TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, May 14, 2016

WAZIRI MWIGULU ATOA HOJA YA KUIDHINISHIWA KWA BAJETI YA 2016/2017 MBELE YA MWALIMU WAKE WA DARASA LA KWANZA.

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akitoa hoja kwa Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma huku akishudiwa na mwalimu wake Maria Mnkumbo (hayupo pichani) aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida.(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma)
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na mwalimu wake Maria Mnkumbo (katikati) aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya waziri huyo kutoa hoja ya Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma. Kushoto ni mke wa Waziri Mwigulu Neema.
Mwalimu msataafu Maria Mnkumbo aliyemfundisha Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma.Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba akiwa na mwalimu wake Maria Mnkumbo aliyemfundisha darasa la kwanza na la pili katika shule ya msingi Makunda iliyopo wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya waziri huyo kutoa hoja ya Bunge kuidhinisha makadirio na matumizi ya fedha ya wizara yake kwa mwaka 2016/2017 leo mjini Dodoma.

Benki ya Exim yazindua kampeni kuhamasisha huduma bora kwa wateja


SHILINGI BILIONI 8 KUTUMIKA KWA RUZUKU YA WACHIMBAJI WADOGO.







MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA), YAAZIMISHA SHEREHE ZA KODI JIJINI DAR ES SALAAM.


Sehemu ya wadau mbalimbali waliohudhuria hizo wakimsikiliza Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro kwenye sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016. Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Victor Kimaro (wa kwanza kushoto) akizugumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) juu ya uwezo wao wa kumudu ukusanyaji wa kodi vizuri ili waweze kufanikisha vizuri malengo waliyo jiwekea mwaka huu. Pia aliwashukuru (ITA) kwa kujitolea kutoa elimu kwa wawekezaji wote wanaofika hapa nchini iliwaweze kulipa kodi wanapo wekekeza hapa nchini. alizungumza hayo Siku ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya kodi zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano (TRA) Mwenge jijini Dar es Salaam 2016.

TIB Corporate Bank yadhamini mkutano mkuu wa Bodi ya usajili wa Wakandarasi nchini







Serikali itaendelea kusimamia haki ya mtoto wa kike ya kupata elimu










MBUNGE COSATO CHUMI AMBWAGA MPINZANIA WAKE KESI YA UCHAGUZI










TAASISI YA MISAADA YA KIJAMII YA HAMISI KIGWANGALLA KUMSOMESHA GETRUDE CLEMENT

a32603a8-b5b0-41d7-8533-7baf03333277




ce18d8f2-cd50-4b46-8193-3351745537ac

 

MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BIMA NCHINI (TIRA) YAKUTANA NA WADAU WAKE JIJINI MBEYA .

Picha ya Pamoja Meza kuu na washiriki wa semina hiyo.

BENKI YA KILIMO YATOA MKOPO WA 890MILIONI KWA WAKULIMA WA WILAYA YA KILOMBERO

CHAMA CHA WALIMU CWT WILAYA YA RUFIJI CHAMVAMIA MKURUGENZI KIKAONI KUDAI MALIMBIKIZO YA MADAI YAO

LAPF YAKABIDHI MADAWATI YA SHILINGI MILIONI KUMI KWA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI

WADAU WAJADILI TOZO DARAJA LA NYERERE

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Joseph Nyamhanga amewataka watumiaji wa Daraja la Nyerere (Kigamboni) kuzingatia matumizi bora na sahihi ya daraja hilo ikiwemo usafi ili kuliwezesha kukidhi matarajio ya serikali na kudumu kwa muda mrefu.

Akizungumza katika kikao maalum cha wadau kutathimini viwango vya tozo vitakavyotumiwa katika daraja hilo Eng. Nyamhanga amewataka waendeshaji wa daraja hilo Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuimarisha huduma ya ulinzi na usalama na kuwataka watumiaji wa daraja hilo kutumia fursa za uwepo wake kiuchumi na kijamii.

“Hakikisheni tozo zitakazowekwa ziwiane na hali ya maisha ya wananchi ili kuwavutia wengi kupita katika daraja hili na kupunguza msongamano katika vivuko”, amesema Eng. Nyamhanga.Tozo hizo ambazo zitaanza kutozwa kwa watumiaji wa Daraja la Nyerere hivi karibuni zinalenga kuwezesha NSSF kurudisha gharama za uwekezaji katika daraja hilo.

Aidha, Katibu Mkuu huyo amesema hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuhujumu miundombinu na kukemea vitendo vya watu kufanya biashara katika daraja hilo.Naye Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyarara amesema tozo kwa watumiaji wa Daraja la Nyerere itaanza hivi karibuni baada ya kupitishwa na Waziri mwenye dhamana ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, hivyo amewataka watumiaji wa daraja hilo kutoa ushirikiano kwa watendaji ili kuwezesha huduma kufanyika kama ilivyokusudiwa.

“Tumejipanga Vizuri na tutaanza kutoza watumiaji wa Daraja la Nyerere muda mfupi kuanzia sasa.” amesema Prof. Kahyarara.Zaidi ya shilingi Bilioni 214 zimetumika katika ujenzi wa Daraja la Nyerere ambapo asilimia 60 zimegharamiwa na NSSF na asilimia 40 zimegharamiwa na Serikali Kuu.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Eng. Joseph Nyamhanga (katikati) akitoa ufafanuzi kwa wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji katika kikao cha kujadili viwango vya tozo zitakazotumika katika Daraja la Nyerere (Kigamboni). Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof Godius Kahyarara na kushoto ni Mkurugenzi wa barabara (Ujenzi) Eng. Ven Ndyamukama.

Mkurugenzi wa Barabara Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Ven Ndyamukama (Kushoto) akifafanua jambo katika kikao cha wadau kujadili tozo za matumizi ya Daraja la Nyerere (Kigamboni). Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawsiliano Eng, Joseph Nyamhanga
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Prof. Godius Kahyarara (kulia) akitoa taarifa ya namna tozo zitakavyokusanywa kwa wadau mbalimbali wanaotumia Daraja la Nyerere zoezi litakaloanza hivi karibuni.

Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Baiskeli akitoa maoni ya namna ya kuwahudumia waendesha baiskeli katika kikao cha kujadili tozo zitakazotumika kataka Daraja la Nyerere.
Wadau wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kujadili tozo zitakazotumika katika Daraja la Nyerere, Tozo hizo zitatangazwa hivi karibuni.

BODI YA FILAMU YASITISHA USAMBAZAJI WA “IMEBUMA”








 

No comments:

Post a Comment