TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, September 26, 2011

Waliosoma Kusini waaswa kuchangia elimu

Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Jimbo la Lindi Mjini, Salum Baruany amewashauri watu waliowahi kusoma katika mikoa ya Kusini mwa Tanzania kushirikiana katika kufanikisha tamasha la kuchangia maendeleo ya elimu kwa ajili ya mikoa hiyo.
Baruany aliyasema hayo juzi katika kikao cha maandalizi ya tamasha la kuchangia maendeleo ya elimu kwa mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma kilichofanyika Ukumbi wa Imasco, Temeke jijini Dar es Salaam.
Akiwa mmoja wa waalikwa wa vikao hivyo vya kila wiki, Baruany alielezea kukunwa kwake na ubunifu wa baadhi ya wanafunzi walioamua kuwahamasisha wenzao kukumbuka walikotoka kielimu, kwa lengo la kuwainua wengine.
“Nawapongeza sana. Ni wachache wanaoweza kukumbuka walikotoka, hasa kielimu. Hapa mmelenga, mikoa ya kusini iko nyuma kielimu, naamini wa kusaidia kupandisha hadhi ni ninyi wenyewe mliosoma kule na wadau wengine wanaoguswa na suala hili.
“Msikate tamaa, mtafanikiwa. Cha msingi ni kuwashirikisha na kuwashawishi wengine waliosoma ana kuwa karibu na mazingira ya kielimu ya mikoa hii. Nchi hujengwa na wananchi wenye moyo, nanyi kwa kuguswa kwenu, naamini elimu ya kusini itainuka kwa sababu ni vigumu mtu mmoja mmoja kuchangia na bado maendeleo ya kweli yakaonekana, bali kupitia mshikamano kama wenu,” alisema mbunge huyo.
Naye Mratibu wa tamasha hilo, Asanterabbi Mtaki, licha ya kumshukuru mbunge huyo kwa nasaha zake, aliwataka wadau wa elimu nchini kuungana na waliosoma mikoa ya kusini ili kufanikisha azma ya kuiinua kusini kielimu.
“Tangu awali tumeelezea hali ya elimu ya mikoa ya Kusini, kwa kweli si nzuri na inahitajika nguvu ya ziada, ndiyo maana tumeungana kuhakikisha tunafanikisha kitu kwa ajili ya shule za kusini na wanafunzi wake, hasa yatima, walemavu na wasiojiweza ili wapate haki ya kupata elimu bora,” alisema Mtaki.
Alisisitiza kuwa, kasi ya maandalizi ya tamasha hilo inaridhisha na kuongeza kuwa, nafasi ya waliosoma kusini kuchangia mawazo bado ipo, hasa kupitia vikao vya kila mwisho wa wiki vinavyofanyika ukumbi wa Imasco.

Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Mohamed Mpinga (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo baada ya kupatiwa na TBL msaada wa fulana na kofia vyenye thamani ya sh. mil. 10 kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama yatakayofanyika mkoani Kagera kuanzia Oktoba 3-8, mwaka huu. Hafla hiyo ilifanyika Dar es Salaam juzi.
 

Na Gladness Mushi, Arusha Taasisi ya maendeleo ya jamii hapa nchini (CDTF) imefanikiwa kutoa msaada wa kimaendeleo, ambapo imechangia zaidi ya milioni 43 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mawili pamoja na ofisi ya walimu wa shule ya walemavu iliopo katika eneo la Ilboru Mjini hapa Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukabidhi vyumba hivyo vya madarasa pamoja na ofisi ya walimu ambayo itatumika kwa watoto hao ambao ni walemavu Mkurugenzi wa taasisi hiyo Bw Hendry Mgingi alisema kuwa watoto ambao ni walemavu kwa kuwa nao wana nafasi kubwa sana ndani ya jamii ya watanzania aidha aliendelea kusema kuwa wao kama taasisi ya maendeleo wamefikia uamuzi huo mara baada ya kuona kuwa watoto ambao ni walemavu wana nafasi kubwa sana ya kuweza kusaidika hata kama wanaulemavu wa aina mbalimbali. aliongeza kuwa kama jamii ya watanzania itaweza kuwasaidia watoto hao ambao ni walemavu basi wataweza kufanya hata idadi ya wanafunzi ambao wana ujuzi mbalimbali kuongezeka kwa hali ya juu sana hapa nchini. "unajua endapo kama baadhi ya taasisi zitaweza kuona mchango ambao wanao hawa watoto walemavu basi hawa watoto wataweza kukua kwa kiwango cha hali ya juu sana na hata kama hawataweza kufanya kazi ngumu basi wanaweza kufanya kazi ambao ni raisi na hivvyo kusaidia jamii katika kutatua tatizo la ajira"aliongeza Bw Hendry hataivyo alisema kuwa walemavu wanaweza kuibua mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuweza kutengeneza ajira ambazo zimo kwenye jamii kwa kuwa mpaka sasa baadhi ya walemavu wameonekana kuwa wabunifu wa hali ya juu sana. alisisitiza kuwa ubunifu huo ambao wanao baadhi ya walemavu utaenda sanjari na upokeaji wa vipaji kutoka kwa walemavu hao ambapo kama jamii ya leo itaweza kuwasaidia ni wazi kuwa kazi mbalimbali za walemavu zitakubalika na jamii ya watanzania. 'leo kuna baadhi ya walemavu ambao wapo tu lakini cha ajabu ni kwamba bado hawajaweza kusaidika lakini huu ndio wakati muafaka wa kila mwananchi kuweza kuwasaidia hawa walemavu kwa kuwa kwa kutowasaidia basi asilimia kubwa ya walemavu hao wanashindwa kutimiza ndoto za kuondokana na umaskini"alisema Bw Hendry. Alimalizia kwa kusema kuwa walemavu hao wanatakiwa kuhakikisha kuwa elimu ambayo wanapata wanaitumia vema katika kazi zao na masomo kwa kuwa ili napo waweze kufanikiwa ni lazima kwanza kuwepo na mipango mikakati ya elimu bora.

Maandali ya kuujenga Mkoa mpya wa Njombe

Mabweni ya wanafunzi
Jamii maskini kwa kawaida huwa na vipaumbele vingi. Matokeo yake ni kushindwa kuvitekeleza. Wananchi wa mkoa mpya wa Njombe ambao ni wachapa kazi kweli kweli wameikataa falsafa hiyo na wamejiwekea vipaumbele vichache na vya uhakika ili kuujenga mkoa wao. Vipaumbe vya wananjombe ni:
1. Elimu- Kwa kujitolea wananchi wa vijiji na kata za Katulila, Madobole, Miva, Lusitu, Mtila, Mbega, Matola, Luponde, Itulike, Ramadhani, Kihesa, Utalingolo, Ihalula, Nolle, Mamongoro, Makowo, Ng’elamo, Yakobi, Igominyi, Idunda, Idihani, Lugenge na Kiyaula wameamua kujikita katika suala zima la elimu kwa shule za awali, msingi na sekondari. Majenfo mzuri ya ya kisasa yako katika hatua mbali mbali. Ombi lao ni waalimu wa kutosha.
2. Afya: Ili kuimarisha afya wananchi hao wako katika mpango wa kuwa na zahanati katika kila kata. Tayari kwa kujitolea wameanza ujenzi wa zahanati hizo. Ombi lao ni kupatiwa wauguzi wa kutosha.
3. Kilimo: kutokana na hali ya hewa nzuri ya nyanda za juu kusini, wananjombe hawa wamejizatiti katika kilimo cha chai, mahindi, viazi mviringo na misitu ya mbao.
4. Miundombinu: kwa sehemu kubwa wananjombe wamejitahidi sana kutengeneza barabara za ndani na wanaamini ni kwa barabara nzuri wataweza kufaidika na fursa zitokanazo na migodi ya machimbo ya chuma na mkaa wa mawe ya Mchuchuma na Liganga
Kilimo cha chai Njombe
Ujenzi wa zahanati
Ujenzi wa kituo cha Afya

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohammed Shein jana amefanya uteuzi wa nyadhifa mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk Abdulhamid Yahya Mzee Rais amewateuwa Sheikh Saleh Omar Kabhi kuwa Mufti Mkuu wa Zanzibar,Sheikh Khamis Haji Khamis kuwa Kadhi Mkuu wa Zanzibar ambapo Sheikh Hassan Othman Ngwali kuwa Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar.
Aidha Dk Shein amemteuwa Muumin Khamis Kombo kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka Zanzibar,Khalifa Hassan Choum kuwa Kamishna wa Vyuo vya Mafunzo Zanzibar, Abdulrahman Mwinyi Jumbe kuwa Mshauri wa Rais Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi .Pia Mwinyi Jumbe ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Watu wa Zanzibar.
Vile vile Rais amewateuwa Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa kuwa Mshauri wake katika mambo ya Ushirikiano wa Kimataifa na Uwekezaji. Ramia aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Sweden na India pia alikamata nafasi mbali mbali za Uwaziri katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Burhani Saadati Haji ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makaazi. Kabla ya Uteuzi huo Burhani aliwahi kuwa Waziri wa Kilimo pia Waziri wa Ardhi,Maji na Nishati.Pia Dk Shein amemteuwa Issa Ahmed Othman kuwa Mshauri wa Rais Utalii. Issa aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar.
Uteuzi huo unaanza juzi

Pichani Juu na Chini Mgeni rasmi Hoyce Temu akiwapa risala wahitimu wa kidato cha IV katika shule ya Cambridge. Hoyce aliwasihi wahitimu hao kuhakikisha kuwa wanafanya mitihani yao kwa utulivu na kujiamini sambamba na kuwasisitiza kuchagua masomo yenye masoko katika ajira na kujiendeleza binafsi. Aidha aliwaomba wazazi na walezi kuwasaidia vijana hao katika safari yao ya Maisha na kuwataka kuwa wavumilivu wakati wote ili waweze kufikia mafanikio.
Mwanafunzi Monica Mwaipopo akipokea cheti kutoka kwa mgeni rasmi Hoyce Temu cha kufanya vizuri katika taaluma na Vilabu Shuleni hapo.
Wahitimu wa Kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Cambridge wakiingia rasmi katika sherehe za mahafali yao kwa wimbo maalum. Sherehe hizo zilifanyika Shuleni hapo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali pamoja na ndugu na jamaa.
JAPO NI KIDOGO TUNAKUOMBA UZIWASILISHE KWA SESILIA, ndivyo anavyosema Meneja wa Shule ya Sekondari Cambridge Bi. Laura Mataita wakati akimakabidhi mgeni rasmi na Mwendeshaji wa kipindi cha Mimi na Tanzania Bi. Hoyce Temu.
Umati wa wageni waalikwa, walezi na wazazi waliohudhuria mahafali hayo ya kumi na moja shuleni hapo.
Meneja wa Shule ya Sekondari Cambridge Bi. Laura Mataita akihamisha uchangiaji wa fedha za Mtoto Sesilia Edward ambaye anasumbuliwa na maradhi ya moyo anayetarajiwa kupelekwa nchini India kwa ajili ya matibabu. Mtoto Sesilia aligundulika kufuatia kipindi cha Mimi na Tanzania kinachorushwa na Channeli Ten na kuendeshwa na Hoyce Temu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya shule hiyo.
 

Hatimaye lile shindano la kumsaka mlimbwende wa mkoa wa Mara katika maswala ya utalii, litafanyika Ijumaa ya tarehe 07/10/2011, katika ukumbi wa Bwalo la Magereza mjini Musoma, ambapo takriban warembo 15 watapanda jukwaa moja kuchuana kumpata muakilishi wa mkoa katika mashindano yan Miss Tourism Lake Zone yatakayofanyika baadae mwezi december. Kampuni ya Stoppers Entertainment inayoandaa mashindano hayo, imejipanga kuyapa hadhi mashindano hayo ambapo warembo mbali na kupita jukwaani, watashiriki katika shughuli za kijamii, kuimba na kucheza ngoma za makabila ya mkoa wa Mara. Hata hivyo waandaji wamewaomba wadhamini kuendelea kujitokeza kudhamini shindano hilo, kutokana na kugusa utalii, utamaduni na uchumi wa nchi yetu, yote kwa minaajili ya kuitangaza Tanzania. Shindano la Miss Tourism Mara 2011, litasindikizwa na burudani kutoka kwa Ditto na Linah wote kutoka jumba la vipaji THT. Pia burudani za ngoma za asili zitakuwepo.

Na Mwandishi wetu
TIMU ya Leaders Club imeisambaratisha timu ya Bongo Movie bao 1-0 katika mchezo maalum wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja wa Leaders Club jana.
Mchezo huo ulikuwa mkali na wa kusisimua kutokana na wachezaji wote kuonyesha viwango vya hali ya juu.
Leaders Club ikiongozwa na Doyi Moke, Adam Sapi, Christopher Semi, Baraka, Makoye, Juma Pinto, Idd Janguo, Abdul Tall, Michael, Kibwana Matephone na Charles Nyarusi walitawala mchezo huo ambao ulivuta mashabiki wengi kutoka kona mbali mbali za jiji.
Bongo Movie iliongozwa na Jacob Steve, (JB), Masoud Bitebo, Steven Nyerere na Vincent Kigosi ‘Ray’ ilishindwa kumudu kasi ya timu ya Leaders.
Baada ya kosa kosa nyingi, Leaders Club ilipachika bao la ushindi kupitia kwa Juma Tall kufutia ushirikiano mzuri na Adam Sapi na Juma Pinto.
Bao hilo liliwachangaya zaidi Bongo Movie ambao walipoteza ‘network’ uwanjani na kuanza kumvamia mwamuzi kila wakati wanapocheza faulo.
Tofauti na mchezo wa soka, mchezo huo ulionekana kuwa wa upande mmoja zaidi kutokana na uwezo mkubwa wa Leaders Club.
Baada ya mchezo, timu ya Bongo Movie iliondoka mapema uwanjani hapo tofauti na awali kwani mara kadhaa huwa wanadumu uwanjani hapo kwa vinywaji na vitafunwa vingine.

AFISA Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Elias Msese akitoa maelezo kuhusiana na miradi ya nyumba inayoendeshwa na shirika hilo kwa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, Ardhi, Maliasili na Mazingira Abdulkarim Shah, katika viwanja vya Mashujaa vya Mnazi Mmoja kabla ya kufunga maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi jana. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Shirika hilo, Suzan Omari. (Na Magreth Kinabo - Maelezo ).

Na mwandishi wetu
WANAFUNZI wametakiwa kusoma kwa bidii ili kupata ujuzi na maarifa yatakayowawezesha kumudu ushindani katika soko la ajira katika ukanda wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC).
Pia, wameaswa kuacha kuiga tabia na tamaduni za kigeni ambazo mwisho wake zinaweza kuwaingiza kwenye vitendo vya kihuni ikiwemo uvutaji bangi.
Wito huo umetolewa jana na Meneja Utawala na Utumishi wa Kampuni ya Uhuru Publications Ltd, wachapishaji wa magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani, Lucas Kisasa, wakati akizungumzia kwenye mahafali ya wanafunzi wa kidato cha nne katika Sekondari ya Actas, iliyopo Mbezi, Dar es Salaam.
Alisema kuwa soko la ajira kwa nchi wanachama wa EAC limekuwa na changamoto kubwa na kwamba, wanafunzi hasa vijana hawana budi kusoma kwa bidii ili kutoa upinzani kwa wenzao.
“Hakuna muda wa kupoteza kwa sasa, mnapaswa kusoma kwa bidii na maarifa ili kuweza kumudu upinzani katika soko la ajira. Hakikisheni mnafany vizuri kwenye masomo ili muweze kupata nafasi na kutumia fursa za ajira kwenye soko la jumuia yetu,” alisema Kisasa.
Pia, Kisasa alikemea tabia za baadhi ya vijana kuiga tamaduni za kigeni, ambazo zinakwenda kinyume na maadili ya Mtanzania.
Alisema kuwa uigaji huo umekuwa na madhara makubwa kwa vijana kutokana na wengi kujikuta wameangukia kwenye matendo ya kuhuni ikiwemo uvutaji wa bangi, ukahaba hivyo hawana budi kuwa makini.
Katika mahafali hayo ambayo ni ya tatu tangu kuanzishwa kwa shule hiyo, Kisasa alikabidhi vyeti kwa wahitimu 264 kati yao wasichana wakiwa 147 na 117 ni wavulana.
Mahafali hayo yalihudhuriwa na wazazi, walezi, wageni mbalimbali na majirani wanaozunguka shuleni hapo na wanafunzi, ambapo yalifana vilivyo kwa kupambwa na burudani za kila aina.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimshukuru Mbunge wa Rorya, Lameck Airo kwa kutoa mchango wa zaidi ya shilingi milioni 530 kwa shughuli mblaimbali za maendeleokwenye jimbo lake wakati alipozungumza na wananchi kwenye shamba la umwagiliaji la mpunga la Irienyi wilayni Roraya akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara Septemba 22, 2011.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizindua mradi wa umwagiliaji wa kilimo cha mpunga katika kijiji cha Irienyi wilayani Rorya akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara Septemba 22,2011.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
WIZARA YA Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imejipanga kwa makini ili kuhakikisha kuwa maeneo yote ya wazi yanarudishwa kwa wananchi ambapo matumizi yake yatakuwa kwa manufaa ya watanzania wote.
Aidha wizara hiyo imesema kuwa itatoa muda maalum kwa watu wote walivamia maeneo hayo kuondoka wenyewe na utakapokwisha muda uliopangwa itakuja kubomoa hivyo hakutakuwa na msamaha.(hakuna cha msalie mtume).
Kauli hiyo ilitolewa (leo) na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi na Maliasili na Mazingira, Abdulkarim Shah, wakati akifunga maonesho ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara ya wizara hiyo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mashujaa, Mnazimmoja, jijini Dares Salaam.
Shah alitoa kauli hiyo ikiwa ni matazamio ya miaka 50 ijayo ya wizara hiyo huku akisema maeneo hayo yamepangwa kwa faida ya wananchi wote.
“Napenda kusisitiza kwamba taaluma ya upangaji miji inahitajika kutiliwa maanani na serikali haitakubali mipango hiyo kubadilishwa matumizi kiholela. Natoa rai hii kwa jamii kushirikiana na serikali kulinda maeneo ya wazi yaliyoko katika maeneo yao,” alisema Shah.
Aliwataka watendaji husika hasa wa halimashauri kutobalidilisha matumizi ya ardhi .
Aliongeza kuwa wizara hiyo imeandaa mikakati ya kuwa na mipango shahidi ya uendelezaji miji itakayokidhi mahitaji ya idadi kubwa zaidi ya watu watakaoishi mijini.
Pia kuwa na mipango itakayowezesha ujenzi wa miji nadhifu, ya kisasa na endelevu,kuzijengea uwezo halimashauri kusimamia na kudhibiti uendelezaji wa miji na kuwa na mipango ya matumizi ya ardhi kwa kila eneo la makazi nchini.
“ Wizara imedhamiria kuongeza kasi ya upimaji wa ardhi nchini kwa matumizi mbalimbali pamoja na kupunguza gharama za upimaji, ambapo nchi itakuwa imejenga kituo cha kupokea na kusambaza picha za saltillite, vituo vingi zaidi cha upimaji vitajengwa,” alisema.
Makamu Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa wizara hiyo itaanza kutunza kumbukumbu za upimaji na ramani kwa kutumia teknolojia ya kisasa, ambapo sasa inatumika mikoa 15 baadae itakuwa mikoa yote hadi wilayani kulingana na uwezo wa bajeti.
Alisema ili kuwawezesha wananchi kutumia ardhi kama mtaji wizara itahakikisha kuwa mashamba ya wananchi vijijini kote nchini yanabainishwa yanapimwa na wamiliki wake wanapewa hatimiliki za kimila.
Alisema kwa upande wa Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) limejipanga kujenga nyumba 150,000 katika kipindi cha miaka 50 ijayo na kujenga nyumba kwa ubia kwa kuwashirikisha wawekezaji wengine.

Rais Jakaya Kikwete akiongea na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Bernard Membe na maofisa wengine leo wakati
akiondoka New York kurejea nyumbani baada ya kuhitimisha ziara yake ya Marekani ambapo alihudhuria mkutano wa 66 wa Umoja wa Mataifa na wa Diapora jijini New York na Virginia, Washington DC.
Picha na Ikulu
Rais Jakaya Kikwete akiagana na Mbunge wa Bukombe Profesa Kahigi huku Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii wa Zanzibar Mh Juma Duni Haji akiangalia leo wakati
akiondoka New York kurejea nyumbani baada ya kuhitimisha ziara yake ya Marekani ambapo alihudhuria mkutano wa 66 wa Umoja wa Mataifa na wa Diapora jijini New York na Virginia, Washington DC.

IMBA YASHINDA 1-0 DHIDI YA MTIBWA SUGAR YA MANUNGU

Mshambuliaji wa timu ya Simba Emmanuel Okwi akishangilia huku akiwa amembeba mchezaji mwenzake Amri Kiemba, mara baada ya kufunga goli dhidi ya timu ya Mtibwa Sugar ambao mpaka mpira unakwisha hawakupata goli, katika mchezo wa ligi kuu uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa jioni ya leo mpira umekwisha na Simba wameshinda goli 1-0. Ulikuwa ni mchezo mgumu kwa pande zote kwani wamekuwa wakishabuliana na kukosa magoli mara nyingi pande zote huku magolikipa wakijitahidi kuzuia mipira ya hatari. Simba wamepata penati dakika za nyongeza hata hivyo beki wa timu hiyo Victor Costa amekosa penati hiyo baada ya golikipa wa timu ya Mtibwa Sugar Dida kupangua mpira huo.
KIjana Mpondela ambaye amevaa skafu nyekundu katikati akishangilia kwa nguvu na mashabiki wenzake wakati timu ya simba ilipopata goli la kuongoza dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mchezaji Emmanuel Okwi wa Simba akikokota mpira mbele ya mabeki wa timu ya Mtibwa Sugar kabla ya kufunga goli katika mpambano huo.
Mchezaji wa Simba Gervas Kago akiongoza wenzake wakati wachezaji hao walipokuwa wakisalimiana kabla ya kuanza kwa mchezo huo.
Kikosi cha Timu ya Mtibwa Sugar katika picha ya pamoja.
Kikosi cha Timu ya Simba katika picha ya pamoja.

Sunday, September 25, 2011

BONANZA LA UJIRANI MWEMA STAKISHARI LEO

Timu ambazo tayari zimefika ni pamoja na Kitunda na Ulongoni ambazo mchezo unaendelea, Mbagala ambayo itaingia uwanjani muda mfupi kucheza na timu ya Makangalawe kabla ya Timu za Tabata dhidi ya Vituka kuinmgia kupepetana, mchezo mwingine ambao unatazamiwa kuwa mkali kutokana na Timu Mwenyeji ambao ni Staki shari kuikaribisha Timu ya Wadhamini Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) kUPITIA KINYWAJI CHAKE CHA KILIMANJARO.

Michezo Mingine itakayofuatia ni kati ya Timu za Kunduchi, Charambe, Bandari, Kigamboni, Skopioni, na Vingunguti 

Kwamujibu wa Waandaji wa Mashindano hayo Meneja Emmanuel Urembo amesema kuwa Kila Timu imepangwa kucheza mchezo mmoja kutokana na kubanwa na Ratiba ya mashindano na Mshindi wa Kila mchezo atapatiwa zawadi kutoka kwa wadhamini wa michezo hiyo

Lengo kubwa la mashindano ni kuimarisha wachezaji wa zamani, kuimarisha na kukuza vipaji vya wanamichezo kupitia wachezaji hao ambao kutokana na kutambua Soka ni chachu ya kupatikana kwa wachezaji ikiwa ni sehemu ya Burudani kutokana namajukumu ya kila siku.

Mchezo uliopo Dimbani kwa sasa Timu ya Ulongoni Inaongoza kwa Mabao 3-0 ambayo yamepachikwa kipindi cha kwanza na bado mpira Unaendelea isipokuwa mchezo ni mzuri na timu zote zinashambuliana kwa zamu.









Saturday, September 24, 2011

Rais wa Zambia akubali kushindwa

Rais wa Zambia Rupiah Banda amekubali kushindwa kwake na kiongozi wa upinzani Michael Sata.
Bw Sata, aliyegombea urais mara nne, alitangazwa kuwa mshindi usiku baada ya kupata asilimia 43 ya kura zote.
"Watu wa Zambia wamezungumza na lazima sote tusikilize," Bw Banda aliwaambia waandishi wa habari, huku akifuta machozi baada ya kumaliza kutoa hotuba yake.
Chama chake cha Movement for Multiparty Democracy kimeongoza Zambia kwa miaka 20.
"Nikizungumza kwa nafsi yangu na chama changu, tunakubali matokeo. Sisi ni chama cha kidemokrasia na hakuna namna nyingine yeyote ile," Bw Banda alisema.
Siku ya Alhamis, kulikuwa na ghasia eneo la kaskazini lenye migodi zilizofanywa na wanaounga mkono upinzani wakiwa hawana subra na matokeo ya Jumanne.
Matokeo hayo yalitangazwa huku majimbo saba yakiwa bado kura zao kuhesabiwa, lakini maafisa wa uchaguzi wamesema Bw Banda hatoweza kumfikia Bw Sata.
Mwandishi wa BBC Louise Redvers kwenye mji mkuu, Lusaka, alisema kuhusu tangazo hilo, wasiwasi uliogubika matokeo hayo ulisababisha makelele huku wafuasi wa Patriotic Front wakishangilia ushindi wao.
Maelfu ya watu walifurika nje ya geti lenye ulinzi mkali wakipiga ngoma, wakipiga honi na kupeperusha bendera.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal akizungumza na Rais Mstaafu wa Zambia,Mh. Ruphia Banda kwenye ofisi za Mahakama Kuu ya Zambia wakati wa sherehe ya kuapishwa Rais Mpya wa Nchi hiyo Michael Sata zilizofanyika jana mjini Lusaka Zambia.
(Picha na Amour Nassor VPO).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal akizungumza na Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini,John Tendwa kwenye sherehe ya kuapishwa Rais mpya wa Zambia Michael Sata mjini Lusaka jana
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal (wa pili kulia), Mama Asha Bilal (kulia) na Rais mstaafu wa Zambia Ruphia Banda, wakimsikiliza Rais mpya wa Zambia Michael Sata alipokuwa akijitambulisha kwa viongozi wakuu wa Nchi mbalimbali waliohudhuria kwenye sherehe ya kuapishwa kwake iliyofanyika jana katika Mahakama Kuu ya Nchi hiyo mjini Lusaka Zambia
katikati ni Mama Asha Bilal.Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia) na mkewe Mama Asha Bilal (wa pili kushoto), Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini John Tendwa (kushoto) na Rais wa kwanza wa Zambia,Dkt. Keneth Kaunda wakiwa katika picha ya pamoja walipokutana kwenye sherehe ya kuapishwa Rais mpya wa Zambia Michael Sata iliyofanyika jana katika Mahakama Kuu ya Nchi hiyo mjini Lusaka Zambia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Mohammed Gharib Bilala akisalimiana na Rais wa Malawi,Bingu wa Mutharika walipokutana kwenye Ofisi za Mahakama Kuu mjini Lusaka Zambia jana wakati wa sherehe ya kuapishwa Rais mpya wa Zambia Michael Sata

TUKIO LA MADEREVA WA MBEYA KUGOMEA TOCHI NYINGI BARABARANI KULIKONI!

Madereva wa Mabasi na Matrafiki katika Stand kuu - Mbeya.
Tukio la Madereva wa Mabasi ya masafa marefu kutoka Mbeya kugoma kuendesha mabasi yao kwa kulalamikia 'TOCHI' nyingi barabarani limenishangaza sana, kwa faida ya wasioelewa, TOCHI ni Kamera za usalama barabarani zinazotumiwa na Matrafiki kuangalia magari yanayokwenda mwendo wa kasi katika eneo ambalo hawastahili kwenda mwendo huo.
KAPINGAZ Blog inapata shaka kidogo, ni kweli hao Madereva wanagomea TOCHI! au kuna kitu kingine Chini ya kapeti? nadhani wao madereva wanalijua hili. Wosia wangu, kama Madereva wanagomea TOCHI kama TOCHI isitende kazi yake, nitapingana nao kwa asilimia 100; ila kama kuna lingine nje ya hapo nawasapoti vile vile kwa asilimia hizo hizo.
"TAFADHALINI, TAIFA BADO LINAZIHITAJI NGUVU HIZI ZA WATANZANIA WANAOPOTEA KILA SIKU KWENYE AJALI AMBAZO NYINGI ZINASABABISHWA NA UZEMBE"

Tumepokea ombi la kusogeza mbele kwa siku moja mechi iliyotajwa hapo kutokana na Uwanja wa CCM Kirumba kuwa awali ulikuwa umeombwa kwa ajili ya shughuli nyingine ya kijamii inayofanyika kesho (Septemba 25 mwaka huu).
Ombi hilo limekubaliwa, hivyo mechi kati ya Toto Africans na Oljoro JKT sasa itachezwa Jumatatu ya Septemba 26 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.
Nawatakiwa mchezo mzuri ambao bila shaka utakuwa burudani tosha kwa mashabiki wa mpira wa miguu wa Mwanza na mikoa ya jirani.

Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inayoongozwa na Kamishna wa Polisi mstaafu Alfred Tibaigana imempiga faini ya sh. 500,000 na kuwekwa chini ya uangalizi kwa miezi sita Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu baada ya kumuona ana hatia kwa mashtaka yaliyowasilishwa dhidi yake na TFF.
Uamuzi wa kamati hiyo iliyokutana leo (Septemba 24 mwaka huu) umetokana na ushahidi uliowasilishwa na TFF, na pia Sendeu mwenyewe kukiri kuwa alifanya makosa.
Sekretarieti ya TFF ilimshtaki Sendeu kwenye kamati hiyo kutokana na matamshi yake dhidi ya mwamuzi Alex Mahagi mara baada ya mechi kati ya Yanga na Ruvu Shooting iliyochezwa Septemba 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Sendeu aliita mkutano na waandishi wa habari na kumshutumu Mahagi kuwa alisababisha timu yake ikose ushindi kwa kuwabeba wapinzani wao na kudai anamfahamu Mahagi kuwa ni mwanachama wa Simba, kadi nyekundu aliyompa kiungo wao Haruna Niyonzima si halali na alifanya hivyo kwa lengo la kuisadia Simba ili iendelee kukaa kileleni mwa ligi.
Kauli hiyo ililenga kumjengea chuki Mahagi mbele ya mashabiki wa Yanga kama ilivyo kwa viongozi na watendaji wa TFF wakati Sendeu akiwa ofisa wa Yanga alikuwa anajua taratibu za kufanya pale klabu yake isiporidhishwa na uamuzi wa mwamuzi au suala lingine lolote.
Kamati hiyo haikusikiliza mashtaka dhidi ya Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage kwa vile hakufika kwenye kikao kutokana na kuwa katika kampeni za uchaguzi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania ubunge wa Jimbo la Igunga mkoani Tabora.
Pia kamati hiyo haikusikiliza mashtaka ya kwanza ya Sendeu kwa vile yanakwenda pamoja na yale ya Rage. Kamati itapanga tarehe nyingine kwa ajili ya kusikiliza mashtaka dhidi ya viongozi hao ambapo watapewa taarifa.

Wakati michuano ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara inayoshirikisha timu 18 imepangwa kuanza Oktoba 15 mwaka huu timu ambazo hazijakamilisha usajili wa wachezaji zimeongezewa muda hadi Oktoba Mosi mwaka huu.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Septemba 24 mwaka huu) chini ya Mwenyekiti wake Makamu wa Pili wa Rais, Ramadhan Nassib pia imepanga makundi ya ligi hiyo itakayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Oktoba 3-9 mwaka huu majina ya wachezaji walioombewa usajili na timu zote 18 yatabandikwa kwenye ubao wa matangazo wa TFF kwa ajili ya pingamizi, na Kamati ya Mashindano itakutana Oktoba 10 mwaka huu kwa ajili ya kupitia majina hayo.
Kundi A litakuwa na timu za Mgambo Shooting Stars ya Tanga, Morani ya Manyara, Polisi Dar es Salaam, Temeke United ya Dar es Salaam, Transit Camp ya Dar es Salaam na Burkina Faso ya Morogoro.
Timu zinazounda kundi B ni Majimaji ya Songea, Mbeya City Council, Mlale JKT ya Ruvuma, Polisi Iringa, Small Kids ya Rukwa na Tanzania Prisons ya Mbeya. Kundi C ni 94 KJ ya Dar es Salaam, AFC ya Arusha, Polisi ya Morogoro, Polisi ya Tabora, Rhino Rangers ya Tabora na Samaria ya Singida.

Tusker Lager yazindua Kampeni Mpya

Leo, Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) inayomiliki kinywaji cha Tusker, inazindua kampeni mpya kusheherekea ubora na urithi wa kinywaji hicho uliodumu tangu ilipoingia nchini mwaka 1922.
Tusker inayozalishwa Tanzania kwa vimelea asilia kwa 100% inaonyesha uasilia wa kinywaji cha Afrika kwa 100%. Kampeni hiyo itakayokuwa na hamasa za kipekee itahusisha Matangazo ya mvuto wa kipekee,Ubalozi maalumu kuwakilisha kinywaji cha Tusker na Matukio ya kipekee katika maeneo mbalimbali nchi nzima katika Promosheni maalumu itakayojulikana kama Tusker ‘Life and Soul’.
“Ikiwa ni bia ya pekee iliyokuwepo wakati Tanzania ikipata uhuru wake mwaka 1961, Kinywaji cha Tusker kimeendelea kuwa na ladha yake ya kipekee na ubora wa kipekee tangu wakati huo”, alisema Ephraim Mafuru,Mkurugenzi wa Masoko wa SBL.
Aliongeza kusema kuwa “Tusker imekuwa kinywaji bora kwa wakati wote na kimekuwa kinywaji kinachoweza kutumika katika sherehe na hafla mbalimbali huku kikitumika kuwakusanyana kuwaweka pamoja watu wenye rika na hulka tofauti katika maisha ya kila siku”,
Alisema promosheni ya kitaifa kwa wateja wote iliyomalizika hivi karibuni iliyojulikana kama ‘Tusker Milioni 500 kwa Mashabiki’ ilikuwa ya mafanikio makubwa ambapo zaidi ya watanzania 121 walijazwa mamilioni ya shilingi.
“Tunajivunia kinywaji cha Tusker ambacho kupitia promosheni hiyo kimeweza kutengeneza mamilionea ambao kwa hakika fedha hizo zimeingia katika uchumi wa Tanzania”, alisema Mafuru
Alisema kinywaji hicho pia kinajivunia udhamini wake katika shindano la Tusker All Stars ambapo Peter Msechu mwakilishi wa Tanzania alishiriki katika mashindano ya kimataifa yaliyofanyika Nairobi, Kenya wiki chache zilizopita.
Kwa upande wake, Meneja wa kinywaji hicho Rita Mchaki alisema “Kujihusisha kwetu katika matukio tofauti ya kihuduma katika taifa hili kunatupa ujasiri wa kujivuna na kutembea kifua mbele”.
Mchaki alisema kinywaji cha Tusker kitaendelea kusaidia mambo mbalimbali ya kimaendeleo katika maeneo tofauti katika kuhakikisha jamii ya kitanzania inakuwa na maisha bora.
“Tuna furaha kushiriki na jamii ya kitanzania katika kampeni yetu mpya ambayo itaanza hivi karibuni.Tunaomba watanzania waangalie mara kwa mara matangazo yetu yatakayoanza kurushwa hivi karibuni”, alisema.

Shirikisho la Mpira wa Miguu la Morocco (FRMF) limehamisha mechi ya kundi D ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Morocco kutoka Casablanca na sasa itachezwa Marrakech.
Mechi hiyo itachezwa saa 1.30 jioni Oktoba 9 mwaka huu. Pia Algeria na Jamhuri ya Afrika ya Kati ambazo ziko kundi hilo zitacheza Oktoba 9 mwaka huu na muda huo huo ili kuepuka kupanga matokeo. Mechi hiyo itachezwa jijini Algiers.
Kwa vile hakuna mashirika ya ndege ya kimataifa yanayokwenda Marrakech, FRMF ndiyo itakayogharamia usafiri wa Taifa Stars kutoka Casablanca hadi Marrakech. Kwa mashabiki wa Tanzania wanaotaka kwenda kuishangilia Taifa Stars nauli kwa ndege za Morocco kutoka Casablanca- Marrakech- Casablanca ni dola 120.
Waamuzi wa mechi kati ya Stars na Morocco watakuwa Gassama Bakary, Jawo Dickory, Touray Sulayman na Camara Bakary, wote kutoka Gambia. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Zoumaro Gnofame kutoka Togo.
Kocha Jan Poulsen anatarajia kutangaza kikosi Septemba 26 mwaka huu kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco na kitaingia kambini Septemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

JAMII imeshauriwa kujiunga na mfumo wa kisasa wa usimamizi wa vyombo vya habari wa kampuni ya Push Observer

Na Mwandishi wetu
JAMII imeshauriwa kujiunga na mfumo wa kisasa wa usimamizi wa vyombo vya habari wa kampuni ya Push Observer ili kuweza kupata taarifa mbalimbali sahihi za kisiasa, kiuchumi, kibiashara na kiafya.
Wito huo ulitolewa na gwiji la masuala ya usimamizi wa vyombo vya habari, Joe Taylor kutoka Marekani katika hafla fupi iliyowakutanisha wafau mbali mbali wa sekta ya habari, uchumi na biashara.
Bw. Taylor alisema kuwa kila mtu anawajibu wa kujua mambo mbali mbali kuhusiana na jamii na njia halisi ni kuputia mfumo wa kisasa (Digital Media Monitoring) ambao urekodi na kuhifadha taarifa hizo.
Alisema kuwa mfumo huo umeenea sana nchi za Amerika na Ulaya na kuishukuru kampuni ya Push Observer kuanzisha utaratibu huo ambao pia usaidia waandishi wa habari na wanafunzi.
Alifafanua kuwa kwa wafanya biashara, mfumo huo ndiyo utawapa mwanga zaidi wa biashara zao kwani utawawezesha kujua mwenendo wa biashara yake, kujua mpinzani au mshindani anafanya nini katika soko husika.
“Ni muhimu kwa wafanyabiashara kupata taarifa sahihi za mwenendo wa biashara husika, makampuni mengi nchi za Marekani na Ulaya yamefanikiwa kutokana na kutumia mfumo huo kwani biashara bila taarifa sahihi ni hasara,” alisema Taylor.
Afisa Mwendeeshaji Mkuu wa Push Observer, Omari Salisbury akimshukuru Bw. Taylor kwa ujio wake na kutoa mwanga wa mfumo huo ambao Tanzania haujaenea sana.
Salisbury alisema kuwa tokea kuanzishwa kwa kampuni yake, mpaka sasa makampuni sita yamejiunga na yanafanya vizuri katika soko.
“Kwa kweli tumefarijika sana na ujio wa Bw. Taylor na tunaamini wadau mbali mbali mbali pamoja na waandishi wa habari watafika katika ofisi zetu ili kupata kumbukumbu taarifa mbali mbali.
Alisema kuwa wameamua kuanzisha kampuni hiyo ili kuiweka Tanzania katika ramani ya kisasa ya mambo ya usimamizi wa vyombo vya habari na kuwapa taarifa wadau masuala ya kijamii kuweza kupata maendeleo ya kisasa.

Participants of a Good Governance workshop, in a group picture with the Minister of State in President’s Office Responsible for Good Governance Hon. Mathias Chikawe shortly after he opened a workshop on good governance organized by Oikocredit Tanzania. Oikocredit which is one the world’s largest sources of private funding to the microfinance sector, has so far loaned out Tshs44 billion to 44 Saccos in Tanzania. The workshop was held at Kuduchi Beach Hotel in Dar es Salaam this week.
Participants of a four-day good governance workshop,follow a lecture on good governance related topic in Dar es Salaam on Wednesday. The workshop has been organized by Oikocredit which is one the world’s largest sources of private funding to the microfinance sector. Oikocredit has so far loaned out Tshs44 billion to 44 Saccos in Tanzania. The workshop was held at Kuduchi Beach Hotel in Dar es Salaam this week.

Upi ? Msimamo wa viongozi wa nchi Afrika kuhusu Libya?
Je ? wanamtambua kiongozi halali wa Libya?
Vipi ? kiongozi wa waasi Mustafa Abdel-Jalil anatambulika na Viongozi wetu?
Wakati viongozi wa nchi mbali mbali wamekutanika mjini New York,kwa ajili
ya mkutano wa umoja wa mataifa UN,katika mkusanyiko huo wamo pia viongozi
wetu kutoka nchi za kiafrika ambao pia ni wanachama wa umoja wa Afrika AU,
ambayo Libya pia ni mwanachama wa AU,lakini utata unakuja nani kiongozi halali
wa nchi hiyo Libya? Kanal Gaddaf au Mstafa Abdel-Jalil ambaye nae yupo huko
New York.
Swali lingine kubwa ambalo wengi wetu tunajiuliza je ?viongozi wa nchi za
Afrika wanautambua uhalali wa Mstafa Abdel- Jalil ?kama hawautambui
je? watakubali kuwepo ukumbini na kumsikiliza otuba ya kiongozi huyo aleyeingia
madarakani kwa njia ya bunduki tena kwa kusaidiwa na NATO? au watakuwepo
ukumbini kwa mithali za kiswahili kila moja na lwake? yaani ya Ngoswe muachie
Ngoswe! je? fadhila za Kanal Gaddaf na mchango wake katika bara la Afrika
ndio zitakua zimesauliwa.
Mengi tunajiuliza lakini siye wafrika tunategea sikio uko UN kusikiliza msimamo
wa viongozi wetu juu ya kauli ya pamoja kuhusu maslahi ya bara la Afrika.