- Mukama ang'aka
- Hukumu ya Lema ilipotikisa Arusha
- MLIPUKO FELI
- Mzimu wa Arumeru wamgeukia Mrema
- Utamaduni wa kutoa rushwa sasa tuukatae
- Wakulima washauriwa kuongeza thamani ya korosho
- Majambazi yavamia viongozi wa kanisa
- Polisi Dar wakamata dawa za kulevya za bilioni 1.4/-
- Watumishi wazorotesha mapato ya halmashauri
- MAZUNGUMZO
- Babati yapewa siku 14 kuwasilisha mchanganuo
- HATARI
- Adha ya umeme yawakumba wabunge
- Kandoro awashukia mafisadi wa dawa
- Adhabu za Yanga zaitoa 'kamasi' TFF
TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, April 12, 2012
Mukama ang'aka
Maskini Lulu, ombi lake latupwa
Na: Elizabeth Michael
Suleiman Mbuguni
MSANII wa filamu nchini, Elizabeth Michael 'Lulu' jjuzi ameshindwa kutoa salamu za mwisho kwa msanii mwenzake katika tasnia hiyo, Steven Kanumba ambaye anadaiwa kabla ya kifo chake walikuwa pamoja nyumbani kwa marehemu Sinza Vatcan jijini Dar es Salaam.
Lulu ambaye anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Osterbay, Kinondoni jijini Dar es Salaam inadaiwa kwamba aliomba kwenda kutoa salamu za mwisho kwa msanii huyo nguli wa filamu ambaye alifariki Aprili 7, mwaka huu nyumbani kwake Sinza, Dar es Salaam.
Hata hivyo msanii huyo alishindwa kutokea katika shughuli za kumuaga Kanumba, kutokana na habari zilizodai kwamba ni za kiusalama.
Juzi Kamanda wa Mkoa wa Polisi Kinondoni, Charles Kenyela alinukuliwa katika vituo vya televisheni nchini akisema kwamba Lulu anashikiliwa katika cha Oysterbay, lakini kwa kuwa suala hilo lipo kisheria alikuwa anasubiri matokeo ya daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Kanumba.
"Ni kweli tunamshikilia Lulu, lakini hata hivyo hatuwezi kulizungumzia lolote kwa kuwa suala hili lipo kisheria na bado mwili wa marehemu unafanyiwa uchunguzi hospitalini," alisema Kenyela.
Hata hivyo katika shughuli za kuuga mwili wa Kanumba yaliyofanyika katika viwanja Leaders Klabu, Dar es Salaam maelfu waliojitokeza kutoa salamu za mwisho kwa nyota huyo wa filamu nchini walishindwa kufanya hivyo kutokana na wingi wa watu waliojitokeza.
Ilikuwa ni simanzi, majonzi na vilio katika viwanja hivyo baada ya mwili wa Kanumba kuwasili sehemu iliyotayarishwa, huku baadhi ya wanawake wakidondoka na kupoteza fahamu.
Hatua hiyo iliwafanya watoa huduma ya kwanza kutoka Msalaba Mwekundu kuwa na shughuli pevu ya kuwapeleka katika magari yao kwa ajili ya kuwahudumia.
Kutokana na tafrani hiyo MC alilazimika kutangaza kusitisha shughuli ya kumuaga Kanumba, kitu ambacho watu waliofika katika viwanja hivyo kuanza kupiga kelele za kutoridhishwa.
Hata hivyo kabla ya kutangaza kusitisha viongozi wa serikali walioongozwa na Makamu wa Rais, Mohamed Ghalib Bilal kupewa nafasi ya kuuga mwili huo pamoja na baadhi ya ndugu wa karibu.
Viongozi wengine waliopata nafasi ya kutoa salamu za mwisho kwa marehemu Kanumba, alikuwa mke wa Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete, Mke wa Makamu wa Rais Mama Bilal, Waziri Ardhi Anna Tibaiujka, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe.
Viongozi wengine ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mecky Sadiq, Mbunge wa Kinondoni Idd Azzan, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana na Meya wa Manispaa hiyo, Yusuf Mwenda.
Tuesday, March 13, 2012
Lipumba arejea kuinusuru CUF
- Sitta: Lazima tuisafishe CCM yetu
- Mkapa kuzindua kampeni Arumeru kwa kishindo
- Udhalilishaji walimu Karatu haukubaliki!
- Mifuko ya NHIF, CHF yakwamishwa
- Serikali yatangaza kuwapa wakulima miche ya karafuu
- CHADEMA wajitokeza kuwania Ubunge EAC
- Wachezaji Yanga tuhuma nzinto
Sunday, March 11, 2012
RC awashukia watendaji wenye majungu ofisini
Na Charles Mwakipesile, Mbarali
MKUU wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro, amewataka watumishi wenye tabia ya kuwasema wenzao ofisini 'majungu', kuacha mara moja ambapo watakaobainika kuwa na tabia hiyo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Bw. Kandoro aliyasema hayo juzi katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri Wilaya ya Mbaarali, mkoani hapa Bw. George Kagomba.
Hafla hiyo ilifanuyika katika Makao Makuu ya halmashauri hiyo baada ya kustaafu utumishi wa umma na kuongeza kuwa, siri ya mafanikio kwa mtendaji yeyote wa Serikali ni kuchapa kazi kwa bidii, kuepuka majungu.
Alisema kitendo cha kuwagawa wafanyakazi kinakwamisha maendeleo ya wannchi na utekelezaji wa shughuli za Serikali.
“Kiongozi ambaye leo tunamuaga, amefanya kazi kwa bidii na kufanikiwa kuleta mabadiliko makubwa, kufyeka kichaka porini na kujenga Makao Makuu ya Halmashauri.
“Bw. Kagomba ni kielelezo cha watendaji bora wa serikali wasio na majungu ambaye amewaunganisha wafanyakazi kuwa kitu kimoja na kuharakisha maendeleo,” alisema.
Alisema watendaji wa Serikali ambao wanaendeleza majungu badala ya kufanya kazi, huambulia kufukuzwa na kutokumbukwa kwa lolote walilofanya wakati wa utumishi wao serikalini.
“Sipendi kusikia Mkoa wetu unakosa maendeleo kwa sababu watumishi hutumia muda mwingi kuzungumza habari za majungu badala ya kufanya kazi kwa bidii,” alisema.
Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Bw. Keneth Ndingo, alisema Bw. Kagomba atakumbukwa kwa mambo mengi pamoja na kujenga Makuu Makuu ya halmashauri hiyo ambayo ina majengo ya kisasa yaliyozinduliwa na Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya kufanikisha ujenzi wa majengo hayo pia ameweza kukuza pato la halmashauri na ujenzi wa majengo ya sekondari za kata hivyo aliiomba Serikali iangalie uwezekano wa kumuongezea muda wa utumishi kwa mkataba maalumu.
Kwa upande wake, Bw. Kagomba alisema bila kupata ushirikiano kutoka kwa watumishi wengine, asingeweza kufanikisha majukumu aliyopewa ambayo yamezaa matunda.
MKUU wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro, amewataka watumishi wenye tabia ya kuwasema wenzao ofisini 'majungu', kuacha mara moja ambapo watakaobainika kuwa na tabia hiyo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
Bw. Kandoro aliyasema hayo juzi katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri Wilaya ya Mbaarali, mkoani hapa Bw. George Kagomba.
Hafla hiyo ilifanuyika katika Makao Makuu ya halmashauri hiyo baada ya kustaafu utumishi wa umma na kuongeza kuwa, siri ya mafanikio kwa mtendaji yeyote wa Serikali ni kuchapa kazi kwa bidii, kuepuka majungu.
Alisema kitendo cha kuwagawa wafanyakazi kinakwamisha maendeleo ya wannchi na utekelezaji wa shughuli za Serikali.
“Kiongozi ambaye leo tunamuaga, amefanya kazi kwa bidii na kufanikiwa kuleta mabadiliko makubwa, kufyeka kichaka porini na kujenga Makao Makuu ya Halmashauri.
“Bw. Kagomba ni kielelezo cha watendaji bora wa serikali wasio na majungu ambaye amewaunganisha wafanyakazi kuwa kitu kimoja na kuharakisha maendeleo,” alisema.
Alisema watendaji wa Serikali ambao wanaendeleza majungu badala ya kufanya kazi, huambulia kufukuzwa na kutokumbukwa kwa lolote walilofanya wakati wa utumishi wao serikalini.
“Sipendi kusikia Mkoa wetu unakosa maendeleo kwa sababu watumishi hutumia muda mwingi kuzungumza habari za majungu badala ya kufanya kazi kwa bidii,” alisema.
Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Bw. Keneth Ndingo, alisema Bw. Kagomba atakumbukwa kwa mambo mengi pamoja na kujenga Makuu Makuu ya halmashauri hiyo ambayo ina majengo ya kisasa yaliyozinduliwa na Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya kufanikisha ujenzi wa majengo hayo pia ameweza kukuza pato la halmashauri na ujenzi wa majengo ya sekondari za kata hivyo aliiomba Serikali iangalie uwezekano wa kumuongezea muda wa utumishi kwa mkataba maalumu.
Kwa upande wake, Bw. Kagomba alisema bila kupata ushirikiano kutoka kwa watumishi wengine, asingeweza kufanikisha majukumu aliyopewa ambayo yamezaa matunda.
Posted: 08 Mar 2012 10:45 PM PST
Na Zahoro Mlanzi
SERIKALI
imesema mpaka kufikia mwishoni mwa Aprili mwaka huu Uwanja wa Uhuru,
Dar es Salaam utakuwa tayari umekamilika kwa asilimia 75 na utaanza
kutumika kwa shughuli mbalimbali rasmi Juni, mwaka huu.
Uwanja huo awali ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru lakini mpaka kufikia Desemba 9, mwaka jana ulikuwa haujakamilika, hivyo sherehe hizo kulazimika kufanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Serikali ulisimamisha shughuli za uwanja huo, tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2010/2011.
Akijibu swali kuhusu uwanja huo utakamilika lini, baada ya kushindwa kukamilika kabla ya kuanza kwa sherehe za Uhuru wa miaka 50 Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Leonard Thadeo alisema ni kweli ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za Uhuru, lakini kikubwa kilichokwamisha ni mkandarasi alichelewesha baadhi ya mambo muhimu.
“Hivi sasa ujenzi unaendelea kama kawaida na ninakuhakikishia mpaka kufikia mwishoni mwa Aprili, mwaka huu utakuwa umekamilika kwa asilimia 75, kwani kazi kubwa iliyobaki ni kuweka viti katika jukwaa mbalimbali zilizojengwa,” alisema Thadeo.
Alisema wakati maboresho hayo yakiendelea kwa kuhakikisha viti vinawekwa na mambo mengine, mpaka kufikia Juni mwaka huu ana imani kila kitu kitakuwa kimekamilika na shughuli mbalimbali zilizokuwa zikifanyika katika uwanja zitaendelea kama kawaida.
Thadeo alisema kukamilika kwa uwanja huo kutapunguza matumizi ya Uwanja wa Taifa, kwani mechi zitakazokuwa si za lazima kuchezewa kwenye uwanja huo, zitafanyika Uwanja wa Uhuru kama ilivyokuwa hapo awali.
Pia alitoa wito kwa mashabiki na wanamichezo kwa ujumla kuhakikisha kuutumia vizuri uwanja huo, pindi utakapokamilika ili kuepusha madhara yatakayoweza kujitokeza kama ilivyokuwa katika mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba na Kiyovu ya Rwanda.
Katika mechi hiyo ya Simba, viti 152 viliharibiwa na 11 vilivunjwa kutokana na mashabiki hao kuvunja na kurushiana wakati mechi hiyo ikiwa mapumziko.
Uwanja huo awali ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za miaka 50 ya Uhuru lakini mpaka kufikia Desemba 9, mwaka jana ulikuwa haujakamilika, hivyo sherehe hizo kulazimika kufanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Serikali ulisimamisha shughuli za uwanja huo, tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2010/2011.
Akijibu swali kuhusu uwanja huo utakamilika lini, baada ya kushindwa kukamilika kabla ya kuanza kwa sherehe za Uhuru wa miaka 50 Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Leonard Thadeo alisema ni kweli ulitakiwa kukamilika kabla ya sherehe za Uhuru, lakini kikubwa kilichokwamisha ni mkandarasi alichelewesha baadhi ya mambo muhimu.
“Hivi sasa ujenzi unaendelea kama kawaida na ninakuhakikishia mpaka kufikia mwishoni mwa Aprili, mwaka huu utakuwa umekamilika kwa asilimia 75, kwani kazi kubwa iliyobaki ni kuweka viti katika jukwaa mbalimbali zilizojengwa,” alisema Thadeo.
Alisema wakati maboresho hayo yakiendelea kwa kuhakikisha viti vinawekwa na mambo mengine, mpaka kufikia Juni mwaka huu ana imani kila kitu kitakuwa kimekamilika na shughuli mbalimbali zilizokuwa zikifanyika katika uwanja zitaendelea kama kawaida.
Thadeo alisema kukamilika kwa uwanja huo kutapunguza matumizi ya Uwanja wa Taifa, kwani mechi zitakazokuwa si za lazima kuchezewa kwenye uwanja huo, zitafanyika Uwanja wa Uhuru kama ilivyokuwa hapo awali.
Pia alitoa wito kwa mashabiki na wanamichezo kwa ujumla kuhakikisha kuutumia vizuri uwanja huo, pindi utakapokamilika ili kuepusha madhara yatakayoweza kujitokeza kama ilivyokuwa katika mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Simba na Kiyovu ya Rwanda.
Katika mechi hiyo ya Simba, viti 152 viliharibiwa na 11 vilivunjwa kutokana na mashabiki hao kuvunja na kurushiana wakati mechi hiyo ikiwa mapumziko.
Subscribe to:
Posts (Atom)