuwa Msemaji Rasmi wa CCM leo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam

Ole Sendeka akizungumza baada ya kuteuliwa. Kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ambaye pia ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Picha: Bashir Nkoromo)
TAARIFA ILIYOSOMWA NA OLE SENDEKA BAADA YA KUTAMBULISHWA KWA WAANDISHI WA HABARI LEO.
Subscribe to:
Posts (Atom)



Meneja
wa bidhaa wa Samsung,Rayton Kwembe(kushoto) Meneja Uhusiano wa Vodacom
Tanzania,Matina Nkurlu, Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa wa Vodacom
Tanzania,Samson Charles, Meneja masoko wa Samsung,Tulisindo
Mwachula,wakionesha simu aina ya Galax S7 na S7 Edge kwa waandishi wa
habari(hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa simu hizo ambazo haziingizi
maji ulifanyika Makao Makuu ya Vodacom Tanzania Mlimani City jijini Dar
es Salaam.








