TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Friday, April 15, 2016
EALA Tanzania wakutana na Kamati za Bunge la Tanzania
Alisema Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki
inajengwa katika mfumo wa ushindani wa soko na kwamba kila fursa iliyopo
katika Jumuiya inapatikana kwa ushindani miongoni miongoni mwa wananchi
wa nchi wanachama.
"Hivyo, Watanzania kama raia wa nchi zingine wanachama ni lazima
wachangamkie fursa na kuzitumia. Ili kushindana, Watanzania wanatakiwa
kujiamini na kuacha kujiona wanyonge ndani ya Jumuiya ya Afrika
Mashariki kwani akili tunazi, uwezo tunao na nguvu tunazo," alifafanua.
Akichangia katika mkutano huo, Mbunge wa Iramba Mashariki (CCM), Allan
Kiula, alisema ni vema elimu kuhusu mtangamano wa Afrika Mashariki,
hususan kuhusiana na fursa za kibiashara, ikatolewa pia kwa wafanyakazi
wa taasisi zinazofanya kazi kwenye maeneo ya mipakani, kama vile Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa kikwazo kwa
wafanyabiashara kutokana na utendaji wao usioridhisha.
Alisema watumishi katika vituo vya mipakani wamekuwa wakiwakatisha tamaa
wananchi wanaofanya biashara kiasi cha kuwafanya waendelee kutumia njia
za panya.
Naye mbunge wa Moshi Vijijini, Anthony Komu (Chadema) alisema Tanzania
bado ina kazi kubwa katika ushindani ndani ya Jumuiya akitolea mfano wa
Kenya ambayo imefikia uchumi wa kati kwa kuwa na viwanda vya kutosha
wakati nchi yetu ndio inafikiria kufufua na kuanzisha viwanda.
Alisema kuna hatari ya Tanzania kubakia kuwa soko wakati nchi kama Kenya
zinapambana kufanya uzalishaji mkubwa wa viwandani na kuimarisha ubora
wa bidhaa zake.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Adadi
Rajabu aliwataka Watanzania kutafuta mbinu za kuwa wabunifu zaidi katika
ushindani ndani ya Jumuiya ili kuweza kufanikiwa kukamata fursa za
mtangamano.
Wabunge wa Afrika Mashariki ambao wapo katika shughuli za kuhamasisha na
kuelimisha umma kuhusu fursa za mtangamano wa Afrika Mashariki wamesema
siku za usoni wanatarajia kufanya mkutano na wabunge wote ili
kubadilishana nao uzoefu kuhusiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania,
(EALA), Makongoro Nyerere akifafanua jambo wakati wabunge kutoka EALA
walipokutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ulinzi na Usalama
pamoja na Kamati ya Viwanda Biashara na
Mazingira jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kadumu
ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Adadi Rajabu na Mwenyekiti wa
Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Dk. Dalali Kafumu. (Picha
na Francis Dande)
Wakazi Dar ‘kuonja’ daraja la Kigamboni bure kesho
Wakazi
wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake kesho wanatapa fursa ya
kulitumia kwa mara ya kwanza Daraja la Kigamboni linalotarijiwa
kufunguliwa rasmi na Rais John Pombe Magufuli siku ya Jumanne ya wiki
ijayo ili ‘kuonja’ na kujionea ubora wa daraja hilo kisasa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja mradi kutoka kampuni ya China Railway Construction Engineering Group ambao wametekeleza mradi huo kwa ushirikiano na kampuni ya China Railway Major Bridge Group Bw.Zhang Bangxu, alisema siku ya kesho, wataruhusu wakazi hao na magari kupita katika daraja hilo lililogarimu Dola za Kimarekani milioni 135 kujengwa.
“Kama wajenzi kesho tutaruhusu magari kupita kwenda upande wa Kurasini na upande wa Kigamboni siku ya Jumamosi tu kama ikiwa ni sehemu ya majaribio yetu kitaalamu ikiwa ni pamoja na kutumia fursa hiyo kufanya majaribio ya mitambo na mashine zote ambazo zitatumika katika kufanya tozo mbali mbali baada ya kuanza rasmi kwa mradi," alifafanua.
Kwa mujibu wa Bw. Bangxu, daraja la Kigamboni ndiyo daraja refu kuliko yote katika ukanda wa Afrika Mashariki lililotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya matumizi ya kamba (cable) kubeba uzito wa daraja, ambayo itaunganisha jiji la kibiashara la Dar es Salaam na eneo la Kigamboni na Kurasini. Ujenzi ulianza mnamo Tarehe moja Februari mwaka 2012.
“Pamoja na kujengwa katika ubora wa hali ya juu, daraja hili lina jumla ya njia sita yaani njia tatu kwa kila upande, pamoja na njia mahususi kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli ambayo ina upana wa mita 2 na nusu (2.5 meters) katika kila pande. Daraja hilo litaruhusu magari yenye uzito usiozidi tani 30 kupita.,’’ aliongeza
Bw. Bangxu alisema kwamba kaskazini mwa daraja hilo, litaungana na barabara lenye urefu wa kilometa moja ambayo inakatiza reli ya TAZARA kisha kuungana na barabara ya Mandela. Kwa upande wa Kigamboni, daraja litaungana na barabara lenye urefu wa Kilometa 1.5 ambayo inaungana na barabara ya Kigamboni Ferry - Kibada.
Aliongeza kwamba kukamilika kwa daraja hili ni ya maendeleo kwani inatarajiwa kuchochea kasi ya maendeleo ya mji wa kisasa wa Kigamboni (Kigambani satellite city), kutengeneza fursa za ajira katika sekta ya ujenzi wa maeneo ya makazi pamoja na sekta za huduma ambazo zitastahimili ongezeko kubwa wa idadi ya wakazi wapya katika mji huo mpya.
Kukamilika kwa daraja hilo kunatajwa kuwa kutawapafusra wakazi wa Kigamboni na viunga vyake ikiwa ni kutoa njia mbadala ya kufikia makazi yao, biashara zao au shuguli zao za ujenzi wa taifa kwa njia ya barabara.
Maeneo ya Kigamboni na Kurasini kwa sasa hufikika kwa kutumia vivuko viwili vya MV Magogoni na MV Kigamboni ambazo kwa pamoja zinaumezo wa kubebe abiria 1000 na magari 78 kwa kila safari.
Mradi huo umedhaminiwa kwa kwa ubia kati ya Shirika la Hifadhi ya Jamii ya Taifa (NSSF) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Meneja mradi kutoka kampuni ya China Railway Construction Engineering Group ambao wametekeleza mradi huo kwa ushirikiano na kampuni ya China Railway Major Bridge Group Bw.Zhang Bangxu, alisema siku ya kesho, wataruhusu wakazi hao na magari kupita katika daraja hilo lililogarimu Dola za Kimarekani milioni 135 kujengwa.
“Kama wajenzi kesho tutaruhusu magari kupita kwenda upande wa Kurasini na upande wa Kigamboni siku ya Jumamosi tu kama ikiwa ni sehemu ya majaribio yetu kitaalamu ikiwa ni pamoja na kutumia fursa hiyo kufanya majaribio ya mitambo na mashine zote ambazo zitatumika katika kufanya tozo mbali mbali baada ya kuanza rasmi kwa mradi," alifafanua.
Kwa mujibu wa Bw. Bangxu, daraja la Kigamboni ndiyo daraja refu kuliko yote katika ukanda wa Afrika Mashariki lililotengenezwa kwa kutumia teknolojia ya matumizi ya kamba (cable) kubeba uzito wa daraja, ambayo itaunganisha jiji la kibiashara la Dar es Salaam na eneo la Kigamboni na Kurasini. Ujenzi ulianza mnamo Tarehe moja Februari mwaka 2012.
“Pamoja na kujengwa katika ubora wa hali ya juu, daraja hili lina jumla ya njia sita yaani njia tatu kwa kila upande, pamoja na njia mahususi kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli ambayo ina upana wa mita 2 na nusu (2.5 meters) katika kila pande. Daraja hilo litaruhusu magari yenye uzito usiozidi tani 30 kupita.,’’ aliongeza
Bw. Bangxu alisema kwamba kaskazini mwa daraja hilo, litaungana na barabara lenye urefu wa kilometa moja ambayo inakatiza reli ya TAZARA kisha kuungana na barabara ya Mandela. Kwa upande wa Kigamboni, daraja litaungana na barabara lenye urefu wa Kilometa 1.5 ambayo inaungana na barabara ya Kigamboni Ferry - Kibada.
Aliongeza kwamba kukamilika kwa daraja hili ni ya maendeleo kwani inatarajiwa kuchochea kasi ya maendeleo ya mji wa kisasa wa Kigamboni (Kigambani satellite city), kutengeneza fursa za ajira katika sekta ya ujenzi wa maeneo ya makazi pamoja na sekta za huduma ambazo zitastahimili ongezeko kubwa wa idadi ya wakazi wapya katika mji huo mpya.
Kukamilika kwa daraja hilo kunatajwa kuwa kutawapafusra wakazi wa Kigamboni na viunga vyake ikiwa ni kutoa njia mbadala ya kufikia makazi yao, biashara zao au shuguli zao za ujenzi wa taifa kwa njia ya barabara.
Maeneo ya Kigamboni na Kurasini kwa sasa hufikika kwa kutumia vivuko viwili vya MV Magogoni na MV Kigamboni ambazo kwa pamoja zinaumezo wa kubebe abiria 1000 na magari 78 kwa kila safari.
Mradi huo umedhaminiwa kwa kwa ubia kati ya Shirika la Hifadhi ya Jamii ya Taifa (NSSF) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Subscribe to:
Posts (Atom)







