TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, April 27, 2016

USAID WAZINDUA MRADI WA UIMARISHAJI MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA MKOANI MTWARA LEO

JIJI LAUNDA KAMATI KUCHUNGUZA MALI ZAKE.


 





Wasanii waaswa kutoingia mikataba kiholela

WANAMTANDAO WAITAKA DAWASCO KUTUPIA JICHO TABAKA LA WASIOJIWEZA








NEWS ALERT: Harry Kitilya na wenzake wafutiwa shtaka moja, dhamana yagonga mwamba

Sherehe za miaka 5 ya kitchen party gala zafana!

afya,ujasiriamali n.k.


mkuu wa wilaya ya kinondoni akagua miradi mbalimbali ya maendeleo manispaa ya Kinondoni



Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam Mh . Ally Salum Hapi akielekezwa jambo alipokuwa akikagua moja ya mradi ndani ya wilaya hiyo.
 Mh. Hapi akikagua na kupokea taarifa ya miradi mbalimbali iliyokamilika na inayoendelea kukamilika.
Mh. Hapi akipata maeelezo mara baada ya kagua na kupokea taarifa ya miradi mbalimbali iliyokamilika na inayoendelea kukamilika.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA MAKATIBU TAWALA WAPYA WA MIKOA 10 IKULU JIJINI DAR ES SALAAM



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaapisha Makatibu Tawala wapya kumi aliowateua tarehe 25 Aprili, 2016 na kuwapangia vituo vyao vya kazi.
Makatibu Tawala hao wameapishwa leo tarehe 27 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam na kisha wametia saini hati ya ahadi ya uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi lililoendeshwa na Kamishna wa maadili Sekreatieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Mheshimiwa Jaji Salome Kaganda na kushuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi.
Makatibu Tawala walioapishwa ni;
1. Arusha - Richard Kwitega
2. Geita - Selestine Muhochi Gesimba
3. Kagera - Armatus C. Msole
4. Kilimanjaro - Eng. Aisha Amour
5. Pwani - Zuberi Mhina Samataba
6. Shinyanga - Albert Gabriel Msovela
7. Singida - Dr. Angelina Mageni Lutambi
8. Simiyu - Jumanne Abdallah Sagini
9. Tabora - Dkt. Thea Medard Ntara
10. Tanga - Eng. Zena Said
Makatibu Tawala wengine wa Mikoa ambao hawakuapishwa leo, ni wale waliohamishwa vituo vya kazi na wale waliobaki katika vituo vya kazi walivyokuwep,o ambao tayari walishakula kiapo cha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Aprili, 2016

Benki ya Exim yazindua mashine yake ya kwanza ya kuweka pesa kwenye akaunti.


BENKI ya Exim Tanzania imezindua mashine yake ya kwanza ya kuweka pesa (CDM) itakayowawezesha wateja wa kampuni ya Pacific International Lines, PIL kuweka pesa kwenye akaunti zao moja kwa moja bila kulazimika kufika kwenye ofisi au kuhudumiwa na wafanyakazi wa benki hiyo.

Ufunguzi wa mashine hiyo ulifanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni ukihusisha mwakilishi wa benki hiyo ambaye ni Mkuu wa Huduma za matawi Bw Eugine Massawe pamoja na Meneja Mkuu wa kampuni ya PIL Bw. Kevin Stone.

“Mteja atapokea ujumbe mfupi wa maneno kuhusiana na mwenendo ya muhamala alioufanya,’’ alisema Bw Massawe huku akisisitiza: “Benki ya Exim itabaki kuwa benki pekee yenye kubuni huduma zinazokidhi matakwa ya wateja kulingana na mabadiliko ya kimahitaji katika huduma za kibenki,’’

Alisema huduma hiyo imewekwa jirani na makao makuu ya benki hiyo ili kuwawezesha watumiaji wa huduma hiyo kupata msaada kwa urahisi kutoka kwa wafanyakazi wa benki pale wanapohitaji.“Itakapofikia kipindi ambacho wateja wetu watakuwa tayari wamejenga uelewa wa kutosha kuhusiana na matumizi sahihi ya mashine hii tutakuwa tayari kuongeza mashine nyingine katika maeneo mbalimbali ili waweze kufurahia huduma hii zaidi,’’ aliahidi.

Mbio za Heart Marathon zafana jijini Dar es Salaam

MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ,SAID MECKY SADICK AFANYA ZIARA YA UTAMBURISHO WILAYA YA HAI.

Rais Magufuli awaapisha Makatibu Tawala wapya wa Mikoa

MDAU ALFRED LUCAS ATEULIWA KUWA AFISA HABARI MPYA TFF

Naibu Katibu Mkuu ampongeza Getrude Clement

MADEREVA BODABODA WATAKIWA KUINGIA DARASANI KUELIMISHWA ELIMU YA USALAMA BARABARANI

Waendesha bodaboda wametakiwa kwenda darasana kupata elimu ya usalama barabarani ili kuweza kuepusha ajali za maramara kwa mara zisizo tarajiwa .Hayo yalibainishwa na diwani wa viti maalumu kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kata ya Usariver Mary Antony wakati akiongea na madereva wa bodaboda hao mara baada ya kuwalipia ada ya mafunzo ya usalama barabarani, madereva 45 wa kata ya usa river.Alisema kuwa ni wajibu wa kila dereva bodaboda kwenda kupata elimu ya usalama barabarani ili kupunguza ajali za barabarani zinazotokea mara kwa mara, kwa kusababishwa na uzembe wa madereva hao.“mimi kama diwani wa viti maalumu niliamua kwenda kuwalipia ada ya mafunzo madereva hawa wa bodaboda ili angalau waweze kujua sheria za barabarani na pia waweze kupata leseni, maana hawa wote hawana leseni na si hivyo tu nadhani iwapo madereva hawa watazijua hizi sheria za bara barani, itasaidia kupunguza ajali za mara kwa mara ambazo zinatokea”alisema MaryAlibainisha kuwa ni wajibu wa kila dereva kujua sheria na iwapo atajua sheria watajiamini na pia awatasumbuliwa ata na polisi wa usalama barabarani njiani kwani watakuwa wanajua sheria hivyo ata akiambiwa amefanya kosa ataweza kujua ni kosa kweli au amedanganywa kwakuwa tayari anajua sheria hizi za usalama wa barabarani.Kwa upande wake mmoja wa vijana wa bodaboda wa kata hiyo ya Usariver alisema kuwa anamshukuru diwani huyo kwa kuwasaidia kwani wamejitambua na wanajua sheria na aliwasihi madereva wenzake kwenda mashuleni kujua sheria hizo.Alisema kuwa mafunzo hayo ambayo wameyapata yatawasaida kujiamini na pia yamewasaidia pia kutowaogopa askari wa barabarani kama zamani ,kwani kwa sasa wanajua sheria ya usalama barabarani na sio hivyo tu katika mafunzo hayo pia wamefundishwa mafunzo ya ulinzi shirikishi ili kuweza kuwatambua wezi na jinsi ya kujiepusha na wateja ambao hawaeleweki