TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, April 15, 2016

RAIS WA SUDANI KUSINI SALVA KIIR ATIA SAINI MKATABA WA KUJIUNGA RASMI NA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


EALA Tanzania wakutana na Kamati za Bunge la Tanzania






Alisema Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki inajengwa katika mfumo wa ushindani wa soko na kwamba kila fursa iliyopo katika Jumuiya inapatikana kwa ushindani miongoni miongoni mwa wananchi wa nchi wanachama.
"Hivyo, Watanzania kama raia wa nchi zingine wanachama ni lazima wachangamkie fursa na kuzitumia. Ili kushindana, Watanzania wanatakiwa kujiamini na kuacha kujiona wanyonge ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwani akili tunazi, uwezo tunao na nguvu tunazo," alifafanua.
Akichangia katika mkutano huo, Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Allan Kiula, alisema ni vema elimu kuhusu mtangamano wa Afrika Mashariki, hususan kuhusiana na fursa za kibiashara, ikatolewa pia kwa wafanyakazi wa taasisi zinazofanya kazi kwenye maeneo ya mipakani, kama vile Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa kikwazo kwa wafanyabiashara kutokana na utendaji wao usioridhisha.
Alisema watumishi katika vituo vya mipakani wamekuwa wakiwakatisha tamaa wananchi wanaofanya biashara kiasi cha kuwafanya waendelee kutumia njia za panya.
Naye mbunge wa Moshi Vijijini, Anthony Komu (Chadema) alisema Tanzania bado ina kazi kubwa katika ushindani ndani ya Jumuiya akitolea mfano wa Kenya ambayo imefikia uchumi wa kati kwa kuwa na viwanda vya kutosha wakati nchi yetu ndio inafikiria kufufua na kuanzisha viwanda.
Alisema kuna hatari ya Tanzania kubakia kuwa soko wakati nchi kama Kenya zinapambana kufanya uzalishaji mkubwa wa viwandani na kuimarisha ubora wa bidhaa zake.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Adadi Rajabu aliwataka Watanzania kutafuta mbinu za kuwa wabunifu zaidi katika ushindani ndani ya Jumuiya ili kuweza kufanikiwa kukamata fursa za mtangamano.
Wabunge wa Afrika Mashariki ambao wapo katika shughuli za kuhamasisha na kuelimisha umma kuhusu fursa za mtangamano wa Afrika Mashariki wamesema siku za usoni wanatarajia kufanya mkutano na wabunge wote ili kubadilishana nao uzoefu kuhusiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania, (EALA), Makongoro Nyerere akifafanua jambo wakati wabunge kutoka EALA walipokutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi na Usalama pamoja na Kamati ya Viwanda Biashara  na Mazingira jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kadumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Adadi Rajabu na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Dk. Dalali Kafumu. (Picha na Francis Dande)
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania, Twaha Taslima akifafanua jambo mbele ya wabunge wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama pamoja na Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira jijini Dar es Salaam leo.

WIZARA YAKEMEA MAUAJI YA WAZEE NZEGA











DK.ABDALLA POSSI MGENI RASMI MATEMBEZI YA HIYARI KUAZIMISHA SIKU YA WATOTO WENYE USONJI














OUNT KILIMANJARO WON AFRICA’S LEADING TOURIST ATTRACTION AWARD IN 2016.












“JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI NI SEHEMU SAHIHI KWA SUDANI YA KUSINI” KIIR
















MAJALIWA AKUTANA NA WAZIRI WA VIWANDA WA OMAN

BUNGE LATOA UFAFANUZI KUHUSU MKATABA WA LUGUMI

NAIBU WAZIRI DKT. KIGWANGALLA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA LEO KATIKA VITUO VYA TIBA MBADALA.



WAZEE WA ZANZIBAR WAANZA KUPOKEA PENSHENI


















WABUNGE WAPONGEZA KUANZISHWA KWA TADB



MAKAMPUNI BINAFSI HAYAHUSIKI ULINZI WA NDANI OFISI ZA BANDARI.



RAIS WA SUDANI KUSINI, MHE. JENERALI SALVA KIIR MAYARDIT AWASILI LEO NCHINI



Wakazi Dar ‘kuonja’ daraja la Kigamboni bure kesho



Wakazi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake kesho  wanatapa fursa ya kulitumia kwa mara ya kwanza Daraja la Kigamboni linalotarijiwa kufunguliwa rasmi na Rais John Pombe Magufuli siku ya Jumanne ya wiki ijayo ili ‘kuonja’ na kujionea ubora wa daraja hilo kisasa.
Akizungumza  jijini Dar es Salaam jana, Meneja mradi kutoka kampuni ya China Railway Construction Engineering Group ambao wametekeleza mradi huo kwa ushirikiano na kampuni ya China Railway Major Bridge Group Bw.Zhang Bangxu,  alisema  siku ya kesho, wataruhusu wakazi hao na magari kupita katika daraja hilo lililogarimu Dola za Kimarekani milioni 135 kujengwa.
“Kama wajenzi kesho tutaruhusu magari kupita kwenda upande wa Kurasini na upande wa Kigamboni siku ya Jumamosi tu kama ikiwa ni sehemu ya majaribio yetu kitaalamu ikiwa ni pamoja na kutumia fursa hiyo kufanya majaribio ya mitambo na mashine zote ambazo zitatumika katika kufanya tozo mbali mbali baada ya kuanza rasmi kwa mradi," alifafanua.
Kwa mujibu wa Bw. Bangxu, daraja la Kigamboni ndiyo daraja refu kuliko yote katika ukanda wa Afrika Mashariki lililotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya matumizi ya kamba (cable) kubeba uzito wa daraja, ambayo itaunganisha jiji la kibiashara la Dar es Salaam na eneo la Kigamboni na Kurasini. Ujenzi ulianza mnamo Tarehe moja Februari mwaka 2012.
“Pamoja na kujengwa katika ubora wa hali ya juu, daraja hili lina jumla ya njia sita yaani njia tatu kwa kila upande, pamoja na njia mahususi kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli ambayo ina upana wa mita 2 na nusu (2.5 meters) katika kila pande. Daraja hilo litaruhusu magari yenye uzito usiozidi tani 30 kupita.,’’ aliongeza
 
 Bw. Bangxu alisema kwamba kaskazini mwa daraja hilo, litaungana na barabara lenye urefu wa kilometa  moja ambayo inakatiza reli ya TAZARA kisha kuungana na barabara ya Mandela. Kwa upande wa Kigamboni, daraja litaungana na barabara lenye urefu wa Kilometa 1.5 ambayo inaungana na barabara ya Kigamboni Ferry - Kibada.

Aliongeza kwamba kukamilika kwa daraja hili ni ya maendeleo kwani inatarajiwa kuchochea kasi ya maendeleo ya mji wa kisasa wa Kigamboni (Kigambani satellite city), kutengeneza fursa za ajira katika sekta ya ujenzi wa maeneo ya makazi pamoja na sekta za huduma ambazo  zitastahimili ongezeko kubwa wa idadi ya wakazi wapya katika mji huo mpya.
Kukamilika kwa daraja hilo kunatajwa kuwa kutawapafusra wakazi wa Kigamboni na viunga vyake ikiwa ni kutoa njia mbadala ya kufikia makazi yao, biashara zao au shuguli zao za ujenzi wa taifa kwa njia ya barabara.
 
Maeneo ya Kigamboni na Kurasini kwa sasa hufikika kwa kutumia vivuko viwili vya MV Magogoni na MV Kigamboni ambazo kwa pamoja zinaumezo wa kubebe abiria 1000 na magari 78 kwa kila safari.
Mradi huo umedhaminiwa kwa kwa ubia kati ya Shirika la Hifadhi ya Jamii ya Taifa (NSSF) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

Waziri Nape afanya Ziara mkoani Kagera