TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, January 19, 2016

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ATEMBELEA IDARA YA UHAMIAJI ZANZIBAR. TAXES, ACCOUNTING AND LIFE INSURANCE SERVICES HATUA AMBAZO ZIMECHUKULIWA DHIDI YA STANBIC BANK TANZANIA LIMITED KUHUSU USHIRIKI WAKE KUWEZESHA MKOPO WA SERIKALI WA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 600 RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI AWAASA WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU KUSIMAMIA NA KUDUMISHA MILA NA TAMADUNI ZA DINI YAO Peter wa P-Square mgonjwa, anahitaji maombi KIPINDI CHA JUKWAA LANGU KINACHORUSHWA LIVE KILA SIKU YA JUMATATU USIKOSE I WAS LOST, VIDEO MPYA YA ROSE KACHUCHURU Kichupa cha leo Sheikha - Bahati (Official HD Music Video) TCRA kufungia vituo sita vya televisheni, redio 20 Hupandi ndege bila barua, kibali cha Ikulu Wataka Mwinyi, Mkapa, JK wapunguziwe mishahara UCHAMBUZI WA MAGAZETI WAJAPANI KUWEKEZA KWENYE UZALISHAJI UMEME NCHINI DAWASCO YABAINI WIZI WA MAJI KIWANDA CHA BAHARI CHEMICALS LTD SERIKALI YALIFUTA GAZETI LA MAWIO YALIYOJIRI KWENYE MECHI YA SIMBA NA MTIBWA SUGAR KATIKA PICHA Wakazi New Video: Kanuni Za Hela CUF kuandamana Pemba kisa Hamad.



=========================================================================









We Offer Coverage from $25,000 to Over $1,000,000.

No Medical Check Up for the Life Insurance up to $250,000.

The Premium Starts as low as $15 a month .

YOU CAN ALSO USE THE LIFE INSURANCE AS 
A TAX FREE RETIREMENT FUNDING




      ========================================================================

                                                                                                                        Utangulizi

      Mwezi Julai 2013, Benki Kuu ya Tanzania kupitia ufuatiliaji wa kawaida wa shughuli za mabenki iligundua matatizo yaliyohusiana na hasara itokanayo na mikopo na pia kuacha na kuondolewa kazini kwa viongozi waandamizi wa Stanbic Bank Tanzania Limited (Stanbic) katika muda mfupi. 



               Matokeo ya Ukaguzi wa Benki Kuu

      Katika ukaguzi huo, wakaguzi wa Benki Kuu, pamoja na mambo mengine walibaini miamala ya kutia shaka iliyohusu malipo kwa kampuni ya kitanzania ya Enterprise Growth Market Advisors (EGMA). Kampuni ya EGMA ilihusika katika uwezeshaji wa upatikanaji wa Mkopo kwa Serikali ya Tanzania ambapo Standard Bank Plc (ambayo kwa sasa inajulikana kama ICBC Standard Bank) na Stanbic Bank Tanzania Limited kwa pamoja walikuwa “Mwezeshaji Mkuu” (Lead Arranger). 



      Taarifa ya ukaguzi huo iliwasilishwa kwa benki ya Stanbic kwa mujibu wa taratibu, na Benki Kuu iliiagiza Bodi ya Wakurugenzi ya benki hiyo kuchukua hatua stahiki za kurekebisha kasoro zilizoonekana. 



      Mnamo 29 Septemba 2015, Benki Kuu ilipokea barua toka Idara ya Serikali ya Uingereza inayohusika na Upelelezi wa Makosa ya Kugushi na Rushwa (Serious Fraud Office – SFO) ikiiomba Benki Kuu ruhusa ya kutumia ripoti yake ya ukaguzi kama ushahidi katika kesi dhidi ya Standard Bank Plc ambayo ilikuwa ni mshirika wa Stanbic Bank Tanzania Limited katika kuwezesha mkopo wa dola za kimarekani milioni 600 kwa Serikali na kwamba ripoti hiyo ingekuwa wazi kwa umma. 



      Hatimaye, Standard Bank Plc ilikubali makosa na ilitozwa faini ya jumla ya dola za kimarekani milioni 32.20, ambapo kiasi cha dola za kimarekani milioni 7 zinalipwa kwa Serikali ya Tanzania (dola za kimarekani milioni 6 zilikuwa ni fidia na dola za kimarekani milioni 1 ni riba).

      Kwa kuzingatia mapungufu ya kufanya miamala iliyohusisha EGMA na pia kutokuweka taratibu madhubuti za udhibiti wa ndani, na kwa kuzingatia Kifungu 67 cha Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Benki Kuu imeiandikia benki ya Stanbic barua ya kusudio la kuitoza faini ya shilingi bilioni 3. Sheria inaitaka benki ya Stanbic kutoa utetezi katika kipindi cha siku ishirini (20) ambacho kitaisha tarehe 30 Januari 2016. Endapo Benki Kuu haitaridhika na utetezi, benki ya Stanbic italazimika kulipa faini hiyo.

           Hitimisho

      Benki Kuu imechukua hatua hizo kama onyo kwa benki ya Stanbic na ili iweze kuwa makini katika kuhakikisha kuwa shughuli zake zinaendeshwa kwa mujibu wa taratibu za kibenki na kuzingatia Sheria.

      Aidha, hatua hii ni onyo kwa mabenki na taasisi za fedha zisijihusishe na makosa ya aina hii ambayo ni kinyume cha taratibu za kibenki na ni uvunjaji wa Sheria za nchi. Hatua kali zitaendelea kuchukuliwa kwa benki au taasisi ya fedha yoyote itakayobainika kwenda kinyume na taratibu za kibenki na Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006.
      ======================================================================
      Makamu wa Rais Mstaafu wa Tanzania Dr. Moh’d Gharib Bilal akitoa salamu wakati wa hafla ya kusherehekea maulidi ya kuzaliwa Mtume Muhammad {SAW } yaliyoandaliwa na Uongozi wa Kiwanda cha Nguo cha NIDA.
      Rais Mstaafu wa Tanzania wa Awamu ya Pili Al – Hajj Ali Hassan Mwinyi kushoto akimkabidhi zawadi ya Msahafu Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi uliotolewa na Uongozi wa Kiwanda cha Nguo cha NIDA.

      Rais Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Al –Hajj Ali Hassan Mwinyi alisema Waumini wa Dini ya Kiislamu wanapaswa kusimamia na kudumisha mila na Tamaduni za Dini yao kwa kuendelea kuwafunza Watoto na Wajukuu wote juu ya kumpenda Kiongozi wa Dini ya Kiislamu Ulimwenguni Mtume Muhammad { SAW }wakiwa bado wadogo.

      Alisema endapo utaratibu na juhudi hizo zitajengewa mipango madhubuti kizazi hicho kitachipua vyema na kuwa tayari kumpenda, kumuelewa ipasavyo pamoja na kumtukuza Muokozi wao huyo Nabii Muhammad { SAW }.

      Al Hajj Ali Hassan Mwinyi alisema hayo wakati wa sherehe za Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad {SAW }yaliyoandaliwa na Uongozi wa Kiwanda cha Nguo cha Nida {NIDA TEXTILE} na kufanyika katika Mtaa wa Indira Ghandhi Mjini Dar es salaam.

      Alisema waumini wa Kiislamu wakati huu wa sasa wanapaswa kujikita zaidi katika kushughulikia Dini yao hasa katika utekelezaji wa maamrisho yote yalioagizwa katika Kitabu chao kitukufu kwa lengo la kupata mafanikio ya milele.

      Rais Mstaafu wa Tanzania alieleza kwamba katika kipindi hichi cha mabadiliko ya utandawazi yaliyozikumba jamii nyingi duniani Wazazi wana kazi kubwa ya kuwafunza Watoto wao mwenendo aliokuwa nao Mtume Muhammad {SAW } hasa suala zima la uadilifu ambalo kwa sasa linaonekana kupotea kwa nguvu kubwa ndani ya Jamii.

      Alisema Watoto washirikishwe ipasavyo katika kufundishwa dini itakayokuwa dira ya kuzoeshwa nyoyo zao jambo ambalo litakuwa ishara ya mazoezi ya roho ikiwa ni sehemu ya utaratibu utakaowaongoza katika maisha yao ya kila siku.

      Aliupongeza na kuushukuru Uongozi wa Kiwanda cha Nguo cha Nida {NIDA TEXTILE} kwa uamauzi wake wa makusudi wa kuandaa sherehe hiyo ya Maulidi jambao ambalo huleta Baraka na kheir ndani ya maisha ya kila siku ya Jamii.

      Akitoa salamu kwenye hafla hiyo ya Maulidi ya Kuzaliwa Mtume Muhammad {SAW } Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balosi Seif aliwakumbusha Waumini wa Dini ya Kiislamu juu ya wajibu wao wanaotakiwa kuutimiza wa kuzitukuza ishara na alama zote za Dini ya Kislamu ukiwemo uwepo wa utukufu wa Mtume Muhammad { SAW } ili kufikia daraja kubwa ya ucha Mungu.

      Balozi Seif aliwaomba waislamu katika mikusanyiko yao ya kheir ukiwemo huu mkubwa wa hafla za maulidi ya uzawa wa Kiongozi wao wajielekeze kuhimizana zaidi juu ya umuhimu wa kutunza amani na Utulivu wa Nchi ili upendo uliopo miongoni mwa Jamii ya Watanzania uendelee kudumu.

      Alisema mizozo ndani ya Mitaa inafaa kukemewa kwa nguvu zote jambo ambalo litasaidia kuwa kinga ya kujiepusha na mifarakano inayoweza kuzaa shari na hatimae kuukaribisha uadui usiokwisha.

      Naye Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Moh’d Gharib Bilal alisisitiza umuhimu wa kuyaendeleza yale yote yaliyoibuka ndani ya sherehe hizo yaliyofanywa na Vijana kama usomaji wa Quran na Maulidi ili kuwajengea msingi mwema watoto hao.

      Dr. Bilal alisema uendelezaji huo kwa kiasi kikubwa utakuwa dira kwa waumini hao kutekeleza wajibu wao wa kudumisha mazuri kwa kuwarithisha watoto wao mambo ambayo yamesisitizwa sana hata katika Kitabu cha Quran na Hadithi za Mtume Muhammad { SAW }.

      Mapema akitoa nasaha kwa waumini waliohudhuria Sherehe hiyo ya Maulidi ya Uzawa wa Nabii Muhammad {SAW } Sheikh Juma Sadiq kutoka Kigamboni alisema kufurahia Uzawa wa Kiongozi huyo ni wajibu kwa Kila Muumini wa Dini ya Kiislamu.

      Sheikh Juma Sadiq alieleza kwamba si vyema ndani ya Umma wa Kiislamu wakatokea mabaghili wa kupinga au kujiepusha na jambo hili muhimu linalotekelezwa na hata malaika wa mwenyezi Muungu.

      Othman Khamis Ame
      Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
      17/1/2016.
      ========================================================================









      ==========================================================================

      Rose Kachuchuru ni dada anaeishi katika jimbo la Maryland nchini Marekani akijishughulisha na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumtukuza Mungu kwa nyimbo za injili. Rose ambae ni mama wa watoto wawili Mathew Baraka na Marina Zawadi amekuwa akijishughulisha na kazi hii ya uimbaji wa nyimbo za injili kwa Muda sasa akiwa ni zao la kikundi cha nyimbo za injili cha kanisa la The Way of the Cross Gospel Ministries kilichoko Washington DC kwa sasa, ambako huko alikuwa ni mmoja wa waimbaji mahiri.

      Akiongea na mwandishi Rose alieleza ni kwa namna gani amefika hapo alipo sasa, yafuatayo ni maneno yake mwenyewe..... "Mimi kwa jina naitwa Rose Kachuchuru. Nimetoka kwenye familia ambayo inamcha Mungu sana. Wazazi wangu walikuwa ni wacha Mungu wa kweli. Baba yangu alikuwa anampenda sana Mungu.

      Yeye alikuwa analala kanisani siku za sikukuu kama Christimas na Pasaka. Alikuwa ni muombaji sana. Wazungu huwa wanawaita Prayer warriors. He was one of those people. Japokuwa nilitoka katika familia ya kumcha na kumpenda Mungu sana mimi kiukweli nikiangalia nyuma sasa naona sikuwa na uhusiano mzuri na Mungu.

      Enzi hizo mimi nilidhani kwenda kanisani kila siku ilikuwa inatosha kabisa. Sikujuwa kwamba kuna mambo mengi nilitakiwa niyajue na kuyafanya. Ninaposema sikuwa na uhusiano mzuri na Mungu namaanisha sikumjuwa Mungu kama ilivyotakiwa nimjuwe Mungu. Ninavyomjuwa Mungu leo ni tofauti na nilivyokuwa namjuwa zamani.


      Leo nimeona matendo yake mengi ya ajabu katika maisha yangu. Nimeyaona haya yote pale tu nilipoamua kuwa na uhusiano mzuri na yeye. Nikirudi nyuma kidogo nikupe tu historia fupi ya kwangu. Mimi tangu nilipokuwa mdogo nilikuwa napenda saana kuimba. Nakumbuka usiku nyumbani kwetu tulikuwa tunaimba sana nyimbo za tenzi za rohoni. Nanilipoanza shule ya msingi nilikuwa katika band na kwaya ya shule. Pia hata kanisani nilijiunga na kwaya za kanisani.

      Nakumbuka nilipokwenda secondary school niliendelea kuimba mpaka kuna kipindi nilitunga wimbo na tukaenda kushindana na shule zingine za mikoa na tukashinda. Wakati huo mimi sikuona kama ni kitu kikubwa sana nimefanya. Na hata wengine pia sidhani waliona ni kitu kikubwa. Kama tunavyojuwa familia nyingi za kiafrika hazithamini vitu kama hivyo. wazazi wengi wa kiafrika wanapenda watoto wao wawe Madaktari, Ma lawyer au Ma judges. Mambo ya kuimba huona ni upuuzi tu.

      Nikiwa hapa Marekani mwaka 2008 nilijiunga na kanisa linaloitwa The way of the Cross Gospel Ministries. Mimi nilikuwa mmoja wa wanzilishi wa kanisa hilo. Wakati nikiwa kwenye kanisa hilo tuliunda kikundi cha kuimba ambacho sasa kinaitwa The Sound of Glory Singers. Mara nyingi nilpokuwa nikipata nafasi za kuimba mwenyewe watu wengi walikuwa wakija na kuniambia nimewagusa roho zao na nimewabariki sana katika uimbaji wangu. Hiyo ilinipa motisha kubwa sana. Nikasema labda Mungu anataka nimuimbie.

      Wengi walinisisitiza sana kwamba nina kipaji cha kuimba. Wengine waliniambia nipige magoti nimuombe Mungu aniongoze katika hili. Na mimi nilichukuwa ushauri wa watu hao nikaanza kumuomba mungu anipe direction na kwakweli nilianza kumuona mungu aniongoze katika kumuimbia yeye. Niliamua kuondoka The Way of the Cross Gospel Ministries na nikaanza kuconcentrate na kutengeza nyimbo za kumtukuza na kumsifu bwana.

      Nilipitia majaribu makubwa sana wakati huo mpaka nikawa sielewi ni kwanini? Niliamua kumuuliza Mungu ni kwa nini anaruhusu mapigo mazito namna hiyo yanifuate baada ya mimi kuamua kumtumikia kwa kumwimbia. Kiukweli mimi sikujuwa kuwa unapoamua kumtumikia Mungu kwa kumsifu shetani atakuandama ili uache. Mapigo yalikuwa makubwa sana. Lakini Mungu kwa rehema na neema yake aliniona na akanipigania.

      Kuna wimbo wangu mmoja unaitwa I was lost (tazama video juu, huu ni wimbo ambao unamaana kubwa sana katika maisha yangu. Niliandika huu wimbo kuhusu jinsi nilivyokuwa nimepotea sikujuwa nilipokuwa nakwenda na sikujua maisha yangu yatakuwaje baadae. Nilianza kumlilia Mungu sana nikasema napenda kuwa na mahusiano Mazuri na yeye. Hapo tu nilipoamua kumkabidhi yeye maisha yangu yote, ni hapo ndipo nilipoanza kuona mabadiliko mengi sana katika maisha yangu.

      Nimeona jinsi gani Mungu ananipenda sana, ananitakia mema siku zote na jinsi gani hawezi kuniacha niangamie. Sikuweza kuyaona haya yote kwasababu nilikuwa nimefungwa lakini Mungu sasa amenifungua na naweza kuyaona makuu yake mengi katika maisha yangu. Yeye ni kimbilio langu, mwamba wangu, na yeye ni kila kitu katika maisha yangu. Nimempata yeye siwezi kumuacha kamwe. Ushauri wangu kwa wale wote wanaomjua Mungu na kumwabudu. Wamkabidhi yeye pekee maisha yao yote, wafanyapo hivyo tu watayaona makuu na matendo yake ya ajabu katika maisha yao. Yeye atawapigania, atawalinda, atawatendea mema na hatawaacha waangamie kamwe. Mungu ni mwema siku zote”. div dir="ltr" style="text-align: left;" trbidi="on">
      Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy

      By Kalunde Jamal, Mwananchi


      Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), imevifungia kwa miezi mitatu, vituo sita vya televisheni na vingine zaidi ya 20 vya redio hadi pale vitakapolipa ada mbalimbali.

      Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy alivitaja vituo hivyo kuwa ni Star TV, Sumbawanga TV, Tanga TV, Mbeya TV na Mussa Television Network.

      Redio Uhuru, Kiss FM, Redio Free Africa, Breeze FM, Counntry FM, Generation FM, Hot FM, Redio Sengerema, Impact FM, Iringa TV, Rock FM, Kifimbo FM, Sibuka FM, Kili FM, Pop FM, Ulanga FM, Kitulo FM, Standard FM, Pride FM na Huruma Redio.

      Alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya kuwatumia taarifa ya kulipa madeni wanayodaiwa ndani ya mwezi mmoja, Julai 21, mwaka jana, lakini hadi Septemba 28 walikuwa hawajalipa na kutumiwa taarifa nyingine ya kuwataka kufanya hivyo.

      Hata hivyo, Meneja wa Redio Uhuru, Angela Akilimali alisema hawajafungiwa kama inavyoelezwa, bali wamepewa taarifa ya kulipa deni ndani ya miezi mitatu, iwapo hawatalipa deni watakatiwa matangazo.

      “Madeni hayo siyo mapya ni ya zamani hata kabla sijakaa katika nafasi hii nimeyakuta, tutalipa ndani ya miezi hiyo mitatu waliyosema,” alisema.

      Mmiliki wa Sahara Media Group, inayomiliki vituo vya Star Tv, Redio Free Afrika, Anthony Diallo alisema hawajapata taarifa za kudaiwa na mara ya mwisho alipokutana na TCRA aliwalalamikia kuwapa ankara ya malipo kwa dola badala ya shilingi.

      “Hatujapata taarifa rasmi, kama wameita waandishi wa habari wakazungumza nao bila kuwaambia wahusika ambao ni sisi. Wanatuchafulia jina ilhali matatizo ya msingi hawajamaliza,” alisema Diallo.

      Akizungumzia madai hayo, Mungi alisema walitumiwa taarifa ya mara ya pili pamoja na kuwakumbusha kulipa kwa kuwatumia gharama wanazodaiwa huku wakiongezewa muda kabla ya Desemba 31, lakini hakuna aliyelipa.

      Alisema kila kampuni katika hizo zilizotajwa imepelekewa taarifa na wahusika wamesaini kuzipata.

      Kuhusu kupelekewa ankara kwa dola, Mungi alisema sheria ya ankara za malipo ipo hivyo lakini kulipa ni kwa shilingi na kwamba hakuna ambaye aliwahi kukataliwa kulipa kwa sababu hana fedha za kigeni.

      Alisema wataendelea kurusha matangazo lakini; “ikifika saa sita kamili usiku wa kuamkia kesho, vituo vyote nilivyovitaja tutakuwa tumevifungia matangazo, ingawa atakayelipa kabla ya muda huo ataendelea kubaki hewani,” alisema Mungi.
      Katika kile kinachoonekana kwamba serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli haitalegeza kamba linapokuja suala la kusitisha safari holela za nje za watumishi wa umma, Idara ya Uhamiaji imesema bado inakagua uwapo wa barua ya mwajiri na kibali maalum cha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

      Awali, ili kusafiri nje ya nchi mtumishi wa umma alihitaji pasi ya kusafiria yenye viza na tiketi.

      Akizungumza na Nipashe kwa niaba ya Kamishna Mkuu wa Uhamiaji, Sylvester Ambokile, Msemaji wa Idara hiyo Tabu Burhan, alisema idara hiyo inaendelea kusimamia kikamilifu maelekezo ya Rais.

      Katika utekelezaji wa agizo hilo, kila mtumishi wa umma anayesafiri nje ya nchi anatakiwa kuonyesha barua ya mwajiri wake na kibali cha Ikulu, alisema.

      Burhani alisema Idara hiyo inafanya ukaguzi huo katika vituo vya usafiri kama viwanja vya ndege na mipakani ili kubaini watu watakaokiuka kwa makusudi agizo la Rais Magufuli.

      Burhan alisema ingawa kazi ya kuwadhibiti watumishi wa umma wanaosafiri nje ni ngumu kutokana na hati zao za kusafiria kutoonyesha kazi wanazofanya, lakini wamejipanga vizuri kutumia mbinu mbalimbali kuwabaini.

      “Tutawabana wakija kugonga mihuri hati za kusafiria, tukigundua ni mfanyakazi wa serikali tutamuomba atupatie barua kutoka kwa mwajiri na kibali cha Ikulu, kama hana tunamrudisha na hataweza kusafiri,” alisema Burhan.

      Alisema zamani ilikuwa rahisi kwa kila mtumishi aliyetaka kusafiri nje ya nchi kutambulika kazi yake kwasababu walikuwa wakitakiwa kujaza fomu iitwayo TIF 10 na TIF 12, mfumo ambao ulisitishwa mwaka 2005 baada ya kuanza kutumika hati za kusafiria za kieletroniki.

      “Tunawashauri watumishi ambao wanataka kusafiri wajiridhishe wenyewe kwanza, itakuwa usumbufu na hasara endapo tutawarusidisha wakiwa tayari uwanja wa ndege,” aliongeza.

      Akizungumzia idadi ya watu waliozuiliwa tangu kuanza kwa utekelezaji wake, msemaji huyo alisema mpaka sasa hakuna mtumishi aliyenaswa mbali na wafanyakazi wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) ambao tayari wamesimamishwa kazi.

      Watumishi hao ni Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani, Rukia Nikitas na Mary Mosha.

      Agizo la kuwazuia watumishi kusafiri nje lilitolewa na Rais Magufuli siku moja baada ya kuapishwa kwa lengo la kubana matumizi ya serikali na hadi sasa ameshaokoa mabilioni ya fedha.

      Akilihutubia Bunge la 11 na kulizindua mwishoni mwa mwaka jana, Rais Magufuli aliwataka watanzania na wabunge waunge mkono uamuzi wake wa kupiga marufuku safari za nje ambapo fedha nyingi zitaokolewa na kutumika kwenye huduma za jamii kama barabara, afya na elimu.

      Alitoa mfano kuwa katika mwaka wa fedha wa 2013/2013 na nusu ya 2014/2015 pekee, safari za vigogo nje ya nchi ziligharimu Sh. bilioni 356.3 fedha ambazo alisema zingeweza kujenga barabara yenye urefu wa Kilomita 400 au kutimiza miradi mbalimbali ya jamii.

      Alisema tiketi za ndege pekee ziligharimu Sh. bilioni 183.160, mafunzo ya nje ya nchi Sh. bilioni 68.612 na posho za kujikimu Sh. bilioni 104.552.

      Novemba mwaka jana, Ikulu ilisambaza mwongozo unaoweka masharti ambayo watumishi wa umma wanaotaka kusafiri nje ya nchi watatakiwa kuyatimiza ili wapewe kibali cha kusafiri.

      Sharti la kwanza ni kuomba kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue na maombi yawasilishwe kwa Msajili wa Hazina kabla ya kwenda kwa Sefue ili aweze kujenga hoja kwa kuzingatia umuhimu wa safari hiyo na tija itakayopatikana kutokana na safari hiyo.

      Sharti lingine linamtaka Mtendaji Mkuu wa Shirika ama taasisi apime kama safari hiyo ni muhimu kuombewa kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi, kabla ya kuwasilishwa Hazina na aeleze manufaa ambayo nchi itapata kutokana na safari hiyo.

      Pia sharti lingine linataka mhusika aeleze umuhimu wa safari hiyo na isipofanyika itaathiri vipi nchi. Mwombaji aanatakiwa aeleze manufaa ya safari hiyo kwa taasisi na taifa; kama imewahi kufanyika huko nyuma ilisaidia nini.

      Ofisi za Umma zilipokea barua kutoka kwa Msajili wa Hazina Novemba 12 mwaka jana ikieleza kuwa Rais Magufuli ametoa zuio la jumla kwa safari za nje ya nchi katika utumishi wote wa umma na mihimili yake. Barua hiyo ya Hazina ilisema zuio hilo litadumu hadi pale itakavyoelekezwa vinginevyo.
      ===============================================================================
      Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), limesifu kasi ya Rais John Magufuli ya kutumbua majipu, lakini limemwomba ageukie mishahara ya marais wastaafu na kuipunguza hadi nusu ikiwa ni mwendelezo wa hatua zake za kubana matumizi ya fedha za umma.

      Aidha, shirikisho hilo limemtaka Rais Magufuli ajielekeze pia kwenye halmashauri za majiji na miji nchini ambako limesema fedha za miradi ya maendeleo zimegeuzwa hazina mwenyewe.

      Rai hizo zilitolewa na Rais wa TUCTA, Gratian Mukoba katika mazungumzo maalumu na Nipashe, kuhusu masuala mbalimbali ya wafanyakazi na mambo ambayo wanatarajia kutoka kwa Rais Magufuli.

      Mukoba alisema mishahara wanayolipwa sasa marais wastaafu, Alhaji Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete ni mikubwa wakati walishamaliza utumishi wa umma.

      “Rais mstaafu anapata asilimia 80 ya mshahara anaolipwa rais aliye madarakani, sisi TUCTA tunaona huo nao ni ufisadi na tunamuomba Magufuli aipunguze ifike angalau nusu ya mshahara wa Rais aliyeko madarakani,” alisema Mukoba ambaye pia ni rais wa Chama cha Walimu (CWT).

      Hakuna taarifa rasmi kuhusu mshahara wa Rais, hata hivyo.
      Alisema Rais Magufuli pia anapaswa kupunguza mafao makubwa wanayopata viongozi wa kisiasa kama wabunge, ambayo waliyaweka wenyewe wakiangalia maslahi yao binafsi watakapostaafu lakini yamekuwa mzigo mzito kwa walipa kodi.

      Kiinua mgongo cha wabunge baada ya miaka mitano tu ya utumishi ni Sh. milioni 250.

      Mukoba alisema hatua anazochukua Rais Magufuli kwa sasa ni kama utekelezaji wa ushauri wa TUCTA ambao wamekuwa wakiutoa miaka mingi iliyopita, ikiwemo kupunguza safari za nje na misafara isiyo na tija.

      Alisema shirikisho hilo liliishauri serikali ya wamu ya nne kupunguza idadi ya wajumbe wanaosafiri na viongozi kama Rais nchi za nje ili kuokoa fedha za walipa kodi, lakini iliziba masikio.

      “Kasi ya Rais wetu ni nzuri hasa anapobana matumizi ili kufanya vitu vya maana," alisema. "Inatupa moyo kwamba tunakoelekea ni kuzuri zaidi.
      "Ila hatujajua kama kasi hiyo itaendelea hivyo hivyo au itafika wakati itapungua.

      "Magufuli amethibitisha kwamba tunaweza kubana matumizi na kufanya mambo ya maana hilo halina ubishi.”

      Katika kubana matumizi huko, Rais Magufuli aliamuru Sh. bilioni nne zilizokuwa zimetengwa na Hazina kwa matumizi ya sherehe za siku moja ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanganyika, zitumike kupanua km nne za barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini Dar es Salaam.

      Aidha, punde baada ya kuzindua Bunge la 11 mjini Dodoma Novemba mwaka jana, Rais Magufuli aliamuru Sh. milioni 230 kati ya fedha zilizokuwa zimetengwa kwa sherehe hiyo, zikanunue vitanda na mashuka kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

      Tangu aingie madarakani, Rais Magufuli amepiga marufuku safari holela za nje ya nchi kwa watumishi wa serikali.

      Akihutubia katika ufunguzi wa Bunge, Rais Magufuli alisema katika mwaka wa fedha wa 2013/2013 na nusu ya 2014/2015 pekee, safari za vigogo nje ya nchi ziligharimu Sh. bilioni 356.3 fedha ambazo zingeweza kujenga barabara yenye urefu wa Kilomita 400 au kutimiza miradi mbalimbali ya jamii.

      Alisema tiketi za ndege pekee ziligharimu Sh. bilioni 183.160, mafunzo ya nje ya nchi Sh. bilioni 68.612 na posho za kujikimu Sh. bilioni 104.552.

      Mukoba alisifu hatua ya Rais Magufuli kufuta safari nyingi za nje ya nchi alizozielezea kuwa hazikuwa na manufaa kwa nchi na hatua yake ya kupunguza msusuru wa wajumbe waliokuwa wakisafiri na viongozi ughaibuni.

      “Mfano msururu wa viongozi wanakwenda Dubai kwenye mafunzo badala ya kuita wataalamu wawili kutoka huko waje wawafundishe mkiwa hapa hapa ili kubana matumizi," alisema Mukoba.

      "Kwa kweli haya anayofanya Magufuli yametukosha na tunaona anafikiri sawa sawa na sisi maana ndiyo maono yetu ya muda mrefu.”

      Aidha, alisema ni matarajio ya wafanyakazi kwamba Rais Magufuli atapunguza kodi ya mishahara ya wafanyakazi hadi kufikia chini ya asilimia 10 kama ambavyo alikuwa akiahidi kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu uliomwingiza madarakani Oktoba mwaka jana.

      Mukoba alisema mfumuko wa bei na kodi kwenye mishahara umekuwa mzigo mkubwa kwa wafanyakazi, hivyo kupunguzwa kwa kodi kunaweza kuwasababishia unafuu wa maisha wafanyakazi wa sekta mbalimbali.

      Kuhusu majipu ya kwenye Halmashauri na Manispaa, Mukoba alisema ingawa Rais Magufuli amekuwa na kasi nzuri katika kuwashughulikia wakwepa kodi na watendaji wasiowajibika, majipu ambayo hayajatumbuliwa bado ni mengi hasa kwenye halmashauri na manispaa nchini.

      “Majipu ambayo Rais ameyatumbua ni sehemu ndogo tu, bado kuna majipu mengi sana ya kutumbua hasa kwenye halmashauri ambako fedha za walimu zimekuwa zikitafunwa mchana kweupe, huku nako akija ataona mambo ya ovyo ovyo yanayofanywa na viongozi,” alisema Mukoba.

      “Mfano Manispaa ya Kinondoni inakusanya Sh. bilioni 40 kwa mwaka na madai ya walimu ni Sh. milioni 500 tu lakini utashangaa kuona mwaka unaisha lakini hela ya kulipa madai mbalimbali ya walimu hawaitengi.

      "Ndo maana nasema bado kuna majipu mengi sana huku chini... akimaliza juu ashuke ajionee uozo uliopo huku.”

      Mukoba alisema wakurugenzi wengi wa manispaa na halmashauri wameshindwa hata kuwapandisha madaraja walimu tangu mwaka 2013, hali ambayo imewafanya waishi kwa masikitiko na kupunguza ari ya kazi.

      Alisema malimbikizo ya madai mbalimbali ya walimu nchini yamefikia zaidi ya Sh. bilioni 67 hivyo alimuomba Rais Magufuli kuwashinikiza wahusika walipe madeni yote ya walimu kama hatua ya kuwafuta jasho na kurejesha ari ya kazi.

      “Aliahidi kwamba atakuwa rafiki wa wafanyakazi na sisi tunasubiri tuone namna atakavyowajali,” alisema Mukoba ambaye kwa miaka mingi amekuwa akikwaruzana na serikali kuhusu malimbikizo ya malipo ya walimu.

      ==========================================================================



      ===================================================================






      No comments:

      Post a Comment