TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, May 26, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA MASHAURIANO WA BODI YA USAJILI WA MAKANDARASI NCHINI CRB.

Makandarasi 4572 wafutiwa leseni nchini

Bodi ya Usajili wa Makandarasi imefuta usajili wa jumla ya makandarasi 4572 kwa kushindwa kutimiza matakwa ya Sheria ya Usajili wa Makandarasi ya mwaka 1997.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Bw. Rhoben Nkhori wakati wa Mkutano wa Mashauriano wa CRB uliofanyika jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bw. Nkhori amesema kuwa katika jukumu la kuratibu mwenendo wa kazi za makandarasi, Bodi ilikagua miradi 2735. Katika miradi hiyo iliyokaguliwa, miradi 1873 sawa na asilimia 68.5 haikuwa na kasoro.

Ameongeza kuwa miradi mingine ilikuwa na kasoro za kutofanywa na makandarasi waliosajiliwa, kutozingatia usalama wa wafanyakazi, kutokuwa na bango wala uzio na miradi kutosajiliwa. Kwa mujibu wa Bw. Nkhori miradi yote iliyopatikana na upungufu wahusika walichukuliwa hatua mbali mbali kwa mujibu wa sheria.

Aidha, Bwana Nkhori amesema kuwa kwa mwaka jana, Bodi ilisajili miradi 3,172 yenye thamani ya shilingi trilioni4.23. Katika miradi hii asilimia 44.4 ilifanywa na Makandarasi wazawa na asilimia 55.6 ilifanywa na makandarasi wa kigeni.

Licha ya mafanikio hayo CRD ilikumbana changamoto kadhaa ikiwemo kuwasilisha nyaraka za kugushi wakati wa usajili hususani kadi za magari na mitambo, vyeti vya wataalam, kutumia majina ya makandarasi kwa udanganyifu kwa kuuza vibao, waendelezaji kutotoa taarifa sahihi za umiliki kwa Bodi na baadhi ya makandarasi kushindwa kuwalipa wafanyakazi na vifaa vya ujenzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi, Bi Consolata Ngimbwa amemwomba Mhe. Rais John Pombe Magufuli kuwapa kipaumbele Makandarasi wa humu nchini ili kuwawezesha kiuchumi. “Mhe. Rais tunaomba utupe kipaumbele kwani sisi tukipata hiyo miradi tutawekeza hapa nchi na kuongeza soko la ajira,”alisema Bi Ngimbwa.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema serikali yake itawapa kipaumbele makandarasi wazawa lakini akawataka wajipange na kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia maadili ikiwemo kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Mkutano huu pamoja na mamabo mengine utajadili jinsi ya kuwajengea uwezo makandarasi nchini. Kauli mbiu ya Mkutano huo ni “Juhudi za Makusudi za kukuza uwezo wa makandarasi wazawa, changamoto na mustakhabali.” 
 
==========================================================

SERIKALI YAWAPA MIEZI MIWILI WAISHIO KIJJIJI CHA MICHEZO CHANGAMANI KUHAMA.

DAWATI LA MALALAMIKO KUFANYA KAZI MASAA 24 HOSPITALI YA MWANANYAMALA.











 
=============================================

Wenye simu feki watakiwa kubadilisha simu zao kabla ya kuzimwa


Wadau na wateja mbalimbali wanaotumia mtandao wa mawasiliano unaoongoza nchini Vodacom Tanzania,Wanakumbushwa kwamba kununua simu zinazoendana na viwango vya mamlaka ya mawasiliano nchini na kuachana na simu zisizo na viwango vilivyobainishwa na Mamlaka hiyo ili wasiachwe nje ya mtandao tarehe 15 Juni ambayo imetangazwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuwa zoezi hilo la kuzima simu zisizo na viwango litafanyika.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia amesema kuwa Vodacom ikiwa kampuni inayoongoza kwa kuwa na mtandao mkubwa na watumiaji wengi wa mtandao wake inaamini kuwa kuna baadhi ya wateja wake wako hatarini kuachwa nje ya mtandao kutokana na kutokuwa na simu zenye viwango vilivyobainishwa na Mamlaka ya Mawasiliano.

“Natoa wito kwa wateja wetu ambao hadi kufikia sasa hawajaangalia kama simu zao zinakidhi viwango ama wameangalia lakini hawajachukua hatua ya kununua simu zenye viwango vinavyotakiwa wafanye hivyo kwa kuwa umebaki muda wa siku chache kabla ya simu zao kuzimwa na kuwaacha nje ya mtandao” alisema Mworia.

Katika kuhakikisha wateja wake hawaachwi nje ya mtandao alisema kuwa Vodacom kwa kushirikiana na wadau wanaotengeneza simu tayari imeingiza simu zenye kiwango cha ubora na gharama nafuu nchini ambazo zinapatikana katika maduka yake yaliyopo sehemu mbalimbali nchini.

“Tusingependa wateja wetu waachwe nje ya mfumo wa mawasiliano na kukosa huduma za mawasiliano hivyo tutaendelea kufanya kazi na serikali na taasisi nyingine za mawasiliano kuhakikisha watanzania wanaendelea kupata huduma bora za mawasiliano. Simu zenye viwango na zenye gharama nafuu kuanzia shilingi 18,000/= na kuendelea zinapatikana kwenye Maduka yetu yalioyosambaa kote nchini ” alisema. 
====================================================

MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA MWANAHABARI MAKONGORO OGING' KUZIKWA MKOANI MARA KESHO KUTWA.

 
=================================================

ESRF yafanya warsha kujadili Mpango wa Maendeleo Endelevu (SDG)




DSC_2311
DSC_2330
 

No comments:

Post a Comment