TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, September 13, 2013

Uwanja wa nyumbani wa Yanga, Kaunda, ulianza kujengwa mwaka 1973 kwa gharama ya Sh3 milioni.

Dar es Salaam. Wakati klabu ya Simba ikidhihirisha kuwa imekwama kujenga uwanja, uongozi wa Yanga umeanza visingizio na kudai kuwa serikali ndiyo inayowakwamisha kuanza kwa ujenzi wa uwanja wao wa Kaunda.Ujenzi wa viwanja katika klabu hizo mbili kubwa na zenye mashabiki wengi zaidi nchini ni sawa na tamthilia maarufu ndefu ya Afrika Kusini ya Isidingo ambayo haifikii tamati.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga aliliambia gazeti hili jana wameandika barua muda mrefu serikalini ili wapate kibali cha Serikali cha kuongeza eneo la uwanja huo.Yanga ipo katika mikakati ya kuujenga uwanja wake wa Kaunda ili uweze kuwa wa kisasa zaidi na kuwa katika nyasi bandia ambapo awali walieleza kuwa ungeanza mwezi Juni ukiwa unagharimu Sh32 bilioni.
“Ramani ya uwanja ambayo wametupa Wachina inaingia sehemu kidogo ya uwanja wa wazi wa serikali, ni muda mrefu sasa tumeandika barua watuongezee kipande kilichozidi lakini bado hawajatuambia chochote ndio maana tumesimama.“Tumekwama hata kusaka vyanzo vya mapato kwa ajili ya uwanja ila kwa sasa tumeshapata mtu wa masoko atashughulikia,” alisema Sanga muda mfupi baada ya kumtangaza George Simba kuwa mmoja wa watu muhimu katika sekretarieti ya Yanga katika kusaidia kuboresha mapato ya klabu hiyo.
Alisema Simba ndiye atakayefanikisha mapendekezo ya uongozi kwa wanachama ya kuchangia Sh250 kila mmoja kila wiki kwa lengo la kupata Sh8 bilioni, kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ikiwamo makusanyo ya ada za uanachama, michango mbalimbali, harambee, kalenda na mauzo ya jezi na bidhaa zenye nembo ya Yanga pamoja na kusaka taasisi mbalimbali za kibenki kwa ajili ya kuwezesha kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo.
Hata hivyo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Goodlucky Ole Medeye aliwahi kuliambia gazeti hili kuwa hawajapokea barua yoyote ya Yanga ya kuomba kupewa sehemu hiyo ya Jangwani na kwamba iwapo itawafikia hawana pingamizi. Yanga ipo katika mikakati ya kuujenga uwanja wake wa Kaunda ili uweze kuwa wa kisasa zaidi na kuwa katika nyasi bandia ambapo awali walieleza kuwa wangeanza ujenzi mwezi Juni.
Desemba mwaka jana uongozi wa Yanga ulitoa ahadi ya kuijengea klabu hiyo uwanja wa kisasa na Januari mwaka huu ukamtangaza  mkandarasi, Kampuni ya Beijing Constructions Engineering Group iliyojenga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kwamba ndiye atakayejenga uwanja huo mpya wa Yanga. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, ujenzi huo wa uwanja utakuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki 30,000 hadi 40,000 lakini hadi sasa hakuna hata dalili za kuanza.

No comments:

Post a Comment